Kwanini Mama Janeth Magufuli asingesubiri msiba Chato?

Kwanini Mama Janeth Magufuli asingesubiri msiba Chato?

Wachambuzi wa mambo ya kisiasa hawana tofauti na wachambuzi wa mambo ya mpira, yani timu ifungwe ama ishinde hayatakosekana ya kuongelea kwenye hiyo mechi.

Mkijitoa nyinyi mnaolalamika mama anateswa kisa amehudhuria hapo dodoma, wangekuja wengine kulalamika kama asingekuwepo hapo leo.
 
Nimekuwa naangalia msafara na shughuli ya kumuaga Hayati John Pombe Joseph Magufuli tangu Dar es Salaam mpaka leo Dodoma kila sehemu naona mama Janeth analia kwa uchungu sana. Lakini watu wanavyolia wanamuongezea uchungu kwa maeneo yote mwili unapoagwa...
Sawa ni maswala ya kiitifaki. Lakini ni busara yafanyike with some senses of reasoning and common sense.

Huyu mama anaumia sana. Kwasababu Kitaifa msiba umeshaondoka Dodoma, huyu mama angeenda kupumzika Chato kwa hizi siku mbili tatu kabla ya mazishi.

Machozi yana tabia ya kuambukiza. Kuna wakati akiona wananchi wa kawaida wanalia unakuta na yeye anaanza kulia hapohapo. So sad. Mungu amtie nguvu kwakweli.
 
Namuhurumia sana huyu mama. Natamani wangesubiri siku ya mazishi ndio aonekane. It's tough for her.
 
Ni swala la itifaki kuzingatiwa alafu akiondoka tu wale jamaa wasio kuwa na kazi za maana, kazi kuangalia snow ubelgiji na canada wataanza kupiga kelele
 
Wanazidi kumtia uchungu tu mama wa watu, angeenda Chato kumsubiri mumewe amzike, ila bongo ndivyo ilivyo, imeshangaza sana sana..
 
Mbaya zaidi wanamuacha sana alone kama leo Dodoma wale mabinti wanaomlinda walikua wanajisahau sana mpaka wanakuna maskio thats shame. Wamtaftie mtu mzima wa kumfariji anaumia sana akiwa hivyo alone.
Gafla najikuta napenda Avatar yako na mwandiko tu [emoji8]
 
Kwa tukio la jana alilazimika kuwepo maana ni state funeral (mazishi ya kitaifa) huko kwingine anaweza kuwa hayupo akasubiria Chattle kwenye siku ya mazishi ni kweli amechoka ila ni utaratibu tu, hata mzee baba mwenyewe sikuona sababu ya kumzungusha kooote huko mpaka watu wanakanyagana na kufa ilitakiwa apewe heshima yake tu na wawakilishi wachache basi azikwe period.
 
Mama anateseka sana...
 
Back
Top Bottom