Kwanini Kikwete alikataa kumleta Ballali?

Kwanini Kikwete alikataa kumleta Ballali?

Bunge haliwezi kupiga "kura ya kutokuwa na imani na Rais" linaweza kufanya hivyo kumuhusu Waziri Mkuu.

Nakumbuka jana nilikuuliza kuhusu option ya jeshi.
Maana yangu halisi ilikuwa ni Rais kuivunja serikali na kuikabidhi nchi kwa jeshi wakati wa uchunguzi wa EPA na maandalizi ya uchaguzi wa 2010 ikiwa ni pamoja na uchaguzi huru na tume huru itakayosimamia shughuli zote za uchaguzi huru na wa haki ikiwa ni pamoja na uwezekano wa kuendelea na uchunguzi bila ya watu kuwa na kinga ya serikali ama uongozi wowote ule kwasababu muda uliobaki ni mfupi.
Kusema ni demokrasia halafu tutegemee CCM ipigwe chini kirahisi inaweza ikawa wishfull thinkin.
Pesa wanazo nyingi sana tu.
Na pia ni heri jeshi lisimamie kwasasa kwasababu wanaweza kusubiri halafu machafuko yakaja kutokea na watu kupoteza maisha yao.
Ni vizuri kukinga badala ya kutibu.
CCM ikishinda kuna uwezekano wa machafuko.
MKJJ naomba unieleweshe hapo kuhusu option ya jeshi.
 
Nakumbuka jana nilikuuliza kuhusu option ya jeshi.
Maana yangu halisi ilikuwa ni Rais kuikabidhi nchi kwa jeshi wakati wa uchunguzi na maandalizi ya uchaguzi wa 2010 kwasababu muda uliobaki ni mfupi.
Kusema ni demokrasia halafu tutegemee CCM ipigwe chini kirahisi inaweza ikawa wishfull thinkin.
Pesa wanazo nyingi sana tu.
Na pia ni heri jeshi lisimamie kwasasa kwasababu wanaweza kusubiri halafu machafuko yakaja kutokea na watu kupoteza maisja yao.
Ni vizuri kukinga kbadala ya kutibu.
MKJJ naomba unieleweshe hapo kuhusu option ya jeshi.



Jeshi la CCM.Jeshi la Chama Kimoja.Jeshi liko kwa maslahi ya CCM.Unaongelea jeshi lipi kwa mkuu wa majeshi yupi? Kwa wana jeshi wapi ambao hawajui maana ya vyama vingi ? They talk openly kwamba CCM ikipigwa chini hawakabidhi madaraka .Mfano ni Zanzibar .Bado una imani na jeshi na usalama na Polisi ?
 
Jeshi la CCM.Jeshi la Chama Kimoja.Jeshi liko kwa maslahi ya CCM.Unaongelea jeshi lipi kwa mkuu wa majeshi yupi? Kwa wana jeshi wapi ambao hawajui maana ya vyama vingi ? They talk openly kwamba CCM ikipigwa chini hawakabidhi madaraka .Mfano ni Zanzibar .Bado una imani na jeshi na usalama na Polisi ?

Ni ukweli kuwa huu uchunguzi wa mafisadi hauwezi kuwa wa haki under the same adm kwa sababu wameshaonyesha hivyo.
Na hatuwezi kuguarantee kwamba hawatashinda uchaguzi mkuu ujao..Unakumbuka kina Chenge na Lowassa walivyopokelewa kishuja huko majimboni mwao na pia sasa Lowassa bado anaendelea kutuwakilisha huko London kwenye miradi ya serikali.
Sasa haki ya Mtanzania itapatikana vipi Lunyungu?
 
Ni ukweli kuwa huu uchunguzi wa mafisadi hauwezi kuwa wa haki under the same adm kwa sababu wameshaonyesha hivyo.
Na hatuwezi kuguarantee kwamba hawatashinda uchaguzi mkuu ujao..Unakumbuka kina Chenge na Lowassa walivyopokelewa kishuja huko majimboni mwao na pia sasa Lowassa bado anaendelea kutuwakilisha huko London kwenye miradi ya serikali.
Sasa haki ya Mtanzania itapatikana vipi Lunyungu?

naomba kunukuu; " SIASA NI MCHEZO MCHAFU' mwisho wa kunukuu
 
Jamani, Rais hawezi kuvunja bunge kwa kujisikia tu. Hawezi kuamka asubuhi moja na kusema "Bunge sucks" halafu akalivunja.

a. Rais akivunja Bunge na yeye anapoteza Urais wake kwani yeye ni sehemu ya Bunge.
b. Bunge likileta mashtaka dhidi ya Rais na kumvua Urais, Bunge linaendelea kuwepo na Makamu wa Rais anachukua nafasi.
c. Bunge likikataa kupitisha mswada au bajeti ya serikali linaonesha kutokuwa na imani na serikali hivyo Bunge linavunjika, Rais anapoteza Urais na wote wanarudi kwa wananchi. Kwa wanaokumbuka watakumbuka Nyerere aliwahi kuwapiga mkwara wabunge hili kuwa wasipopitisha sheria fulani hivi basi watarudi kwa wananchi.

Kuna namna nyingine yoyote ile ambayo Bunge linaweza ku dissolve zaidi ya pale wanapoikataa budget?
Ni mazingira gani mengine yatakayowezesha kulivunja Bunge ili serikali nayo ikitoe zake na kila mtu arudi kwa wananchi?
Nimeipenda sana hiyo kauli ya kurudi kwa wananchi!
Tunataka warudi ili tuanze upya!
 
Nakumbuka jana nilikuuliza kuhusu option ya jeshi.
Maana yangu halisi ilikuwa ni Rais kuivunja serikali na kuikabidhi nchi kwa jeshi wakati wa uchunguzi wa EPA na maandalizi ya uchaguzi wa 2010 ikiwa ni pamoja na uchaguzi huru na tume huru itakayosimamia shughuli zote za uchaguzi huru na wa haki ikiwa ni pamoja na uwezekano wa kuendelea na uchunguzi bila ya watu kuwa na kinga ya serikali ama uongozi wowote ule kwasababu muda uliobaki ni mfupi.
Kusema ni demokrasia halafu tutegemee CCM ipigwe chini kirahisi inaweza ikawa wishfull thinkin.
Pesa wanazo nyingi sana tu.
Na pia ni heri jeshi lisimamie kwasasa kwasababu wanaweza kusubiri halafu machafuko yakaja kutokea na watu kupoteza maisha yao.
Ni vizuri kukinga badala ya kutibu.
CCM ikishinda kuna uwezekano wa machafuko.
MKJJ naomba unieleweshe hapo kuhusu option ya jeshi.

