Elections 2010 Kwanini ni vigumu kuiba kura katika Uchaguzi Wetu - Tusitafute visingizio

naomba tuchukue muda kumwelewa mwanakijiji, anauliza mbona kila mara moshi mjini cc, wanashindwa kuiba kura? Mbona kwa zitto walishindwa? Mbona tarime walishindwa. Kilichofanyika huko mwaka 2005 na katika uchaguzi mdogo ndicho kinachotakiwa kufanyika mwaka 2010 na hoja ya kura kuibiwa itashindwa kufanya kazi. Hebu tujiulize ni nini kilfanyika katika majimbo hayo ambayo chadema ilipata ushindi?
Kilchofanyika Tarime tunakijua; watu wa kule ni jasiri sana kiasi kwamba hawaogopi hayo maji ya upupu na hata wakiamua risasi hawaiogopi pia. Tunajua watu walivyoumizana na walivyokuwa tayari kuumia ili mradi wapate haki yao - damu ilimwagika kule!. Wadanganyika wengi hatuko hivyo ndiyo maana mtu akisema tulinde kura zetu hata kama ikibidi 'kumwaga damu', anaonekana mtu wa ajabu. Kweli hatutaki damu imwagike, kwa hiyo hatutaki kilichotokea Tarime kitokee Tanzania nzima. Kwa zitto nako watu ni ngangari sana ila sikumbuki wao walifanyaje.
Ninachojua, hasa kwa kura za ubunge, tofauti ikiwa ndogo ni rahisi kuiba lakini tofauti ikiwa kubwa sana inakuwa vigumu kuiba kwani inabidi wabadilishe masanduku mengi sana. Kwa upande wa Moshi, uelewa wa kule ni mkubwa kuliko sehemu nyingi Tanzania; wanajitokeza wengi kupiga kura na kule umaskini si mkubwa sana hivyo hawanunuliki kirahisi. Kwa mfano huwezi kununua shahada kule kwa shs 1000 kama inavyofanyika karagwe!
Sehemu nyingine CCM wanakuwa hawajui kama watashindwa na hivyo wanaacha 'kujiandaa', matokeo yanakuja kama surprise kama ilivyotokea kwa Kaunda. Kwa mfano katika uchaguzi wa 2005 ilionekana kuwa Chadema ingepata viti zaidi ya 40, lakini haikuwezekana kwani mbinu za kuiba kura, kuwanunua wapiga kura, nk zilifanyika katika maeneo yote waliyotabiriwa kushindwa na unajua Chadema waliambulia viti vingapi! Kwa ujumla ni mkusanyiko wa mambo mengi mpaka uone CCM imekubali kushindwa. Kuna nguvu ya Dola pia - kumbuka ya Bukoba mjini, ya Biharamulo (uchaguzi mdogo) nk
 
