sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 2,525
- 7,377
Kwanza hakuna ubishi Zuchu ndio msanii wa kike namba moja East and Central Afrika.
Pili ndio msanii mwenye influence kubwa kwa sasa Tanzania kwenye lifestyle kuliko msanii yoyote yule.
Kila binti sasa hivi anataka kuwa Zuchu kuanzia mavazi, mapozi, swaga na ustaa.
Ama kwa hakika amejua kuwa brand.
Kwa hiyo anaposema anakuja na brand yake ya mavazi kazi yake itakuwa ndogo sana.
Mpaka sasa kuna hereni tayari zinaitwa Zuchu, kuna rasta zinaitwa Zuchu na kila dada mjini anataka kuweka pin puani kama Zuchu.
Kwa kifupi kizazi jeuri au wanawaita generation Z ni kijiji cha Zuuh.