Kwanini Mama Janeth Magufuli asingesubiri msiba Chato?

Kwanini Mama Janeth Magufuli asingesubiri msiba Chato?

Author

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2014
Posts
1,745
Reaction score
8,230
Nimekuwa naangalia msafara na shughuli ya kumuaga Hayati John Pombe Joseph Magufuli tangu Dar es Salaam mpaka leo Dodoma kila sehemu naona mama Janeth analia kwa uchungu sana. Lakini watu wanavyolia wanamuongezea uchungu kwa maeneo yote mwili unapoagwa.

Msiba umefika viwanja vya Dar na watu wengi wameupokea kwa vilio huku mama Janeth akiendelea kupata uchungu na kuanza kulia upya. Leo Dodoma hali ni hiyo hiyo. Namuonea huruma sana na naona anachoka sana.

Ingekuwa amri yangu ningemwomba abaki Chato asubiri msiba. Maeneo ya viwanjani tunamuona analia. Sijajua kwenye misafara na vilio vya watu njiani vinamuongezea uchungu kiasi gani.

Hapo bado Zanzibar, Mwanza na Geita. Tangu March 17 (labda kabla ya hapo). Mama Janeth atakuwa analia tu.

Imetosha sasa tumpumzishe JPM...na Mama Janeth apumzike
 
Mbaya zaidi wanamuacha sana alone kama leo Dodoma wale mabinti wanaomlinda walikua wanajisahau sana mpaka wanakuna maskio thats shame. Wamtaftie mtu mzima wa kumfariji anaumia sana akiwa hivyo alone.
 
Uchungu wa kuaga siku mbili tatu, watu huwa wanazima sasa patia picha huyo mama anajisikiaje anapowekwa katika mazingira yanayomvunja moyo kila saa

huyo ni kiongozi, mume na baba wa watoto wake. Ana maumivu makubwa kuliko watu wengine. Mungu amtie nguvu.
 
Duu mama wanamtesa huyu. Hivi kuna mwenye uchungu kumzidi kwa hao viongozi? Wangemwacha tu jmn watamsababishia na shida zingne za kimwili😪😪 namwonea huruma sanaaa, kuna muda namwona mama samia akimpoza duu. So painful. Na camera zinaenda kwake, kwanini lkn wasimwache tu jmn.
 
Kwako ni msiba kwake ni MUME.sawa kijana jifunze kuchutama
 
Yaani unamwona jinsi anavyoumia.so painful. Mungu amtie nguvu katika kipindi hiki kigumu
 
Yaani unamwona jinsi anavyoumia.so painful. Mungu amtie nguvu katika kipindi hiki kigumu
 
Sasa utamlazimisha cyril.ramaposa aende chato je kama ana limited time table
Tofauti ni nini? Kama hiyo ingekuwa ndio ratiba inavyotaka na yeye kaamua kwa moyo wake kuhudhuria, angekwenda.
 
Back
Top Bottom