Kwa ukweli kura huibiwa, na hii siyo dhana, ni ukweli uliotokea kwa mbinu mbali mbali. Mwaka huu kinyume na miaka yote kuna mikakati ya kuiba kura kwa kutumia wizi au unyanganyi. Kwa ambaye siyo mwizi kama MKJ anaona haiwezekani, lakini kwa waledi huona kitu cha kawaida. Na ndio maana inaitwa wizi wa kura.
Wizi ni pale ambapo mbinu imetumika kwa ridhaa ya mawakala au kwa kuzidiwa ujanja, hapa wengi wametoa mifano. Unyanganyi ni pale baada ya kuhesabu kwenye kituo au hata kabla nguvu za dola hutumika kupokonya nayo hii imetolewa mifano pia.
Matayarisho ya wizi na unyanganyi na hata wa kutangaza kwa nguvu umefanyika kwa kuwa tayarisha wananchi kiakili. Kwanza kuaminisha kura haziwezi kuibiwa eti wamechapizha karatasi mithili ya noti ya malkia. Tujiulize nani ametengeneza makaratasi na nani anayeiba? Ni mtu yuleyule kwa hivi anajua karatasi na hata namba zake ili zisihitilafiane kati ya za halali na za wizi. Matayarisho mengine ni tafiti za kuhalalisha uwizi kama ilivyofanywa na redet na siynovate. Propaganda za ushindi ni lazima na maonyo ya vyombo vya dola na matangazo kuwa lazima kukubali matokeo.
Ni muhimu sana kuelewa kuwa wizi hutumika kwa kuwarubuni mawakala au kutumia mawakala ambao ni wa sisi m
Sasa naomba ni changie kwa kutoa mifano ya ukweli kabisa.
Kubadili masanduku - hii imetumika mara nyingi sana. Vyombo vya usafiri vinavyoaminika na jamii hutumika na masanduku hubadilishwa kwa ridhaa ya mawakala wote waliopo. Au pia iwapo kuna vyumba vya ziada na makabati masanduku hufichwa humo. Natoa mifano miwili iliyotokea kwenye kura ya maoni ya CCM mwaka huu. Kwenye maeneo fulani ambapo mwizi anauhakika wa kushindwa alitumia mbinu ya kubadili masanduku mchana lakini walimshindwa wakala mmoja kwa vile hahongeki. Walitumia mbinu ya kuitwa na wakala mwenzie wa kituo cha jirani aliyehongwa, mara tu alipoondoka masanduku yalibadilishwa na yeye kabla ya kuhajafika aliombwa arudi kwani shida imeisha lakini kikubwa wizi tayari. Aliombwa mwishowe ahesabu ili aweshahidi wa ushindi wa mwizi.
Mfano wa pili kuna jamaa aliamua kulinda masanduku kwa bidii sana na hakutaka atoke, na wezi walificha masanduku ndani ya chumba kingine ( ofisi hizi huwa na ukumbi pa kupiga na kuhesabu kura na kuna ofisi ya VEO na ya WEO) na walishindwa kutoa kwa ajili ya uangalifu wa wakala huyu. Walichelewesha sana kuhesabu kwa vile mbinu za kutoa masanduku haya ilishindikana mpaka ilipofika saa 2 usiku. Mwishowe mmoja akajaribu mbinu ya mwisho kwani lijamaa hata kukojoa haendi kwa kuwahofia wenzake, basi alifungua dirisha akaenda nje akavuta sigara na lijamaa lilipopata harufu ya sigara tamaa ilimjia, ndipo akaambiwa atoke nje ili apige pafu. Alipofika nje jamaa alimwomba wavute pembeni kidogo ilikuzuia moshi usiwapate wengine. Dakika hizo zilitosha kubadili masanduku. Mbinu ni nyingi sana.
Kuongeza kura vituoni kwenye masanduku --hii hutumika sana pale ambapo wapiga kura wengine hawajaenda au wanajulikana wamehama au hawatapiga kwa sababu yoyote ile. Mbinu hupangwa ili kuziba hizo nafasi na kura hugawanywa kwa uwiano kuwa lazima wampe mbunge raisi na diwani ili kuwa na uwiano.
Hizi ni za ukweli
Muhimu, nilazima kupiga kura ili kuondoa mfano wa pili na kubakiza mbinu zingine lakini wapiga kura hujua ukweli
 
I know the perception.. wanaibaje kura? Mawakala hawahesabu kura!

Mkuu,makala yako ni nzuri sana hususan katika kuhamasisha kupiga kura.Hata hivyo,wizi wa kura sio tu ni jambo linalowezekana bali pia linafanyika.Kwani tatizo lililopelekea vurugu Kenya ni nini kama si wizi wa kura.Call it any name-uvurugaji,uharibifu,uchakachuaji,etc-lakini lengo linabaki paleplale kuwa aliyeshinda awe aliyeshindwa,and vice versa.

Kutaka uthibitisho wa namna gani,kwa mfano kura za CUF zimekuwa "hazitoshi" huko Zanziba,italazimu kumpata mzalendo mmoja kutoka TISS aueleze umma field manual ya wizi wa kura inaelezeaje.

Sikubaliana nawe kuwa haiwezekani kuiba kura bali nachoweza kuafikiana nawe ni umuhimu wa wapiga kura kujitokeza kwa wingi kumpigia kura mgombea wao,sambamba na usimamizi mzuri wa kura.Ni rahisi kuchakachua ushindi wa tofauti ya tarakimu moja lakini ugumu unaongezeka zinapokuwa tarakimu mbili in terms of asilimia (ie rahisi kuchakachua 2% lakini vigumu relatively iwapo ni asilimia 12 au zaidi).

