Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,811
- 6,506
Hizi sintofahamu zote zinakuja kwa sababu tulichagua njia isiyo sahihi katika safari yetu ya kuutafuta utaifa na mshikamano ambazo ndiyo nguzo za Muungano.
Kwa sasa tuko katikati ya safari tunashindwa kuamua kama tuendelee na safari au turudi mwanzo.
Ni vigumu sana kurekebisha jambo la kisiasa ambalo mwanzo wake ulifanyika kimakosa. Hiki ndiyo tunachokiona kwa sasa.
Kama Tume ya Jaji Warioba isingekuwa imefungwa na hadidu za rejea kuhusiana na Muungano, basi ninatumaini tungekuwa kwa sasa tunafahamu nini wananchi wanataka kuhusu hili 'dudu' muungano kwa ustawi wa 'mataifa' yao. Kitu cha kushangaza kwa sasa tunasema tunataka serikali tatu wakati hata hiyo serikali ya pili haijulikani muundo wake na hata wananchi wake sijui wanaishi wapi.
Kura ya maoni ndiyo mzizi wa fitina na kuwepo kwanza kwa nchi ya pili ndiyo mwanzo wa usawa katika kutafuta political legitimacy kwenye negotiation table.
Serikali tatu kwenye political environment hii iliyopo ni hukumu ya kuvunja muungano lakini katika gharama kubwa ambayo ingekuwa offset na kura ya maoni.
Kwa sasa tuko katikati ya safari tunashindwa kuamua kama tuendelee na safari au turudi mwanzo.
Ni vigumu sana kurekebisha jambo la kisiasa ambalo mwanzo wake ulifanyika kimakosa. Hiki ndiyo tunachokiona kwa sasa.
Kama Tume ya Jaji Warioba isingekuwa imefungwa na hadidu za rejea kuhusiana na Muungano, basi ninatumaini tungekuwa kwa sasa tunafahamu nini wananchi wanataka kuhusu hili 'dudu' muungano kwa ustawi wa 'mataifa' yao. Kitu cha kushangaza kwa sasa tunasema tunataka serikali tatu wakati hata hiyo serikali ya pili haijulikani muundo wake na hata wananchi wake sijui wanaishi wapi.
Kura ya maoni ndiyo mzizi wa fitina na kuwepo kwanza kwa nchi ya pili ndiyo mwanzo wa usawa katika kutafuta political legitimacy kwenye negotiation table.
Serikali tatu kwenye political environment hii iliyopo ni hukumu ya kuvunja muungano lakini katika gharama kubwa ambayo ingekuwa offset na kura ya maoni.