GE2025 Kwanini maandamano ya 29 October yatafeli vibaya sana

GE2025 Kwanini maandamano ya 29 October yatafeli vibaya sana

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
34,061
Reaction score
79,418
MAANDAMANAO YA 29OCT YATAFELI VIBAYA MAPEMA SANA KUTOKANA NA SABABU KUU ZIFUATAZO;


Anaandika, Robert Ng'apos Heriel
Mtibeli


1️⃣ Ukosefu wa Miundombinu ya Kiufanisi.


Maandamano makubwa yenye lengo la mabadiliko ya utawala yanahitaji:


a) Kamati za mipango (planning committees)
Hizi kamati naona hazipo. Ukimfuatilia Mange Kimambi na Maria Sarungi ambao ndio vinara wa maandamano haya unagundua hawana kamati zozote zaidi ya vikao vyote vinafanyika mitandaoni na inakuwa live.
Kamati ndio msingi mkuu wa goo organization na mobilization ya maandamano haya. Kama hazipo atafanikiwa vipi? Embu msaidieni Mtibeli aelewe.


b) Mfumo wa mawasiliano ulio salama,
Udukuzi, kufuatiliwa kuliko kupitiliza, usaliti wa mawasiliano ndani ya wenye nia ya kuandamana. Hayo yote yatakwamisha maandamano.


c) Mpangilio wa uongozi wa ngazi mbalimbali (national → regional → district → ward).
Unaweza kujiuliza kama wewe ni muandamanaji. Kwenye kata au mtaa wako kuna mfumo wowote wa kuyaratibu ili yatokee. Au ndio upo pekeako kwenye actual ground lakini mtandaoni ndio upo na na wenzako?
Tumia hiyo kama scale yako.


Mazingira ya Tanzania ya sasa, upinzani au wanaharakati wengi hawana mtandao thabiti wa ndani (grassroot network).
Hii inamaanisha hawana uwezo wa kuunganisha watu hata Laki moja kwa wakati mmoja bila kutambulika mapema.
Serikali inamiliki taasisi zote za mawasiliano, usalama, na inafanya doria usiku na mchana katika mitandao ya kijamii, hivyo hufahamu mipango kabla haijatekelezwa.
Kwa mantiki ya kiintelijensia, maandamano hayo yatakufa kabla hayajaanza, kwa sababu mpangilio wake utavujishwa na kusambaratishwa mapema.


2️⃣ Ukosefu wa Uratibu wa Malengo.


Maandamano yenye mafanikio lazima yawe na lengo moja linaloeleweka na kukubalika kitaifa.
Lakini maandamano haya yana malengo zaidivya moja yanayokinzana, mfano;


a). Kupinga uchaguzi,
b). Kuiondoa serikali iliyoko madarakani kumaanisha kuindoa CCM
c) Kupinga utekaji na mauaji. Wasiojulikana. Na sababu zingine.


Lengo la kwanza ni la kisiasa (kupinga uchaguzi)
lakini la pili ni la mapinduzi (kuiondoa serikali ya Samia madarakani) ambalo kisheria na kiusalama linachukuliwa kama uhaini au uasi.
Lengo la tatu ni la kijamii na haki za binadamu za msingi yaani haki ya kuishi. (Hili lingeunganisha watu wengi zaidi).


Hivyo, wapo wanaoamini wanapigania haki za uchaguzi, na wapo wanaoamini ni vita dhidi ya serikali. Na wapo wanaoamini wanatetea haki za binadamu za kuishi kwa waliotekwa na kuuawa na kutojulikana walipo.
Kukosekana kwa umoja wa tafsiri ya malengo kunafanya maandamano hayo yasifanane kihoja, kimkakati, wala kiitikadi, hivyo yatakosa mwelekeo mapema.


3️⃣ Udhaifu wa Uongozi wa Harakati.


