Kwanini si muumini wa Serikali Tatu...

Kwanini si muumini wa Serikali Tatu...

Inawezekana kabisa Mwalimu Nyerere alikuwa sahihi wakati anaongea mambo aliyoyanukuu MMM. Ila ukweli ni kuwa kuongelea serikali moja kwa sasa ni kupingana na uhalisia wa mambo ulivyo. Mambo yamebadilika sana tangu Nyerere alipoongea. Zanzibar ina katiba mpya ambayo kimsingi imeifanya kuwa nchi kamili yenye rais, bunge, mahakama, jeshi, wimbo wa taifa, utaifa-uzanzibari, na eneo kama lilivyoainishwa kwenye katiba yao. Leo hii muungano ukivunjika wenzetu wa Zanzibar hawana shida kwani tayari wana mfumo wa kiutawala unaofanya kazi. Sasa kuongolea serikali moja ni sawa kabisa na kuwaambia wazanzibari wavunje serikali yao, bunge lao na utaifa wao ambao wamekuwa nao kwa miaka mingi. Hili halitawezekana na utakuwa ni ubeberu mbaya hata kuliko ule wa mkoloni. Kwa watanganyika hakuna shida kwani tayari serikali yetu ilishavunjwa na kugeuzwa kuwa ya kiruhani ambayo ni mali ya wote.

Mfumo wa sasa wa Serikali mbili haubebeki tena kwani umekuwa ni kero kwa muungano hasa kwa wazanzibari ambao wanauona kama kikwazo cha wao kupata uhuru kamili wa kusimamia mambo yao. Lakini pia ni kero kwa watanganyika kwani tunaona wazanzibari wakipata fursa ya kujadili na kusimamia mambo ya Tanganyika kwa kisingizio cha utanzania wao. Tuna kamati za bunge zenye wajumbe wazanzibari ambazo zinajadili taasisi zisizokuwa za muungano na vile vile tuna mzanzibari amepewa uwaziri wa wizara ya afya ambayo ni ya Tanganyika.

Tanganyika haiwezi tena kuendelea na uruhani katika mazingira ya sasa yanayotaka kuwepo kwa uwazi katika uendeshaji wa masuala ya serikali. Hivyo kuna njia mbili tu zenye uhalisia zaidi:ya kwanza ni kuwa na serikali tatu ikiwepo ya Tanganyika inayoonekana wazi na inayojulikana inachosimamia kwenye muungano na Zanzibar na pili kuvunja muungano na kila mmoja achukue hamsini zake ila tuwe na mikataba ya ushirikiano wa kiuchumi na labda kiulinzi. Kwa kuwa tume ilipewa hadidu za rejea zinazoitaka kulinda muungano basi waliona hii ya kuwepo kwa serikali ya Tanganyika kama option pekee inayofaa na mimi nawaunga mkono kwa asilimia mia moja.
 
.......
Mimi napinga serikali tatu - naamini kama kweli watu wanataka tuimarishe Muungano basi ni kuunda nchi moja, serikali moja mifumo mbalimbali au utengano! Kwani nani kasema ni lazima tuungane? Hatutakuwa nchi ya kwanza duniani kuvunjika na watu kuendelea kuishi pamoja na ujirani mwema.
Pole sana Mwanamtaa/kijiji, nyongo yangu ilikuwa imepanda ila baada ya kusoma kipande hicho imetelemka kidogo. Ugomvi wangu ni mtu kama Nape anayesema serikali mbili ziendelee. Kwa msimamo wako naweza kukubaliana nao ila Wazenj hawataki na kama hawataki basi solution ni serikali tatu.
 
MM,
Tusidanganyane, tumebakiwa na option mbili tu, Kuwa na serikali moja au tatu. Serikali mbili haiwezekani tena. Hata ccm leo wakilazimisha itachukua miaka michache tutarudi kwenye tope la matatizo ya kero za muungano.

Na kwa kuwa Wazanzibari hawataki kuua utaifa wao kama sisi watanganyika tulivyoua tanganyika yetu, basi kama Yereck wa Nyerere anavyosema serikali tatu haikwepiki. Naishukuru Chadema kuliona hili mapema na kuiweka ktk sera yake.

Tatu, ktk dunia ya Leo kama ni kweli kwamba serikali tatu itavunja muungano na kama muungano utavunjika kweli miaka kadhaa ijayo, kwani kuna tatizo gani? watz hawatakuwa wakwanza kuvunja muugano wao, duniani kote mifano iko mingi ya miungano iliyovunjika, and by the way ndivyo tulivyokuwa kabla ya 1964.

Nne, Muungano uliopo hauwatendei haki watanganyika. Ni muugano wa chako ni chako, ila changu ni chetu sote. Yaani mimi siwezi kuwa waziri Zanzibar, ila mzanzibari anaweza kuwa waziri Tanganyika kupitia Serikali ya MUUNGANO. Leo hii mzanzibar ni waziri wa Afya wakati afya haiko ktk muungano. Zanzibar kuna waziri wa afya. Waziri wa afya wa Muungano kiuhalisia ni waziri wa afya wa Tanganyika. kwa hiyo waziri wa afya kutoka zanzibar anaongoza wizara ya Serikal ya Tanganyika iliyofutwa kiaina huko nyuma. SASA kwa nini iwe hivyo?

Tano, Ni jambo la bahati nzuri sana kwamba, wanaoongoza kuupinga muungani ni wazanzibar, na naomba tuwape haki yao. Wazanzibar wamediriki kusema wao hawataki kuwa koloni la Tanganyika. sisi tuna hofu nini?

Mwanasheria mkuu wa zbar kasema kero kubwa ya muungano ni kutokuwepo kwa serikali ya Tanganyika. We should not fear the unknown, we should face the challenges of 3 governments, na kama muungano utavunjika, tutakuwa kama tulivyokuwa kabla ya mwaka 1964, si vita.

