Elections 2010 Kwanini ni vigumu kuiba kura katika Uchaguzi Wetu - Tusitafute visingizio


wizi unatokea pale mtu mwenye authority kama aliyokuwa nayo mwalimu nyerere mwaka 1995 kumshurutisha mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya zanzibara kutangaza kitu tofauti na hali halisi; kama ambavyo dtv walikuwa wajumlisha matokeo kutoka vito vyote na cuf kuibuka kidedea.

Hata mwaka huu dalili zinajionyesha kuwa wenye authority watatumia mamlaka waliyo nayo kuishurutisha tume ya uchaguzi kutangaza matokeo according to their wishes.
je huu sio wizi wa kura? Kama sio puatie msamiaati wake mpya.
 
Uwizi upo kwenye kuwarubuni mawakili! kuna jamaa aliniambia ilivyotekea jimbo la Arusha mjini nilitamani nimpige ila basi ndo ilitokea, Anasema kuwa yeye alikuwa ni WAKALA wa chadema, Walipewa laki 3 kwa ajili ya kubadilisha matokeo ya ubunge, na anasema walipokea na matokeo yakabadilishwa. NDO MAANA CHADEMA INATAKIWA WATAFUTE MAWAKALA WAAMINIFU SANA! wasiweke Bora liende!
 
habari ndo hiyo:
 
Mzee Mwanakijiji umetoa mchango wako tunashkuru sana
Ila hapa usitarajie (baadhi) ya watu kukuelewa, kwasababu akili zao kwa kipindi hiki ziko likizo, kinachofanya kazi ni UPENZI na sio UBONGO

Natamani ningezisogeza hizo siku iwe kesho tutoke kwenye hii situation
 
I know the perception.. wanaibaje kura? Mawakala hawahesabu kura!

kaka yale matokeo huwa yanageuzwa wakati wa kutangaza yaani wana swap zile namba tu basi. na wale mawakala wanakuwa wameshapewa chochote. Umaskini ndilo jambo ambalo linatutesa.
 
Kama hakuna wizi wa kura mbona hata wao tume ya uchaguzi wa wanalijua na kuwatahadharisha wapiga kura wasiuze shahada zao za kupigia kura! Hao wanaopita mitaani na kunakili shahada za wapiga kura wanafanya hivyo kwa manufaa gani? Kwa hili sitaki kuamini!
 


aah wapi! hata picha moja hamna na wote mnajua matokeo yasiyohojiwa ni yale ya Rais tu, ya wabunge wote na madiwani yanautaratibu maalum. Inanitisha sana kuona watu wanaamini kweli kuwa ni rahisi sana kuiba kura kiasi kwamba sitoshangaa watu wengine wamekata tamaa hata ya kupiga kura kwa sababu wameshajiambia kuwa kura zitaibwa au kutakuwa na uwezekano wa kuiba ili wawatangaze CCM kuwa ni washindi. Hiki ni kisingizio cha kutotaka kushinda.

Tuwahamasishe watu waende kupiga kura kwa wingi kuchagua mgombea tunayemtaka na mabadiliko tunayoyataka. Kama watu wengi wataenda kupiga kura uwezekano wa jambo lolote la kijinga kutokea utakuwa ni mdogo sana. Lakini watu wakiamini kuwa kura zao zitaibwa no matter what.. why vote?
 
kaka yale matokeo huwa yanageuzwa wakati wa kutangaza yaani wana swap zile namba tu basi. na wale mawakala wanakuwa wameshapewa chochote. Umaskini ndilo jambo ambalo linatutesa.

jamani, matokeo ya kura yakibadilishwa mtu anaweza kwenda kufungua kesi kwani masanduku yale hayatupwi. Kwamba kuna uwezekano wa kuwa na ukiukwaji wa taratibu hilo lawezekana lakini massive rigging sasa hivi nimesema ni "ngumu mno"... Tusiwatishe watu kuwa kura zao zitaibwa. Kura wakapige kwa wingi kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuzuia uwezekano wa wahalifu kuchakachua upigaji kura.
 

Kama matokeo yalibadilishwa kwanini Chadema hawakwenda mahakamani ili matokeo yaangaliwe upya? Tena mwaka huu na sheria imebadilishwa ili kuharakisha kesi za uchaguzi. Kuiba kura siyo rahisi hivyo kama kumchomolea mtu stendi!
 


Kama "wenye authority" watafanya hivyo mnachosema watafanya kwanini watu waende kupiga kura? Kama mawakala wanaweza kuhongwa kirahisi hivyo na kubadilisha matokeo wakati ni kosa la jinai kwanini watu waende kupiga kura. Maana kila ninapowasoma ninaona kuwa ni hopeless case kwenda kupiga kura:

a. NEC watamtangaza wanayemtaka
b. Kura zitaongezwa kwa wagombea wa CCM vituoni
c. Mawakal wa vyama watakatiwa kitu kidogo ili wachakachue kura
d. Kura hazitolindwa vizuri.


Kama yote a - d yana ukweli (hasa ukisoma sentiments za watu hapa), ni wazi kuwa mpiga kura wa Tanzania hana sababu ya kwenda kupiga kura. Hiki ni kisingizio cha kuwapatia ushindi CCM kirahisi, na miye nina hofu wanaokieneza wana lengo hilo kabisa.. KUWAKATISHA TAMAA WAPIGA KURA WA UPINZANI WASIPIGE KURA KWANI KURA ZAO ZITAIBWA! CCM wanajua hili. Ni lazima tukatake.. KURA HAZIIBWI NA KILA MTU AKAPIGE KURA YAKE!!!! LETS CHANGE THE MESSAGE!
 