Harakati yoyote ya kisiasa inahitaji:


a) Kiongozi mwenye karisma,
Najaribu kuangalia nani ni kiongozi aliyenyuma ya haya maandamano mwenye ushawishi. Kama ni Tundu Lisu yupo zake gerezani anapambana na kesi yake ya mchongo.


b) Mtu anayeaminika na umma,
Mwenye uwezo wa kujenga hadithi ya matumaini, hadithi zenye kuchochea chuki ya wananchi kwa serikali. Humphrey Polepole naye alitoa matumaini lakini amekamatwa dakika ya sabini ya mchezo kipindi cha pili.


Tanzania kwa sasa, licha ya kuwa na wanasiasa wa upinzani, hakuna kiongozi mmoja anayekubalika kitaifa kama sauti ya mabadiliko ya kweli.
Wengi wamechoka, wamegawanyika au wamo katika mikakati ya kisiasa ya muda mfupi. Na serikali inajaribu kila njia kuwavunja vunja na kuwagawanya kadiri inavyowezekana. Jana mumemwona Ezekiel Wenje. Ni kwamba wanawakatisha tamaa na kuwavunja moyo watanzania.


Bila kiongozi thabiti mwenye command structure, watu wanakuwa kama kundi lisilo na kichwa. Yaani kundi linajiendea endea bila mwelekeo. Hayatakuwa na tofauti na vuguvugu la Luddism kwa wale mliosoma Advance History 2.
Ndiyo maana kwa kitaalamu, maandamano kama haya huanza kwa makelele mitandaoni na kufa siku ya tukio. Haitakuwa mara ya kwanza.


4️⃣ Udhibiti Mkali wa Vyombo vya Usalama.


Kitaalamu, Tanzania ni nchi yenye mfumo wa ulinzi na usalama ulio wa kiintelijensia zaidi kuliko wa nguvu.
Taasisi kama:


I). TISS (Usalama wa Taifa),


ii) Jeshi la Polisi,


Iii) JWTZ (Jeshi la Wananchi)
Na vitengo vya cyber intelligence
vina uwezo mkubwa wa kutambua, kuvuruga, au kuzuia matukio kabla hayajafanyika.


Kwa mfano:


a) Mawasiliano ya Wapanga maandamano hufikiwa kupitia “surveillance”,


b) Viongozi wa maandamano hufuatiliwa kimyakimya,


c) Wengine huchukuliwa “preventive custody” kabla ya siku ya tukio.
Ndio hao unasikia kila siku wanakamatwa mara leo huyu kesho yule.
Wahamasisha maandamano mtandaoni au watu wenye mrengo huo nao huchukuliwa mapema kabisa kabla ya siku husika.
Mtu kama John Heche, John Mnyika, na wenzake hawawezi kuwa uraiani kufikia tarehe 29.


Watahifadhiwa kwa muda huku wakipewa usumbufu kidola mpaka upepo utakapotulia wataachiwa.


Hii inaondoa uwezekano wa maandamano kuanza kwa wingi au kwa ufanisi.
Kitaalamu, tunaita hii “preemptive disruption model” njia ambayo huzima uasi kabla haujaanza.


5️⃣ Hofu ya Kijamii.


Wengi wetu Watanzania ni watu wa amani tusiopenda vurugu, na tumelelewa kwenye misingi ya “amani ni bora kuliko vurugu, au funika kombe mwanaharamu. Apite".
Kisaikolojia, jamii imejengwa kuwa risk-averse (uepukaji wa hatari).
Hivyo, hata kama wanakubaliana kimoyomoyo na hoja za maandamano, wengi hawatashiriki hadharani.


a) Mfumo wa kiutamaduni, kiimani (dini), na kijamii unahimiza utii kwa mamlaka.
Wengi wataishia kusema “Mungu ataingilia” "Mungu atajibu", "tumuachie Mungu" au “Tusubiri uchaguzi mwingine”, hivyo kuua nguvu ya umoja wa kuandamana.


