Kwanini maisha ni Ubatili?

Kwanini maisha ni Ubatili?

Ikiwa afanyacho mtu kinaingilia mpangalio wa shughuli za vitu vingine, maana yake maisha ni ubatili.
 
Kiufupi haya maisha kama huna mtoto au wazazi wanaokutegemea usishangae usipoona thamani ya Uhai au kuishi maana vingine vyote ikiwepo mali tunazotesekea ni UPUUZI MTUPU yani mwisho wetu ni mauti ndo reward ya uhakika katika hustle zetu zote thats why matajiri huwa hawaoni shida kugawa kiasi kikubwa cha utajiri kwa maskini vyote utaviacha na unaondoka FUVU.
 
Maisha ni ubatili .

Mfano Mwanasiasa anaanzisha VITA anapeleka wanajeshi vitani na wanakufa wakifa wanaitwa mashujaa Ila yeye hakubali kuuliwa au kufa kifo kibaya .

So maisha yapo ili kuyaishi ila Watu wachache wameamua kwa makusudi kujipatia Faida kupitia watu wengine wenye ufahamu mdogo.
Lakini hata wao mwisho wao ni mauti tu lakini binadamu wachache sana hasa wenye madaraka huwa wanaliona hilo..tamaa ni kubwa sana juu ya mali na vyeo.
 
Ndio, ni ubatili mtupu.

Futuhii

Ukiwa mjinga utayafurahia ila ukiwa mwerevu na mwenye kuchunguza kwa mapana utajua ubatili wake kisha utateseka.
Ukitambua hili wakati hujapata watoto hatokubali kamwe kuleta watoto duniani. Kwa nini?
Kwasababu hamna maana yoyote umpate mtoto wako mpendwa kisha aje azunguke duara ulilozunguka alafu aishie

Uwe masikini au tajiri mkubwa mwenye hadi jeshi binafsi, utagundua maisha hayana maana kwa yeyote sababu utaishi kisha utaishia

Hakuna mwanadamu timamu atakaekubali kuzaa!

Ukiona mwenye hekima ambaye ana uzao wake katika dunia hii, basi elewa alipata uzao kabla hajaipata hekima au alitegeshewa.

Ubatili mtupu
Indeed ni ubatili Kwa kweli
 
Maisha yanakuwa ubatili kama unajilisha upepo. Lakini kwa wengine, maisha yana maana.
Still ni ubatili cuz hawato kiepuka kifo magonjwa na mateso mbali mbali ktk maisha yao
 
Binadamu hawezi kuwa na akili timamu kwa sababu ni mtumwa wa maisha bila ya maamuzi yake ,utaona akaza kupambana ila hajui anapambania nn ? Kiuhalisia kuzaa na maisha kwa ujumla ni upatu na utapeli mkubwa kuwahi kutokea.

Baadhi ya wanafalsafa na great thinkers wa awali kabisa walichunguza wakaona kuishi ni utapeli ...
Kuishi ni utapeli ni meaningless
 
Hii ni siri kubwa hasa kuzaliana kama ukitambua ,watu wa zamani hata waafrika walitaka kuzaliana ili wafalme waendelee kupanua himaya zao ..Hao wafalme walikuwa mstari wa mbele kuhamasisha ; walioa wake wengi na kuzaa sana ili kuongea ukubwa wa tawala zao.

Hii ni siri binadamu wamefumbwa bila ya kujijua ,siku zote binadamu anafurahi anapokuwa juu ya mwingine si kwa mali ,elimu ,madaraka ,wala idadi ya watoto..

Leo hii Musk anahamasisha watu wazaliane ili azidi kuongoza watu wengi ,anajihisi fahari kuwa tajiri mkubwa ...Hata leo utaona binadamu mafanikio yake hinafsi yanamtesa ;atataka kupost nyumba aliyojenga ,gari alilonunua ,mtoto aliyezaa mwenyewe ili kujionesha kwamba yuko juu ya wengine...

Maisha ni ubatili mtupu tena uthenge fulani.
Aisee !!! Nakubaliana na huo ukweli kwamba maisha ni ubatili but naomba kuuliza iwapo binaadamu wataacha kuzaliana sindio utakuwa mwisho wa uwepo wa binaadamu duniani na vipi kuhusu kuumbwa kwetu lengo haswaa lilikuwa ni nini !? Au ndio tuli kuwa cron na annunak ili tuje kukamilisha mission zao !?
 
Existence ya viumbe wote hai Dunia inategemea KUZALIANA...... Binadamu wakikoma kuzaliana watapotea kwenye uso wa Dunia......
Ndio maana Kuna sababu kwanini Sex(reproduction) is so pleasurable ili kuchochea kuzaliana

Viumbe wote ni GREED na SELFISH, kila mmoja anataka kuwa na HUHAKIKA wa kupata mahitaji ya kushibisha nafsi yake kwanza...... hii ndio NATURE ya viumbe wote
Ndio maana watu wote TUNACHUANA kuwa kwenye NAFASI ya kuwa na UHAKIKA wa kukidhi matakwa ya nafsi zetu.

LIFE is about
Be born
Fight to stay alive
Then die

Ukiijua hii CODE huwezi kusema maisha ni ubatili

Kwanza watu watasukumwa na UTAMU wa kujamiiana, itafuata Mimba kisha Mtoto..... Kuna sababu kwanini viumbe vingi vya kike vinakua so protective kwa vichanga vyao
Kwasababu vichanga vikifa hakuna MUENDELEZO

Baada ya kukua unatakiwa upambane kuishi..... nothing given for granted.....
Hapa ndio uta pambanua maisha yako utakayo fanikiwa kuishi yatakua ya namna gani

Baada ya hapo YOU DIE......


