Kwanini ikitokea mfanyakazi mmoja wa ofisi za umma akawa mtenda haki, sio mpenda rushwa anachukiwa sana?

MWANAHARAKATI MWEMA

Senior Member
Dec 16, 2022
192
270
Nawasalimu Kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa kusamehe, nawashukuru wazazi wangu Kwa kunizaa hivi nilivyo nashukuru.

Mimi nimekuwa miongoni mwa watu ambao nimezaliwa nikajikuta nina moyo ambao muda wote unaitaji amani, na sipendi kuonea mtu wala sipendi kuona mtu mwingine akionewa.

Nimekuwa katika maisha haya kuanzia utoto mpaka ukubwani na mpaka nimeajiliwa nipo vilevile.

Shida kubwa kabisa ambayo nimeiona ofisi nyingi za umma ni Ile hali kwamba endapo utakuwa tofauti na mitazamo na wenzako ambao wao wanaweza kuwa wazee wa madili, unakuta mtu anafanya jambo mpaka unashangaa ukimuuliza anakwambia wewe unadhani mimi nimekuja kucheza hapa.

Yaani mitazamo ya walio wengi kwenye ofisi za umma ni kwamba "CHUKUA CHAKO MAPEMA" lakini ukiangalia watu wanaoumia ni wananchi wa hali ya chini, na ikitokea wewe ambaye una hofu ya mungu unataka kulifanya jambo lile kwa haki unachukiwa huku ukipewa majina ya hajabu, utaitwa mjuaji, bush loyar, mzee wa protocol, mlokole nk.

Sasa Kuna nyakati huwa najiuliza hivi kama sisi tutakuja kujikomboa kweli kwenye hali hii inayoitwa ya umaskini au ndio bhasi tuendelee kuumizana mpaka Mungu mwenyewe atakapoamua kututoa kwenye hili janga.

Ni kweli kwamba asilimia kubwa ya watu ambao wanakula na kuchezea ofisi za Umma ni watu wanamaisha mazuri na wale wanaopenda haki wengi ni maskini ata maisha yao ya kawaida sana, sasa hali hii ndio inafanya wachache wapate mali na wengi wanaishia kwenye umaskini.

Na hakuna kitu kinakela sana kama mtu ukiwa unakibiashara flani ambacho wewe kama mtumishi umekianzisha na kinakulunguzia shida ,maneno utakayopewa ni kukatishwa tamaa tu, yaani watu hawaami katika kujiwekeza badala yake wanakutengenezea mazingira ukwame kiukweli inasikitisha sana.
Asanteni.
 
Yaani mitazamo ya walio wengi kwenye ofisi ZA UMMA Ni kwamba "CHUKUA CHAKO MAPEMA" lakini ukiangalia watu wanaoumia ni wananchi wa Hali ya chini,
Ukipata nafasi ya kuiba pesa ya serikali iba kadiri uwezavyo usiionee huruma pesa ya serikali rushwa kula

Ukipata nafasi ya kutolipa kodi usilipe usionee huruma serikali


MSAFARA WA BASHITE

20240209_095750.jpg


20240209_095729.jpg
 
Endelea kujiwekea hazina 'Mbinguni' na usitazame mwanzo wako huo wala hauna Maana yoyote Ila mwisho wako ndo Una maana Sana.

Peace of mind ndo kila kitu katika haya maisha Hivyo usiache kutenda haki na kuwa mwema maana malipo yake watafaidi hadi wajukuu zako.


When you steal from others you steal from your-self.

You need to know where your treasure is

Life without Fear of GOD is a movement

But life with GOD is a progress.
 