1. Hizo options zimetoka wapi? Ni asilimia ngapi ya wazanzibari na watanganyika separately wanataka muungano mpaka utoe hizo options?

2. Utaifa hahusiani na serikali, hii siasa mmesomea wapi? Kuna state, nation na nation-state. Siyo kila taifa lina nchi na siyo kila nchi ina taifa moja.Na taifa moja linaweza kuwa na nchi nyingi au kwenye nchi nyingi. Tibet, Balochi, Kurdi hata Yahudi siyo makabila, ni mataifa yaliyo kwenye nchi nyingi tu.

3. Kwanini tufanye kitu ambacho unafikiri kuwa hakitafanikiwa? ... kwanini usiende step by step kama alivyopendekeza Lisu? Bring tanganyika first, then claim political will. Do not institute political will.

4.Muungano wowote ule ni lazima uwe na seikali ya pamoja, ziwe mbili au mia mbili, haijalishi. The issue here is the constitutional features of a polity, not administrative au fiscal management of a polity.... sijui unaelewa??

5. Watanganyika hawajapewa nafasi ya kuchagua kama wanataka au hawataki muungano, vilevile wazanzibari. Tupe data.
 
Nikiwa Rais wa Tanzania pendekezo langu la kwanza ningeuvunjilia mbali muungano huu uliowekwa kwa ajili ya maslai ya walafi wachache..Ni muungano wa ajabu sana unaopatikana kwenye nchi ya ajabu sana..Wanao nufaika na huo muungano ni walafi kama akina Dr. Shein ambao wanajipatia mafao ya pande zote mbili..Muungano wa kihuni kabisa!!
 
Mi nadhani huu mjadala wa Muungano uahirishwe kwa miaka 20, na watu wa elimishwe, historia ya kweli iandikwe na ifundishwe mashulei Kizazi kijacho kiamue muungano uweje
Wazo zuri ila Wazanzibar hawahitaji kuelemishwa kuhusu muungano! tayari wanajitambua wanajua ni kitu gani wanataka, Zanzibar yao.

Kuuahirisha Muungano miaka ishirini kwa ajili ya kuelemishana kuhusu Muungano ni kutowatendea haki Wazanzibar.
 
Hivi wadanganyika hakuna nchi nyengine ya kuungana nayo lazima iwe zanzbr?
 
Ukimsoma Baba wa Taifa ukamwelewa vizuri utashangaa jinsi tunavyofikiri sasa!! Mwalimu alikuwa anajadili muungano bila kujifunga na serikali mbili tu lakini unaona anashangaa wanaong'ang'ania serikali tatu bila kujadili alternative zingine tena bila majadiliano rasmi kuhusu aina zingine zote za muungano kabla hatujasimama na kutaka serikali tatu tu ambayo inakwenda kuvunja muungano taratibu.

Natamani kuona maoni ya wanasiasa wa sasa hasa kwa kupangua hizi hoja za Mwl Nyerere zilizowekwa hapa (maana wote wanataka serikali tatu).

CC Zitto , John Mnyika , Wilbroad Slaa , Nape Nnauye , Tundu Lisu bila kumsahau Mchambuzi
 
Last edited by a moderator:
Hivi wadanganyika hakuna nchi nyengine ya kuungana nayo lazima iwe zanzbr?
Anayetaka kuungana na Zanzibar nani? .... tulikuwa tunakuja na passports huko, mkasema haina haja. Nyie ndo mmejazana huku. Msipende kuhalalisha mambo ambayo hayapo.

Mbona hata Rufiji kuna mafenesi?
 
MMM

nanukuu.

Nyerere anasema hivi:


Muundo wa Muungano, pamoja na kwamba hatutaki uwe ukitibuliwatibuliwa mara kwa mara, ni suala
la sera, si amri ya Mungu.
Vyama vya siasa mbalimbali vinaweza vikawa na maoni mbalinbali kuhusu
muundo unaofaa kwa Katiba ya nchi yetu. Muundo utakaokubaliwa na wananchi walio wengi ndio
utakaokuwa sehemu ya Katiba ya nchi yetu. Muundo wa Serikali mbili unakubaliwa na wananchi,
lakini unatokana na sera ya TANU na ASP, na kwa sasa CCM. Chama Cha Mapinduzi kikipenda
kinaweza kubadili sera hiyo ya muundo wa Serikali mbili bila kuuliza wananchi kwanza. Kinaweza
kufunya hivyo kwa kuhisi kuwa hivyo ndivyo wananchi wengi watakavyo; lakini pia kinaweza kufanya
hivyo kwa sababu kinaamini kuwa inafaa kufanya hivyo, hata kama wananchi wengi hawakudai au
hawapendi mabadiliko.


Kauli hii ya Mwl Nyerere hususani hapo kwenye bluu inathibitisha kuwa hata utetezi wa Mwl Nyerere kwa serikali mbili ilikuwa ni suala la sera kulingana na wakati. Tukijiuliza kuwa je wakati tulionao unasadifu kuwa na serikali tatu ama lah tutapata jibu. Binafsi nakubaliana na mapendekezo ya serikali tatu maana sera ya serikali mbili haijajibu kero sio tu za muungano, bali sera hii haijawanufaisha Watanzania waliomo kwenye muungano kwa kiasi cha kuridhisha ndio maana haishangazi kuona kuwa hoja iliyoibuliwa takribani miaka 20 iliyopita bado inasimama leo hii.

Hivyo basi, tushughulikie sera hii ya serikali tatu tuone itafanikisha maendeleo ya watu kwa kiasi gani badala ya kushikilia sera ya serikali mbili inayoendelea kuumiza na kukwaza watu kila uchao.
 
