Kwanini ninagombea Ubunge wa EAC - My Case!


MkamaP,

..sasa kwanini hatujaribu hata project kati ya ulizotaja??

..project ya bandari na reli ya kenya inakuwa financed na China.

..lakini sisi ndiyo marafiki wa China wa muda mrefu, nini kimeshindikana??

..mimi nadhani huu uongozi tulionao ni incompetent.
 

Mkuu,
Siamini kama kweli viongozi ni incompetent lakini yawezekana wanafanya hayo kwa sababu wanaambiwa na mataifa ya magharibi nini cha kufanya na nini cha kutofanya, ili ufanye project kama hizo unatakiwa usipige kelele kwenye vyombo vya habari na wala usiende kukopa kwa ajili ya project hizo.

Ukipiga kelele wataku GBAGBO ama ku-GADAFFI, fanya taratibu kwa ukimya wakija kungutuka umeshamaliza kazi-inakuwa imekula kwao tayari.

Mfano, lakini unaweza usiwe mfano wenye tija nao ni hivi, hakuna haja ya kuwatoza kodi ama kuwauzia hawa wachimba madini yetu ingekuwa nzuri kama wangefanya butter trade nayo ni hivi:

-Wewe chukua mgodi wa buzwangi nijengee chanzo cha uhakika cha umeme life span miaka 60
-Wewe chukua mgodi wa mwadui nijengee bandari ya Mtwara na Tanga life span miaka 60
-Wewe chukua mgodi wa Nzega resolute nijengee Reli za umeme kuunganisha miji hiyo life span miaka 60
-Wewe chukua mgondi wa chamongo lakini unizalishie chakula tani kadhaa kwa mwaka kwa mda wa miaka 60.
-nk
Kwa hiyo kama hawana utalaam wakujenga ktk maeneo husika, ni wao watarudi kwao wakodi makampuni ya ujenzi na waje wajenge, wewe wakukabidhi tu kitu tayari, nafikiri hiyo itapunguza rushwa na tutakuwa tunaona sababu ya madini kuchimbwa.
 
wakuu page ya 14.....sijaelewa william alikusudia nini kuandika hii thread???
 
sishangai maana hata na wewe uliwahi kuja na vihoja vyako mfu ukala kona......

....Kwanini ninagombea Ubunge wa EAC - My Case!


waiting.......
 
Wana JF tujaribu kuwa wakweli hata kwa mara moja tuachane na unafiki ambao unatutafuna kama taifa na kujikuta hapa tulipo. Hii hoja imeletwa na William Malecela mwenyewe tena kwa mbwembwe tosha eti, kwa nini ninagombea Ubunge wa EAC - My case! Nilitegemea kweli angekuja na hoja ya kitu gani kinampa msukumo huo na sisi kama taifa tutafaidika vipi na kuwepo kwake huko. Lakini ukiyatafakari yote aliyoyatamka unapata picha halisi kuwa kigezo pekee anachokitegemea katika kuukwaa ni jina Malecela, period. Elimu (ya kuungaunga), sifa, uwezo, uzoefu (wa kiujanjaujanja) na lugha (ya kuokotezaokoteza)... zote haziko upande wake na ukimvua ubini anabaki mtupu kabisaa asiye na sifa ya kugombea hata udiwani, huo ndio ukweli ingawa mchungu kwake na kwa mashabiki wake. Hii ni JF and I rest my case.
 
Umesoma mambo mengi so what is ur profession.

 
Mkuu kusema kweli nami niltegemea hoja mujarabu toka kwa mkuu kutuonyesha anaenda kutufanyia nini sisi Watanzania kwenye hilo Bunge. Nilitegemea aje na vipaumbele japo vitatu vya haja ambavyo ingekuwa ndio agenda yake kila akiingia kwenye ukumbi wa Bunge hilo.

