Kwanini mtu huogopa? Hasa kufa kwa nini?

Kwanini mtu huogopa? Hasa kufa kwa nini?

Mimi naogopa tu yale maumivu ya kwenye mchakato wa kifo mfano ugonjwa wa maumivu makali ajali

Ila kama naweza kufa kwa amani mfano usingizini au nimekaa zangu sebuleni wala hakuna tabu 🄰
OK. So kwako maumivu ndo hofu yenyewe?
Maana kuna wengine huogopa kile wasiicho kijua baada ya kufa..

Wamekuwa attached na maisha to the point akiambiwa aache kila kitu afe anapata hofu..
 
OK. So kwako maumivu ndo hofu yenyewe?
Maana kuna wengine huogopa kile wasiicho kijua baada ya kufa..
Mimi naogopa maumivu ya mchakato wa kifo kama kuna namna ya kufa kimya kimya ningependa hivyo
Wamekuwa attached na maisha to the point akiambiwa aache kila kitu afe anapata hofu..
Wewe uache kila kitu ufe huko kufa unakujua?
Lazima mtu achague anachojua ambacho ni kuishi
 
Fear is your brain's built-in alarm system designed to keep you alive. It is a natural and healthy emotion that helps you react quickly to danger.
Mshana umejibu short and clear ila ubongo una jitahidi kupingašŸ˜‚
Ila mbona tunaweza kuovercome fear of other things except death?
 
Unatumia analogy ya usingizi kuelezea kifo, yani umeshindwa kuona utofauti hapo?

Usingizi ni mchakato wa kibiolojia ndani ya mwili ulio hai, unapokuwa umelala, mwili wako bado unakuwa unafanya kazi, mapigo ya moyo yanaendelea kama kawaida, ubongo unaendelea na activity yake lakini kifo ni utengano wa mfumo mzima.

Ni makosa ya kifikra kulinganisha state of rest na cessation of existence, hauwezi kusema kifo ni kama usingizi kwa sababu kwenye usingizi kuna continuity ya maisha, wakati kwenye kifo, mtoa-ushuhuda ambaye ni wewe unatoweka kabisa.
Ukiwa unaishia usingizini unajua kwamba hapa ndio naishia hivyo?

Au unajikuta tu umepanda kitandani, asubuhi umeamka bila kujua uliishia usingizini muda gani?

Mtu akiwa anakufa anajua hapa ndio nakufa hivyo?

Huoni kwenye situation zote mbili mtu anakuwa unaware hajui chochote kile?

Kwenye situation zote mbili unakuwa unconscious .

utofauti ni kwamba usingizi ni temporary unconsciousness.

Kifo ni permanent unconsciousness.
 
Moto ukizimika unaenda wapi?

Ukipuliza mshumaašŸ•Æukazima, moto unakuwa umezimika na kwenda wapi?

Maana unajiuliza mtu akifa anaenda wapi?

Kana kwamba binadamu ni "so special" anahitaji mahali pa kwenda akishakufa.
Hapa umefanya makosa ya kulinganisha event na observer.

Labda nikueleweshe kwa upande wa sayansi unakotaka, sayansi yenyewe inasema energy cannot be created or destroyed, only transformed, moto ni energy.

Moto unapoonekana kuzima nishati yake huwa haipotei isipokuwa huwa inabadilika na kuwa joto linalotawanyika kwenye entropy,
kwahiyo, hata kwenye hoja yako ya moto, moto hauendi popote isipokuwa huwa unabadilika hali tu.

Kama binadamu ni nishati/fahamu basi kifo siyo non existence bali ni transformation ya hali ya fahamu ambayo hatuijui kwa sasa ,ukikubali sheria ya conservation of energy, basi hoja yako yote inaishia hapa.
 
Ukiwa unaishia usingizini unajua kwamba hapa ndio naishia hivyo?

Au unajikuta tu umepanda kitandani, asubuhi umeamka bila kujua uliishia usingizini muda gani?

Mtu akiwa anakufa anajua hapa ndio nakufa hivyo?

Huoni kwenye situation zote mbili mtu anakuwa unaware hajui chochote kile?

Kwenye situation zote mbili unakuwa unconscious .

utofauti ni kwamba usingizi ni temporary unconsciousness.

Kifo ni permanent unconsciousness.
Usingizi una continuity yani ubongo wako unajua kuwa wewe ni nani na unajiandaa kurudi, kifo ni total erasure ya mfumo wako.

