Jibu limejibiwa na Kabila01 japo hutaki kusikia na kasema hivi "Mie sio mwanachama wa chama chochote lakini napinga sana suala la mbio za mwenge. Wananchi wanajichanga wanajenga kadarasa kamoja, harafu unakuja kuzindua mwenge ambao ndani yake watu wamejilipa posho za 80,000 per day times 50 people. Bado wametumia magari waliyojaza mafuta pamoja na gharama za uchakavu. tunatumia milion 10 kwenda kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa choo cha shule? Kwa kweli tubadilike"
Na mimi naongezea, mbali na kuzindua mradi labda wa Zahanati iliyojengwa kwa michango ya wananchi na si serikali lakini mwenge unakuja unachangisha hao watu tena ili wazidue mradi wao, tuseme kwa uchache kila mtu kachanga 500, mfanya biashara 5000 zimepatikana katika kijiji hicho laki tano. Kwa hiyo wamekaribisha mwenge kuzindua zahanati yao kwa gharama za sh. 500000, sasa hao watu wazinduzi au wakimbiza mwenge nao wamelipwa posho ya kila siku 80000 watu 50 yaani (80000x50)+500000(michango ya kijiji)=4,5000,000, je wangemuita mkuu wa wilaya au mganga mkuu wa wilaya angekula hiyo milioni nne na nusu kwa siku moja? Sasa piga hesabu kuukimbiza nchi nzima ni mabilioni mangapi yameteketea. Ndio Chadema wanapinga ufisadi huo.
Nyongeza nyingine mwenge ni source ya ufusika na usambazaji wa ukimwi. Ukiangalia pale mwenge umelala yanayofanyika hapo Mungu tuhurumie, ni ulevi na kusambaza ukimwi tu.
Ningeendelea kukupa hasara za mwenge ila naona uchungu acha tu niishie hapo
Ni upotezaji wa muda na nguvu kazi maana badala ya watu kufanya kazi wako wanakimbiza mwenge tu