Kwanini Mbeya waweze Mwanza mshindwe?

Kwanini Mbeya waweze Mwanza mshindwe?

2kd inaweza bila matata.
Umbali wa Dar-Mwanza ni kama km 1150.
2kd lita 1 itatumia kwa 12km.
1150÷12= 96 mafuta tuweke Lita 100 ambayo ni 100×1600=160,000

750,000-160,000=590,000
50,000 emergency njiani inabaki 540,000

40,000 itatumika kwa watu wa kupakia abiria. Inabaki 500,000 posho ya dereva 100,000/=.

Tajiri unaletewa shilingi 400,000, kwa usalama wa gari ikifika mwanza au dar walau weka 50,000 ya check up wewe ubakiwe na 350,000.

Dereva mlipe vizuri, msikilize na gari ifungie Gps, service za kutosha usibanie.
Dereva anachukua hela la mizigo na parcel wewe muachie siku hesabu ikiwa ngumu anajazia mambo yakiwa vizuri hiyo yake.
Shukran sana mkuu
 
Kwa kweli miji huwa inatofautiana sana. Kitu kingine ni daladala za mbeya ni coaster wakati Arusha na Tanga bado wako na mfumo wa hiace mjini. Pole sana kwa kuwa stuck huko Mwanza
Mbeya wataishinda kwa vitu vingine lakini kwenye suala usafiri wa daladala hakuna mkoa wa kufananisha,town bus ni Rosa tena bomba zote,ukija kwenda wilayani ni coaster pamba ambazo hata Dar hawana kiukweli hongereni mby kwa hilo!
 
Iweje jiji dogo kama la Mbeya waweze kuwa na usafiri hadi jioni lakini jiji kubwa kama Mwanza washindwe kuwa na usafiri wa uhakika wa kutoka Mwanza -Dar (jioni)

Sio wote tuna uwezo wa kukwea mwewe jamani. wekeni coaster jioni jamani walau mara 2 kwa wiki!

Wadau wa usafirishaji hii imekaaje? Leo mtu anakata tiketi anaambiwa hadi alhamisi kwenda Dar kisa usafiri ni mgumu inakuja kweli? Mbona hili jiji linamuingiliano sana na mikoa ya mbali? Wekeni gari jioni jamani! Watu wa Musoma na Sirari hawatasumbuka..

Watu tumestuck!👎
Saizi kutoka Dar mpaka Tinde kuna usafiri wa Coaster za mchana na jioni zinaanzia Pugu Mnadani zinabeba wafanyabiashara wa ng'ombe na kwenda kufika asubuhi Tinde zinaenda na kurudi.
 
Back
Top Bottom