With all due respect to the Zanzibari AG, I beg to differ. Kero kuu ya Muungano si kukosekana kwa serikali ya Tanganyika bali ni former Empire Zanzibar kutaka kutambulika kama nchi kamili. Hakuna federation yenye upuuzi huo. AG wa Zanzibar anazungumzia Marekani na uswisi kama mifano ya kuigwa wakati anasahau kuwa hakuna siku California (ambao uchumi wake ungeifanya nchi tajiri mno) au canton moja ya Uswisi ( K.M. Zurich au Geneva au Ticino) zimedai kuwa ni sovereign nation. Panapoanza choko choko za sovereignity ndipo matatizo yanazuka. Mfano ni Spain (Catalan) na Canada (Quebec).

Mfumo wa nchi tatu utafanikiwa tu pale ambapo constituent parties zote zitakubali kupoteza sovereignity zao, yaani Tanganyika inakuwa si nchi bali jimbo na Zanzibar hivyo. Kufanya vinginevyo ni ku-postpone the inevitable ambao ni kuvunjika kwa Federation. Kwa sababu Zanzibar wanatuambia kuwa haitakuja siku wakubali kuwa wao ni jimbo (State) basi serikali tatu itakuwa doomed kuanzia mwanzo. Ndio maana baadhi yetu tunasema, badala ya kuumizana na kupoteza muda basi uamuzi ufanywe Muungano uvunjwe na kila mmoja achukue hamsini zake. Tuwaige Czechoslovakia na si Yugoslavia.

Kinachoshangaza ni pale ndugu zetu wanaotaka sovereignity yao wanapokataa hili na kusititiza tuwe na Muungano hata kama hauna tija yeyote. Hii ni kutaka kula keki yako na kubaki nayo wakati mmoja.

Mimi nakubaliana na wenzaku kuwa pafanyike referendum ambapo watu wa bara na visiwani wataulizwa kama wanaoutaka Muungano. Ikiwa pande moja itakataa, tuanze taratibu za kuagana.

Amandla.........
 
My perceptions ni kuwa Mwanakijiji ni mmoja kati ya watu ambao wanapenda muungano uvunjike ndio maana kaja na hoja ya serikali moja. Kwa mazingira ya sasa serikali moja haiwezekani kwani itapoteza Identity ya Zanzibar. Serikali mbili hatuzitaki kwa kuwa zinalalamikiwa sana na wazanzibari na pia zimepoteza Identity ya Tanganyika. Suluhisho ni serikali tatu maana imefikia hadi watu wa CCM wanaikana historia na kusema tisa disemba ni uhuru wa Tanzania Bara, hatuwashangai ni malimbukeni wa historia. Serikali mbili zimekumbatia sana ufisadi na pia wamekuwa waki adjust mambo ya muungano kwa faida zao binafsi. Pia suala la Rais wa Zanzibar kuchaguliwa Dodoma halitufurahishi watanganyika wengi kwa minajili kuwa Amiri jeshi mkuu wa nchi ya Zanzibar atachaguliwaje Tanganyika!?

Serikali tatu ndio suluhisho, tusiwaza katika misingi ya Rais wa Muungano hatakuwa na nguvu kwani tutengeneza taasisi na sio kuangalia maslahi binafsi ya wanaCCM kuwa ndani ya serikali tatu itakuwa vigumu sana kwao ku COVER ufisadi na wizi mkubwa waliolifanyia taifa kwa miaka 50 hivyo wanajua serikali mbili zitaendelea kuweka mambo kama ya EPA na Richmond chini ya kapeti. Ikija serikali tatu rais wa Tanganyika anaweza kufunua kapeti na kukuta uvundo na kufuatilia huo uvundo na kuwasweka Limande wanCCM waliohusika, ndio maana wanaCCM hawataki kusikia serikali tatu
 
My perceptions ni kuwa Mwanakijiji ni mmoja kati ya watu ambao wanapenda muungano uvunjike ndio maana kaja na hoja ya serikali moja. Kwa mazingira ya sasa serikali moja haiwezekani kwani itapoteza Identity ya Zanzibar. Serikali mbili hatuzitaki kwa kuwa zinalalamikiwa sana na wazanzibari na pia zimepoteza Identity ya Tanganyika. Suluhisho ni serikali tatu maana imefikia hadi watu wa CCM wanaikana historia na kusema tisa disemba ni uhuru wa Tanzania Bara, hatuwashangai ni malimbukeni wa historia. Serikali mbili zimekumbatia sana ufisadi na pia wamekuwa waki adjust mambo ya muungano kwa faida zao binafsi. Pia suala la Rais wa Zanzibar kuchaguliwa Dodoma halitufurahishi watanganyika wengi kwa minajili kuwa Amiri jeshi mkuu wa nchi ya Zanzibar atachaguliwaje Tanganyika!?

Serikali tatu ndio suluhisho, tusiwaza katika misingi ya Rais wa Muungano hatakuwa na nguvu kwani tutengeneza taasisi na sio kuangalia maslahi binafsi ya wanaCCM kuwa ndani ya serikali tatu itakuwa vigumu sana kwao ku COVER ufisadi na wizi mkubwa waliolifanyia taifa kwa miaka 50 hivyo wanajua serikali mbili zitaendelea kuweka mambo kama ya EPA na Richmond chini ya kapeti. Ikija serikali tatu rais wa Tanganyika anaweza kufunua kapeti na kukuta uvundo na kufuatilia huo uvundo na kuwasweka Limande wanCCM waliohusika, ndio maana wanaCCM hawataki kusikia serikali tatu

Ndipo hapa mnapokosea. Hamuwezi kuwa na Muungano halafu kila mmoja akawa na Identity yake. Mmarekani anajulikana kwanza kama mmarekani halafu ndipo unapofuata u-jimbo (m-california, m-alabama n.k.). Hautamsikia mtu anajitambulisha kama yeye ni m-New Soutyh Wales bali m-Australia. Kama kweli tunataka kujulikana au kutambuliwa kama waTanganyika na Wazanzibari basi tutatimiza azma hiyo kwa kuvunja muungano tu. Hatuwezi kuwa na nchi Tanzania halafu m-tanganyika anajivunia utanganyika wake kuliko uTanzania na hali kadhali kwa m-Zanzibari. Wanaotaka identity yao waseme wazi kuwa tuwe nchi mbili tofauti ambazo kama zitataka zitakutana kwenye jumuia kama EAC, UN n.k. Tusijidanganye na hii "mirage" ya serikali tatu.

