Kwanini Mama Janeth Magufuli asingesubiri msiba Chato?

Kwanini Mama Janeth Magufuli asingesubiri msiba Chato?

Kamati ya utaratibu wa mazishi mko wapi?

Mnamchosha mama Janet hali yake sio nzuri, ana majonzi sana kwanini asingeachwa apumzike nyumbani au atangulie Chato kusubiri msiba?

Situation anayopitia mama Janet sasahivi ni ngumu sana, anahitaji muda mwingi wa faraja na kumpumzika.

Sijapenda kabisa

Kwahiyo atazunguka safari zote hizo za kuagwa au? Mtampa maumivu zaidi na mnamchosha.
Kabisa kaka...huyu mama anachoka sana
 
Ccm wanataka afe kwa uchungu..... Wana lao jambo haya sio majitu kabisa. Si unaona yalificha watz wasijue km rais anaumwa wangepata nafasi ya kumwombea
 
Duu mama wanamtesa huyu. Hivi kuna mwenye uchungu kumzidi kwa hao viongozi? Wangemwacha tu jmn watamsababishia na shida zingne za kimwili[emoji25][emoji25] namwonea huruma sanaaa, kuna muda namwona mama samia akimpoza duu. So painful. Na camera zinaenda kwake, kwanini lkn wasimwache tu jmn.
Natamani kamati ya maadalizi wangelielewa hili
 
Ccm wanataka afe kwa uchungu..... Wana lao jambo haya sio majitu kabisa. Si unaona yalificha watz wasijue km rais anaumwa wangepata nafasi ya kumwombea

Ungemwombea tu Mkuu. Hayo maombi yangefika huko alikokua amejificha, tuache mkumbo
 
... msiba huu sio tu wa taifa ni wa kwake pia. Wageni wanatoa pole sio tu kwa serikali na taifa lakini pia kwa familia na mke wa marehemu in particular na wageni hawa hawataenda Chato kuzika.

Itakuwa ajabu wageni wamekuja kukupa pole halafu wewe haupo, umekimbia umewaacha! Haiingii akilini. Ni maumvu makali ila hakuna namna yampasa kuvumilia.
 
Wasingeweza kwenda toa hizo pole kwenye mazishi chato?
... tunazungumzia wakuu wa nchi na serikali zaidi ya 15 among other high level diplomats and officials. Miundombinu ya kijijini Chato itaweza kuhimili ugeni wa aina hii at par?

Hawa sio aina ya wageni msiba ukitokea kijijini kwenu wanakuja na mafurushi ya kunde, unga, kuku, mtama, n.k. kutoa pole; wageni ambao hawana hiana kutandika majamvi na mawe shughuli ikaendelea!

Hawa ni wageni wa kimataifa; kila mmoja ana maafisa sio chini ya 20 nyuma yake! Pata hiyo picha!
 
... tunazungumzia wakuu wa nchi na serikali zaidi ya 15 among other high level diplomats and officials. Miundombinu ya kijijini Chato itaweza kuhimili ugeni wa aina hii at par?

Hawa sio aina ya wageni msiba ukitokea kijijini kwenu wanakuja na mafurushi ya kunde, unga, kuku, mtama, n.k. kutoa pole; wageni ambao hawana hiana kutandika majamvi na mawe shughuli ikaendelea!

Hawa ni wageni wa kimataifa; kila mmoja ana maafisa sio chini ya 20 nyuma yake! Pata hiyo picha!
Hapo hapo wakae mwezi mzima hadi waanue matanga....
 
Kwa kweli aende tu Chato Mama yetu
Leo yani she was in so much pain
Na kila siku pain hiyo itakua inajirudia rudia mpaka ijumaa just imagine! Vitu vingine ni kutumia tu common sense na ubinadamu. Hakuna logic ya kumzungusha yule mama sehemu zote hizo.
 
Back
Top Bottom