Kwa hivyo, uungwaji mkono utakuwa wa moyoni na mitandaoni lakini si wa miguu kwa mguu sako kwa bako. Watu wanakubaliana mtandaoni, lakini hawatokei barabarani.


6️⃣ Udhibiti wa Habari na Mitandao.


Serikali ina uwezo wa:


a) Kufunga mitandao ya kijamii.
Ikifunga mitandao wananchi wangapi wanauelewa wa kutumia VPN na mambo ya kidijitali. Wangapi?


b) Kudhibiti vyombo vya habari,
Media zote, redio zote, na wenye followers wengi watadhibitiwa iwe kinguvu au kwa kupewa pesa kuwatuliza
Si ndio yale mtaishia kumlaumu Millard Ayo wa watu. Atafanya nini?


c) Kuendesha kampeni za kupotosha


Vitengo vya propaganda kwa sasa vipo kazini: hakuna wakati vinatakiwa kufanya kazi kama wakati huu. Propaganda za kupotosha jamii mfano
“Maandamano yamehairishwa,”
“Viongozi wamekamatwa,”
“Maeneo fulani ni hatari.”
" Wanataka kuchafua nchi"
"Wanavuruga amani"
" Wanatumiwa na mabeberu"
" Watanzania ni waoga sana" hii pia ni. Propaganda iliyofanikiwa sana na ambayo kwa sasa watawala huipigia msumari ili iwe ni kama culture ya watanzania


Hii hufanya hata waliokuwa tayari kushiriki wakose maelekezo sahihi na motisha ya pamoja. Kwa mtazamo wa psychological operations (PSYOPS), hii ni silaha ya kisaikolojia inayotawanya umoja wa wanaharakati. Niliwaambia Saikolojia na soshiolojia ni msingi mkuu wa serikali kutawala watu.


Matokeo yake, maandamano hufa kabla ya saa sita mchana, na wale wachache waliotoka hukamatwa bila upinzani. Kisha baadaye watu huanza kulaumiana. Hoo hamjatoka. Nyie waoga n.k.


Kufikia hapa TaikonMaster sina la ziada. Nimejaribu kujadili. Kwa uhalisia na kwa kuzingatia siasa za nchi yetu, Saikolojia ambayo ninaifahamu kwa sehemu, intelijensia ambayo naifahamu kidunchu, na kwa kutumia falsafa (mantiki na hoja).
So kama utakuja kichwa kichwa na kutoa matusi yako sitaingilia uhuru wako na jinsi unavyoelewa mambo.


Nawatakia sikukuu njema ya Nyerere day.


Acha nipumzike sasa.

TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
 
Maelekezo Maalum kuhusu tarehe 29 Oktoba.

Siku hiyo kazi ni rahisi sana

Viongozi wa CCM tunaishi nao mitaani; Nyumba zao zipo mitaani kwetu, mali zao zipo mitaani kwetu.

Ofisi za CCM zipo mitaani kwetu. Ofisi za Umma nazo zipo mitaani kwetu

VItuo vya kupigia kura vipo mitaani kwetu

Mawaziri, Wabunge na Madiwani tunaishi nao mitaani kwetu, familia zao na ndugu zao tunaishi nao mitaani kwetu. Machawa na mali zao tunaishi nao mitaani kwetu.

Ndugu watanzania, mafuta ya taa, petroli na viberiti havijawahi kuwa adimu.

Tukafanye kazi iliyotukuka hiyo Oktoba 29 hadi hawa Mafisadi watuheshimu na wakome kutuchezea na kutuua.

Share na mwenzako
 
Inaweza kuwa hizi kelele za maandamano ni muendelezo wakutishia watu ili watoke kwa idadi ndogo zaidi kwenda kupiga kura.Sijui hapo wanaohamasisha maandamano wanafaidikaje labda watatusaidia kujua hilo.

Nikija kwenye suala la maandamano kiuhalisia hilo halipo kama watathubutu basi ni wachache na watajuta wala nisiwe mnafiki katika hilo.Nikisema watajuta namaanisha watakuwa wameponzwa na wengine waliowaaminisha kuwa watakuwa wengi.