Nijibu hivi: Hii option unayopendekeza ya utawala wa kiraia kujivua madaraka na kuwapa wanajeshi utawala wa nchi iko kwenye Katiba ya nchi gani? Huwezi kwenda na kutunga taratibu au mazoea nje ya Katiba. Katiba iko wazi kabisa, Rais akijiuzulu nani anafuatia, Bunge likivunjika nini kifanyike n.k Katiba yetu ina utaratibu ulio wazi kabisa wa kubadilisha madaraka.

Kuna njia za kawaida na njia zisizo za kawaida.

Njia ya Kawaida - Ni sanduku la kura ambapo wananchi wanachagua nani awaongoze na nani asiwaongoze. Hili hufanyika kila baada ya miaka mitano au pale inapotokea uchaguzi mdogo isipokuwa kwenye kiti cha Urais.

Njia zisizo za kawaida:
- Ni njia ya mahakama (kwa wabunge madiwani na viongozi wengine). Hii ya mahakama haimhusu Rais kwani akishatangazwa kuwa Rais hakuna uwezekano wa kufungua kesi dhidi yake ya kupinga uchaguzi huo kwenye mahakama yoyote. (hatupendi sheria hiyo tubadili Katiba)

- Njia ya Kujiuzulu/kustaafu - Hapa ni pale kiongozi anapolazimika kuachia nafasi yake aidha kwa sababu fulani au kutokana na umri au afya. Kiongozi mwingine ataingia madarakani. Hili pia linahusu Waziri Mkuu akijiuzulu taratibu za Kikatiba zinafuata kama ilivyotokea Februari.

- Kiongozi anapokufa - taratibu za kujaza nafasi yake zipo wazi. Rais akifa madarakani Makamu anachukua Urais, Makamu akifa au kupanda kuwa Rais Basi makamu anachaguliwa na Bunge linafanya kikao cha dharura kumpitisha. Waziri Mkuu akifa Baraza la Mawaziri linavunjika na utaratibu wa kikatiba kujaza nafasi unafuatwa.

n.k

Nakushauri usome Katiba utapata majibu ya maswali yako maana nitajikuta nafanya kazi ambayo mtu yeyote anaweza kufanya nayo ni kusoma Katiba kwani majibu yapo.
 
Nijibu hivi: Hii option unayopendekeza ya utawala wa kiraia kujivua madaraka na kuwapa wanajeshi utawala wa nchi iko kwenye Katiba ya nchi gani? Huwezi kwenda na kutunga taratibu au mazoea nje ya Katiba. Katiba iko wazi kabisa, Rais akijiuzulu nani anafuatia, Bunge likivunjika nini kifanyike n.k Katiba yetu ina utaratibu ulio wazi kabisa wa kubadilisha madaraka.

Kuna njia za kawaida na njia zisizo za kawaida.

Njia ya Kawaida - Ni sanduku la kura ambapo wananchi wanachagua nani awaongoze na nani asiwaongoze. Hili hufanyika kila baada ya miaka mitano au pale inapotokea uchaguzi mdogo isipokuwa kwenye kiti cha Urais.

Njia zisizo za kawaida:
- Ni njia ya mahakama (kwa wabunge madiwani na viongozi wengine). Hii ya mahakama haimhusu Rais kwani akishatangazwa kuwa Rais hakuna uwezekano wa kufungua kesi dhidi yake ya kupinga uchaguzi huo kwenye mahakama yoyote. (hatupendi sheria hiyo tubadili Katiba)

- Njia ya Kujiuzulu/kustaafu - Hapa ni pale kiongozi anapolazimika kuachia nafasi yake aidha kwa sababu fulani au kutokana na umri au afya. Kiongozi mwingine ataingia madarakani. Hili pia linahusu Waziri Mkuu akijiuzulu taratibu za Kikatiba zinafuata kama ilivyotokea Februari.

- Kiongozi anapokufa - taratibu za kujaza nafasi yake zipo wazi. Rais akifa madarakani Makamu anachukua Urais, Makamu akifa au kupanda kuwa Rais Basi makamu anachaguliwa na Bunge linafanya kikao cha dharura kumpitisha. Waziri Mkuu akifa Baraza la Mawaziri linavunjika na utaratibu wa kikatiba kujaza nafasi unafuatwa.

n.k

Nakushauri usome Katiba utapata majibu ya maswali yako maana nitajikuta nafanya kazi ambayo mtu yeyote anaweza kufanya nayo ni kusoma Katiba kwani majibu yapo.

Nashukuru kwa maelezo..Samahani kama swali limekuwa la kijinga!

Kumbuka sijasema mtu ajivue madaraka..Lakini kumeshakuwa na matukio ya jeshi la nchi kusimamia haki kati ya pande mbili za kisiasa ili kuepusha machafuko.

Njia za kawaida na zisizokuwa za kawaida...Then...

Ina maana jeshi likiona kuwa kuna hatari ya nchi kuingia kwenye machafuko halina uwezo wa kuingilia kati? Na njia hiyo ni ya kawaida ama si ya kawaida?

Naelewa upande wa maelezo yako ya kikatiba..Lakini hauonyeshi ile urgency ya namna ambayo haki inaelekea kupotea kwa watanzania!
Kama ikitokea CCM wakashinda...Then yatakuja kama yale ya wazimbabwe ama wakenya.
 
Itakuwa ni sheria ya kinamna gani hiyo ambayo ilimweka Ballali kwenye kundi la wasiohitajika either kama mashahidi ama mtuhumiwa?
Haukumbuki kuwa barua iliandikwa na Mama Meghji kwa Ballali kuwa pesa ni za usalama wa taifa?
Ballali si alimwambia Mama kuwa Kikwete ndiye aliyetaka iwe hivyo kuwa barua iandikwe kutoka serikalini kuwa hizo pesa zitatumika kwa ajili ya usalama wa taifa?
Na baada ya kushtukiwa Mama si aliandika barua ya pili ili kui cancel ile ya kwanza na kusema eti Ballali alimdanganya baada ya yeye mama mwenyewe kugundua kuwa si Kikwete aliyetoa hiyo Rhuksa ya pesa kutolewa?
Sasa ili tujue kama si Kikwete aliyemwambia Ballali aruhusu hizo pesa then kwanini hakuhojiwa wala Kikwete kutaka ahojiwe?
Si ndio ule mchezo wa kinyume nyume kuanza kwenye hukumu halafu ndio uchunguzi?
Pesa kuanza kurudishwa si ndio kuanza na hukumu halafu uchunguzi si ndio baaada ya jambazi kufa?
Ndio sheria zetu hizo huh?

