Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,097
- 43,309
- Thread starter
- #61
Hivi MKJJ anaweza akaandika barua kama hajaamua?
Nadhani hiyo ni past tense so na kwa maana hiyo aliposema "Ameamua" kwa wakati ule,ina maana kwamba ni jambo ambalo alishalifanyia maamuzi na kulitekeleza,unless kuna technicallities hapo mtueleze...Nilivyoelewa mimi hilo alilizungumzia kama past tense.
hapa mnacheza na lugha. As a matter of fact ukiisoma vizuri ni kama anasema hivi:
"Nimeamua kujiunga na timu ya Mpira" - Hii ina maana ameshajiunga au ni jambo ambalo atalitelekeza mara? Kama angekuwa tayari amejiunga anasema "nimejiunga na timu ya mpira" na kama kuelezea kitu ambacho kimekwisha fanyika angesema "baada ya kutafakari bla bla bla, niliamua kumuandikia Rais Barua ya kutaka kujiuzulu, naye amekubali kujiuzulu kwangu"!
Jmushi (happy birthday); huwezi kusema "nimeamua kumwandikia" ukamaanisha wakati uliopita. Unapoweka "kumwandikia" tendo hilo haliwezi kuwa limeshatokea ila ina maana linatokea hivi punde au linatokea as we speak.
Wakati Lowassa anazungumza Bungeni juu ya huu uamuzi wake, hakuna mtu mwingine aliyekuwa anajua isipokuwa bila ya shaka mke wake mama Lowassa. Uliza mtu yeyote akuambie, siyo Kikwete, siyo Spika, bali Lowassa labda na mtu mwingine (beside rais na spika).