Wachache kushughulikiwa ni rahisi sana kuliko wengi.Sasa kama watajaribu basi ni wachache.

Nchi ambazo jeshi linaamua kuunga mkono raia ni yale maandamano ambayo yamehusisha raia wengi.Hao wanajeshi wana ndugu pia kwahyo hawezi kwenda kuua mama,baba,kaka,dada zake/ndugu kisa mtawala.

Hii kampeni ya maandamano inanikumbusha ile ya UKUTA na ilipoishia kila mtu anajua.

Haya maandamano yenye sura ya uchama hivi hayawezi kufanikiwa.Maandamano yanapaswa yaunganishe raia wote na ajenda kuu iwe moja.Kama itabadilika basi mbeleni na itakuwa msimamo wa wote.

Sasa mnaandamana huyu anasema NRNE,mwingine anataka serikali iondolewe,mwingine utekeji ukomeshwe,mwingine gharama za maisha mbona ni mtihani sana.
 
Inaweza kuwa hizi kelele za maandamano ni muendelezo wakutishia watu ili watoke kwa idadi ndogo zaidi kwenda kupiga kura.Sijui hapo wanaohamasisha maandamano wanafaidikaje labda watatusaidia kujua hilo.

Nikija kwenye suala la maandamano kiuhalisia hilo halipo kama watathubutu basi ni wachache na watajuta wala nisiwe mnafiki katika hilo.Nikisema watajuta namaanisha watakuwa wameponzwa na wengine waliowaaminisha kuwa watakuwa wengi.

Wachache kushughulikiwa ni rahisi sana kuliko wengi.Sasa kama watajaribu basi ni wachache.

Nchi ambazo jeshi linaamua kuunga mkono raia ni yale maandamano ambayo yamehusisha raia wengi.Hao wanajeshi wana ndugu pia kwahyo hawezi kwenda kuua mama,baba,kaka,dada zake/ndugu kisa mtawala.

Hii kampeni ya maandamano inanikumbusha ile ya UKUTA na ilipoishia kila mtu anajua.

Haya maandamano yenye sura ya uchama hivi hayawezi kufanikiwa.Maandamano yanapaswa yaunganishe raia wote na ajenda kuu iwe moja.Kama itabadilika basi mbeleni na itakuwa msimamo wa wote.

Sasa mnaandamana huyu anasema NRNE,mwingine anataka serikali iondolewe,mwingine utekeji ukomeshwe,mwingine gharama za maisha mbona ni mtihani sana.

Ni kweli kabisa. Alafu tarehe imewekwa mbali sana kiasi kwamba serikali lazima i- relax kuyashughulikia na kuyamaliza bila nguvu kubwa.

Njia ya Ambush mara nyingi ndio njia sahihi kushinda mechi zilizo ngumu
 
Kwa mtazamo wako unashauri coordinators wa haya maandamano wafanye ili wafanikiwe?
Swali zuri ila nasikitika sana kuwa hana majibu sahihi, aje na mbinu zilizotumiwa Nepal na nchi nyingine zilizofanikiwa kuandamana aseme kama hawakupitia haya yanayopitiwa sasa.

Kwenye ushindani wowote kujipanga ni lazima, kumbuka kadri unavyojipanga nao wanajipanga ila kikubwa nguvu ya wananchi ndio inaamua ushindi.
 
Whether watu watatoka au hawatatoka, kuna namna tofauti za kufikisha ujumbe. Maandamano ni njia mojawapo ya kufikisha ujumbe kwa walengwa kuwa hamkani si shwari hata kidogo.

Turn out ya wapiga kura ikiwa ndogo, italeta picha mbaya sana kwa watawala kuwa mambo hayapo sawa na hata kama sio mwaka huu, ila mabadiliko yanakuja. Huko Cameroon ni makondoo kama Tanzania ila wamevumilia miaka 43 ya mzee Biya na yamewashinda. Wameanza kuandamana kutaka mzee atoke, wamechoka. Hata sisi, baada ya miaka 48 ya ccm watu wamechoka, ni swala la muda tu.