Sasa hivi wenzetu Kenya wanajiimarisha kiuchumi kwa kujinyakulia makoloni; tayari wanalo Sudan Kusini na wanakaribia kujitwalia Somalia. huko mote wanawekeza na makampuni yao yanapata kandarasi (exclusively siyo EAC) wakija kwenye Jumuiya bado wana nguvu nyingi tu. Tunashuhudia kampuni za Kenya zikipata kandarasi hapa kwetu ila hakuna kampuni za Tanzania.huko Kenya ama kwingineko ndani ya Jumuiya; na kama zipo basi ni chache mno. Achilia mbali ardhi ambapo sasa jamaa.wanakuja kwa mtaji.wa kuoa dada zetu na kujimilikisha ardhi na kisha kuwatema.
Jamaa yetu anayajua hayo? Atatusaidia kujinasua?
 

.......on the other side........ni bora amesema/ameandika........na atleast tumemfahamu kwa machache aliyojieleza hapa JF na kwenye ile interview..........kuna maswali mengi sana zaidi ya majibu kuhusu maelezo yake.........
 

Mkuu naona ni kweli viongozi wetu ni incompetent, angalia tangu Kenya ipate uhuru imejenga viwanja vingapi vya ndege, hospitali, shule, barabara ngapi etc linganisha na Tanzania, utaona kuwa Tanzania hakuna kinachofanyika, ni kukarabati barabara alizijenga mjerumani na Mwingereza.
Viongozi wetu hawajaweza kusema ni nini ni priority ya Tanzania na kufanyakazi kuifikia, ni kula tu kusafiri na kupiga politiki majukwaani. Unless tunaanza kuwa makini na kuhakikisha kuwa tunarekebisha dosari zetu, tutaendelea kwenda chini. Tukitaka kuwa na mabadiliko ni lazima tujifunze kufikiri kama nchi, na sio kama mtu mmoja mmoja mwenye uchu na madaraka na maslahi binafsi.
 
Mkuu kwanini mahojiano yako, uliyoyaweka kwenye blog ya michuzi, hukuyaleta na huku JF ili watu wasikilize?. Naamini kule ndio ulieleza kwa nini umeamua kugombea
 
mimi siasa siijui,lakini watanzania wenzangu huyu mtu HANA SIFA YOYOTE YA UONGOZI,hapa tu ameshatuonyesha jinsi alivyo mtumwa wa lugha,sasa kama lugha tu inamtawala,je hao wakubwa ataweza kuwadhibiti?huyu hana hata moja la maana zaidi ya tamaa ya hela,kaona wazazi wake wamevuna nayeye anataka avune,angalia sana,haya mambo yanamwisho.
 
Sasa ukitaka kujua ccm wanabebana we subiri siku hiyo ya uchaguzi uone will atavyopita kiurahisi japo hana sifa kabisa ya kuwa mbunge wa EAC.
Ushauri wa bure Will jaribu kazi nyingine siasa bado kabisaaaaa
 

Tutaendelea kujiona panzi mbele ya Wakenya na waganda mpaka lini?Tunajianda vipi kufika walipofika wenzetu?Woga utazidi kuturudisha nyuma tu.Side note,nijuavyo mimi according to my sources including Encarta,Uganda ndio inamiliki eneo kubwa la ziwa viktoria.
 
- Well, back to the campaign after a brief suspension yesterday in order to attend the Steve Kanumba's wake, in Sinza Vatican. Today we are back with the campaign, here in Dar.

- Otherwise, this has been an experience I mean trying to communicate with people, trying to inform people of what we are doing, but the reality requires that we put more focus on the campaign and since this is our home we can always come back at anytime when we have time in our hand, so people thank you much you all have been heard, but now it is time to move on but I promise that we will be back whenever we have time.

Respect!


William.
 
Kwani kuwakilisha ccm popote unahitaji any proffession? Kwani Prof Maji Marefu aka Majini ana proffession gani? Muacheni kaka wa watu abadili kazi, ubaharia unachosha!
Umesoma mambo mengi so what is ur profession.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…