Kwanini CHADEMA wanauchukia Mwenge wa Uhuru?

Kwanini CHADEMA wanauchukia Mwenge wa Uhuru?

mtu mwenye utimamu wa akili lazima ajue mwenge ni kichocheo cha umaskini.
 
Kuna vitu katika nchi ni culture, wengine tumezaliwa tumeukuta mwenge now let's make it our culture..... Mbona kuna mwenge wa olympic na unakimbizwa dunia yote ...do u guys condem this too?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ni ujinga ambao unataka kujengwa katika taifa hili, kwa watu wenye akili hawawezi kuchukia mwenge kwani imekuwa.ikihamasisha miradi mingi sana ya serikali na binafsi na michango yake ni ya hiyari na kila mwaka imekuwa ikibeba ujumbe maalum ktk kuhamasisha jambo fulani la kitaifa, watanzania mbinu zinazorumiwa na cdm kutaka kuingia madarakani ni za kuchungwa na kuogopwa sana maana wanatumia kila njia kuonyesha kila jambo linalofanywa na serikali halina maana, hata kuchangia maendeleo wao ni dhambi huku wao wamekuwa wakitembeza bakuli kila mkutano wao kuchangisha pesa ambazo hata matumizi yake hayana maelezo ya kutosha.

hivi tunAa hitaji mwenge kuzindua miradi? au mwenge una hitaji miradi kuzinduliwa na kuzungushwa?
Mwenge ni moja ya kichocheo cha kusambaa kwa v.v.u hili haliitaji kuwa na degree kuelewa hili.

Mwenge umekuwa ukiongeza matumizi yasiyo na msingi wa tija.

hivi kweli kwa karne hii tuna hitaji mwenge hili kuleta maendeleo? na kama mwenge ungekuwa ni kichocheo cha maendeleo bila shaka wanafunzi mashuleni hadi leo wasinge kuwa wana kaa chjini?

Mwenge huu unachochea umaskini na magonjwa na hili haliitaji kuwa chadema kulijuwa hili.
Nani kakudanganya kuwa tuana hitaji torchi hili tuwe na maendeleo?

Mwenge ulikuwa na maana hapo zamani maana hata mawasiliano yalikuwa ni shida hivyo ilikuwa unatumiwa kueneza umoja na utamaduni lakini si sasa.
 
mwenge ni hasara kwa taifa,mwenge unazindua hadi grosari!,huu ni wehu wa aina yake,eti unamulika wezi? ina maana mwenge umeshindwa kumulika familia ya panya?.mbona wanaoukimbiza nao wezi? UKIONA JAMBO LINASHABIKIWA SANA NA MASISIEMU UJUE KUNA HARUFU YA UFISADI.
 
Mkuu umepinga nini na umekubari nini,sioni kama kuna gharama zozote za kuendesha mwenge ukilinganisha na faida zinazopatikana.

Mwenge haina faida yoyote. Infact hasara ni kubwa mno. Kwanza watumishi wanakatwa fedha pasipo kupenda. Watu wanlazimishwa kukesha wakiulinda mwenge kila unapokuwa. Kisha angalia gharama za kuukimbiza ikiwa ni pamoja na per diem za wanaoukimbiza. Lakini angalia kiasi cha kondomu zinazokusanywa mahali unapolala mwenge. Mwenge ungewekwa kwenye makumbusho ya taifa. Kwanza huo upendo na amani vipo wapi? Tuache kudanganyana.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Hujajibu swali kwa nini chadema wanaupinga mwenge wa uhuru hata sababu wanazotoa hazina maana.

kwa sababu mafisadi kupitia mgongo wa mwenge wanatafuna fedha za watanzania wakati umaskini unaongezeka.naamini bajeti inayotengwa kwa ajili ya mwenge kama ingewekwa hata kununua madawati nadhani nchi ingekuwa mbali sana.ni bora mwenge ukae makumbusho tuwe tunaupandisha mlima kilimanjaro kila 9 dec,yaani wakati wa sherehe za uhuru tu.lazima tufanye mambo kulingana na hali ya uchumi.nani alisema mwenge unaleta matumaini?nani alisema unaleta amani?nani alisema unamulika nje ya mipaka yetu?AMANI ITAPATIKANA WAPI WAKATI BAADHI YA WATU WAMEJIFANYA WAFALME NCHI HII,KAZI YAO KUBWA NI KUTUMIA MATATIZO YA NCHI KUPIGA HELA BADALA YA KUTAFUTA UFUMBUZI?MATUMAINI GANI NA WAKATI VIJANA WETU WANATEKETEA NA DAWA ZA KULEVYA AMBAZO ZINAUZWA NA HAO HAO WANAOSEMA MWENGE UNALETA MATUMAINI?AM SORRY BUT THIS IS STUPIDITY OF THE HIGHEST CALLIBAR.....INA MAANA BILA MWENGE MIRADI HAIZINDULIWI?MBONA MIRADI KIBAO INAZINDULIWA WAKATI MWENGE UMEZIMWA?ANAEZINDUA MIRADI NI MWENGE AU NI MTU?UNASHANGAA WATU WANACHOMA MAELFU YA KILOMETA NA KUTEKETEZA MAMILIONI YA SHILINGI KWA KUZINDUA DARASA LA LAKI TANO.HII AKILI AU MATOPE?MBONA MABADILIKO YA TECHNOLOJIA YAMEFANYA TUTOKE KWENYE ANALOGY KWENDA DIGITAL?KWANINI HALI YA UCHUMI NA UMASKINI WETU USITUFANYE TUTUMIE FEDHA YETU VIZURI.KWANGU MIMI MBIO ZA MWENGE NI USHENZI WA HALI YA JUU.
 