Kwa bongo sababu kubwa ni hizi:
1. VYOMBO VYA ULINZI KUWA SEHEMU YA WATAWALA.
2. Kutumia nguvu kuliko maarifa,
3. Kutokuwa na checks and balance kwa vyombo vya usalama.

Nani wa kuwasimamia, kuwahoji na kuwadhibiti, kwa Tanzania wanajiongoza, wanajihoji na kujidhibiti wenyewe, don't expect miracles, watalima watu risasi and nobody will be answerable.
 
Kwa mtazamo wako unashauri coordinators wa haya maandamano wafanye ili wafanikiwe?

1. Tayari wanafahamiana hasa kwa level ya vyama vya siasa.
Hivyo wangeendelea na vikao vya siri kwa kutumia mitandao ambayo sio maarufu kuwasiliana.

2. Hawakupaswa kuwa front wakati wa mapema hivi ili kuzuia vyombo vya dola kuwakatamata.
Mfano Polepole,, au Heche, au yule Tesha mambo waliyoyafanya yalitakiwa yawe katika operation in field.
Siku saba kabla ya tukio ndio wangejitokeza tena mmoja baada ya mwingine.
Siku saba zisingetosha kuwadaka viongozi wote hasa walio mafichoni na mahiri.

3. Kutoka kimkakati wa waratibu na siku zikiwa zimesalia chache au kwa ambush

4. Viongozi walishakamatwa automatically kundi linasambararika.
Ndio maana serikali inakamata vinara iwe ni ground au mtandaoni.

5. Viongozi waliopo mafichoni lazima wawahakishie raia kuwa siku hiyo watakuwepo na itakuwa siku ya ukombozi.
6. Kwenye vita kuna maana kubwa ya kumlinda kiongozi au kiongozi kujilinda sana ili kufikia malengo.

7. Fikiria wale wamahasisha maandamano waliopo nchini wenye followers zaidi ya 100k wakahifadhiwa kwanza.
Wakabakizwa ambao hawana wafuasi wala ushawishi.
Mfano Lord dening ambaye hana followers hata miambili humu Jf ataleta athari gani kwenye maandamano hata akiachwa?
 
Whether watu watatoka au hawatatoka, kuna namna tofauti za kufikisha ujumbe. Maandamano ni njia mojawapo ya kufikisha ujumbe kwa walengwa kuwa hamkani si shwari hata kidogo.

Turn out ya wapiga kura ikiwa ndogo, italeta picha mbaya sana kwa watawala kuwa mambo hayapo sawa na hata kama sio mwaka huu, ila mabadiliko yanakuja. Huko Cameroon ni makondoo kama Tanzania ila wamevumilia miaka 43 ya mzee Biya na yamewashinda. Wameanza kuandamana kutaka mzee atoke, wamechoka. Hata sisi, baada ya miaka 48 ya ccm watu wamechoka, ni swala la muda tu.

Kwa bongo sababu kubwa ni hizi:
1. VYOMBO VYA ULINZI KUWA SEHEMU YA WATAWALA.
2. Kutumia nguvu kuliko maarifa,
3. Kutokuwa na checks and balance kwa vyombo vya usalama.

Nani wa kuwasimamia, kuwahoji na kuwadhibiti, kwa Tanzania wanajiongoza, wanajihoji na kujidhibiti wenyewe, don't expect miracles, watalima watu risasi and nobody will be answerable.

1. Vyombo vya ulinzi sio Alliens. Ni watanzania wenzetu. Kutumia nguvu kutokana watanzania waliowengi wamewapa nguvu hiyo hao wanausalama na wanaulinzi.
Jeshi halizidi wetu milioni moja. Linakuwaje na nguvu dhidi ya watu milioni 60?