Nimeshalijibu hilo soma article hapo juu
......Endapo hesabu ya idadi ya kura za mgombea zinakosewa kwa malaki halafu taarifa inatoka nani wa kutujulisha kuwa kuna kasoro?nani wa kufuatilia irekebishwe?

Utaratibu upo.. soma article.. au sheria... wale wasimamizi hawajifanyii mambo kutoka katika mawazo yao.

......Watu wote tunafika vituoni kupiga kura pamoja na wasimamizi wanaotoka katika vyama vyote,je kuna nafasi ya kukagua masanduku yote ambayo yatatumika kupigia kura ili kujihakiki wenyewe .

soma article nimejibu hilo mweh!

......Kama kuna masanduku ambayo yanatoka sehemu nyingine na tukaambiwa yametoka vituo vingine vya kupigia kura nani atakaye hakikisha kuwa ni kura halali?

Hakuna masanduku yanayohama kituo cha kura au kuingia kituo cha kura, na kama kuna haja ya nyongeza kuna utaratibu ulio wazi kabisa wa kusimamia hilo. Soma article.

Hii yote ni shuku, kama hujui ni kuwa kura zikianza kuhesabiwa hatoki au kuingia mtu kituoni hadi matokeo yatangazwe!

Basi hakuna haja ya kupiga kura!

....Kwa mtazamo wako nina uhakika kwa kipindi hiki watanzania wameungana na watajaribu kwa njia zote hizi kuainisha njia za panya hili serekali iundwe kwa uhalali.
Thanks Mwanakijiji.

ur welcome
 
Kuna habari zinazunguka hapa mjini Arusha kwamba kuna gari limekamatwa sehemu za Kisongo zenye kura bandia na Wananchi wamelivamia kwa mawe.

Mwenye taarifa zaidi atupe habari!
 
Kuna habari zinazunguka hapa mjini Arusha kwamba kuna gari limekamatwa sehemu za Kisongo zenye kura bandia na Wananchi wamelivamia kwa mawe.

Mwenye taarifa zaidi atupe habari!

Your signature is a symbol of hatred.
 
MMM,

Nakubaliana na wewe kwamba kwenye kelele zote za kuibwa kura sijawahi kusikia unatia timu huko! Binafsi sijawahi kufikiri kura zinaibwa kumbe siko mwenyewe.
Lakini nakubaliana nawe kwamba uchaguzi ukivurugwa yes. ndio maana siungani na watu wanazungumzia sana vyombo vya ulinzi maana ukivizungumzia sana... ndio vitakuwa deployed and that will be even worse.
 
Mwanakijiji tupo pamoja. hili la kuiba kura ni kutafuta visingizio tu, lakini cha msingi hapa wagombea watafute mbinu mbalimbali za kuomba kura na pia kuwashawishi watu wafike vituoni na kupiga kura period. mtu akipata kura nyingi haziwezi kuibwa/kubadilishwa
Tatizo tulilonalo sasahivi ni ku judge matokeo kwa kuangalia watu wanaohudhuria mikutano sasa hivi lakini lazima tujue kuwa katika hao wapo wasiojiandikisha, wapo ambao hawatapiga kura, wapo na mashabiki wa vyama vingine (hawabadiliki), nk nk.
 

MMJ, Hapo kwenye red ni ukweli kabisa watu baadhi naskia wakisema hawatapiga kura kwa ajili hiyo au wengine wanatamani kupigia upinzani lkn wanahofia kupoteza kura kwa kile wanachokiamini CCM kuiba kura! imani inaathiri maamuzi ya walio wengi!
 
MMM,

Naomba u-evaluate response za watu kwenye hii post yako... ndio utajua kwamba Tanzania elimu ya uraia (au elimu ya kupiga kura iko chini sana)... Cha kusikitisha sana tena sana... Mgombea Urais mmoja kuji-involve kwenye upuuzi kama huu....

We have a long way to go kaka:mmph:
 
Mkuu Mwanakijiji, kwa utaratibu uliouleza katika makala yako, kinadharia nakubaliana na wewe kwamba hakutakuwa na wizi wa kura.

Hata hivyo, uzoefu unaonyesha kwamba wizi haufanyiki kabisa maeneo ambayo yana upinzani wa kutosha, bali hufanyika kule ambako hakuna upinzania kabisa kwa kuhakikisha chama tawala wanapata 100% ya kura kutoka maeneo hayo. Maeneo yenye upinzani haki itatendeka na mtagawana hizo kura lakini kule ambapo upinzani ni dhaifu sana, wenzenu wana-maximize kura za huko na majumuisho yanakuja chama tawala wakiwa mbele.

Hebu fikiria; nini kitatokea katika yale majimbo 21 na kata karibia 500 ambayo wagombea wa chama tawala wamepita bila kupingwa? hii in maana kura zote a uraisi zitaishia kwao vilevile. Nakumbuka mwaka 2005; tena hii ilikuwa Dar es Salaam, baadhi ya vituo mawakala wa vyama vya upinzani hawakupewa kitu zaidi ya 'lunch box' na mawakala wa chama tawala na wakaishia kusaini fomu za matokeo bila hata kuhakiki hizo kura.

Matokeo ya mwaka huu yawazindue viongozi wote wa mageuzi ili walipe umuhimu suala la kujenga matandao wa matawi mikoanai na vijijini. Sidhani kama tungekuwa na wasiwasi huu kama upinzani ungekuwa na wenyeviti wa vijiji na vitongoji wa kutosha.
Kama mageuzi yatashindwa, tutakuwa tunalipa dhambi ya kutomsikiliza Chacha Wangwe (RIP)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…