Sasa KUFA isiwe ndio sababu ya kuona maisha ni UBATILI
Hata ukizaliwa ukafa na siku moja...... utakua tayari ume play part yako
Umeongea mengi yana maana but still umeshindwa kutetea hoja yako inayo Pinga kuwa maisha ni ubatili


Still maisha ni ubatili cuz yana mambo mengi yenye kuumiza hata ukiwa umefanikiwa kiuchumi kiasi gani bado jinamizi la maumivu haliwezi kukuacha , na maisha yana create maumivu ktk nafasi nyingi sana ,

Na mwisho wa Yale yote inayo yapigania lazima utakuja kuyapoteza ama kuyaacha so maisha ni ubatili mtupu
 
Hauoni kama ni ubatili tena utapatu kabisa , just assume wewe unajua kama utakufa kwa akili ya kawaida ila haujui utakufa lini?

Just assume hata maisha yako hauna uhakika ila una utaratibu ulijipangia wa kuishi,leo unafanya biashara kesho unaweza kuanguka kweupe...Mimi nilikuwa kitengo miaka kama 2.5 nyum tena ajira za serikali za uhakika ,leo sipo kule ,hauoni kama ni kubeti huko?


Maisha yote ni ubatili hapo kweny kupambana ,: je ,uliambiwa kabla ya kuzaliwa au ulijikuta ushaingia mkenge Duniani kupitia tamaa za wazazi wako ? Binadamu ana akili usione watoto wakizaliwa wanalia kuna jambo hapa duniani..

Sheria za haki zote duniani ni ubatili , ingekuwa ziko sawa watu wangeanza kufanya kuzaa ni faragha ya anayezaliwa sio unajifanya maamuzi ya kuleta maisha ya mwingine tena hana hatia , maskini wanazaliana kama panya bila ya kuwa na huruma ya mtoto anayezaliwa kama wataweza kuwahudumia.
Ni Mambo ya hovyo sana kwa kweli na kwanini palikuwa na hii mechanism ya kuzaliwa pasipo kumshirikisha mzaliwa

Imagine mtu ana zaliwa halafu anakuja duniani mara anaanza kuumwa cancer mara Figo zimefeli mara kapata ajali kakatwa miguu na mikono mara sijui kafilisika mara kafukuzwa kazi , maisha ni us**nge mtupu kmmk 🚮🚮🚮🚮



Ni ubatili sana Kwa kweli assume maisha ya watu wa Palestine na Ukraine the yalivyo !!! Hapo ndio utaelewa kwamba kuishi ni ubatili
 
Maisha ni ubatili .

Mfano Mwanasiasa anaanzisha VITA anapeleka wanajeshi vitani na wanakufa wakifa wanaitwa mashujaa Ila yeye hakubali kuuliwa au kufa kifo kibaya .

So maisha yapo ili kuyaishi ila Watu wachache wameamua kwa makusudi kujipatia Faida kupitia watu wengine wenye ufahamu mdogo.
😁😁😆😆 Yaani ninecheka kama mazuri vile , bad enough huyo mwabasiasa na yeye anakuja kufa na kuyaacha Yale yote Aliyo kuwa anayapigania , maisha ni ubatili for sure 100%
 
Exactly 💯..Mfano mzuri mzuri Putin...anakomaa hataki vita isimame wakati yeye kavaa suti katulia ikulu....hao underprivileged ndio wapo front wakiumia kwa kivuli cha kiapo....
Hakika ni ubatili...
So sad
 
Basi ubatili wenyewe ndio huu,kama una "Fight to stay alive",then unakufa. Kunakua na umuhimu gani wa kupambania kuishi wakati lazima ufe?
😆😆😆😆😆

Nimecheka sana hoja yako nzito mnooo

Sasa katika mambo ambayo huwaga siyaelewi unakuta inatokea Kuna mtu Amenusurika Kupata ajali Au amepata ajali halafu hajafa --- Halafu anasema anamshukuru mungu hajafa Wakati huo huo anashukuru kuwa hajafa Wakati ipo siku lazima atakufa tu , kuna haja gani sasa ya kushukuru wakati kifo huwezi kukiepuka na nilazima uje kufa !!!!

Kuishi ni ubatili Kwa kweli
 
Naona wengi tunapata tabu sana kuhsu kufahamu lengo halisi la sisi kuletwa duniani,ila ndg zangu kwa yeyote anaehtaji kufahamu lengo la kuletwa kwake Hapa Duniani Basi namsihi atenge muda asome kitabu Cha Quran tukufu,kitabu kinachosomwa na waislam.
Quran imetoa majibu yote Khs Kwann sisi tupo Hapa duniani.
Moja ya mistari inayoelezea Hilo ni Hapa Mungu muumbaji aliposema ktk Quran kwamba "HATUKUUMBA MAJINI NA WATU ILA WAPATE KUNIABUDU"....Hapa Kwenye "KUNIABUDU" ndipo unahitajika kuipata elimu yake na hapo ndipo lilipo jibu la Haya yote tunayojadili hapa ikiwemo Hili neno "PUMBAO LA DUNIA"
Someni Quran ndg zangu Mungu ameweka majbu yote hapo.
 
Back
Top Bottom