Si kila jambo haliwezekani kwa vile tu haijawahi kuthibitishwa.Na ni vigumu kuthibitisha wizi hadi mwizi atapokamatwa.Unfortunately,wezi wa kura ni professionals wanaofanya wizi huo kizani.Kinadharia,mashushushu wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi.Practically,wanafanya shughuli zao according to their own rules of the game.

Someone somewhere must be laughing aloud at you...wakikumbuka "maumivu wanayowapa CUF come any election".
 
Mwanakijiji hujui wizi unavyofanyika; ngoja tukujuze

1)Wizi wa kuwanunua mawakala katika vituo vya kupigia kura
Hapa mara nyingi zile kura za watu ambao hawakujitokeza, zote hupigiwa chama fulani kwa makubaliano ya kifedha

Kubadilisha kura zote ndani ya sanduku na kuweka nyingine zenye tiki ya chama husika
(Hapa lazima mtu kutoka nje alete hizo kura mpya na ndiyo dhana ya kuambiwa ukishapiga kura nenda nyumbani)

Kuharibu kura za chama kimojawapo kwa kuongeza tiki ya pili
Kwa kuwa katika hatua hii ni makubaliano ya wasimamizi wa kituo na mawakala, fomu zote hujazwa baada ya wizi huo kufanyika

2)Wizi wakati wa kusafirisha masanduku kwenda jimboni

Baada ya kura kuhesabiwa na mawakala kupewa nakala ya matokeo, huo siyo mwisho. Masanduku hupelekwa kwenye kata ambapo kura za diwani hujumlishwa na kutangazwa; lakini kura za rais na mbunge hazifanyiwi kazi pale, masanduku hubaki yamefungwa tu lakini hupelekwa kwa msimamizi wa jimbo kwa majumuisho na uhakiki.

Wizi hapa hutokea njiani wakati wa kuyasafirisha kwani huwa hayana wakala wa chama chochote. Mawakala mara nyingi hawakubaliwi kuyasindikiza kwa visingizio kuwa si kazi yao au gari limeshajaa masanduku.
Humo njiani, hasa usiku kura ndani ya masanduku huondolewa na kuchomwa moto na kuwekwa kura nyingine. Msimamizi wa sanduku la kituo husika hutafutwa (kwa kweli kuwa anajua mpango mzima) na kutengenezwa fomu nyingine za matokeo, na wakala wa chama husika huitwa na kuweka saini kwenye fomu mpya ya matokeo na ile ya zamani huharibiwa. Kwa saini za mawakala wa vyama vingine, huwekwa saini za kufoji.

Wakati wa kujumlisha matokeo ukifika ni wazi kutakuwa na fomu mbili tofauti za matokeo ya kituo hicho; moja ni ile iliyojazwa kituoni (ambayo huwa ndiyo sahihi) na ile ambayo imejazwa njiani baada ya kuchakachua. Kwa vyovyote vyama vitabishana juu ya fomu ipi ni sahihi, kila chama kikivutia upande wake – suluhu ni kufumgua tena lile sanduku na kuona exactly kuna nini ndani. Na kwa kuwa kura zilishabadilishwa njiani, fomu ya chama husika itaonekana kuwa na matokeao sahihi na hata kama kutakuwa na utofauti bado, kura zitakazotambuliwa ni zile zitakokuwa kwenye sanduku – zilizochakachuliwa. (nadhani umenielewa)

3)Wizi mezani: Hapa ni mabavu ya dola tu hutumika na kutangaza kuwa Fulani kashinda,Utakuta FFU na Polisi wamejaa na magari ya maji ya upupu yamewekwa standby kabla ya matokeo kutangazwa. Ukiona dalili hizo ujue kuwa dola inajiandaa kutoa matokeo yasiyowaridhisha wananchi (Hii sijui njia ya kuidhibiti)



Njia za kudhibiti wizi huo:

Kwa kuwa kila karatasi ya kupigia kura huwa ina namba, na kwa kuwa kila msimamizi wa kituo hukabidhiwa vitabu hivyo kwa namba; yafuatayo yafanyike