Marekebisho kwenye issue ya Mama Meghji baada ya mazungumzo na MKJJ ambaye alishawahi kumuhoji mama Meghji.

Kwa maelezo kamili na kama nilivyoelewa ni kuwa Mama Meghji ali approve uoza wa kifisadi wa Basil Pesambili Mramba...Halafu baadae akaandika barua ya pili kuipinga ile barua yake ya kwanza iliyokubaliana na kauli ya Mramba kuwa pesa za EPA zilikuwa za usalama wa mafisadi mara baada ya Mama kuwa na taarifa za audit querry.
 
jeshi letu kwanza halioni tatizo lolote la machafuko hadi sasa! tanzania haitotokea machafuko leo wala kesho kwa kuibiwa pesa zao na jeshi linajua hivyo!
watanzania hatuko organized enough kufanya machafuko ya kuwa watu wanapinga vitendo vya serikali.....na jeshi linajua hayo
na hata inapokuwa vyenginevyo kama vile zanzibar, unaona jeshi litapendelea upande gani (wa ccm) na wananchi wanaishiwa nguvu, na jeshi linajua hayo.

sasa naona mushi, jeshi usilihusishe kwenye mawazo yako ya kupatikana mageuzi kwa sababu nia wala sababu ya kufanya hivyo hawana
 
jeshi letu kwanza halioni tatizo lolote la machafuko hadi sasa! tanzania haitotokea machafuko leo wala kesho kwa kuibiwa pesa zao na jeshi linajua hivyo!
watanzania hatuko organized enough kufanya machafuko ya kuwa watu wanapinga vitendo vya serikali.....na jeshi linajua hayo
na hata inapokuwa vyenginevyo kama vile zanzibar, unaona jeshi litapendelea upande gani (wa ccm) na wananchi wanaishiwa nguvu, na jeshi linajua hayo.

sasa naona mushi, jeshi usilihusishe kwenye mawazo yako ya kupatikana mageuzi kwa sababu nia wala sababu ya kufanya hivyo hawana

Wewe unalijua Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Hawana hisia za kuibiwa maana wao ni miongoni mwa wanaoishi peponi kwa namna fulani. Kila regime ina takrima kwa wajeshi wetu..regime ya BWM walipewa mitsubishi pick-up nyingiii TZJ (mwenzenu nilizipanda kama daladala ya mwanajeshi huko vijijini), regime hii wamepewa Huyundai nyeusi za kikorea...Kwa hiyo wananchi waibiwe EPA, kwa vile wameshiba, hiyo haja mioyoni mwao haimo kabisaaaa
 
Naelewa upande wa maelezo yako ya kikatiba..Lakini hauonyeshi ile urgency ya namna ambayo haki inaelekea kupotea kwa watanzania!

MKuu MUSHI, urgency nani awe nayo kaka ilhali utawala una rungu kubwa na wananchi wana hofu kuu mioyoni?? Zama za urgency ya kuondokana na regime mbaya Tanzania hazijafika. Baada ya Lowassa, Chenge kuchafuka, wananchi walikuwa na kiu ya kuwapongeza! Kweli kuna urgency ya kubadili regime kwa asilimia kubwa ya watanzania hapo!

Mapambano yaendelee ila yalenge pia kuwasomesha wananchi walio wengi kuona shida inayoikabili nchi hasa pale viongozi wabovu wanapokuwa mdarakani. Na kwa hili ndo tungekazana haswa kulifanikisha.
 
Wewe unalijua Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Hawana hisia za kuibiwa maana wao ni miongoni mwa wanaoishi peponi kwa namna fulani. Kila regime ina takrima kwa wajeshi wetu..regime ya BWM walipewa mitsubishi pick-up nyingiii TZJ (mwenzenu nilizipanda kama daladala ya mwanajeshi huko vijijini), regime hii wamepewa Huyundai nyeusi za kikorea...Kwa hiyo wananchi waibiwe EPA, kwa vile wameshiba, hiyo haja mioyoni mwao haimo kabisaaaa

Na mfano wao halisi ni pale wanapo staafu na kuanza kutangaza nia ya kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM.. unaona ni kiasi gani wame lelewa kiCCM
 
Wakuu nakubaliana na ushauri na mawazo yenu.

Cha muhimu hapa tunataka kauli moja kutoka kwa serikali ili tujue kama tuachane na haya mambo ya Ballali ama la.

Kama wanakataa kuwa hakuwa shahidi wala mtuhumiwa licha ya kuwa ndiye aliyekuwa Kiongozi mkuu wa BOT aliyesimamia uharamia huo...Then tunataka ripoti zote za ukaguzi pamoja na ripoti ya kamati ya EPA aliyoiunda Mh Rais ili sisi wananchi tujue kuwa mashahidi na watuhumiwa ni wepi hao tofauti na Ballali pamoja na wengine 10 waliokuwepo kwenye ile list of shame aliyoitoa DK Slaa kwenye tukio la kihistoria pale kunako viwanja vya mwembe Yanga.
 
Katika haya Maisha usijetegemea kwamba ukiwa nyikani utakutana na Simba ambaye analinda Swala!!! hata siu moja!!! Hili suala zima ni la mafisadi kulindana wao kwa wao...

Hiyo pesa ya EPA mwisho wa siku kashfa ilikuwa inafumukia Ikulu sasa ulitegemea kwamba Kikwete atasema tu huyu Ballali arudi na achunguzwe na ukweli ukijulikana achukuliwe hatua stahili ambazo uhakika ni kwamba Waangukaji wangekuwa wengi..!!!

Ndio hivyo sasa wanasema amekufa...yameisha!!! Hakuhojiwa na Tume ya uchunguzi na yeye akiwa ndio FUNGUO ya hii kashfa nzima. Tutamuomboleza na kama kawaida, ukifa ni kwamba mazuri yooote duniani ni wewe!

Tunaumia sana na Serikali ya Awamu ya Nne!!! Sauti zetu ndio Zitakuwa Ukombozi Wetu!
 
