Kwanini Iran inakatazwa kuwa na Nuclear?

Kwanini Iran inakatazwa kuwa na Nuclear?

Jf sijui imekuwaje siku hizi katika mada makini kama hii

Moderator Active Refiner kwa hizi comments JF sio jukwaa la great thinkers tena
Ondoa shaka, hawa unaona wanaropoka bila hoja za msingi baada ya miaka 10 - 15 wakishaturn 30 - 35 years wataacha utoto... Trust me ukiona mtu hoja zake zimebase kwenye dini, huyo kama si mtoto, basi ni mwendawazimu
 
Mmarekani ndiye aliyewahi kutumia Nuclear weapons je naye ni muislamu??
Hata kama siyo muislamu, nae ni mwehu tu.

Kuna vichaa wengi tu ambao siyo waislamu, mojawapo ni Putin na Korea kaskazini.

Hao hawatakiwi kuwa na nyuklia.
 
Ndio maana hatutaki sasa wendawazimu wengine waendelee kupata nyuklia, yatakuja kufanya uwendawazimu kama mwenzao US alivyofanya, yataiangamiza dunia.
Unataka iwe rahisi tu kwa mataifa makubwa kuyaonea madogo ?

Palestine angekuwa na Nyuklia Israel isingefanya huu uendawazimu inao endelea nao, hivyo hivyo kwa Ukraine
 
Panga ni silaha ya kawaida Sana ukikutana na mtu kaibeba, wala hutarudi nyuma kwa hofu.
Ila ukimwona kichaa kabeba anakuja usawa wako hata Kama Hana habari na wewe sidhani Kama utasubiri akukaribie!
Dawa ni kuhakikisha vichaa hawabebi mapanga hata Kama hawakati watu.
Sahihi kabsa! Twanga pepeta waliimba" kichaa kapewa rungu usijaribu KUPITA mbele yake" Allah ametuhalibia sana dunia yetu
 
Hata kama siyo muislamu, nae ni mwehu tu.

Kuna vichaa wengi tu ambao siyo waislamu, mojawapo ni Putin na Korea kaskazini.

Hao hawatakiwi kuwa na nyuklia.
Nani anatakiwa kuwa nazo ? Israel na anacho endelea kukifanya Gaza kwa Palestine asie hata na kifaru kimoja ?
 
Ondoa shaka, hawa unaona wanaropoka bila hoja za msingi baada ya miaka 10 - 15 wakishaturn 30 - 35 years wataacha utoto... Trust me ukiona mtu hoja zake zimebase kwenye dini, huyo kama si mtoto, basi ni mwendawazimu
Hapana.

Kama dini zinaamrisha kuua watu, kwa nini hoja zisibase huko.

Kama mtu anaambiwa akimuua adui yake ataenda peponi, huyo mtu akiwa na nyuklia atashindwa kuilipua kuua maadui zake? Nani asiyezitaka raha za peponi?
 
Hapana.

Kama dini zinaamrisha kuua watu, kwa nini hoja zisibase huko.

Kama mtu anaambiwa akimuua adui yake ataenda peponi, huyo mtu akiwa na nyuklia atashindwa kuilipua kuua maadui zake? Nani asiyezitaka raha za peponi?
Dini gani ilimtaka Marekani kulipua wajapan kwa Nyuklia ? Na dini gani inawataka watu kulipua wenzao kwa mabomu ?
 
Nani anatakiwa kuwa nazo ? Israel na anacho endelea kukifanya Gaza kwa Palestine asie hata na kifaru kimoja ?
Hakuna anaetakiwa kuwa nazo, ndiyo maana tunazuia nchi kutaka kuwa na nyuklia.
 
Hapana.

Kama dini zinaamrisha kuua watu, kwa nini hoja zisibase huko.

Kama mtu anaambiwa akimuua adui yake ataenda peponi, huyo mtu akiwa na nyuklia atashindwa kuilipua kuua maadui zake? Nani asiyezitaka raha za peponi?
Kwahiyo wewe umeona hoja kubwa ni dini na si kingine.? Japo fuatilia uhasama wa Iran na mataifa ya ulaya pamoja na Marekani hata kabla ya mapinduzi ya kiislamu huko iran kisha urudi uje useme kama hoja kubwa ya wao kuzuiwa ni dini ama kuna sababu nyinginezo
 
Naomba kuuliza ni kwanini Iran haruhusiwi kua na Nuclear? Wakati India, south africa, uk, russia, israel, pakistan, china nk wanazo!!! Kwanini Iran haruhusiwi?
Kwa sababu 100% ni wavaa makobasi
 
Dini gani ilimtaka Marekani kulipua wajapan kwa Nyuklia ? Na dini gani inawataka watu kulipua wenzao kwa mabomu ?
Siijui dini iliyomtaka Marekani kulipua japan, ila uislamu unafundisha waumini kujilipua kwa mabomu, ili waende peponi.
 