1)Kila chama kipate nakala ya namba za vitabu vya kupigia kura vilivyopelekwa kila kituo
2)Mawakala waelekezwe kunukuu namba za vitabu kwenye kituo kabla upigaji kura haujaanza na msimamizi awadhibitishie kuwa hivyo ndivyo vitabu alivyopokea toka msimamzi wa jimbo
3) Iwe ni lazima kwa kila wakala kusaini fomu ya matokeo kituoni na kama ana malalamiko yoyote yale ajaze kwenye fomu ya malalamiko (unajua mkiachia wa CCM pekee akasaini, hata ikijabadilishwa anatafutwa huyo mmoja anasaini na mchezo unakuwa umeisha)
4) Wakati wa kuhesabu kura, iwe vituoni au wakati wa kuhakiki katika ngazi ya jimbo (ambako huwa ndipo matokeo huwa yameshachakachuliwa), kila sanduku la kura lihesabiwe peke yake na ihakikishwe kuwa namba za karatasi zilizozomo zinaoana na namba alizokuwa amekabidhiwa msimamizi wa kituo na mawakala wawe wametoa taarifa kwa vyama vyao juu ya namba zilizotumika kwenye vituo vyao.
5) Kwa kuwa mawakala ndio wameaminiwa na vyama vyao, wayasindikize masanduku ya kura hadi jimboni pale uhakiki na utangazaji unapofanyikia. Kuyasindikiza hadi kwenye kata na kuishia hapo hutoa mwanya kwa watendaji wa kata kushirikiana na CCM kuyabadili. Sanduku lolote litakalowasilishwa bila mawakala litengwe na lihasabiwe tofauti na kama litakuwa na kura tofauti na fomu za mawakala, likataliwe - Nakumbuka hii ilifanyika Temeke wakati Mrema akigombea. Ni marufuku mawakala kusafiri tofauti na masanduku yao - magari yabebe masanduku kidogo na mawakala.


6) Mwakala wapewe elimu ya kutosha na wajue kuwa wanamuwakilisha mgombea, wasiwe tayari kununuliwa –kuna thread nzuri humu yenye kipeperushi juu ya elimu.

NImesoma maelezo yako na ni wazi kabisa kuwa hujui kura za Tanzania zinapigwaje, kuhesabiwa vipi na namna gani. Yote uliyoyasema yanatokana na imani tu. Masanduku ya kura hayahamishwi kwenda Jimboni kuhesabiwa!
 
"MgonjwaUkimwi;"
"Mada hii ingeletwa na mtu mwingine kama MS kungejaa matusi hapa au shutuma kwamba katumwa. Kaileta Mwanakijiji JF wamesalimu amri. Double standard!! "

Usilalamike tuuu, wivu utawauweni. Hivi kweli unaamini kuwa MS anaweza kujenga hoja itakayowafanya watu waijadili?
Kinachotakiwa ni hoja yenye nguvu, hata ukiitowa wewe au MS itajadiliwa sana.
On the other hand wewe na kila mtu anajua the kind of rubbish MS anazoweka hapa. Kwa hiyo usishangae na majibu unayo!
 
Regardless of what Mwanakijiji believes, hakuna kisichowezekana kwenye siasa hapa Tanzania. Sasa hivi kuna mwelekeo wazi kabisa kuwa Wilbroad Slaa atashinda kwenye uchaguzi wa urais, lakini kushinda na kuongoza ni mawili tofauti. We have done that in Zanzibar before, it is open secret kuwa CUF walishinda mara zote lakini hawakutawala. Tumeona Kenya mpaka leo Kivuitu analia. Na uzuri ni kuwa Mwanakijiji amesema "it is hard" hajasema "it is impossible" so this means that it can be done. Results have in many cases been doctored it will not be something new. Lakini kipya kinaweza kuwa ni reaction ya watu baada ya doctoring.
 
CCM wamezoea kuiba na ufisadi, iwe kura,viwanja,fedha, wake za watu, waume za watu, haki za raia,maeneo ya wazi, uwanja wa kirumba mwanza. CCM imeweza kufanya ujambazi Central Bank kwa kusaidiwa na Gavana itashindwaje kuiba kura?tupige kura ili hata wakiiba Dr.Slaa ashinde. Tukajaribu bahati yetu,Mungu atakuwa upande wetu sisi tulio wazalendo wa ukweli.
 