‘Mzimu wa Ballali’ waitesa Ikulu



na Tamali Vullu



MZIMU wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), marehemu Daudi Ballali, bado unaisumbua Ofisi ya Rais (Ikulu), ambayo imetoa kauli nyingine mpya kuhusiana na gavana huyo.
Hali hiyo ilibainika jana baada ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, kueleza kuwa wakati gavana huyo anaugua alifanyiwa upasuaji mara mbili, jambo ambalo halijapata kuelezwa na kiongozi yeyote wa serikali.
Rweyemamu, aliyekuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, alisema gavana huyo alifanyiwa upasuaji mkubwa mwaka 2002 nchini Afrika Kusini na upasuaji mwingine mdogo alifanyiwa mwaka 2007.
Mkurugenzi hiyo alisema baada ya hapo, Ballali alikuwa akipatiwa matibabu Boston, nchini Marekani.
“Ballali alifanyiwa upasuaji mkubwa mwaka 2002 Afrika Kusini na mwaka jana alifanyiwa ‘minor operation’ (upasuaji mdogo), halafu akawa anaendelea na matibabu Boston (Marekani),” alisema Rweyemamu alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na mwandishi mmoja wa habari.
Alisema suala la kifo cha Ballali limefanywa kisiasa na kukuzwa na vyombo vya habari, na akawasihi Watanzania kuiacha familia yake kuomboleza msiba huo.
Aidha, mkurugenzi huyo alisema serikali haijafanya siri suala la gavana huyo na kueleza kuwa Agosti mwaka jana aliposafiri kwenda nchini Marekani kwa matibabu ilitangaza, alipovuliwa ugavana ikatangazwa na hata alipofariki dunia serikali ilitoa taarifa.
“Vyombo vya habari vinavuka mipaka. Dhamana yenu ni kubwa… jadilini vitu vya msingi kama kupanda kwa bei ya mafuta na chakula,” alisema Rweyemamu ambaye wakati akiwa Mhariri Mtendaji katika magazeti ya Habari Corporation, alikuwa mstari wa mbele kuandika habari mbalimbali kuhusu viongozi serikalini.
Alisema kutokana na msiba huo kwa hapa nchini, serikali iligharamia chakula, ubani, viti, vinywaji na mahema na kuongeza kuwa kuhusu mzazi wa Ballali kupewa ulinzi mkali nyumbani kwake, alisema hafahamu ulinzi huo amepewa na nani.
Alisema anachofahamu ni kwamba katika nyumba hiyo iliyopo Boko, uliwekwa ulinzi wakati wananchi walipovamia.
Jana, gazeti hili liliripoti kuhusu kuzuiwa kwa watu wasio na kibali kuingia katika nyumba hiyo ya Ballali ambayo sasa anaishi mama yake mzazi mwenye umri wa miaka 94.
Ballali alifariki dunia Mei 16 mwaka huu, Washington nchini Marekani na si Boston kama inavyoelezwa na serikali kila mara na akazikwa huko huko Ijumaa iliyopita katika makaburi ya Wakatoliki ya Gate of Heaven, Silver Spring.
Ballali amekuwa akiripotiwa kuugua muda mrefu, lakini muda wote serikali haikuwahi kutoa taarifa rasmi kuhusu maendeleo ya kiafya ya gavana huyo wa zamani wa BoT hadi baada ya kufariki dunia. Hata alipofariki, serikali haikuwahi kutangaza kifo chake kwa muda wa siku nne na ikalazimika kufanya hivyo baada ya Tanzania Daima kutoa taarifa hizo. Habari za kifo hicho cha Ballali, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Jakaya Kikwete Januari 8 mwaka huu, zimekuja siku chache baada ya serikali kupitia Ofisi ya Rais Ikulu, kutangaza kwamba ilikuwa haimtafuti gavana huyo wa zamani wa BoT na wala haifahamu alipo kwa wakati huo.
 
