GE2025 Kwanini maandamano ya 29 October yatafeli vibaya sana

GE2025 Kwanini maandamano ya 29 October yatafeli vibaya sana

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
MAANDAMANAO YA 29OCT YATAFELI VIBAYA MAPEMA SANA KUTOKANA NA SABABU KUU ZIFUATAZO;


Anaandika, Robert Ng'apos Heriel
Mtibeli


1️⃣ Ukosefu wa Miundombinu ya Kiufanisi.


Maandamano makubwa yenye lengo la mabadiliko ya utawala yanahitaji:


a) Kamati za mipango (planning committees)
Hizi kamati naona hazipo. Ukimfuatilia Mange Kimambi na Maria Sarungi ambao ndio vinara wa maandamano haya unagundua hawana kamati zozote zaidi ya vikao vyote vinafanyika mitandaoni na inakuwa live.
Kamati ndio msingi mkuu wa goo organization na mobilization ya maandamano haya. Kama hazipo atafanikiwa vipi? Embu msaidieni Mtibeli aelewe.


b) Mfumo wa mawasiliano ulio salama,
Udukuzi, kufuatiliwa kuliko kupitiliza, usaliti wa mawasiliano ndani ya wenye nia ya kuandamana. Hayo yote yatakwamisha maandamano.


c) Mpangilio wa uongozi wa ngazi mbalimbali (national → regional → district → ward).
Unaweza kujiuliza kama wewe ni muandamanaji. Kwenye kata au mtaa wako kuna mfumo wowote wa kuyaratibu ili yatokee. Au ndio upo pekeako kwenye actual ground lakini mtandaoni ndio upo na na wenzako?
Tumia hiyo kama scale yako.


Mazingira ya Tanzania ya sasa, upinzani au wanaharakati wengi hawana mtandao thabiti wa ndani (grassroot network).
Hii inamaanisha hawana uwezo wa kuunganisha watu hata Laki moja kwa wakati mmoja bila kutambulika mapema.
Serikali inamiliki taasisi zote za mawasiliano, usalama, na inafanya doria usiku na mchana katika mitandao ya kijamii, hivyo hufahamu mipango kabla haijatekelezwa.
Kwa mantiki ya kiintelijensia, maandamano hayo yatakufa kabla hayajaanza, kwa sababu mpangilio wake utavujishwa na kusambaratishwa mapema.


2️⃣ Ukosefu wa Uratibu wa Malengo.


Maandamano yenye mafanikio lazima yawe na lengo moja linaloeleweka na kukubalika kitaifa.
Lakini maandamano haya yana malengo zaidivya moja yanayokinzana, mfano;


a). Kupinga uchaguzi,
b). Kuiondoa serikali iliyoko madarakani kumaanisha kuindoa CCM
c) Kupinga utekaji na mauaji. Wasiojulikana. Na sababu zingine.


Lengo la kwanza ni la kisiasa (kupinga uchaguzi)
lakini la pili ni la mapinduzi (kuiondoa serikali ya Samia madarakani) ambalo kisheria na kiusalama linachukuliwa kama uhaini au uasi.
Lengo la tatu ni la kijamii na haki za binadamu za msingi yaani haki ya kuishi. (Hili lingeunganisha watu wengi zaidi).


Hivyo, wapo wanaoamini wanapigania haki za uchaguzi, na wapo wanaoamini ni vita dhidi ya serikali. Na wapo wanaoamini wanatetea haki za binadamu za kuishi kwa waliotekwa na kuuawa na kutojulikana walipo.
Kukosekana kwa umoja wa tafsiri ya malengo kunafanya maandamano hayo yasifanane kihoja, kimkakati, wala kiitikadi, hivyo yatakosa mwelekeo mapema.


3️⃣ Udhaifu wa Uongozi wa Harakati.