Wizi upo na pia wewe ambae hutapiga kura utakuwa umekiibia chamachako purposely
 
wakati wa kura za serkali za mitaa kuna sanduku lenye kura za wizi lilikamatwa likiletwa kituoni. Wananchi walikakamaa na kukataa kuondoka kituoni baada ya kupiga kura. Matokeo yalitangazwa saa 11 alfajiri kwa shinikizo la polisi. kamanda wa polisi wa w alichosaidia ni kuwanyanganya wananchi sanduku hili (bila shaka kupoteza ushahidi) na kuliingiza ndani ya chumba cha kura ingawa alililinda na kura zake hazikuchanganywa na kura zilizopigwa kituoni.
 
Hii ndio lala salama, wengine wamekata tamaa, sasa wanatafuta kukubali matokeo hata kama ya wizi ( Mwanakijiji umejiunga na team ya Kina Gen.Shimbo nini?). Ukiona watu wanaoheshimika, wanatumia sanaa ya lugha na baseless arguments to try to convice the mass! It could be due a number of things , and the major being that their price has been determined. Tuachie tu-judge after elections kama kura zimeibwa au la? Don't try to pre-empty us MMKJ!
 
Kura huwa zinaibiwa, na zinaibiwa kwa namna nyingi, na mara nyingi kura haziibiwi vituo vya kupiga kura huwa wanabadilisha matokeo kwenye karatasi sasa ni nani anafanya hivyo anaweza kuwa ni returning officer wa jimbo au mkoa au taifa. Nilipokuwa msimamizi pale mianzini tulihesabu vizuri tukasaini matokeo kila mtu akaondoka na karatasi iliyosaidiwa na mawakala wote pamoja na msimamizi wa nec.

Matokeo yaliyokuja kutangazwa yakawa kichekesho tulihoji tukaambiwa kuwa inabidi wafungue tena mabox ambayo yalikuwa tayari yamekusanywa pale makao makuu ya wilaya ya Kinondoni. Ikashindikana mwaka ulikuwa 1995. Watu wa kubanwa ni tume wakubali matokeo halali ni yale ya kituoni na wakubali nakala za wasimamizi kuwa ni nyaraka halali za tume. Vyama vya siasa lazima wawe makini kuwa na maofisa wa kutosha watakao kusanya matokeo na kujumlisha kabla tume haijatangaza namba zao. Bila hivyo bao litakuwa la mkono.
 
Kinachofanyika sio wizi wa kura kama ulivyo wizi wa vitunguu. Hapa ni "wizi" wa kimamlaka. Kura zikihesabiwa kila kituo uweka matokeo yake hadharani, hata hivyo matokeo ya kata (kwa Madiwani),jimbo (kwa wabunge) na Taifa (kwa rais) hutolewa na ngazi husika ya tume ya uchaguzi baada ya kujumlisha matokeo yote. Kumbuka matokeo toka kona mbalimbali za nchi hutumwa kwa njia ya fax kwenda NEC headquartes. NEC ikishatangaza matokeo, yeyote anayepinga inabidi aende mahakamani. Wakati kesi iko mahakamani ndio ushahidi unafutwa kwa kubadilisha mabox ya kura.
Mwanakijiji, hata kama utasema wizi wa kura hakuna, lakini nakutegemea uwe umepevuka kiasi cha kujua kuwa "ubadhilifu" wa kutangaza washindi wasiochaguliwa na wengi unawezekana na unfortunatelly the sad reality ni kwamba unafanyika sana tu katika ngazi mbalimbali za uchaguzi.
 
Jk mwenyewe alikiri pale mwanza kwamba si kila mara watu wanaipenda ccm lakini inashinda kila uchaguzi, meaning kuna namna. Lisemwalo lipo, kama halipo laja.
 
naomba tuchukue muda kumwelewa mwanakijiji, anauliza mbona kila mara moshi mjini cc, wanashindwa kuiba kura? Mbona kwa zitto walishindwa? Mbona tarime walishindwa. Kilichofanyika huko mwaka 2005 na katika uchaguzi mdogo ndicho kinachotakiwa kufanyika mwaka 2010 na hoja ya kura kuibiwa itashindwa kufanya kazi. Hebu tujiulize ni nini kilfanyika katika majimbo hayo ambayo chadema ilipata ushindi?

waulize vizuri watu wa moshi na huko karatu. Huwa wanaweka mawakala very strong na wakuaminika, na wanawatoa kwa posho nono, ndio maana wanaachana na rushwa ya kijinga ya ccm, siri ipo hapo mzee.
 