Huwezi kulinganisha safari ya kwenda na kurudi na safari ya kwenda na usirudi.
 
usidanganye watu hakuna mtu aliehai anayejua mtu anahisi vipi wakati wa kufa ni kwasababu waliokufa hawawezi kurudi tena wakatuelezea
Ili uweze kuhisi lazima uwe hai kwanza.

Kuhisi kunahitaji uhai.

Ukishakufa huwezi kuhisi wala kujua chochote.

Sisi tupo hai, ndio maana tunajua kwamba ukishakufa huwezi kujua wala kuhisi tena.
 
Iko hivi Mkuu binadamu tuna uwezo wa kuwaza future, huu uwezo wa wa kuwaza ndio umetupa uwezo wa kujenga ustaarabu, lakini pia ndio uliotuletea huzuni ya kifo.

Hatujaijenga huu hofu kwa ajili ya ku-survive labda isipokuwa tumeijenga kwa sababu tumejipa uwezo mkubwa wa kufikiria sana, kadiri akili inavyokua, ndivyo hofu ya kifo inavyozidi kuwa kubwa pia.
So I got another theory that fear exists in the mind... When we quite the mind, thoughts diminish thus fear?

Tumesahau the energy body, which is instinctual haihitaji thoughts inahitaji behavioral conditioning
 
Usingizi una continuity yani ubongo wako unajua kuwa wewe ni nani na unajiandaa kurudi, kifo ni total erasure ya mfumo wako.

Huwezi kulinganisha safari ya kwenda na kurudi na safari ya kwenda na usirudi.
Ubongo wa mtu anayekufa, unajuaje mtu huyu anakufa?

Ubongo wa mtu aliyelala, Unajuaje mtu huyu ataamka?
 
Jamaa Ana point tena kubwa sana, yeye ame surpass the body and mind... Akadive into the metaphysical aspect kuwa before hajazaliwa hakuwepo na so akifa anarudi into That nothingness.. But hiyo hai negate existence ya hofu... Ambayo ni instinctual
Binafsi sijaiona hiyo point kubwa unayo isema wewe, unapoishi katika metaphysical state ya nothingness bado mwili wako unaendelea kufanya kazi kwa silika ya ku survive.

Kujua ukweli wa kifo hakufuti hofu ya kifo, kwa sababu hiyo hofu haitoki kwenye mind.
 
usidanganye watu hakuna mtu aliehai anayejua mtu anahisi vipi wakati wa kufa ni kwasababu waliokufa hawawezi kurudi tena wakatuelezea
Ameelezea baada ya kufa, yaani ile roho imekata, hakuna ajuaye so why tu naogopa na hakuna ajuae..
 
sayansi yenyewe inasema energy cannot be created or destroyed, only ntransformed
Nakubaliana na hii law asilimia mia ila tusisahau hii bado ime base kwenye current understanding ya universe, vipi kama energy inaweza kuwa destroyed au kuwa created ila kwa sasa hatuna calculation sahihi za kujua hilo, mfano kabla ya einstein theory ya relativity dunia nzima ilitumia laws of motion ila relativity ikaja ku challenge hyo, hivyo huenda energy pia inaweza kufa, na mtu akifa hakuna transformation yoyote ya energy yake bali ndio mwisho
 
Binafsi sijaiona hiyo point kubwa unayo isema wewe, unapoishi katika metaphysical state ya nothingness bado mwili wako unaendelea kufanya kazi kwa silika ya ku survive.

Kujua ukweli wa kifo hakufuti hofu ya kifo, kwa sababu hiyo hofu haitoki kwenye mind.
Bado hujanielewa
Anamaanisha kuwa just like the fear of heights kwamba mtu akijua ya kuwa hiyo fear was created by the mind na akae da akai face mpk ikatoweka vivyo hivyo mtu akijua kuwa akifa anarudi kwenye emptiness his fear of death will automatically perish
 
Nakubaliana na hii law asilimia mia ila tusisahau hii bado ime base kwenye current understanding ya universe, vipi kama energy inaweza kuwa destroyed au kuwa created ila kwa sasa hatuna calculation sahihi za kujua hilo, mfano kabla ya einstein theory ya relativity dunia nzima ilitumia laws of motion ila relativity ikaja ku challenge hyo, hivyo huenda energy pia inaweza kufa, na mtu akifa hakuna transformation yoyote ya energy yake bali ndio mwisho
Kama unakiri kuwa hatujui sheria kamili za ulimwengu, kwa nini unahitimisha kwa uhakika kuwa energy inaweza kufa na 'kifo ni mwisho?
 
Back
Top Bottom