Moja ya couple ninayoifahamu ni ndugu na huyo Moi lol! nadhani tangu siku ya harusi yao sijawahi ona wameongozana popote
labda ni sharti la mganga je!
Moja ya couple ninayoifahamu ni ndugu na huyo Moi lol! nadhani tangu siku ya harusi yao sijawahi ona wameongozana popote
kwani uongo?
Uongo ndio, sie hatutiani..... moyo.
hahahahahahaaa mnatia hurumaaa
Unadhalilisha huruma ujue? Nani anayeweza kutia huruma?
Ntake radhi... mie sijui kutia huruma. Najua kutia vingine LOL
Shimo La Panya Halifunikwi Kwa Mkate
Si kweli
Mm nikiongozana na wife nikimtolea macho demu mwingine tukirudi home ANANIPIGA bana
kaka niko mjini aisee, tuonane... nimekupigia jana lakini nehi che............. nilikua napata "mnafu" pale port view
Hilo ni tatizo kwa wanandoa kadhaa sijui kwanini tu. Hata mimi nimeshuhudia wanandoa wakipinga vikali suala la kuongozana, nadhani huwa wana ajenda ya siri hapo.
Katika maswala yetu ya umoja wa kusaidiana na kufarijiana katika kikundi chetu likaletwa wazo la kila mtu aje na mke wake siku ya sherehe ya kikundi chetu... lakini miongoni mwa wadau tulionao katika kikundi wamepinga vikali na kudai kwamba hakuna haja ya mtu kuja na mkewe hapa.. mmoja akadai yeye ndani ya miaka mitano hajawahi kuongozana na mkewe kwenda maeneo yoyote yale... jamani kwa nini iwe noma kuongozana na mkeo kwenye shughuli mbalimbali kama harusini, msibani hata kwenye nyumba za ibada...........
Hahahahahaahahaaa!! umenifanya nicheke, kuna kaka mmoja naye alikuwa anajitapa ile mbaya, mm kwenye mawazo yangu nikadhani kaoa mwarabu, jinsi alivyokuwa anamsifia mkewe, bahati mbaya kukawa na maonyesho ya SYRIAN hapo Diamond Jubilee, tukawa tumekwenda wanawake wengi wa ofisini, Hamadi huyu hapa tukamwona yupo na mkewe, akabaki anababaika, kumtambulisha, na mm kwa umbea nikamuuliza kujua, ndipo alipopata nguvu ya kututambilisha. kwa kweli tulipoachana kila mtu alicheka, Loh!Hawajiamini hao.
Utakuta mtu anajitapa ya nyumbani kwake ila ukiona picha tu ya mkewe unaweza ukapata mkanda mzima.
Tujiamin jamani na tuache kujinadi mwisho wa siku hayo yanawakuta baadhi yenu.
hahahahahah hii nimeipenda...ndoa za ghafla hizo......na hasa cc walume.....umeshamchakaza demu wako ambae ndo mkeo,, then unamuona kama kiroba.....hapo ni wanawake kuwa imara, hata kwa kulazimisha,, huko lazima twende wote...full stop .
Katika maswala yetu ya umoja wa kusaidiana na kufarijiana katika kikundi chetu likaletwa wazo la kila mtu aje na mke wake siku ya sherehe ya kikundi chetu... lakini miongoni mwa wadau tulionao katika kikundi wamepinga vikali na kudai kwamba hakuna haja ya mtu kuja na mkewe hapa.. mmoja akadai yeye ndani ya miaka mitano hajawahi kuongozana na mkewe kwenda maeneo yoyote yale... jamani kwa nini iwe noma kuongozana na mkeo kwenye shughuli mbalimbali kama harusini, msibani hata kwenye nyumba za ibada...........
Aisee mi hapana kujua. Nitafutane kwa voda, tigo ilibuma. Pole kwa maswahibu swahiba, alinifahamisha kijana wa bakery. Bahati mbaya nimepoteza namba zako. Mabaamedi washenzi sana, wanajifanya wanafuta meza baada ya kufakamia mdudu kumbe wanachanganya na simu zetu.kaka niko mjini aisee, tuonane... nimekupigia jana lakini nehi che............. nilikua napata "mnafu" pale port view