Mimi naomba kumwuliza Mwanakijiji kitu kimoja tu, unaamini CCM wako ready kwa uchaguzi wa haki na huru ? Kwamba kama chama tawala hawatafanya juhudi zozote zile za kushinda uchaguzi hata zikiwa nje ya taratibu ? Kwamba wanaingia kwenye ychaguzi kwa moyo mweupe na wako tayari kukubali matokeo hata kama yatakuwa siyo mazuri kwao ? Je wakiamua kucheza faulo kwenye kuhesabu kura kama wanavyofanya sasa hivi katika kampeni kuna vyombo vya dola vitakavyowadhibiti ? Je unatuambia kuwa haki itatendeka na hivyo tusiwe na wasi wasi wowote na baada ya kupiga kura turudi nyumbani tupate usingizi mwororo tukisubiri matokeo ? Baada ya kushuhudia vurumai iliyofuatia kura ya maoni ndani ya CCM yenyewe, bado unatuambia tuamini kuwa haki itatendeka kwa vyama pinzani ? Mimi nataka sana niwe na imani kama yako lakini nafsi yangu inanisuta - kweli naweza kupata usingizi mbuzi wangu nikimfungia nje na huku najua mafisi yanarandaranda huko nje ?
 
sasa wanachadema waambie wanachama wao wakapige kura kwa salama na baada ya hapo waende majumbani kusubiri matokeo

hakuna haja ya kuwasumbua na kuwatesa kwa kuwaweka ati mita 200 kwa kisingizio cha kulinda kura

tuungane pamoja kudumisha amani ya nchi yetu

siku chache zilobaki kila chama kijitahidi kupiga kampeni na kushawishi watu wakapige kura

ila nnaamini wanachadema hawana wapiga kura maana wengi hawajajiandikisha bali ni ushabiki tu

ukiwaona kwenye mikutano ni wengi ila wenye sifa za kujiandikisha hamna kitu kwa kuwasaidia watani uchaguzi ujao ujipange pamoja na kuwahimiza wanachama wao wajitokeze kwenda kujiandikisha
 
Hapa Chadema hawatakuunga mkono MKJJ. Swali la msingi ni hizo kura wataiba vipi? Maana kama kuna mtu ameona udhaifu ambao wataalamu wa mambo ya kura hawajaona ni bora watueleze.
Binafsi, nina imani my vote will count, la sivyo nisingeona umuhimu wa kupiga kura.

Ahsante MKJJ kwa kuwapa wapiga kura imani na kura zao.

Wacha kulalamika kabla ya matokeo, PIGA KURA!
 
@MMM

kuna sehemu umesema ukweli na chagizo lako zuri sana... lakini kuiba kura inawezekana sana tu!!! It has happened na inaweza kutokea hasa kwa nchi yenye njaa kama yetu...
 
Hapa Chadema hawatakuunga mkono MKJJ. Swali la msingi ni hizo kura wataiba vipi? Maana kama kuna mtu ameona udhaifu ambao wataalamu wa mambo ya kura hawajaona ni bora watueleze.
Binafsi, nina imani my vote will count, la sivyo nisingeona umuhimu wa kupiga kura.

Ahsante MKJJ kwa kuwapa wapiga kura imani na kura zao.

Wacha kulalamika kabla ya matokeo, PIGA KURA!

huu waraka hakuwaandikia chadema, amewaandkia watanzania wenye akili timamu!!
 
Jamani msaidieni MKJJ maana hajui kuwa mawakala ndio wanachukua rushwa na kuruhusu hizo taratibu kukiukwa na kuandika idadi nyingine ya kura kinyume na kilichohesabiwa.

CCM wamewekeza kwenye njaa za watanzania, wanajua kabisa mawakala wana njaa kali sana na wakipewa pesa kidogo wanakubali kuchakachua matokeo na kuandika yale inayotaka CCM
 
Back
Top Bottom