Rais wangu Kikwete, kabla ya kuanguka wananchi watajibu

ban.makala.jpg
Paschally Mayega

RAIS wangu, Piyo (Matamshi ya Mwalimu Nyerere kwa Pius) amemgeukia baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kutangaza hadharani rasmi kuunga mkono kwake hoja ya mgombea binafsi. Huyu ni Makamu Mwenyekiti Bara wa chama kinachotawala.
Mwenyekiti wake ndiye mkuu wa nchi. Mungu bwana, ana mipango ambayo mwanadamu hawezi kuijua. Husema na watu wake kwa njia tofauti tofauti. Kwa hili Piyo abarikiwe sana. Kama amesema hivyo baada ya kupata baraka kutoka kwa mwenyekiti wake, basi na wewe baba ubarikiwe sana.
Rais wangu, mzee wetu maskini mchapakazi baada ya kusikia uamuzi wa mahakama aliniambia: “Sasa sisi ndiyo tumekwisha.” Nilimjibu: “Siyo nyinyi CCM tu, bali vyama vyote vilivyofifisha demokrasia. Vyama ambavyo vimegeuka na kuwa vya viongozi badala ya wanachama sasa vimekwisha.” Huu ndiyo mwisho wa wagombea wabovu waliokuwa wanabebwa na vyama vyao.
Mgombea binafsi anakuja kurejesha matumizi ya haki za Watanzania wote. Haki hii aliyopewa Mtanzania na katiba ya nchi yake, kwa muda mrefu imekuwa imehodhiwa na vyama vya siasa. Mahakama imesema huko ni kuvunja katiba ya nchi. Zamani tuliambiwa kuwa kuvunja katiba ya nchi ni uhaini.
Rais wangu, nilipomsikia Mathias Chikawe, Waziri wetu wa Sheria na Katiba anasema serikali itakata rufaa sikumwelewa. Angekuwa mbumbumbu wa sheria kama mimi ningemwelewa kuwa hajui asemalo. Kuna jamaa kaniambia huyu kasoma sheria hasa.
Ina maana lugha iliyotamkwa na mahakama kuwa kuendelea na sheria hii ni kuendelea kuvunja katiba anaelewa inasema nini. Anapotetea kuvunja katiba haiingii akilini.
Ndugu Rais, hawa jamaa huwa wanaapa nini? Wanaelewa wanachokiapa? Au wanafanya kiapo kama ni utaratibu wa mtu kuwa waziri tu na hakina maana yoyote! Huyu alishika Biblia takatifu.
Kwa imani yangu nilidhani anamwapia Mwenyezi Mungu kuwa atailinda na kuitetea katiba ya nchi yetu. Mtu akisema alikuwa anafanya dhihaka au alikuwa anamdanganya tu rais wetu mimi sitamkatalia. Tuangalie upya viapo vya viongozi wetu kama vina maana yoyote tena! Hawa wote ambao kwa lugha ya kisasa wanaitwa mafisadi au majasiri waliapa. Sizungumzii watu wasio na dini hapa.
Rais wangu, wewe uliapa pale Uwanja wa Taifa. Nilikuona ulishika kitabu kitukufu cha Mwenyezi Mungu. Wahakikishie wananchi wako kuwa ulipokuwa unaapa ulikuwa unamwapia Mwenyezi Mungu kuwa utailinda na kuitetea katiba ya nchi yetu kwa ajili ya amani na ustawi wa waja wake. Madhehebu yenu ni tofauti, lakini Mwenyezi Mungu ni mmoja. Waziri wako amekiuka kiapo chake.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaposhupalia kukata rufaa ili kudhulumu haki za raia mimi namwelewa vizuri. Kwanza mimi mwenyewe sijui ipi ni dhambi kubwa kuliko nyingine kati ya kudhulumu haki za raia na kushiriki kuleta maafa kwa raia kwa kuikubali Richmond, kuisafisha na baadaye kuihalalisha Dowans. Najua zote ni dhambi za mauti.
Kwa jinsi ofisi yake ilivyochafuka kwa sasa, na yeye mwenyewe kutakiwa ajiuzulu mwacheni aishupalie hoja hii. Hivi kuna raha gani kufanya kazi ambayo kila upitapo watu wanaonyeshana ‘fulani mwenyewe ndiye yule!’ Huku Mahakama ya Rufaa ikisema mawakili wa serikali waliwasilisha hoja dhaifu. Wengine wanasema udhaifu hufanywa na mtu dhaifu.
Rais wangu, Mungu ni wa ajabu kabisa. Hebu tazama alivyowachanganya wale wanasheria wasomi wa serikali hata wasijue kuwa tarehe ni muhimu. Wanatukumbusha wale wajenzi wa Mnara wa Babeli. Aliyegundua tarehe hakuwa mjinga. Mimi si mwanasheria, lakini tarehe ningeandika.
Enyi wasomi wa elimu dunia tuliisha waambia kuwa kudhulumu haki za waja wa Mwenyezi Mungu ni kumdhulumu Mungu mwenyewe. Siku zote Mungu hukaa upande wa wanaodhulumiwa. Endeleeni tuone nani zaidi kati yenu na yule aliye juu. Naye anasema: “Adui zenu ni marafiki wenu. Waombeeni mema wale wanaowadhulumu. Mwacheni bwana apambane nao.” Hivi nyinyi wanasheria wa serikali mnaotetea hili, hamna dini? Dini zote zinahubiri haki.
Dini zote zinakataza dhuluma. Anayewatuma mahakamani anatenda dhambi, lakini nyinyi mnaofanikisha dhuluma hiyo mahakamani mnatenda dhambi kubwa zaidi.
Rais wangu, hebu tuambie hizi fedha mnazotumia kukatia rufaa zaidi ya mara tatu, mnashindwa halafu mnalipa gharama, mnazitoa wapi? Usituambie kuwa ni kodi ya wale wale mnaotaka kuwadhulumu haki yao! Kama ni kodi yao nawaambieni hamtaikwepa hukumu maana kwa hili Mungu atawalipia.
Tunamchinja raia wa nchi hii kwa kutumia kisu chake mwenyewe. Hakuna dhuluma inayoendelea milele. Hii ya mgombea binafsi imefika mwisho. Wananchi sasa ni waelewa. Sasa wataanza kuja mahakamani kusikiliza kesi yao. Na huko mitaani watawasubiri hao mawakili wa serikali kuwashangilia. Wakishindwa kuwatia mikononi watawazomea. Nani alaumiwe? Tulipokuwa wadogo watu waliokuwa wanazomewa ni wachawi na vikojozi. Wenye akili wataelewa. Wanaotaka kupima mafuta ya moto kwa kichwa waachwe waendelee.
Rais wangu, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu naye kaja na ya kwake. Anasema watu wasiangalie upande mmoja tu, serikali nayo ina upande na haki yake. Ina haki ya kukata rufaa. Sijui kama alikuwa na maana kuwa serikali ya watu inaweza ikawa na msimamo tofauti na watu wale wale walioiweka madarakani, hicho kitu ndio akakiita haki ya serikali, sijui! Nilikuwa najua kuwa serikali ya watu, huchaguliwa na watu ili iendeshe nchi ya watu kulingana na matakwa ya watu wenyewe.