Harakati yoyote ya kisiasa inahitaji:


a) Kiongozi mwenye karisma,
Najaribu kuangalia nani ni kiongozi aliyenyuma ya haya maandamano mwenye ushawishi. Kama ni Tundu Lisu yupo zake gerezani anapambana na kesi yake ya mchongo.


b) Mtu anayeaminika na umma,
Mwenye uwezo wa kujenga hadithi ya matumaini, hadithi zenye kuchochea chuki ya wananchi kwa serikali. Humphrey Polepole naye alitoa matumaini lakini amekamatwa dakika ya sabini ya mchezo kipindi cha pili.


Tanzania kwa sasa, licha ya kuwa na wanasiasa wa upinzani, hakuna kiongozi mmoja anayekubalika kitaifa kama sauti ya mabadiliko ya kweli.
Wengi wamechoka, wamegawanyika au wamo katika mikakati ya kisiasa ya muda mfupi. Na serikali inajaribu kila njia kuwavunja vunja na kuwagawanya kadiri inavyowezekana. Jana mumemwona Ezekiel Wenje. Ni kwamba wanawakatisha tamaa na kuwavunja moyo watanzania.


Bila kiongozi thabiti mwenye command structure, watu wanakuwa kama kundi lisilo na kichwa. Yaani kundi linajiendea endea bila mwelekeo. Hayatakuwa na tofauti na vuguvugu la Luddism kwa wale mliosoma Advance History 2.
Ndiyo maana kwa kitaalamu, maandamano kama haya huanza kwa makelele mitandaoni na kufa siku ya tukio. Haitakuwa mara ya kwanza.


4️⃣ Udhibiti Mkali wa Vyombo vya Usalama.


Kitaalamu, Tanzania ni nchi yenye mfumo wa ulinzi na usalama ulio wa kiintelijensia zaidi kuliko wa nguvu.
Taasisi kama:


I). TISS (Usalama wa Taifa),


ii) Jeshi la Polisi,


Iii) JWTZ (Jeshi la Wananchi)
Na vitengo vya cyber intelligence
vina uwezo mkubwa wa kutambua, kuvuruga, au kuzuia matukio kabla hayajafanyika.


Kwa mfano:


a) Mawasiliano ya Wapanga maandamano hufikiwa kupitia “surveillance”,


b) Viongozi wa maandamano hufuatiliwa kimyakimya,


c) Wengine huchukuliwa “preventive custody” kabla ya siku ya tukio.
Ndio hao unasikia kila siku wanakamatwa mara leo huyu kesho yule.
Wahamasisha maandamano mtandaoni au watu wenye mrengo huo nao huchukuliwa mapema kabisa kabla ya siku husika.
Mtu kama John Heche, John Mnyika, na wenzake hawawezi kuwa uraiani kufikia tarehe 29.


Watahifadhiwa kwa muda huku wakipewa usumbufu kidola mpaka upepo utakapotulia wataachiwa.


Hii inaondoa uwezekano wa maandamano kuanza kwa wingi au kwa ufanisi.
Kitaalamu, tunaita hii “preemptive disruption model” njia ambayo huzima uasi kabla haujaanza.


5️⃣ Hofu ya Kijamii.


Wengi wetu Watanzania ni watu wa amani tusiopenda vurugu, na tumelelewa kwenye misingi ya “amani ni bora kuliko vurugu, au funika kombe mwanaharamu. Apite".
Kisaikolojia, jamii imejengwa kuwa risk-averse (uepukaji wa hatari).
Hivyo, hata kama wanakubaliana kimoyomoyo na hoja za maandamano, wengi hawatashiriki hadharani.


a) Mfumo wa kiutamaduni, kiimani (dini), na kijamii unahimiza utii kwa mamlaka.
Wengi wataishia kusema “Mungu ataingilia” "Mungu atajibu", "tumuachie Mungu" au “Tusubiri uchaguzi mwingine”, hivyo kuua nguvu ya umoja wa kuandamana.


