Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,312
- 33,788
Mkuu MMM, nimesoma bandiko lako na umejenga hoja nzito.Mchambuzi; Sasa ndugu yangu Mchambuzi; serikali tatu inatokana na ukweli kuwa tunataka kurudisha nchi ya Tanganyika. Sasa sina tatizo na kurudishwa kwa Tanganyika lakini ukiirudisha Tanganyika kama nchi NI LAZIMA uwaulize wananchi waka kama Wanataka Muungano na Zanzibar! Huwezi kurudisha nchi ya Tanganyika halafu uwasukumize kwenye Muungano na nchi nyingine ... Zanzibar.
Sasa ili tuzungumzie 'serikali tatu' ni lazima tuamuze kama Zanzibar itaendelea kuwa nchi baada ya shirikisho au la; kama watakuwa tayari kufuta hiyo ibara waliyoibadilisha 2010 ili wasema kuwa wao ni "sehemu" ya Jamhuri ya Muungano. Unafikiri Wazanzibari watakubali? Au Watanganyika tukubali kusema sisi ni "sehemu" ya Jamhuri ya Muungano bila kujitaja kuwa na "sisi" ni nchi?
Niseme kuwa kurejea kwa Tanganyika si kwasababu Zanzibar ipo, la hasha!
Ni miongo takribani minne tangu Tanzania izaliwe rasmi na Tanganyika kutoweka.
Hadi hivi sasa wazanzibar wanaamini kuwa Watanganyika hawashughulishwi na suala la muungano kama wao.Kinachowasukumu kusema hivyo si kwasababu ya ukweli bali ukweli kuwa Tanganyika imeridhika kutoa ili kujenga muungano wa nchi moja yenye kanchi ndani yake kama ilivyo sasa
Matokeo ya ridhaa ya Watanganyika yanapokelewa na wazanzibar ambao basically wanaserikali yao kwa mitazamo mbali mbali.
1. Tanganyika kupitia Tanzania inawanyonya bila chembe ya ukweli na pengine ni kinyume chake
2. Matatizo ya kiuchumi na kijamii ya Zanzibar kutwishwa Mtanganyika
3. Kuitumia Tanganyika katika kupunguza gharama za shughuli zao kwa hisa za 'Tanzania''
4. Kuleta ubaguzi kwa Watanganyika wakati wakuitumia Tanzania kuzuia backfire ya ubaguzi.
5. Kujitambua kama Zanzibar na kuiacha Tanzania isipokuwa katika mafao na fursa
Kwa msingi huo Watanganyika bado wanaamini katika spirit ya muungano ambayo imevunjwa nguvu na Wazanzibar. Ili kuondokana na mambo 5 hapo juu Watanganyika wanajiuliza, katika Tanzania tuliyo nayo wapi mshirika wenzetu?
Kwamba neno Tanzania linatumika katika hisa tu bila kuwa na mafao ya aina yoyote.
Ndipo wanasema ni vema kukawa na mipaka ya mambo ili kila mmoja aangalie ustawi wake bila kumtwisha, kumlaumu au kumsimanga mwingine.Kwamba Tanganyika imetoa lakini 'dividend' ni matusi, kejeli, lawama na dharau. Kuna sababu za kuendelea na hali hiyo?
Hoja ya kurudi Tanganyika inapata nguvu kwa sababu hizo.
Ama hapo chini umeeleza vema sana ya kuwa kama tunahitaji shirikisho basi lazima washiriki wawepo. Kwa bahati mbaya Tanganyika haijarudi rasmi ili kusimamia masilahi yake.
Tumeiuliza tume ya Warioba, hiyo serikali ya muungano imepatikanaje?
Haiwezekana SMZ ikawakilishwa na Tanganyika ikawa ''ghost'' lakini ikatupiwa sheria zinazoihusu.
Leo serikali ya Tanganyika na nchi yake ikirudi itakuta sheria zilizoandikwa na akina Warioba tena wakiwemo Wazanzibar. Wazanzibar wakiandika sheria zao hakuna Mtanganyika aliyeshiriki.
Kwanini basi asirejee Mtanganyika ili naye aamue kama kuna umuhimu wa kushirikiana na znz kwa jambo lolote lile?
Hapa ndipo hoja yetu ya kurudi Tanganyika inapokuwa na nguvu sana.
Tunasikia wazanzibar wakisema wanataka abcd katika rasimu na wala si kura ya maoni. Hii maana yake ni kuwa katika mchakato wa sasa wao wana 'dictate terms za shirikisho''. Sababu za ku-dictate ni kuwa wanafanya debate against 'vacuum'.
Wzn wantaka ulinzi na usalama, sasa nani anyejua kuwa hilo ni hiytaji la Tanganyika?
Je, kama Tanganyika ikirejea ikasema haihitaji hilo hatuoni kama ni kuleta utata siku za usoni?
Hoja ya kurudi Tanganyika inabaki na nguvu zake
Kuhusu Zanzibar kukubali kuwa sehemu ya shirikisho, kwa vile hawakukubali kuwa sehemu ya Tanzania hilo ni wazi hawatakubali kuwa sehemu ya shirikisho. Si wajibu wetu kuwaambia au kuwashawishi, ni wajibu wetu kuwapa 'terms of reference' za hilo shirikisho.
1. Wakubali kuwa wao kama Tanganyika watapoteza 'utaifa' na kuupata kupitia shrikikisho.
2. Kwamba, hakuna kujadili nini kiwemo ndani ya rasimu kwanza bila kujua shirikisho ni la namna gani
3. Waamue kwa kufuata kura ya maoni kama wanapenda shirikisho au hapana.
Hata Nyerere alishawahi kusema kama hawataki hatawapiga mabomu.
Ili mambo yote yaende samba mba kura ya maoni iziangatie mambo haya
1. Kuwauliza Watanganyika kama kuna umuhimu wa muungano na baada ya Tanganyika kurudi
2. Kuwauliza wazanzibar kama wapo tayari kuwa sehemu ya muungano na kupoteza huo unaoitwa 'utaifa''
Matokeo ya hapana kwa yoyote maana yake ni kuwa tuvunje jahazi kila mtu kivyake.
Kwa msingi huo kurudi kwa Tanganyika ni kutoa nafasi ya kujitathmini kama kuna umuhimu wa muungano baada ya kupanga taratibu zake. Ni kutoa fursa kwa zanzibar kujitathmini utayari wa muungano
Tusiogope kurudi kwa Tanganyika kwa hofu ya kuvunjika muungano. Tanganyika haiwezi kubeba muungano yenyewe. Kama uwepo wake utamaanisha kifo cha muungano hilo ni jema zaidi kuliko kuishi kwa matumaini ya seikali moja taifa moja ambayo ni ndoto, serikali mbili ambazo zimeshindwa.
In other words, plan A na B zimeshindikana, ipo moja tu ambayo ni C (serikali 3). Plan C itawezekana baada ya Tanganyika kurudi. Hiyo ikishindikana tunayo plan D ambayo italeta suluhu na amani ya kudumu, vunja muungano kila mtu kivyake.