Amandla.....
 
With all due respect to the Zanzibari AG, I beg to differ. Kero kuu ya Muungano si kukosekana kwa serikali ya Tanganyika bali ni former Empire Zanzibar kutambulika kama nchi kamili. Hakuna federation yenye upuuzi huo. AG wa Zanzibar anazungumzia Marekani na uswisi kama mifano ya kuigwa wakati anasahau kuwa hakuna siku California (ambao uchumi wake ungeifanya nchi tajiri mno) au canton moja ya Uswisi ikidai kuwa ni sovereign nations. Panapoanza choko choko za sovereignity ndipo matatizo yanazuka. Mfano ni Spain na Catalan. Mfumo wa nchi tatu utafanikiwa tu pale ambapo constituent parties zote zitakubali kupoteza sovereignity zao, yaani Tanganyika inakuwa si nchi bali jimbo na Zanzibar hivyo. Kufanya vinginevyo ni ku-postpone the inevitable ambao ni kuvunjika kwa Federation. Kwa sababu Zanzibar wanatuambia kuwa haitakuja siku wakubali kuwa wao ni jimbo (State) basi serikali tatu itakuwa doomed kuanzia mwanzo. Ndio maana baadhi yetu tunasema, badala ya kuumizana na kupoteza muda basi uamuzi ufanywe Muungano uvunjwe na kila mmoja achukue hamsini zake. Tuwaige Czechoslovakia na si Yugoslavia.

Kinachoshangaza ni pale ndugu zetu wanaotaka sovereignity yao wanapokataa hili na kusititiza tuwe na Muungano hata kama hauna tija yeyote. Hii ni kutaka kula keki yako na kubaki nayo wakati mmoja.

Mimi nakubaliana na wenzaku kuwa pafanyike referendum ambapo watu wa bara na visiwani wataulizwa kama wanaoutaka Muungano. Ikiwa pande moja itakataa, tuanze taratibu za kuagana.

Amandla.........
 
Aprili 30, 1992 aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais John Samwel Malecela alitoa hotuba ndefu Bungeni ambapo alipinga hoja ya serikali tatu. Kwanza alipinga kwa sababu tume ya Nyalali ilipata asilimia 49 tu ya watu 36299 waliotoa maoni walitaka serikali tatu. Kwamba watu karibu 17,000 ndio walitaka serikali tatu na kwa hilo tu tume ikapendekeza serikali tatu. Hata sasa suala la serikali tatu hatujaambiwa ni watu wangapi wanataka hilo kwenye tume ya Warioba hadi Tume iliingize kwenye rasimu ya Katiba. Na idadi hiyo inaendana vipi na wale wengine waliotaka mifumo mingine ya serikali.

Malecela alisema kwa uthabiti hivi:

Nyerere akielezea hili kwenye kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (UWHT) anasema hivi:



Nyerere aliona - na mimi nakubaliana naye - suala la kudai Tanganyika wakati ule kama ilivyo leo ni suala la tamaa ya uongozi na matokeo yatakuwa ni yale yale.

Nyerere aliona kuwa watu wa Tanzania wanachotaka ni kuwadhibiti viongozi wao. Yeye aliona kwa usahihi kabisa kuwa kuleta Tanganyika haitatatua tatizo la viongozi wahalifu kwani sasa utakuwa na viongozi wabovu kwenye Muungano na wengine kwenye Tanganyika na Zanzibar. Alisema suala basi ni kuweka utaratibu wa kuwawajibisha viongozi sawasawa.

Nyerere akaelezea vizuri kwanini wakati wa Muungano hatukwenda kwenye serikali moja au kwenda serikali tatu. Alisema hivi:



Ni vizuri kuangalia hizo namba leo hii; Zanzibar ina watu kama milioni 1.3 na Bara kuna zaidi ya watu milioni 45. Hivyo serikali tatu kwa mantiki ya Nyerere bado Tanganyika itabeba mzigo mkubwa zaidi - kuwa na serikail ya kuhudumia watu milioni 45 na pia kuchangia mchango mkubwa kwa serikali ya watu milioni 46.3.

Nyerere alikutana na viongozi wa chama na wabunge wa CCM na kuwashawishi kuipinga hoja ya serikali tatu na serikali nayo. Lakini alipoondoka kwenye Asia akiwa kwenye ziara ya Nchi za Kusini (alikuwa Mwenyekiti) huku nyuma serikali na viongozi wakashindwa kupinga kwa hoja maridhawa kabisa serikali tatu (kama tunavyoona sasa). Nyerere aliandika kwa ukali na uwazi hili tena kwa mshangao. Alisema:



Nyerere alifikia hitimisho ambalo hata leo tunaliona. Watu wanataka serikali ya Tanganyika kwa sababu wamechoka na Wazanzibari. Nyerere anasema hivi:



Muundo wa Muungano unabadilika na si lazima uwe serikali tatu
Mimi siamini katika serikali tatu kwa kiasi kikubwa kwa sababu zile zile za Nyerere. Lakini pia ninaamini kuwa wananchi ndio wana haki ya kuamua mfumo wa Muungano na hata uwepo wa Muungano wenyewe. Sasa hivi watu wanajadili serikali tatu kwa sababu wamekatazwa kujadili kuuvunja Muungano! Watu wamekubali kuwa ni lazima tuungane hivyo tutafute namna ya MUungano. Mimi naamini wananchi ndio wanapaswa kuamua kwanza kama Muungano uwepo na wakishaamua hivyo uwe wa namna gani.