Kwa hivyo, uungwaji mkono utakuwa wa moyoni na mitandaoni lakini si wa miguu kwa mguu sako kwa bako. Watu wanakubaliana mtandaoni, lakini hawatokei barabarani.


6️⃣ Udhibiti wa Habari na Mitandao.


Serikali ina uwezo wa:


a) Kufunga mitandao ya kijamii.
Ikifunga mitandao wananchi wangapi wanauelewa wa kutumia VPN na mambo ya kidijitali. Wangapi?


b) Kudhibiti vyombo vya habari,
Media zote, redio zote, na wenye followers wengi watadhibitiwa iwe kinguvu au kwa kupewa pesa kuwatuliza
Si ndio yale mtaishia kumlaumu Millard Ayo wa watu. Atafanya nini?


c) Kuendesha kampeni za kupotosha


Vitengo vya propaganda kwa sasa vipo kazini: hakuna wakati vinatakiwa kufanya kazi kama wakati huu. Propaganda za kupotosha jamii mfano
“Maandamano yamehairishwa,”
“Viongozi wamekamatwa,”
“Maeneo fulani ni hatari.”
" Wanataka kuchafua nchi"
"Wanavuruga amani"
" Wanatumiwa na mabeberu"
" Watanzania ni waoga sana" hii pia ni. Propaganda iliyofanikiwa sana na ambayo kwa sasa watawala huipigia msumari ili iwe ni kama culture ya watanzania


Hii hufanya hata waliokuwa tayari kushiriki wakose maelekezo sahihi na motisha ya pamoja. Kwa mtazamo wa psychological operations (PSYOPS), hii ni silaha ya kisaikolojia inayotawanya umoja wa wanaharakati. Niliwaambia Saikolojia na soshiolojia ni msingi mkuu wa serikali kutawala watu.


Matokeo yake, maandamano hufa kabla ya saa sita mchana, na wale wachache waliotoka hukamatwa bila upinzani. Kisha baadaye watu huanza kulaumiana. Hoo hamjatoka. Nyie waoga n.k.


Kufikia hapa TaikonMaster sina la ziada. Nimejaribu kujadili. Kwa uhalisia na kwa kuzingatia siasa za nchi yetu, Saikolojia ambayo ninaifahamu kwa sehemu, intelijensia ambayo naifahamu kidunchu, na kwa kutumia falsafa (mantiki na hoja).
So kama utakuja kichwa kichwa na kutoa matusi yako sitaingilia uhuru wako na jinsi unavyoelewa mambo.


Nawatakia sikukuu njema ya Nyerere day.


Acha nipumzike sasa.

TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
Haya maandishi yameandikwa kama na think tank was UVCCM.

Maandamano yasingekuwa na mipango thabiti, usingepost hapa, watu wasingetishwa.

Otherwise taarifa na elimu inafika
 
Turnout ya kujiandikisha kwenye daftari la kupiga kura tu haikuwa nzuri, badala yake wakaamua kupika takwimu(IMO). Kuna namna nyingi za kufikisha ujumbe, binafsi sidhani kama wapiga kura watakuwa kwenye ile misururu tuliyozoea kuiona kila mwaka wa uchaguzi.
Nadhani Turnout ya kujiandikisha ilikuwa nzuri tu mkuu; nilipita sehemu kigamboni nilikuta msururu mrefu kinoma na wengine wakiondoka...

Pia vijijini kule watu wemgi tu wataenda kupiga kura: kuna maeneo machache ya mjini ndiyo yanaweza kuwa na shida...
 
Haya maandishi yameandikwa kama na think tank was UVCCM.

Maandamano yasingekuwa na mipango thabiti, usingepost hapa, watu wasingetishwa.

Otherwise taarifa na elimu inafika
Hii ndio shida ya timu maandamano; hamchukui constuctive ideas ili mboreshe. Kazi kubwa ni attack and attck kila mtu anaefanya reasoning iliyo tofauti na nyie.
 
