Kwanini CHADEMA wanauchukia Mwenge wa Uhuru?

Kwanini CHADEMA wanauchukia Mwenge wa Uhuru?

Kwa mda mrefu sasa wabunge wa chadema wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru,
Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge,
Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi,
Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.

Naheshimu mawazo ya kila mtu.
Ila ndugu yangu nashindwa kuamini kama mtu mwenye akili timamu na mpenda maendeleo anaweza akaunga mkono 'mbio za mwenge'. Yaani unashindwa kufikiri kwamba hiyo miradi inayozinduliwa na mwenge ingekuwepo hata bila mwenge!?
Mwenge haukuleta hiyo miradi, bali ukifika mahali flani wanatafuta kitu cha kuzindua. Ndio maana wamefikia hatua ya kuzindua hata 'Guest houses' za watu binafsi. Nimeshuhudia 'guest house' iliyozinduliwa na kiongozi wa mbio za mwenge.

Nadhani tatizo lako ni CHADEMA na wala sio mwenge
 
Bwana Rasta,naomba bajeti ya Limwenge kwa mwaka wa fedha 2012/2013 tafadhali.
 
Kwan bila mwenge miradi haifunguliwi?Chadema hawapendi mbio za mwenge kwani gharama za kukimbiza ni kandamizo tosha kwa wananchi(gharama za kukimbiza mwenga zinazidi zile za miradi inayofunguliwa),ni heri uwekwa makumbusho itasaidia kuletea pato kwa taifa
 
mbio za mwenge wa uhuru ni muhimu kwa taifa. miradi mingi ya maendeleo huzinduliwa na watu hujumuika na kufurahishwa na ngoma za kitamaduni. mbali na miradi ya maendeleo, mwenge unakuza utamaduni hapa nchini
 
Wewe ulishaona wapi watu wanapinga kila kitu hata cha manufaa kama siyo kupoteza utashi wa kimaendeleo ni nini?,
tafuta hotuba yoyote ya kiongozi wa chadema hutasikia akihamasiaha au kupongeza maendeleo fulani.
 
Wewe ulishaona wapi watu wanapinga kila kitu hata cha manufaa kama siyo kupoteza utashi wa kimaendeleo ni nini?,
tafuta hotuba yoyote ya kiongozi wa chadema hutasikia akihamasiaha au kupongeza maendeleo fulani.

Manufaa ya Mwenge ni nini?
Cant we do without it?
Or it is business as usual?
 
Utamaduni wetu, mbona kuna nchi za kifalme duniani na wale wafalme hawana kazi yeyote lkn wanaenziwa coz ni utamaduni wao
 
chadema walipinga mpaka ujio wa obama lakini wakabariki na kumpokea kiongozi wa denmark tena wakafanya naye kikao na wandishi wa habari.
 
Naheshimu mawazo ya kila mtu.
Ila ndugu yangu nashindwa kuamini kama mtu mwenye akili timamu na mpenda maendeleo anaweza akaunga mkono 'mbio za mwenge'. Yaani unashindwa kufikiri kwamba hiyo miradi inayozinduliwa na mwenge ingekuwepo hata bila mwenge!?
Mwenge haukuleta hiyo miradi, bali ukifika mahali flani wanatafuta kitu cha kuzindua. Ndio maana wamefikia hatua ya kuzindua hata 'Guest houses' za watu binafsi. Nimeshuhudia 'guest house' iliyozinduliwa na kiongozi wa mbio za mwenge.

Nadhani tatizo lako ni CHADEMA na wala sio mwenge
Maneno mengi lakini ya maana ni mawili tu,
kunahaja ya chadema kuacha kuropoka kwa kupinga kila kitu badala yake ijikite kuendeleza jamii zaidi kuliko kupinga.
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa chadema wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru,
Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge,
Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi,
Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.

Mkuu, miradi mingi inayozinduliwa kupitia mwenge wa uhuru ni pigo kwa chadema. hii inadhihirisha kuwa CHADEMA hawana dhamira njema kwa nchi hii
 
Maneno mengi lakini ya maana ni mawili tu,
kunahaja ya chadema kuacha kuropoka kwa kupinga kila kitu badala yake ijikite kuendeleza jamii zaidi kuliko kupinga.
sure Mkuu, viongozi wa CHADEMA ni hodari sana wa kuropoka
 
hili liko wazi chadema ni wapinga maendeleo hatushangai kupinga maendeleo yanayofanywa na serikali.

Tukiacha U-CHADEMA labda tupe mfano wa mradi ulowahi kutekelezwa kwa pesa za MWENGE. Usipende kutoa majibu ya jumla na matusi toa hoja kuthibitisha mchango wa mwenge katika maendeleo na jibu hoja kuhusu matumizi ya hovyo ili kuukimbiza mwenge
 
CHADEMA ni janga kwa taifa hili. Kila kitu kizuri kwao ni kibaya
 
Kwa akili yako mwenge ndio unaoleta maendeleo basi utabaki hivyohivyo. Maendeleo yanaletwa na watu. Unadhani marekani wamekuwa na maendeleo kwa kukimbiza mwenge? Wewe utabaki na mawazo ya kizee mpaka ufe. Chadema wanakwenda na maendeleo ya kisasa sio kula hela za wananchi kwa kukimbiza kibatari kinachoishia kueneza ukimwi. CCM chama kikongwe kanataka kuleta maendeleo ya kileo kwa mbinu za kizamani
 
Tukiacha U-CHADEMA labda tupe mfano wa mradi ulowahi kutekelezwa kwa pesa za MWENGE. Usipende kutoa majibu ya jumla na matusi toa hoja kuthibitisha mchango wa mwenge katika maendeleo na jibu hoja kuhusu matumizi ya hovyo ili kuukimbiza mwenge
Wewe naona umekurupuka. Kwani umeambiwa mwenge unapeleka fedha za miradi? Mbio za mwenge hutumika kuzindua miradi iliyotekelezwa kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato
 
Mwenge gharama yake ni kubwa kupindukia,siku unawashwa mpaka unazimwa hayo mafuta yake ni kiama na ujumlishe na gharama za posho mbalimbali za viongozi na wahamasishaji wengine katika kila wilaya ya Tanzania unapopita na mafuta ya magari yao ndo balaa kabisa.
Miradi inaweza kuzinduliwa hata bila mwenge mbona jamani!
Kituko siku hizi ni kuwa viongozi wa mbio za mwenge huzindua hadi nyumba za kuishi za watu binafsi na sio miradi ya umma.
 
kile ki mwenge kina fanya hao viongozi walio chaguliwa na serikali ya CCM wakipende kwa sababu wanaotea vitambi katika shughuli hiyo,of course katika nchi yetu wachache ndo wanao faidika , wananchi mtaupokea lakin baadae mtaishia kupigwa jua wenzenu wanakula tu chips kuku siku zinaenda
 


Mh.Kessy mbunge wa CCM leo amepinga Mwenge huu wa uhuru bungeni kwa kusema unarudisha maendeleo nyuma na kiini cha matumizi mabaya ya pesa.

mytake;
Mnavyozidi kuforce uwepo wa huu mwenge ndo mnazidi kutupa hari ya kuupinga na soon tutaufungia huu mwenge museum.
 
Back
Top Bottom