Nyerere anasema hivi:


Na Hapa chini ndio msimamo wangu vile vile: Kwanini tunalazimishwa kujadili serikali tatu. Kwanini tumesalimu amri na kufikiria serikali tatu? Kwanini CCM wameamua tujadili serikali tatu na sisi tunajadili serikali tatu. Hivi kweli watu wanafikiria hili wazo la serikali tatu limetokana na wananchi kwenye maoni ya tume ya Warioba au ni carryover ya mjadala wa 1992?

Nyerere anasema:


Na maneno haya ya Nyerere yasikike kwenye masikio yaliyoziba ya watawala wetu walioshindwa!



Serikali tatu haitotatua matatizo ya Muungano itayaongeza tu. Tunaopinga serikali tatu hatupingi kwa sababu ya gharama tu - hili ni jambo dogo zaidi lakini tunapinga kwa sababu ya mantiki nzima ya kuwa na serikali tatu na nchi mbili! lakini wenzetu wanataka tuwe na nchi mbili na serikali tatu!

Mimi napinga serikali tatu - naamini kama kweli watu wanataka tuimarishe Muungano basi ni kuunda nchi moja, serikali moja mifumo mbalimbali au utengano! Kwani nani kasema ni lazima tuungane? Hatutakuwa nchi ya kwanza duniani kuvunjika na watu kuendelea kuishi pamoja na ujirani mwema.
Maswali yangu ni haya: je kwa nini zanzibar wao wawe na rais mwenye mamlaka kamili na sisi tusiwe na rais wetu mwenye mamlaka na Tanganyika? Je kwa nini kama tumeungana hajachaguliwa mtu toka bara kuongoza serikali ya zanzibar kama kweli tumeungana? Nashauri tuwe na uhuru zaidi wa kupambanua masuala haya. Sioni haja ya kuubeba muungano ambao hauko sawa!
 
Namuunga mkono MWANAKIJIJI kwani hata mimi mtazamo wangu ni kuwa na serikali moja tu ya JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. na hii itasaidia kuondoa dhana na malalamiko yanayojitokeza kila kukicha toka pande moja kwa kuilaumu pande nyingine ama kuhisi wengine wanafaidi kuliko wao.
njia ya kufikia serikali MOJA(JAPO NDIO SULUHISHO MUJARAB) ni ngumu na ni ngumu haswaa, kwa yeyote anaefikiria kwa mitazamo huru bila kulegezwa na ushabiki wa kichama anatakiwa afahamu hilo kwa sababu liko wazi sana. na katika kuwakumbusha tu naweza nikawapa sababu za msingi ni kwa nini SULUHISHO SAHIHI(SERIKALI MOJA) ni gumu kulifikia....
1.watanganyika wamekuwa ni watumwa wa wazanzibar kwa miaka yote ya muungano na wamejitolea kwa kila kitu ili kuulinda na kuutetea muungano huu lakini MALIPO wanayoyapata toka kwa ndugu zao WAZANZIBAR si lingine zaidi ya kejeli na kudharauliwa. hili Linawaweka watanganyika katika DILEMMA na kutokuwa na uhakika wa urafiki na undugu huu kutoka kwa wenzetu.
2. WAZANZIBAR wanapotoshana kwa dhana ya KUMEZWA NA TANGANYIKA na kudhani wakiwa nje ya muungano watanufaika zaidi na ndio maana kila uchao wanadai vitu vitakavyowatambulisha kama TAIFA(zanzibar) na sio kama watanzania. hawajali maisha na mitaji mikubwa waliyoipata na kuwekeza tanganyika,hawajali elimu bora wanayoipata tanganyika, hawajali lishe(chakula) wanachokitegemea toka tanganyika, hawajali ulinzi na usalama n.k,n.k.
wao kwao, zanzibar comes first and the consequences can wait. kwa wao huu muungano umewapora sehemu ya mamlaka ya nchi yao ambayo wanaitaka, je watakubali kusalimisha (hiyo nchi yao) moja kwa moja kwa mamlaka ya serikali moja ya JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA?????? kwangu mimi sioni uwezekano wa kulikubali hilo....