Maelekezo Maalum kuhusu tarehe 29 Oktoba.

Siku hiyo kazi ni rahisi sana

Viongozi wa CCM tunaishi nao mitaani; Nyumba zao zipo mitaani kwetu, mali zao zipo mitaani kwetu.

Ofisi za CCM zipo mitaani kwetu. Ofisi za Umma nazo zipo mitaani kwetu

VItuo vya kupigia kura vipo mitaani kwetu

Mawaziri, Wabunge na Madiwani tunaishi nao mitaani kwetu, familia zao na ndugu zao tunaishi nao mitaani kwetu. Machawa na mali zao tunaishi nao mitaani kwetu.

Ndugu watanzania, mafuta ya taa, petroli na viberiti havijawahi kuwa adimu.

Tukafanye kazi iliyotukuka hiyo Oktoba 29 hadi hawa Mafisadi watuheshimu na wakome kutuchezea na kutuua.

Share na mwenzako
Watu walishakujua vzr sana.
WE HAUNA MADHARA YOYOTE YALE!
 
1. Vyombo vya ulinzi sio Alliens. Ni watanzania wenzetu. Kutumia nguvu kutokana watanzania waliowengi wamewapa nguvu hiyo hao wanausalama na wanaulinzi.
Jeshi halizidi wetu milioni moja. Linakuwaje na nguvu dhidi ya watu milioni 60?

Hayo maandamano wakitoka watu laki tano tuu jeshi linatulia na nguvu hazitatumika.

Kusema jeshi kutumia nguvu ni kisingizio tuu
Unafikiri maeneo mengine waliofanikiwa jeshi halikutumia nguvu?

2. Nguvu inakuwa na nguvu kwa watu wachache lakini sio kwa watu wengi
Lawama zote kwa jeshi wakati ishu hapo ni raia wenyewe
Umeelewa nilivyosema hakuna checks and balance kwenye jeshi letu mkuu? Yaani kesi ya nyani unampa ngedere asuluhishe, unategemea nini?

Ukiona nchi nyingine nyingi zinafanya peaceful demonstrations kuna mambo yapo kisheria na hata watu wakiandamana huoni jeshi la polisi likijichukulia sheria mkononi, kwetu haipo. Unaandamana mbele ya polisi anayeweza kushoot risasi za moto na kuuwa watu kadhaa bila yeye kuchukuliwa hatua zozote za kisheria, hii ipo kwetu na baadhi ya nchi chache duniani.

Halafu ujue tu polisi wanachohitqji ni equipment, wala sio idadi. 10,000 wanatosha kabisa kuifanya Dar ikae sawa wakiwa na right artillery/machinery. Kama unadhani kwa jeshi letu ni rahisi kuandamana basi toka peacefully uandamane ndio utaelewa jeshi letu linatumia akili, mabavu, kulinda maslahi ya watanzania au kundi fulani la watu.

Unaweza kumlaumu mtanzania kuwa mwoga na ukasahau weledi wa jeshi letu kumlinda mtanzania vs mtawala.
 
Kila mtu ataandamana kwa style yake.

1. Wengine watatoka kuandamana
2.Wengine wataandamana kwa kukaa ndani hawatapiga kura
3.wengine wataandamana kulinda raia wasiandamane badala ya kwenda kulinda usalama wa vituo vya kupigia kura.
4.wengine wataandamana namagari na maspika kuhamasisha watu watoke wakapige kura.

Yani kila mtu ataandamana kwa style yake sio lazima wote waandamane kwa aina moja.
 
Nadhani Turnout ya kujiandikisha ilikuwa nzuri tu mkuu; nilipita sehemu kigamboni nilikuta msururu mrefu kinoma na wengine wakiondoka...