Ndiyo kusema serikali ya watu siku zote itakuwa upande wa watu maana ni sehemu ya watu hao. Kusigana kokote kati ya watu na serikali yao ndiyo kufanana na usaliti. Mahakamani ni mahali pa kutafuta haki iliyopotea au iliyopokonywa. Ni haki ipi hiyo ambayo serikali inaona imedhulumiwa na watu wake? Ni haki ya serikali kuvunja katiba! Tusije tukamwonea Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, labda tuangalie upande wa pili. Yawezekana alitaka kusema kuwa pamoja na kwamba wewe ndiye mwenye mbwa, lakini mbwa naye ana haki zake. Sawa, mbwa apatiwe chakula atunzwe, atibiwe, lakini si haki ya mbwa kumpangia mwenye mbwa namna ya kuishi au kuendesha maisha yake.
Rais wangu, mahakama imeishatamka kuwa kumzuia mtu kuchaguliwa na wenzake kwa kumwekea sharti la kuwa mwanachama wa chama cha siasa ni kuvuja katiba, serikali yako inakata rufaa. Rufaa ilivyotafsiriwa na kamusi ya Kiswahili sanifu ya Oxford ni maombi yanayopelekwa kwenye baraza au mahakama yenye mamlaka zaidi ili kukataa uamuzi uliokwishafanywa. Serikali yako inayakataa maamuzi ya mahakama kuwa kumnyima raia haki yake ni kuvunja katiba. Inataka na mahakama ya juu ikatae hivyo hivyo. Usaliti maana yake ni nini? Rais wangu, hebu tuangalie muasisi wa taifa hili Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anasemaje kuhusu haki ya mtu kuwa mgombea binafsi. Katika kitabu chake cha ‘Tumetoka wapi, Tuko wapi, Tunakwenda wapi’ ukurasa wa 32-35 Mwalimu Nyerere anasema: “…Tulipokubali tuwe na vyama vingi vya siasa tulisema hivi vyama vingi vina migogoro. Mnaweza mkawa na chama cha dini, kabila, mkoa kinaitwa chama cha Mbeya ama katika nchi kikaitwa cha Wazanzibar au cha Watanganyika tu.
“Tulisema sisi hapana ni taifa changa… Basi, sheria hiyo ndivyo ilivyotungwa na ndivyo ilivyo… Hata hivyo, mimi nadhani sheria imekosea kuzuia wagombea binafsi… Hili jambo limekosewa ni la msingi… Linahusu haki yangu na yako ya kupiga kura. Hii ni haki ya uraia. Madhali wewe ni raia wa Tanzania (huna kichaa, huko gerezani, umetimiza umri unaotakiwa wa miaka kumi na minane) una haki ya kupiga kura. Ni haki yako ya uraia. Iko mfukoni mwako! Hii haki ya kuomba upigiwe kura pia ni haki ya uraia; huwezi kunyimwa. Maadamu wewe ni raia wa Tanzania kisiasa una haki ya kuomba uwe rais. Ukiwa katika chama ama haupo katika chama.
“Aidha, raia wa Tanzania hawezi akanyang’anywa haki hii ya kuomba uongozi wa nchi yake tangu ngazi ya kijiji mpaka ngazi ya taifa… Sina hakika kama vimechukua Watanzania wote. Watanzania wengine hawamo CCM, hawapo wapi na hawana chama chochote. Hata hivyo nikikataa kuingia katika chama isiwe sababu ya kuninyang’anya haki yangu ya kupiga au kupigiwa kura…
“Sasa sheria inawanyima raia wa Tanzania haki hiyo. Mtu mmoja akaenda mahakamani kudai haki hiyo akasema: ‘Sheria hii si haki.’ Jaji mmoja akahukumu akasema ‘naam si haki’. Mimi nakubaliana na maamuzi yale ya jaji kabisa. Jaji alikuwa sahihi… kwa sababu haki hii iko katika katiba. Ingekuwa haiko katika katiba, ungekuwapo ubishi, lakini imo ndani ya katiba…
“Sasa serikali wakafanyaje? Badala ya kukubali uamuzi wa jaji, kwa kweli walichokifanya kwa kweli ni kuifuta. Ndiyo, hamwezi kufuta haki za raia. Hamna uwezo wa kufuta haki za raia. Ndugu waziri, hamna uwezo wa kufuta haki za raia. Hamwezi kweli kabisa kabisa… Sasa mimi nina ugomvi huo na ni ugomvi wa kasoro kubwa, si kasoro ndogo… Hatuwezi kumyima raia haki yake.”
Rais wangu, hamwezi kufuta haki za raia. Hamna uwezo wa kufuta haki za raia. Ndugu Mathias Chikawe, hamna uwezo wa kufuta haki za raia. Hamwezi kweli kabisa kabisa. Kama hamtamsikiliza Baba wa Taifa, hapa duniani mtamsikiliza nani? Wengine Mbeya Mei 1, 1995 mlikuwapo. Mlimwona Mwalimu Nyerere alivyokuwa akiitetea haki hii ya watu wake kutoka serikali ya awamu ya pili. Utadhani alikuwa anadai uhuru kutoka kwa wakoloni. Rais wangu, nchi yako imefikia hapa, tulikuomba uwaondoe wote wanaodhulumu haki za raia kwa kutumia jina la serikali yako. Tukasema, kutwa mchungaji peke yake anahangaika mahakamani kutetea haki ya raia ya kuchaguliwa na wenzake yeye binafsi. Mahakama imetenda haki. Serikali ya watu inakata rufaa dhidi ya watu wake.
Aisee! Nilikuwa sijawahi kusikia Jaji Mkuu na majaji wote wenye uwezo wa kuisikiliza rufaa hii wameteuliwa na rais. Serikali ya rais wao (Mwajiri) inawataka waitengue hukumu hii. Sisemi haki haitatendeka, lakini ni ngumu kama ngamia kupita katika tundu la sindano.
Ni kwa mapenzi ya Mungu tu maana kwake hakuna kinachoshindikana. Wananchi wameinua macho yao juu wakiitizama milima. Msaada wao utatoka wapi? Wanapiga mbiu ganjoni watasikiwa na nani? Matumaini ya wananchi sasa ni kwa mchungaji badala ya wabunge na serikali yao. Hivi usaliti ni kitu gani?
Rais wangu, kwa nini watu wako wamlilie Nyerere na wewe upo? Nyerere hakuzikwa na haki zao. Simama na useme watu wako wafarijike. Ukiwa kimya watu wako watajuaje kuwa upo pamoja nao katika kuhangaika kwao? Baki nao hata siku zako zitakapokwisha, ukifika mbele ya haki uweze kumwambia Muumba wako: “Baba katika wote ulionipa sikumpoteza hata mmoja ila mwana mpotevu.”
Msomaji wangu, mhariri wangu amesema nifupishe maongezi haya, naomba tuonane wiki ijayo, nitakapomfunulia moyo wangu wote rais wangu.