kwa sababu hizo, ni wazi muungano huu HAUHITAJI MAREKEBISHO kama inavyohubiriwa, kwani kimsingi hakuna kero za muungano bali KUNA WATU WASIOUTAKA MUUNGANO kwa gharama yoyote. NA HII YOTE NI KWA AJILI YA MASLAHI MACHAFU YA KISIASA na dhamira chafu zilizojificha.
hekima waliyotumia akina NYERERE /KARUME kuamua kuziunganisha nchi hizi, zilikuwa ni hekima za hali ya juu kabisa na huenda hekima hizo zina mashiko/umuhimu mkubwa hivi sasa kuliko kipindi hicho wakati wanaziunganisha nchi hizi. kwanza SUALA LA USALAMA KIKANDA(REGIONAL SECURITY) ni swala la msingi kuliko kitu chochote hivi sasa haswa katika zama hizi za uadui wa kiarabu na kimagharibi.tukiangalia jinsi ambavyo TANGANYIKA imekuwa kama lulu ya wawekezaji wa KIMAGHARIBI ambao principally NI MAADUI WA ugaidi wa kiarabu, Utaona jinsi ambavyo ni muhimu sana kwa muungano huu wa sasa(serikali mbili ) kuwepo baada ya ule serikali moja kuwa hauwezekani kuweko.
labda hivi sasa tuwaangalie wanasiasa na vyama vya siasa na agenda zao juu ya hili swala la muundo wa muungano.
na hapa nitavimulika vyama vitatu vikubwa ambavyo vinaonyeshana ubavu katika hili swala.. navyo ni CCM,CUF na CHADEMA.
Tukianza na CCM, kwanza katika kulinda hadhi, legacy ya NYERERE na kwa kuangalia maslahi mapana sana ya taifa na kujua ugumu wa kuwepo kwa serikali moja na ufahamu walionao juu ya athari za serikali tatu(serikali tatu ni kuuvunja rasmi muungano), CCM imeamua kufa/kupona na mfumo huu uliopo wa serikali mbili.wana kila sababu ya kupigania hilo kwa sababu yeyote mwenye utimamu akilini mwake ataona kuwa kuipa zanzibar madaraka kamili kama nchi ni mwanzo rasmi wa mwisho wa muungano kwa sababu kama hivi sasa chini ya serikali ya muungano wanajitutumua na kujifanyia mambo kama tunavyoona,je siku madaraka yote yakiwa mikononi mwao???? kwa CCM, serikali mbili ni swala lisilohitaji mjadala na hili sio kwa CCM bara tu,, la hasha bali hata wana CCM woteambao sio wenye asili ya kishirazi/waarabu walioko zanzibar wanaunga mkono serikali mbili kama ilivyo kwani ndio mfumo pekee utakaowahakikishia haki ya kuishi na kutobaguliwa ndani ya zanzibar.
Tukirudi kwa CUF... kwanza tujikumbushe tu kwamba, CUF chimbuko lake na asili yake(baada ya kuwa chini ya SEIF SHARIFF HAMAD) ni HIZBU.. hiki ni kile chama cha waarabu na washirazi pamoja na waafrika wenye asili ya ushombeshombe waliokuwa wanapenda kujinasibisha na waarabu na kudharau UAFRIKA... hiki chama kilikuwa kinaitwa ZNP(ZANZIBAR NATIONALIST PART).. hawa watu wanaishi kwa visasi na visasi vyao vinadumu kwa maisha yote hadi pale wanapokufa na huwa visasi vyao vinarithishwa kwa watoto na vizazi na ndio maana kwa wanaofahamu ukweli, hawa watu hawatakiwi kupewa nafasi ya kutawala.
kwa wale wasiofahamu, ni kwamba MAPINDUZI YA ZANZIBAR 1964 hayakuwa ya kutafuta uhuru wa nchi laa hasha bali yalikuwa mapinduzi ya kuindoa serikali HALALI KABISA iliyowekwa madarakani kwa kura zilizopigwa kidemokrasia na chama cha ZNP kushinda kwa wingi wa kura. chama hiki kilikataa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na ASP na hivyo kuwatenga kabisa waafrika weusi na uongozi wa kisiwa cha zanzibar.na ikumbukwe kuwa SULATANI alikuwa anakiunga mkono chama tawala-ZNP na hivyo akina KARUME na waafrika wengine kuona kama uhuru ule ulikuwa ni dhikaka kwao na kuamua kupanga mapinduzi.
mapinduzi yale yalikuwa yana kila sababu ya kutokea na kwa kweli yalikuwa halali ili kuirudisha zanzibar mikononi mwa wenyewe(WAAFRIKA).wote tunajua jinsi mapinduzi yalivyoendeshwa, na tuliona humu JF ile video ya mauaji ya kutisha kabisa yalivyofanyika katika siku 3 za mapinduzi. waliouwawa ni walewale wenye urangirangi/uarabu. kwa ujumla, WAHANGA WA MAPINDUZI WALIKUWA NI SULTANI,ZNP(HIZBU) na vibaraka wao. na hao ndio haswaa CUF wa leo.
hawa baada ya dhoruba kubwa la mapinduzi kuwapitia, waliamua kuanzisha mkakati wa kuzaliana kwa fujo ili waweze kuwa-outnumber waafrika weusi, na kwa hilo wameshafanikiwa.. wnachokisubiria ni muda kuafaka wa kulipiza kisasi na kuwaangamiza kabisa waafrika weusi toka visiwani. na ndio maana hadi hivi sasa hawajawahi kukataundugu wao na sultan wa oman. nafasi hiyo wanayoisubiri inakwazwa na uwepo wa CCM na huu muungano wanaoulalamikia sana.
pasipo na muungano wa serikali mbili(kwa sababu moja haiwezekani) ni wazi dhamira yao itatimia. wanalilia serikali tatu ili zanzibar iwe na madaraka kamili na hili likifanikiwa, kifo cha CCM zanzibar kitatimia na malengo ya HIZBU yataanza kuonekana na tutakuwa tumeshachelewa sana. zanzibar ndio ngome kuu ya CUF na waarabu,washirazi,wapemba na wangazija ndio wafuasi wakubwa wa CUF. mbaya zaidi ni kwamba hata wale wana CCM walio na asili ya kiarabu wameungana na wenzao wa CUF kuidai zanzibar wote wakiwa na dhamira moja tuu.... kumrudisha sultani na kuangamiza waafrika weusi. kwa CUF swala la serikali tatu ni turufu ya kufikia malengo yao ambayo hawayaweki wazi.
Tukimalizia na CHADEMA....
mpaka sasa nimesikiliza hotuba za viongozi wao kwenye kampeni zao za elimu ya uraia juu ya rasimu ya katiba, nimeshindwa kuwaelewa wana mantiki gani juu ya kuunga mkono mfumo wa serikali tatu. sijui ni kwa sababu tu ya dhana ya upinzani hivyo wameamua KUPINGA kila kinachoungwa mkono na CCM ama ni ukosefu wa weledi juu ya haya mambo ya muungano au nao ni walewale(kama CUF) watakaofaidika na kuvunjika kwa muungano!!!!!!
tukiliangalia hili kwa mtazamo wa kisiasa zaidi, tunaona kuwa ni wazi ZANZIBAR ni kikwazo kwa siasa za CHADEMA..zanzibar na maeneo yote ya pwani ya tanzania yameikataa CHADEMA, maeneo ya pwani ya tanzani sio tatizo kwa sababu yako ndani ya tanzania bara lakini zanzibar ni moja kati ya maeneo mawili yanayounda JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. hivyo kukataliwa upande mmoja wa muungano ni doa kubwa kabisa kwa chama chenye malengo/tamaa ya siku moja huko miongo mingi ijayo kuja kutawala na kuongoza nchi.
hawataki muungano huu wa serikali mbili uwepo kwani utazidi kuonyesha mapungufu yake(CDM) na hivyo serikali tatu zitaharakisha kukamilika kwa dhamira ya chama(kuuvunja muungano) kwa kuipa zanzibar mamlaka kamili na hatimaye wajitangaze kujitenga na kuuvunja muungano.
kwa ujumla na hii iko wazi, zanzibar ni mfupa mbaya kwenye koo la CDM na chadema wanaomba na kufanya kila linalowezekana hili fupa(zanzibar) liondoke kooni(muungano uvunjike) ili wapate nafuu. tumekuwa tukiona kejeli za akina T.LISSU, G.LEMA NA P.MSIGWA dhidi ya wabunge wa zanzibar.. hii yote ni katika kuwa-provoke ili wajione wao sio wenzetu na wachukue hatua!!!!!!
la mwisho kwako MWANAKIJIJI!!!!!
hushangai kwa nini kwenye rasimu ya katiba ni swala la '''''muundo wa muungano'' peke yake ndio linatushughulisha???
je ni kweli kwamba rasimu hii iko 100% perfect kiasi ambacho hatuhitaji kuyajua na kujadili mambo mengine ya msingi sana na kupoteza muda wetu kwa hili la MUUNGANO???
Je hizi ni mbinu nyingine za wanasiasa za kutaka kututoa kwenye BARABARA SAHIHI ya kupata katiba nzuri ambayo itayaweka hatarini maslahi yao???
DOWN HERE IN TROPICS, EVERYTHING IS DONE POLITICALLY
WE FALL IN LOVE POLITICALLY
WE THINK POLITICALLY
WE PREACH POLITICS
WE PRACTICE POLITICS
and our master planners arepoliticians and they are planning everything politically
 
Aprili 30, 1992 aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais John Samwel Malecela alitoa hotuba ndefu Bungeni ambapo alipinga hoja ya serikali tatu. Kwanza alipinga kwa sababu tume ya Nyalali ilipata asilimia 49 tu ya watu 36299 waliotoa maoni walitaka serikali tatu. Kwamba watu karibu 17,000 ndio walitaka serikali tatu na kwa hilo tu tume ikapendekeza serikali tatu. Hata sasa suala la serikali tatu hatujaambiwa ni watu wangapi wanataka hilo kwenye tume ya Warioba hadi Tume iliingize kwenye rasimu ya Katiba. Na idadi hiyo inaendana vipi na wale wengine waliotaka mifumo mingine ya serikali.

Malecela alisema kwa uthabiti hivi:

Nyerere akielezea hili kwenye kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (UWHT) anasema hivi:



Nyerere aliona - na mimi nakubaliana naye - suala la kudai Tanganyika wakati ule kama ilivyo leo ni suala la tamaa ya uongozi na matokeo yatakuwa ni yale yale.

Nyerere aliona kuwa watu wa Tanzania wanachotaka ni kuwadhibiti viongozi wao. Yeye aliona kwa usahihi kabisa kuwa kuleta Tanganyika haitatatua tatizo la viongozi wahalifu kwani sasa utakuwa na viongozi wabovu kwenye Muungano na wengine kwenye Tanganyika na Zanzibar. Alisema suala basi ni kuweka utaratibu wa kuwawajibisha viongozi sawasawa.

Nyerere akaelezea vizuri kwanini wakati wa Muungano hatukwenda kwenye serikali moja au kwenda serikali tatu. Alisema hivi:



Ni vizuri kuangalia hizo namba leo hii; Zanzibar ina watu kama milioni 1.3 na Bara kuna zaidi ya watu milioni 45. Hivyo serikali tatu kwa mantiki ya Nyerere bado Tanganyika itabeba mzigo mkubwa zaidi - kuwa na serikail ya kuhudumia watu milioni 45 na pia kuchangia mchango mkubwa kwa serikali ya watu milioni 46.3.

Nyerere alikutana na viongozi wa chama na wabunge wa CCM na kuwashawishi kuipinga hoja ya serikali tatu na serikali nayo. Lakini alipoondoka kwenye Asia akiwa kwenye ziara ya Nchi za Kusini (alikuwa Mwenyekiti) huku nyuma serikali na viongozi wakashindwa kupinga kwa hoja maridhawa kabisa serikali tatu (kama tunavyoona sasa). Nyerere aliandika kwa ukali na uwazi hili tena kwa mshangao. Alisema:



Nyerere alifikia hitimisho ambalo hata leo tunaliona. Watu wanataka serikali ya Tanganyika kwa sababu wamechoka na Wazanzibari. Nyerere anasema hivi:



Muundo wa Muungano unabadilika na si lazima uwe serikali tatu
Mimi siamini katika serikali tatu kwa kiasi kikubwa kwa sababu zile zile za Nyerere. Lakini pia ninaamini kuwa wananchi ndio wana haki ya kuamua mfumo wa Muungano na hata uwepo wa Muungano wenyewe. Sasa hivi watu wanajadili serikali tatu kwa sababu wamekatazwa kujadili kuuvunja Muungano! Watu wamekubali kuwa ni lazima tuungane hivyo tutafute namna ya MUungano. Mimi naamini wananchi ndio wanapaswa kuamua kwanza kama Muungano uwepo na wakishaamua hivyo uwe wa namna gani.