Pia vijijini kule watu wemgi tu wataenda kupiga kura: kuna maeneo machache ya mjini ndiyo yanaweza kuwa na shida...
Ngoja tuone mambo yatakavyokuwa, ila vyovyote vile Sa100 amejua watanganyika hawamtaki, inaweza isiwe 80% ila walau 50-60% hawapo sawa na uongozi wake.
 
Niliwasikia baadhi ya organisers huko mitandaoni wakisema waandamanaji waanze kwa kuchoma vituo vya mafuta pale Ubungo na sehemu nyingine ati anadai kuwa ni vya Abduli na Kikwete.

Mimi ni muumini wa maandamano ya AMANI siungi mkono kauli hiyo.
Lazima tutiane adabu kidogo

Maelekezo Maalum kuhusu tarehe 29 Oktoba.

Siku hiyo kazi ni rahisi sana

Viongozi wa CCM tunaishi nao mitaani; Nyumba zao zipo mitaani kwetu, mali zao zipo mitaani kwetu.

Ofisi za CCM zipo mitaani kwetu. Ofisi za Umma nazo zipo mitaani kwetu

VItuo vya kupigia kura vipo mitaani kwetu

Mawaziri, Wabunge na Madiwani tunaishi nao mitaani kwetu, familia zao na ndugu zao tunaishi nao mitaani kwetu. Machawa na mali zao tunaishi nao mitaani kwetu.

Ndugu watanzania, mafuta ya taa, petroli na viberiti havijawahi kuwa adimu.

Tukafanye kazi iliyotukuka hiyo Oktoba 29 hadi hawa Mafisadi watuheshimu na wakome kutuchezea na kutuua.

Share na mwenzako
 
Lazima tutiane adabu kidogo

Maelekezo Maalum kuhusu tarehe 29 Oktoba.

Siku hiyo kazi ni rahisi sana

Viongozi wa CCM tunaishi nao mitaani; Nyumba zao zipo mitaani kwetu, mali zao zipo mitaani kwetu.

Ofisi za CCM zipo mitaani kwetu. Ofisi za Umma nazo zipo mitaani kwetu

VItuo vya kupigia kura vipo mitaani kwetu

Mawaziri, Wabunge na Madiwani tunaishi nao mitaani kwetu, familia zao na ndugu zao tunaishi nao mitaani kwetu. Machawa na mali zao tunaishi nao mitaani kwetu.

Ndugu watanzania, mafuta ya taa, petroli na viberiti havijawahi kuwa adimu.

Tukafanye kazi iliyotukuka hiyo Oktoba 29 hadi hawa Mafisadi watuheshimu na wakome kutuchezea na kutuua.

Share na mwenzako
Mimi siungi mkono Riots bali nitaunga mkono maandamano ya AMANI ambayo yako kikatiba.
 
Kila mtu ataandamana kwa style yake.

1. Wengine watatoka kuandamana
2.Wengine wataandamana kwa kukaa ndani hawatapiga kura
3.wengine wataandamana kulinda raia wasiandamane badala ya kwenda kulinda usalama wa vituo vya kupigia kura.
4.wengine wataandamana namagari na maspika kuhamasisha watu watoke wakapige kura.

Yani kila mtu ataandamana kwa style yake sio lazima wote waandamane kwa aina moja
 
Lazima tutiane adabu kidogo
shutterstock_61229197-1024x682.jpg

😂😂😂
 
Kila mtu ataandamana kwa style yake.

1. Wengine watatoka kuandamana
2.Wengine wataandamana kwa kukaa ndani hawatapiga kura
3.wengine wataandamana kulinda raia wasiandamane badala ya kwenda kulinda usalama wa vituo vya kupigia kura.
4.wengine wataandamana namagari na maspika kuhamasisha watu watoke wakapige kura.

Yani kila mtu ataandamana kwa style yake sio lazima wote waandamane kwa aina moja.

Hiki ndicho nimekizungumzi hapa kama ulisoma vizuri
Ndio sababu ya hayo maandamano kufeli vibaya
 
Back
Top Bottom