Kwanini awe kiherehere yani yeye ndo aonekane wa maana sisi ndo tuwe watenda dhambi, tukitenda dhambi na yeye atende dhambi
 
Jibu lako ni moja tu. Hiki ni kizazi cha uzinzi na wizi kinachomkataa Mungu kwa kasi ya 5G. Ukiwa mkweli Mungu asipokulinda wao watakuua tu ili kufanikisha malengo yao ya uovu. Tumeshaona mengi na tulikopita mpaka hapa tulipo ni Mungu tu ametuwezesha. Endelea kutenda mema usijali Mungu atakukumbuka tu na hao wezi wote na waziznzi na wote wamwachao Mungu wa kweli watakachovuna ni kupelekwa kwenye ziwa la moto wa milele na hizo mali walizojilimbikia kwa wizi ndizo zitatumika kuchochea moto huko kuzimu waendako. Waambie tu ukweli hata wakikuchukia wanachofanya si kitu kizuri mbele za Mungu wanatakiwa watubu na kuacha kutenda dhambi ili Mungu aweze kuwasamehe na awapokee kwenye uzima wa milele.
 
Hivi unadhani ukimwaga kikombe kimoja cha maji baharini utakua umeongeza kina cha maji 🤔🤔 ufisadi na wizi ni mfumo rasmi wa uendeshaji wa serikali ya ccm kwa hiyo ukiipata nafasi ya kukwapua usitazame nyuma kwapua kwa kadri utakavyo weza ukijifanya muadilifu sana utakufa mapema
 
Nawasalimu Kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa kusamehe, nawashukuru wazazi wangu Kwa kunizaa hivi nilivyo nashukuru.

Mimi nimekuwa miongoni mwa watu ambao nimezaliwa nikajikuta nina moyo ambao muda wote unaitaji amani, na sipendi kuonea mtu wala sipendi kuona mtu mwingine akionewa.

Nimekuwa katika maisha haya kuanzia utoto mpaka ukubwani na mpaka nimeajiliwa nipo vilevile.

Shida kubwa kabisa ambayo nimeiona ofisi nyingi za umma ni Ile hali kwamba endapo utakuwa tofauti na mitazamo na wenzako ambao wao wanaweza kuwa wazee wa madili, unakuta mtu anafanya jambo mpaka unashangaa ukimuuliza anakwambia wewe unadhani mimi nimekuja kucheza hapa.

Yaani mitazamo ya walio wengi kwenye ofisi za umma ni kwamba "CHUKUA CHAKO MAPEMA" lakini ukiangalia watu wanaoumia ni wananchi wa hali ya chini, na ikitokea wewe ambaye una hofu ya mungu unataka kulifanya jambo lile kwa haki unachukiwa huku ukipewa majina ya hajabu, utaitwa mjuaji, bush loyar, mzee wa protocol, mlokole nk.

Sasa Kuna nyakati huwa najiuliza hivi kama sisi tutakuja kujikomboa kweli kwenye hali hii inayoitwa ya umaskini au ndio bhasi tuendelee kuumizana mpaka Mungu mwenyewe atakapoamua kututoa kwenye hili janga.

Ni kweli kwamba asilimia kubwa ya watu ambao wanakula na kuchezea ofisi za Umma ni watu wanamaisha mazuri na wale wanaopenda haki wengi ni maskini ata maisha yao ya kawaida sana, sasa hali hii ndio inafanya wachache wapate mali na wengi wanaishia kwenye umaskini.

Na hakuna kitu kinakela sana kama mtu ukiwa unakibiashara flani ambacho wewe kama mtumishi umekianzisha na kinakulunguzia shida ,maneno utakayopewa ni kukatishwa tamaa tu, yaani watu hawaami katika kujiwekeza badala yake wanakutengenezea mazingira ukwame kiukweli inasikitisha sana.
Asanteni.
Anayesimamia Haki huwa hapendwi
Hata yeye huyo jamaa aliwachukiaga watu akiwemo Mzee Warioba kwa sababu ya kuisimamia Haki !
Haki na uovu huwa haviendi pamoja !!
 
Nakushauri kitu kimoja usile wala kunywa chochote hapo ofisini na ikiwezekana hata unapoishi hao wafanyakazi wenzako wasipajue. Watu wengi wameuawa kwa sumu au njia nyingine kwa misimamo ya kupenda haki kama wewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom