Kwanini ngumi zinachezwa usiku wa manane?

Kibukuasili

JF-Expert Member
May 15, 2010
1,050
604
Mimi ni mshabiki mzuri wa ngumi. Hivi karibuni kumekua na mwamko mkubwa wa ngumu za kulipwa nchini. Shida kubwa inakuja pale panapokua na pambano zuri lakini muda unakua sio rafiki kabisa.

Tukiangalia ngumi za Marekani ambazo nyingi wanapigana Las Vegas huwa zinakua masaa ya alfajiri kwetu. Kwa kuwa kuna tofauti ya karibu masaa 10 ina maana kwa Las Vegas inakua bado ni mapema tu. Haya ya kwetu main card inaanza saa saba usiku au zaidi. Mimi binafsi siwezi kwenda ukumbini kwa sababu muda sio rafiki. Japo nina usafiri lakini sioni kwa nini niendeshe gari saa 9 usiku mwenyewe eti nimetoka kwenye ngumi. Nafikiri siko peke yangu ambaye nashindwa kwenda kwa sababu hiyo. Mtu asiye na usafiri wa kujitegemea ndio ngumu zaidi. Utapta wapi daladala saa hizo, na bajaji/bodaboda sio salama sana wakati wa usiku mkubwa.

Ningeshauri waandaaji wa ngumi wabadilishe utaratibu. Michezo ya awali ianze mapema ili pambano kubwa lianze kwenye saa 2 hivi ili liishe mapema watu waende majumbani kwao ikiwa bado ni mapema. Wanakosa watazamaiji wengi kwa ratiba yao ngumu.

Hata kuangalia kwenye TV nyumbani nako ni mtihani. Kukaa mwenyewe kwenye TV saa saba usiku unaweza kujikuta umelala na ngumu zenyewe usizione, hasa inapotokea mapambano ya utangulizi hayana msisimko.
 
Mimi ni mshabiki mzuri wa ngumi. Hivi karibuni kumekua na mwamko mkubwa wa ngumu za kulipwa nchini. Shida kubwa inakuja pale panapokua na pambano zuri lakini muda unakua sio rafiki kabisa.

Tukiangalia ngumi za Marekani ambazo nyingi wanapigana Las Vegas huwa zinakua masaa ya alfajiri kwetu. Kwa kuwa kuna tofauti ya karibu masaa 10 ina maana kwa Las Vegas inakua bado ni mapema tu. Haya ya kwetu main card inaanza saa saba usiku au zaidi. Mimi binafsi siwezi kwenda ukumbini kwa sababu muda sio rafiki. Japo nina usafiri lakini sioni kwa nini niendeshe gari saa 9 usiku mwenyewe eti nimetoka kwenye ngumi. Nafikiri siko peke yangu ambaye nashindwa kwenda kwa sababu hiyo. Mtu asiye na usafiri wa kujitegemea ndio ngumu zaidi. Utapta wapi daladala saa hizo, na bajaji/bodaboda sio salama sana wakati wa usiku mkubwa.

Ningeshauri waandaaji wa ngumi wabadilishe utaratibu. Michezo ya awali ianze mapema ili pambano kubwa lianze kwenye saa 2 hivi ili liishe mapema watu waende majumbani kwao ikiwa bado ni mapema. Wanakosa watazamaiji wengi kwa ratiba yao ngumu.

Hata kuangalia kwenye TV nyumbani nako ni mtihani. Kukaa mwenyewe kwenye TV saa saba usiku unaweza kujikuta umelala na ngumu zenyewe usizione, hasa inapotokea mapambano ya utangulizi hayana msisimko.
Ata mimi nawashangaa sana, mda ule wa ngumi wanapoteza mashabiki wengi sana mana wanaelekea kulala, pambano la mwisho angalau lianze saa 4 usiku

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
huo mchezo nilicheza .baadae nikaacha.
Masuala ya kupigana sparingi ulingoni ukishuka mwili wote unauma unaenda kumeza panado sio mazuri.
 
Naunga mkono hoja mleta mada

Mimi mwenyewe ni mapenzi wa Ngumi sana lakini muda wa kuweka pambano kuu saa7 usiku inanishinda kwakweli

Pambano la Mwakinyo na Mfilipino nilikaa macho kodo kwenye kideo mpaka lilipoanza ghafla nikapitiwa na usingizi nakuja kustuka naona Mwakinyo anabebwa juu juu ndo kashinda,, nilisikitika sana

Waandaji waangalie muda mzuri wa kufanikisha hili hasa kwa angalau saa3 usiku au 4 ni muda mzuri sana kuwapambanisha wale magiant
 
Kilichonisikitisha narudia nisikitisha...! ITV Mpo Mubashara....Warembo Wale Eti na wenyewe wanatifuana ili apatikane mshindi....! Ombi langu tuwaongoz
 
Naunga mkono hoja mleta mada

Mimi mwenyewe ni mapenzi wa Ngumi sana lakini muda wa kuweka pambano kuu saa7 usiku inanishinda kwakweli

Pambano la Mwakinyo na Mfilipino nilikaa macho kodo kwenye kideo mpaka lilipoanza ghafla nikapitiwa na usingizi nakuja kustuka naona Mwakinyo anabebwa juu juu ndo kashinda,, nilisikitika sana

Waandaji waangalie muda mzuri wa kufanikisha hili hasa kwa angalau saa3 usiku au 4 ni muda mzuri sana kuwapambanisha wale magiant
🤣 🤣 Inachekesha lakini inauma pia. Kila nikifikiria sababu ya kuweka pambano usiku wamanane siipati. Na hakika wanakosa watazamaji wengi, kwenye TV na hata ukumbini pia. Nahakika hata walioko ukumbini wengine wanakua wamelewa wanapiga kelele tuasubuhi wakiamka hawakumbuki kitu (I've been there :D)
 
  • Thanks
Reactions: tyc
Back
Top Bottom