jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
- Thread starter
- #101
Haya njia ya kura ikaja,wakamchagua tena!Tumetoka mbali na ninaomba Mungu tusiwe na safari ndefu zaidi.Nijibu hivi: Hii option unayopendekeza ya utawala wa kiraia kujivua madaraka na kuwapa wanajeshi utawala wa nchi iko kwenye Katiba ya nchi gani? Huwezi kwenda na kutunga taratibu au mazoea nje ya Katiba. Katiba iko wazi kabisa, Rais akijiuzulu nani anafuatia, Bunge likivunjika nini kifanyike n.k Katiba yetu ina utaratibu ulio wazi kabisa wa kubadilisha madaraka.
Kuna njia za kawaida na njia zisizo za kawaida.
Njia ya Kawaida - Ni sanduku la kura ambapo wananchi wanachagua nani awaongoze na nani asiwaongoze. Hili hufanyika kila baada ya miaka mitano au pale inapotokea uchaguzi mdogo isipokuwa kwenye kiti cha Urais.
Njia zisizo za kawaida:
- Ni njia ya mahakama (kwa wabunge madiwani na viongozi wengine). Hii ya mahakama haimhusu Rais kwani akishatangazwa kuwa Rais hakuna uwezekano wa kufungua kesi dhidi yake ya kupinga uchaguzi huo kwenye mahakama yoyote. (hatupendi sheria hiyo tubadili Katiba)
- Njia ya Kujiuzulu/kustaafu - Hapa ni pale kiongozi anapolazimika kuachia nafasi yake aidha kwa sababu fulani au kutokana na umri au afya. Kiongozi mwingine ataingia madarakani. Hili pia linahusu Waziri Mkuu akijiuzulu taratibu za Kikatiba zinafuata kama ilivyotokea Februari.
- Kiongozi anapokufa - taratibu za kujaza nafasi yake zipo wazi. Rais akifa madarakani Makamu anachukua Urais, Makamu akifa au kupanda kuwa Rais Basi makamu anachaguliwa na Bunge linafanya kikao cha dharura kumpitisha. Waziri Mkuu akifa Baraza la Mawaziri linavunjika na utaratibu wa kikatiba kujaza nafasi unafuatwa.
n.k
Nakushauri usome Katiba utapata majibu ya maswali yako maana nitajikuta nafanya kazi ambayo mtu yeyote anaweza kufanya nayo ni kusoma Katiba kwani majibu yapo.