Tel: 0713-334239
Email: gowe2006@yahoo.com
 
Naona Mh Rais hajagundua bado udhaifu wa kiutawala aliouonyesha!
Udhaifu wa kutokulishighulikia suala la UFISADI vile inavyotakiwa kunaweza kum cost yeye na chama chake cha mapinduzi!
Kwamba sasa kuna watu walioamua kusimama kwenye upande wa wazalendo!

Waraka mzito wa maaskofu kwa JK

na Kulwa Karedia



MAASKOFU wa makanisa kadhaa kupitia kile wanachokiita Ushirika wa Maaskofu Tanzania, wameandika waraka maalumu wenye ujumbe mkali na mzito kwa serikali, wakitaka kuchukuliwa kwa hatua kubwa ili kulinusuru taifa dhidi ya misukosuko linayokabiliana nayo.
Waraka huo wa maaskofu wanaofanya kazi chini ya uenyekiti wa mtu anayetajwa kuwa ni Askofu John Mwela, unaelezwa kuwa ni matokeo ya kikao cha pili cha kamati ya maaskofu hao kilichokutana Dodoma kwa siku nne kuanzia Mei 13 hadi 16 mwaka huu.
Kwa mujibu wa waraka huo wa maaskofu ambao Tanzania Daima imeusoma, pia kuchapwa katika baadhi ya magazeti jana, maaskofu hao wanaeleza kuguswa na matukio kadhaa wanayoyaelezea kuwa yaliyochangia kuliyumbisha taifa.
Miongoni mwa mambo yanayotajwa katika waraka huo wa kwanza wa aina yake, ni pamoja na ufisadi, mpasuko wa kisiasa Zanzibar, uwakilishi wa viti maalumu bungeni, migomo vyuoni na katika mashirika na tatizo la usafiri kwa wanafunzi wa mijini.
Wakirejea matukio ya siku za hivi karibuni, maaskofu hao wanasema kuwa yana sura nne, zikihusisha ubadhirifu wa fedha za Watanzania kupitia Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje katika Benki Kuu (EPA), Taarifa ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu Richmond, na kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na mawaziri wengine kadhaa.
Mawaziri waliojiuzulu wanaotajwa katika waraka huo ni pamoja na Dk. Ibrahim Msabaha, Nazir Karamagi na Andrew Chenge.
Maaskofu hao wanabainisha kuwa mwelekeo wa mambo hapa nchini unaonyesha kuwa serikali inahitaji msaada mkubwa katika kuweka hali sawa.
Wanasema kuwa matukio hayo ya ufisadi yamesababisha Watanzania wagawanyike katika makundi manne, ambayo hata hivyo hawataji chanzo chao cha utafiti kilichowawezesha kufikia katika mpangilio wao huo.
Kwa mtazamo wao, kundi linaloongoza ni lile linalojumuisha watu wanaofikia asilimia 60, wanaochukizwa na kuumizwa na viongozi na watu wachache waliojilimbikizia mali.
Kundi la pili wanalolitaja ni la watu wanaofikia asilimia 25, ambao wao ni wale wanaolia na kutoa hukumu yao kwa kulalamika wakiiona serikali kuwa iliyoshindwa kuwajibika.
Aidha, walilitaja kundi la tatu (asilimia 14.75) kuwa ni lile la watu wasioona shida yoyote, kwa maana wao wana kila kitu, huku kundi la nne na la mwisho likijumuisha watu wachache (asilimia 0.25) wanaomlilia Mungu aliponye taifa la Tanzania.
Kutokana na mambo hayo, maaskofu hao wanatamka kujifunga kuisaidia serikali na hususan Rais Kikwete, katika maeneo kadhaa, kwa kutoa ushauri katika masuala ya ufisadi, mabadiliko yanayohitajika katika kuandaa uchumi wenye nguvu, pamoja na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2010.
Aidha, ushauri wao huo unahusisha pia jinsi ya kufikia muafaka kati ya CCM na CUF huko Zanzibar, na kugusia njia ya kushughulikia migomo katika vyuo vikuu, mashirika ya umma na makampuni binafsi, pamoja na serikalini kwenyewe.
Kwa upande mwingine, wakati serikali imekuwa ikifikiria kuongeza idadi ya viti vya wabunge maalumu hadi kufikia asilimia 50 mwaka 2010, kwa lengo la kukuza ushiriki wa wanawake katika hatua za maamuzi, maaskofu hao wamelitaka Bunge kufuta mara moja sera ya uwakilishi bungeni kupitia utaratibu wa viti maalumu.
Kamati hiyo imesema iwapo Bunge halitachukua hatua hiyo, basi kanisa nalo litaomba viti saba vya uwakilishi, wakivigawa vitatu kwenda kwa makanisa ya kiprotestanti yaliyo chini ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), viwili Kanisa Katoliki chini ya TEC, na makanisa ya kipentekoste yapate kimoja na kimoja kingine kiende kwa makanisa yanayojitegemea.
Tamko la kamati hiyo, lililosainiwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Askofu Mwela na Katibu wake, Godfred Lema, linasema hatua yao hiyo imelenga kuboresha uwiano wa uwakilishi bungeni, tofauti na hali ilivyo sasa.
Katika hayo yote, maaskofu hao wamesema kuwa wapo tayari kusimama kidete kumsaidia Rais Jakaya Kikwete kutafuta suluhisho dhidi viongozi mafisadi ndani ya serikali.
Maaskofu hao wanasema wamejitoa kupambana na ufisadi kwa sababu hali hiyo imefika katika hatua mbaya, ambayo rais anapaswa kusaidiwa haraka, ili kupunguza hatari ya mgawanyiko ndani ya jamii.
“Tumekubaliana kusimama na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume na serikali zao kutafuta suluhisho la matukio haya, kwa sababu tunajua nchi ni ya Watanzania wa dini na rangi zote, hivyo sote tunawajibika mbele za Mungu kuitunza,” inasomeka sehemu ya waraka huo.
Wanasema kuwa wakati umefika kwa makanisa kujiingiza katika vita dhidi ya ufisadi, kwa sababu baadhi ya watu wanaoendeleza vitendo hivyo wamo ndani ya makanisa hayo.
“Wengi wa watu hawa wanaoitwa mafisadi wako katika makanisa yetu, hivyo tutatumia nguvu kutoka kwa Mungu ili kuwaumbua na kuwaongoza, kuwa mabadiliko haya yanahitajika katika kuandaa uchumi wenye nguvu,” inasomeka taarifa hiyo.
Sambamba na vita dhidi ya ufisadi, waraka huo unasema maaskofu hao wamekubaliana pia kushiriki kikamilifu katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Katika hili wanatoa ahadi ya kukutana na viongozi wa vyama vya siasa ili kushauriana kwa pamoja, mambo yanayohusu umoja wa kitaifa na masilahi yake. “Tutawaelekeza na kuwafundisha wale wanaowaongoza, umuhimu wa kutuunga mkono katika azima yetu. Tunaamini kwa kufanya hivi na kwa maelekezo haya sahihi ya Mungu, tutakuwa na umoja wa kitaifa, taifa lisilo na magonjwa kama vile malaria, ukimwi na vifo katika umri mdogo pamoja na kuondokana na umaskini na maisha duni,” inasomeka sehemu ya waraka huo. Katika sehemu moja ya waraka huo, maaskofu hao wanaandika kuwa wanasubiri kuundwa kwa kamati ya kudumu ya maaskofu, baada ya kufanyika kwa vikao vya makanisa yaliyo chini ya CCT, TEC na PCT.
 
Dk Slaa kwa niaba ya wananchi alishawahi kumtaka Mh Rais aamuru Ballali akamatwe...Still Muungwana aligoma..why?
Bado tunaendelea kujiuliza huku imani zetu kwa Mh Rais ikiwa at the all time low...