Hayo maandamano wakitoka watu laki tano tuu jeshi linatulia na nguvu hazitatumika.

Kusema jeshi kutumia nguvu ni kisingizio tuu
Unafikiri maeneo mengine waliofanikiwa jeshi halikutumia nguvu?

2. Nguvu inakuwa na nguvu kwa watu wachache lakini sio kwa watu wengi
Lawama zote kwa jeshi wakati ishu hapo ni raia wenyewe
 
Whether watu watatoka au hawatatoka, kuna namna tofauti za kufikisha ujumbe. Maandamano ni njia mojawapo ya kufikisha ujumbe kwa walengwa kuwa hamkani si shwari hata kidogo.

Turn out ya wapiga kura ikiwa ndogo, italeta picha mbaya sana kwa watawala kuwa mambo hayapo sawa na hata kama sio mwaka huu, ila mabadiliko yanakuja. Huko Cameroon ni makondoo kama Tanzania ila wamevumilia miaka 43 ya mzee Biya na yamewashinda. Wameanza kuandamana kutaka mzee atoke, wamechoka. Hata sisi, baada ya miaka 48 ya ccm watu wamechoka, ni swala la muda tu.
Kuhusu turnout kuwa ndogo hii ni hadithi tu; tuliona uchaguzi wa CCM wa ndani wa wabunge na madiwani namna ambavyo zaidi ya wajumbe wa mikitano mikuu kwenye ngazi mbalimbali zaidi ya Million tatu walivyojitokeza kupiga kura.. hawa kwa lugha nyingine ni viongozi tu.

Kama kila mjumbe akibeba familia yake tu yenye wanafamilia 4 wenye uwezo wa kupiga kura on average (Baba, Mama, watoto Wawili) zitakuwa kura karibu milioni 10 au zaidi.. bado wanaoitwa wnaachama wa CCM, bado mashabiki, nk nk.. subiri utaona dissapointmemt itakavyokiwa kubwa... watapost misururu kwa misururu ya wapiga kura ili 'kujustfy' na hata wakiongeza kura zaidi za maruhani mtu wala asilalamike...
Kwa bongo sababu kubwa ni hizi:
1. VYOMBO VYA ULINZI KUWA SEHEMU YA WATAWALA.
2. Kutumia nguvu kuliko maarifa,
3. Kutokuwa na checks and balance kwa vyombo vya usalama.

Nani wa kuwasimamia, kuwahoji na kuwadhibiti, kwa Tanzania wanajiongoza, wanajihoji na kujidhibiti wenyewe, don't expect miracles, watalima watu risasi and nobody will be answerable.
 
Kuhusu turnout kuwa ndogo hii ni hadithi tu; tuliona uchaguzi wa CCM wa ndani wa wabunge na madiwani namna ambavyo zaidi ya wajumbe wa mikitano mikuu kwenye ngazi mbalimbali zaidi ya Million tatu walivyojitokeza kupiga kura.. hawa kwa lugha nyingine ni viongozi tu.

Kama kila mjumbe akibeba familia yake tu yenye wanafamilia 4 wenye uwezo wa kupiga kura on average (Baba, Mama, watoto Wawili) zitakuwa kura karibu milioni 10 au zaidi.. bado wanaoitwa wnaachama wa CCM, bado mashabiki, nk nk.. subiri utaona dissapointmemt itakavyokiwa kubwa... watapost misururu kwa misururu ya wapiga kura ili 'kujustfy' na hata wakiongeza kura zaidi za maruhani mtu wala asilalamike...
Turnout ya kujiandikisha kwenye daftari la kupiga kura tu haikuwa nzuri, badala yake wakaamua kupika takwimu(IMO). Kuna namna nyingi za kufikisha ujumbe, binafsi sidhani kama wapiga kura watakuwa kwenye ile misururu tuliyozoea kuiona kila mwaka wa uchaguzi.
 
Back
Top Bottom