Kwanini Mkoa Wa Mtwara hawalimi Vitunguu na Maharage?

Kwanini Mkoa Wa Mtwara hawalimi Vitunguu na Maharage?

ormystatus

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2019
Posts
262
Reaction score
464
Hali ya joto na aina ya udongo iliyopo mkoa wa Mtwara inaruhusu kabisa kufanya kilimo cha mazao ya Maharage na Vitunguu endapo tu utakuwa na chanzo cha maji cha kuaminika lakini watu hawalimi mazao hayo.

Je, wadau wa kilimo mnadhani kwa nini watu hawalimi hayo mazao ingawa yanahitajika kwa kiasi kikubwa sokoni ? Nawasilisha .
 
Hali ya joto na aina ya udongo iliyopo mkoa wa Mtwara inaruhusu kabisa kufanya kilimo cha mazao ya Maharage na Vitunguu endapo tu utakuwa na chanzo cha maji cha kuaminika lakini watu hawalimi mazao hayo.

Je, wadau wa kilimo mnadhani kwa nini watu hawalimi hayo mazao ingawa yanahitajika kwa kiasi kikubwa sokoni ? Nawasilisha .
Kasumba tuu ila Kila zao linaweza kubali.

Pili kupata Nguvu kazi huko ni ishu Kwa sababu Vijana wanakimbilia Dar na Pwani.
 
mabwawa yapo kipindi cha mvua kama kweli hili zao linakubali unaweza lima labda inshu inakuja kipindi cha kiangazi, au unamaanisha mikoa mingine ina vyanzo vingi vya maji kwa mwaka mzima ukilinganisha na Mtwara ?
Kwa Maharage hasa uzalishaji mkubwa sharti mvua ziwe za uhakika.
 
Mtwara sehemu kubwa maharagwe hayakubali sababu ya joto na mvua.
Siyo kwamba ukipanda hayaoti la hasha. Yanaota yanastawi Sana lakini hayazai vizuri.
Kuna faida gani kulima kwa gharama au nguvu kubwa unaishia kupata gunia moja kwenye hekari 1?
Fanya uchunguzi utagundua hili suala.
 
Mtwara sehemu kubwa maharagwe hatakubali sababu ya joto na mvua.
Siyo kwamba ukipanda jayaoti la hasha. Yanaota yanastawi Sana lakini hayazai vizuri.
Kuna faida gani kulima kwa gharama au nguvu kubwa unaishia kupata gunia moja kwenye hekari 1?
Fanya uchunguzi utagundua hiki suala.
Lakini kule Kunde zinazaa sana na ni jamii ya Maharage.
 
Hali ya joto na aina ya udongo iliyopo mkoa wa Mtwara inaruhusu kabisa kufanya kilimo cha mazao ya Maharage na Vitunguu endapo tu utakuwa na chanzo cha maji cha kuaminika lakini watu hawalimi mazao hayo.

Je, wadau wa kilimo mnadhani kwa nini watu hawalimi hayo mazao ingawa yanahitajika kwa kiasi kikubwa sokoni ? Nawasilisha
Mkuu ungedadavua kisayansi zaidi pengine tungepata majibu..
Kwa mfano PH ya udongo inayofaa kwa maharage na vitungu na hali ya hewa nyuzi joto. Halafu tuone mtwara inakidhi vigezo hivyo?
 
Mtwara sehemu kubwa maharagwe hatakubali sababu ya joto na mvua.
Siyo kwamba ukipanda jayaoti la hasha. Yanaota yanastawi Sana lakini hayazai vizuri.
Kuna faida gani kulima kwa gharama au nguvu kubwa unaishia kupata gunia moja kwenye hekari 1?
Fanya uchunguzi utagundua hiki suala
Nadhani kwenye joto hapo ndo kipengele kilipo kwa sababu hakuna namna ya kuepuka kuhusu maji unaweza mwagilia kama mvua ikiwa ndogo sana.

Baadhi ya maeneo kama Mewala huwa wanakipindi cha baridi. Kwa mantiki hiyo wao wanaweza kulima.
 
Back
Top Bottom