Slaa ataka Balali akamatwe



na Hellen Ngoromera


KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa, alimtaka Kikwete kuamuru kukamatwa kwa Balali na kuwekwa gerezani, hadi mahakama itakapotoa uamuzi kuhusu tuhuma za ubadhirifu wa fedha za serikali alizokutwa nazo.

Kwa upande mwingine, Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed, alisema kubainika kwa ubadhirifu ndani ya BoT kumedhihirisha kuwa maneno waliyoyasema wapinzani kuhusu suala hilo hayakuwa ya uzushi.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Dk. Slaa alisema hatua ya Rais Kikwete kutengua uteuzi wa Dk. Balali haitoshi.
Kwa mujibu wa Dk. Slaa, wakati walipoibua hoja hiyo, viongozi kadhaa wa serikali, waliwatukana na kusema inabidi sasa wasafishwe, kwani inaonekana walichokisema ni cha uhakika.

Aidha, alishangazwa na rais kuchukua muda mrefu kupata ukweli wa masuala hayo wakati wao walishayasema miezi minane iliyopita.
"Baada ya sisi kutoa hoja yetu rais alitutukana, aliwahi kusema kelele za mlango hazimnyimi mwenye nyumba usingizi…amechelewa kutoa majibu, hata hivyo hatua hiyo haitoshi, Balali amefanya kitu kibaya katika nchi na ni mwanzo wa matabaka.

"Mtu akiiba sh 5,000 anawekwa lupango hadi atakapopelekwa mahakamani na akiwa mgonjwa anakuwa chini ya ulinzi wa askari magereza kitandani lakini Balali anaachwa.

Nasisitiza akamatwe na kukaa gerezani hadi mahakama itakapotoa uamuzi wa suala lake, rais pia alitangazie taifa mara moja kukamatwa kwake kwa sababu pesa zilizoibwa ni zetu," alisema Dk. Slaa.

Akizungumzia kuhusu rais kuagiza Bodi ya Wakurugenzi ya BoT kukutana mara moja ili kujadili taarifa ya ukaguzi na kuchukua hatua zipasazo za kinidhamu dhidi ya maofisa wote wa benki walio chini ya mamlaka yake waliohusika na kusababisha hasara kwa taifa, Dk. Slaa alisisitiza kwa kumtaka rais kutowaachia watendaji wake kuchukua hatua dhidi ya Dk. Balali, bali yeye mwenyewe aelekeze hatua za kuchukua dhidi yake wka sababu ni yeye ndiye aliyemteua.

"Rais aelekeze hatua za kuchukua dhidi ya mapambano hayo ya wizi mkubwa, uzembe mkubwa na ubadhirifu mkubwa ambazo zimetokea, asijifiche kama mbuni, aelekeze hatua za kuchukua dhidi ya Dk. Balali," alisisitiza Dk. Slaa.

Alisema wamesubiri ukaguzi wa suala hilo kwa muda mrefu na matokeo yake kilichotolewa na serikali ni ukaguzi wa Hesabu za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) tu, ambayo alisema kuwa ni tone la maji katika bahari. Alimtaka rais kueleza fedha zilizochukuliwa katika kampuni mbalimbali ikiwemo Meremeta, Mwananchi Gold, Tan Gold na nyingine, zimekwenda wapi na zimetumikaje.

Akizungumzia kuhusu rais kumteua aliyekuwa Naibu Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu kuwa Gavana mpya wa BoT, Dk. Slaa alimpongeza na kumkaribisha BoT lakini alimtaka kutambua kuwa Benki Kuu ni chungu cha Watanzania wote, hivyo aitunze kama mboni ya jicho lake.
Kwa upande wake, Hamad Rashid aliipongeza hatua ya Rais Kikwete kufanya uamuzi huo.

Alimtaka Rais Kikwete kuyashughulikia maeneo mengine yasiyotajwa katika taarifa hiyo kama vile ujenzi wa Benki Kuu. Pia aliitaka serikali kutowabeza wapinzani, hasa wanapozungunza ndani ya Bunge kuhusu masuala mbalimbali, kwani wanachokuwa wanazungumza wanakuwa na uhakika nacho.

"Bunge ni chombo cha kutunga sheria, serikali isitubeze pale tunapozungumza jambo mahali pale, kwani sisi si watoto wadogo. Tunaomba pia ikitokea tumezungumza jambo tusiadhibiwe kabla uchunguzi haujakamilika," alisema.

Aliongeza kuwa kambi ya upinzani itaendelea kushirikiana na rais kufichua ufisadi, rushwa na ubadhirifu katika kusimamia matumizi mazuri ya rasilimali za nchi kama vile madini na nyinginezo.

Alimshauri rais kutafuta njia nyingine ya kushughulikia tatizo lililobainika kwa sababu kuna uwezekano mkubwa kuwa maagizo yake kwa vyombo kama Takukuru, Jeshi la Polisi na kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, yanaweza kuchukua muda mrefu kutekelezwa.
Pamoja na mambo mengine, kiongozi huyo wa kambi ya upinzani aliwataka wananchi kuwaunga mkono wapinzani kwa kuwaongezea nguvu za ziada ili kuwawezesha kufanya kazi kwa ari.

Ukaguzi huo wa hesabu katika akaunti ya malipo ya EPA ambao ulifanywa na wakaguzi wa Kampuni ya Ernst & Young kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, ulianza Septemba mwaka jana na kukamilika Desemba. Ripoti yake ilikabidhiwa kwa Rais Kikwete Januari 7, mwaka huu.

Katika taarifa hiyo, rais aliagiza Bodi ya Wakurugenzi ya BoT ikutane mara moja kujadili taarifa ya ukaguzi na kuchukua hatua zipasazo za kinidhamu dhidi ya maofisa wote wa benki hiyo walio chini ya mamlaka yake waliohusika na kusababisha hasara hiyo kwa taifa.

Aliamua pia shughuli za ulipaji wa madeni katika akaunti ya EPA zisimamishwe mara moja mpaka hapo taratibu za uhakiki na utaratibu mpya utakapotengenezwa. Rais pia amewaagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, kuchunguza na kuchukua hatua zipasazo za kisheria kwa makampuni na watu waliohusika na uhalifu huo. Amewataka pia wahakikishe fedha zilizolipwa isivyo halali zinarudishwa.
 
Ni kweli kabisa inawezekana kifo cha Ballali anachokijua Kikwete ni kazi ya Mungu...Haya sasa tuone kama Mungu atakuwa upande wa Mafisadi Mafioso ama wa wazalendo!
 
Back
Top Bottom