Hakuna anaetakiwa kuwa nazo, ndiyo maana tunazuia nchi kutaka kuwa na nyuklia.
Haiwezi kuzuia dunia ni uwanja wa fujo toka kale sema sasa silaha za mauaji zimekuwa kali tofauti na kale zama za mistake na mikuki.

Soon Iran itazindua bomu lake la Nyuklia nafikiri kuna kiwango cha heshima kitakuwepo pale mashariki ya kati maana bila Nyuklia huwa ni ngumu sana watu kuheshimiana.

Bila Nyuklia North Korea toka muda ingekuwa imekwisha vamiwa tena, anachokutana nacho Ukraine na Palestine wanapaswa pewa Nyuklia ili heshima duniani iwepo
 
Kwahiyo wewe umeona hoja kubwa ni dini na si kingine.? Japo fuatilia uhasama wa Iran na mataifa ya ulaya pamoja na Marekani hata kabla ya mapinduzi ya kiislamu huko iran kisha urudi uje useme kama hoja kubwa ya wao kuzuiwa ni dini ama kuna sababu nyinginezo
Hoja siyo dini peke yake, zipo na sababu zingine.

Ila dini ndiyo inachochea sana Iran kutaka kuua wayahudi, imani za kidini.
 
Kama Pakistani nayo ni Islamic republic, basi itakuwa haina mpango wa kuangamiza watu kama walio nao Iran.

Iran muda wote wanahubiri kuwafuta wayahudi, wakipata nyuklia si watawafuta mara moja.

Vipi yale makombora 300 yaliyorushwa kwenda Israel mwaka jana, yangekuwa ya nyuklia je?
Nchi zote hazitakiwi kumiliki sio tu mabomu ya nyuklia, bali siraha zote za maangamizi. Kwa kusimamia amani duniani na kuzuia machafuko yote, hasa vita tuacheni uselfish, irani hajawahi kushambulia kijeshi taifa lolote bila kuchokozwa.

Pia haingii akilini adui yake marekani anayetaka kumvamia kijeshi ndio ampangie jinsi ya kujilinda.Huku kamruhusu mtoto wake Israel inayokaliwa na wayahudi feki wa kizungu kumiliki mabomu ya nyuklia, alafu iran ndio asimiliki.
 
Nae anatakiwa kupokonywa nyuklia.

Kumpokonya sasa ni ngumu maana ni kichaa, hatutaki kichaa mwingine Iran nae aje atusumbue kumpokonya, ni bora azuiliwe kuipata.
Vipi marekani? Yeye sio kichaa au hujui alichokifanya japani? Mpaka leo wanahangaika na madhara ya nyuklia. Dah ? Utoto raha sana.
 
Hoja siyo dini peke yake, zipo na sababu zingine.

Ila dini ndiyo inachochea sana Iran kutaka kuua wayahudi, imani za kidini.
Iran kuna wayahudi wengi tu.

Hivi Tanzania tatizo ni ujinga au ukosefu wa elimu bora ? Mbona watu wengi wana ukosefu wa maarifa machache tu hata yasiyo na uzito ?
 
Haiwezi kuzuia dunia ni uwanja wa fujo toka kale sema sasa silaha za mauaji zimekuwa kali tofauti na kale zama za mistake na mikuki.

Soon Iran itazindua bomu lake la Nyuklia nafikiri kuna kiwango cha heshima kitakuwepo pale mashariki ya kati maana bila Nyuklia huwa ni ngumu sana watu kuheshimiana.

Bila Nyuklia North Korea toka muda ingekuwa imekwisha vamiwa tena, anachokutana nacho Ukraine na Palestine wanapaswa pewa Nyuklia ili heshima duniani iwepo
Hatutaki dunia iwe uwanja wa fujo, tunataka iwe ya amani.

Vichaa wanaoondoa amani duniani kama Putin na Kagame wanatakiwa kupokonywa silaha.
 
Vipi marekani? Yeye sio kichaa au hujui alichokifanya japani? Mpaka leo wanahangaika na madhara ya nyuklia. Dah ? Utoto raha sana.
Marekani nae anatakiwa kupokonywa nyuklia. Hatutaki nyuklia maana lengo la nyuklia ni kuangamiza binadamu.
 
Hatutaki dunia iwe uwanja wa fujo, tunataka iwe ya amani.

Vichaa wanaoondoa amani duniani kama Putin na Kagame wanatakiwa kupokonywa silaha.
Hao ni vichaa wenye hafadhali kuna kicha mmoja aliyekomaa anaendeleza mauaji ya kimbari pale Palestine na anakingiwa kifua na vichaa wenzake wenye mabomu kama yake ili kuendeleza mauaji ya kimbari.

Najua mabomu ya Nyuklia hayawezi kuangamizwa sasa nataka kuona anatokea wa kumfunga speed governor huyu kichaa anaye endeleza mauaji ya kimbari hapo Palestine.
 
Back
Top Bottom