Nyerere anasema hivi:


Na Hapa chini ndio msimamo wangu vile vile: Kwanini tunalazimishwa kujadili serikali tatu. Kwanini tumesalimu amri na kufikiria serikali tatu? Kwanini CCM wameamua tujadili serikali tatu na sisi tunajadili serikali tatu. Hivi kweli watu wanafikiria hili wazo la serikali tatu limetokana na wananchi kwenye maoni ya tume ya Warioba au ni carryover ya mjadala wa 1992?

Nyerere anasema:


Na maneno haya ya Nyerere yasikike kwenye masikio yaliyoziba ya watawala wetu walioshindwa!



Serikali tatu haitotatua matatizo ya Muungano itayaongeza tu. Tunaopinga serikali tatu hatupingi kwa sababu ya gharama tu - hili ni jambo dogo zaidi lakini tunapinga kwa sababu ya mantiki nzima ya kuwa na serikali tatu na nchi mbili! lakini wenzetu wanataka tuwe na nchi mbili na serikali tatu!

Mmoja mifumo mbalimbali au utengano! Kwani nani kasema ni lazima tuungane? Hatutakuwa nchi ya kwanza duniani kuvunjika na watu kuendelea kuishi pamoja na ujirani mwema.

Nyerere alitaka vyama vingi!
 
Mkeo ukimlazimisha tendo basi tayari utakuwa UMEBAKA, je MKJJ wataka tufike huko? serikali mbili ilikuwa kuelekea serikali moja ambayo ingepunguza matatizo ya Muungano lakini wenzetu tayari wameonyesha hawataki huko..
 
Sisi Watanzania tuna chekesha. Tuna penda kuruka hatua kitu ambacho kina tuletea matatizo mbeleni. Ukisikia wanandoa wana gombana swala la kwamza si kuwauliza mtaokoaje ndoa yenu bali kuwauliza kwanza kama bado wanaitaka ndoa au la kwa sababu kama hawaitaki ndoa basi ni dhahiri hakuna suluhisho litakalo fikiwa.

Serikali ilisha bama maoni ya wananchi kwa kudai muungano hauto jadiliwa kwenye swala la katiba mpya yani swala la kuvunja muungano usiwepo. Kilicho takiwa kufanyika ni kuitisha referendum (kura) kuwa uliza kwanza je bado mnautaka muungano au la. Kama jibu lingerudi muungano bado unatakwa na asilimia kubwa ya pande zote ndipo lingekuja swala la serikali. Tunge ulizwa sasa je mnataka serikali ya aina gani? Kisha wananchi tuamue. Acha wananchi waishi na maamuzi ya yawe mabaya au mazuri ili mbeleni watu waki sononeka serikali muwezi kusema mliyataka wenyewe.

Ukweli ni kwamba CCM tokea mwanzo ilitaka mfumo uliopo wa serikali mbili uendelee ndio maana walizuia mjadala wa uwepo wa muungano kisha tukaona walivyo fura kama mbogo tume ilipo shauri serikali tatu.

Kwa kifupi mimi simuelewi mtu yoyote anaelalamikia tume ya katiba kushauri uwepo wa serikali tatu. Swala lipo kwenye rasimi na rasimu si sheria kwa maana hili swala lina jadilika. Sasa kwa nini watu wana fura kana kwamba hii ni sheria ambayo isha pitishwa?

Ukweli ni kwamba kauli kwamba katiba hii ni ya wananchi ni danganya toto kwa sababu tokea mwanzo viongozi walisha tuamuliwa nini kijadiliwe na nini kisijadiliwe.
 
Mwanakijiji kwanza nataka nikuulize maswali yangu ukiyajibu utakuwa umenishawishi nikubaliane na hoja yako.
1. Kwa nini mpaka sasa kuna serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakati Katiba ya Tanzania inasema Tanzania ni nchi moja
2. Kwa nini wanasema Zanzibar ni nchi katika katiba yao ya Zanzibar
3. Kwa nini wana wimbo wa taifa, wa bendera, wana Majeshi yao na Rais wao ni Amrijeshi wa majeshi hayo.
4. Kwa nini Wao Zanzibar na sisi Tanzania Bara au Tanzania na wala siyo tanganyika
5. Kwa nini chao ni chao na chetu ni chao pia, mfano madini ya muungano mafuta na gasi ya Zanzibar?
6. Kwa nini mpaka sasa hatuna mawaziri katika wizara zao ila wao wana wiziri kwenye wizara zetu mfano wizara ya Afya
7. Kwa nini waitwe Wazanzibar na sisi tusiitwe Watanganyika wakati neno Zanzibar na Tanganyika vilistaili kurokuwepo bali Tanzania
8. Kwa nini mpaka sasa tuwabebe kwa kuchangia pato wakati tukijua wao uchumi wao ni mdogo wakitegemea karafuu zao ambalo sasa kiuchumi haina kitu wakiwa wameua uchumi wa utalii kwa uendawazimu wao wa utamaduni
Nina mengi ya kukuuliza kwanza tujibu haya nane tu.
Nikiwa Mtanganyika niliyezaliwa kabla ya muungano nitafurahia kuitwa tena Mtanganyika. Miungano mingapi imekufa mbona watu wanaishi, mfano Urusi, Yugoslavia etc. Cha muhimu ni kujenga uchumi wa nguvu husio wa kifisadi na kujenga uchumi wa nguvu kwa kutumia raslimali zetu za madini, wanyama, kilimo bakadhalika. Serikali tatu haikwepeki, wameanza wao kudai serikali yao na sisi sasa tunataka Tanganyika yetu, tunawaonea huruma watu wasiotutakia mema mara watuite wakoloni mara wabara, mara makafiri. nadhani sasad ni muda mhafaka
 
Back
Top Bottom