Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #21
mkuu,
sasa hili swala la kuiba kura unataka kusema halipo?
mweh!!!
mkuu,
sasa hili swala la kuiba kura unataka kusema halipo?
Mwanakijiji;
Mwaka 1995 kulingana na takwimu za mawakala wa CUF kule ZNZ ilionyesha kuwa Maalim Seif kashinda kwa asilimia kubwa dhidi ya incumbent Dr Salmin Amour lkn matangazo ya ZEC yalimpa ushindi Dr Salmi kwa aslimia 50.1 dhidi ya 49.9 za CUF!
CUF walienda hata kwenye jumuia za kimataifa kuomba warudie tena kujumlisha matokeo ya kura ya vituo vya uchaguzi lkn ZEC ikasisitiza tena na tena kuwa matokeo waliyotangaza ni halali na hawatarudia tena kujumlisha matokeo;machafuko yaliyotokea hapo baadae hamna asiyeyajua!
Wasi wasi wangu ni kuwa hata kama Dr Slaa atashinda,na hata kama mawakala wa CHADEMA watafanya kazi nzuri sana ya kuwa makini kwenye vituo vya kura,lkn je kama NEC ikatangaza matokeo jinsi wanavyotaka wao na kwa hiki kipengele kinachosema NEC haipingwi popote pale tutafanya nini?
Mwnaakijiji wizi wa kura upo wa namna nyingi.
Moja: zinaandaliwa karatasi nyingine za kupigia kura ambazo tayari zina tick kwa mgombea ambaye anatakiwa kushinda then wakati wa kuhesabu zinafanyiwa exchange na zile karatasi ambazo zina tick kwa mgombea mwingine 'wasiye mtaka'.
Namna nyingine ni kutumia ubabe kama uliotumika 1995 kule Zanzibar.
kashinda Seif lakini anatangazwa Salmin Amour na hakuna wa kuingilia kati.
Malafyale.. hilo tatizo halipo mwaka huu; matokeo yanatangazwa kila kituo na kila jimbo linatangaza rasmi.. hakuna haya ya takwimu za mawakala! Na as a matter of fact.. mawakala hawahesabu kura wao wanaangalia tu, sasa hawa mawakala wa Zanzibar walileta namba zao wote wakazijumlisha na zikapingana na zile za Tume ya Uchaguzi? How realiable was their tally?
Da! Mwnakijiji nikikumbuka kipindi kile ulivyoitetea CCJ, nikijumlisha na hoja yako hii ya leo ya kusema hakuna wizi wa kura,
Nachoka kabisaa.
MKuu unakumbuka kilichotokea Kenya? Jamaa walivyoona matokeo kutoka vituoni sio mazuri wakamwita Kivuitu upesi upesi atangaze matokeo.....
Pengine mwenzetu haujapiga kura au kuangalia mchakato mzima wa kupiga kura, kuzihesabu na matokeo kutangazwa kwa muda mrefu. Sisi wengine tumeyashuhudia haya tangu mwaka 1975. Tuna mengi tumeyaona. Itoshe tu kusema CCM haiko tayari kuondoka madarakani.mbona nimesema hilo.. kuwa kinachoweza kutokea ni NEC huko lakini siyo kuiba kura.. hayo ya NEC nimeshayazungumzia kwa upande mwingine.. Sitaki watu wahofie kupiga kura kuichagua Chadema kwa sababu ati kura zao zitaibwa na CCM watashinda tu.. inakuwa ni kama negative reinforcement..
Kinachofanyika na ambacho huwa kinafanyika ni kuwanunua mawakala wa vyama vya upinzani jambo ambalo ndilo liliigharimu Chadema karibu viti vyote vya Tukuyu na vinginevyo wakati wa By-elections isipokuwa jimbo la Tarime. Kwa hiyo hoja yako hii hapa chini siyo ya kweli hata kidogo:-Lakini, kura zaweza kuchezewa lakini ili zichezewe kunahitaji ushirika wa zaidi ya mtu mmoja. Yaani, msimamizi wa kituo, wawakilishi wa wagombea, waangalizi wa ndani na wa nje na vile vile wapiga kura wenyewe.
Siyo hapo tu, kama kweli Kura zingekuwa zinaibwa kirahisi hivyo, kwanini wameshindwa kuiba kura Pemba ambapo CUF imeendelea kutesa kwa miaka 15 sasa tangu mfumo wa vyama vingi uende na kwanini kura za Jimbo la Darajani (ambalo nadhani sasa limegawanywa - niko tayari kusahihishwa) haziibwi na matokeo yake zinakuwa za karibu sana?
Ipo imani ambayo imejengeka kuwa ni rahisi kwa kikundi cha watu au watu kuiba kura na kumuongezea mtu mwingine kura kinyume cha sheria. Watu wenye imani hii (naiita imani kwani hakuna ushahidi wowote kuwa kura zimewahi kuibwa, yaani ushahidi unaoweza kusimama Mahakamani!) huwa na wasiwasi kuwa uchaguzi unapofanyika basi kuna makundi ya watu ambayo yanakula njama kuiba kura na kubadilisha matokeo.
hayo maeneo machache ambaye vyama vya upinzani vimefanya vizuri ni kuwa vina mtandao mkubwa wa kulinda matokeo yao na wapiga kura walikuwa hawazuiwi kuwa mita 200 nje ya vituo vya kupiga kura kama itakavyokuwa safari hii.Ukweli ni kuwa wenye hofu hii ya "wizi wa kura" ni kwamba hawajui upigaji kura wetu ulivyo na kwanini hatua zilizochukuliwa mwaka huu na Tume ya Taifa ya Uchaguzi zitachangia sana kuondoa wasiwasi wa wizi wa kura. Bahati nzuri nina uzoefu wa kushiriki kama mwangalizi wa Uchaguzi Mkuu katika mojawapo ya chaguzi zetu nchini na kuweza kutembelea maeneo ya Shinyanga, Mwanza na Musoma wakati wa kampeni na wakati wa Uchaguzi kuweza kutembelea vituo vya uchaguzi zaidi ya hamsini vya Mwanza. Nimeshiriki toka kituo kinafunguliwa hadi kura zinamalizwa kuhesabiwa. Kwa hiyo, siandiki kinadharia bali kwa uhakika wa ushuhuda wangu mwenyewe ambao nina uhakika unaweza kurudiwa na mtu mwingine yoyote aliyepata nafasi kama yangu.
mbona nimesema hilo.. kuwa kinachoweza kutokea ni NEC huko lakini siyo kuiba kura.. hayo ya NEC nimeshayazungumzia kwa upande mwingine.. Sitaki watu wahofie kupiga kura kuichagua Chadema kwa sababu ati kura zao zitaibwa na CCM watashinda tu.. inakuwa ni kama negative reinforcement..