Hakuna mtz mwrenye akili timamu ataksye shabikia uendazimu mwenge, labda wewe
 
Hujajibu swali kwa nini chadema wanaupinga mwenge wa uhuru hata sababu wanazotoa hazina maana.

Wanapinga kwa sababu Kabila01 ameshakwambia kuwa Wananchi wanajichanga wanajenga kadarasa kamoja, harafu unakuja kuzindua mwenge ambao ndani yake watu wamejilipa posho za 80,000 per day times 50 people. Bado wametumia magari waliyojaza mafuta pamoja na gharama za uchakavu. tunatumia milion 10 kwenda kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa choo cha shule? kwa saabu hii kwanini CHADEMA wasipinge?
 
Tamko la kuwasha mwenge ni upendo; kama dhana pana na yenye hitajio la uchambuzi angavu. Mwenge ulisadikiwa uwashwe ili pale penye chuki pawe na upendo! Upendo uliolengwa hapa sidhani kama ni ule wa “mapenzi” ya ngono uzembe ambapo kwenye mikesha ya “mbio za mwenge” vijana wa kike na kiume wanajimwaga kama wapo kwenye “fiesta” huku wanakula na kuponda raha kana kwamba wapo Manhattan (New York)! Upendo uliyodhamiriwa na uwashwaji wa mwenge ni hali angavu ya thamani ya utu na ubinadamu wa kujali, kuhurumiana, kusaidiana katika hali zote, kushirikiana katika uzalishaji mali na kugawana pato la taifa kwa njia za uhuru, haki na usawa. Upendo uliyotakiwa ni kujitolea kwa masilahi ya watu wengine.Kukosekana kwa baadhi ya madhumuni ya mwenge na hakuna nia ya kweli kutoka kwa watawala wa chama cha mapinduzi kukemea kupotoshwa kwa madhumuni ya mwenge.umepelekea kuzuka kwa hoja za kuna umuhimu wa kuendelea kuwa na mwenge?
 
Tukiweka siasa pembeni, miaka hii ya 2000 naweza kusema malengo yaliyokusudiwa ya mwenge wa uhuru hayafikiwi kwa kuwa kinachofanyika ni usanii tu kwa watawala na watendaji wa halmashauri, miaka ya nyuma ni kweli kabisa ulikuwa unahamasisha maendeleo na ukipita katika wilaya yako kama hakuna miradi ya maana ya maendeleo basi mkuu wa wilaya na DED watakoma. Hivyo basi kwa mtaji huu walikuwa wanahakikisha bajeti iliyopangwa katika shughuli za maendeleo inatumika kikamilifu na mwenge unapopita inakuwa kama sehemu ya kufanya tathimini ya mradi pia inawafanya hata wale wazee wa kukaa kwenye maofisi kufika field kuona kilichoendelea

Lakini kwa sasa ni usanii, hata individual ukiwa una juhudi zako binafsi pasipo na juhudi ya serikali let say umefuga ng'ombe wako na kuchimba bwawa la samaki watakutafuta na kujifanya wameku-support na vitu kama hivyo au ukikaribia kuja wanaanza kupita kwa wadau kuona kama kuna chochote kama wanaweza kukiweka kwenye msafara wa mwenge huku wao kama serikali wanakuwa hawana cha kuonyesha, kwa mtaji huu ndipo umuhimu wa mwenge unapozidi kupungua
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru.

Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge, Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi.

Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.
Na wewe pia ni Great thinker?
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru.

Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge, Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi.
Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.
We ni mtu wa ajabu sana ,pia wazazi wako wanakazi ya ziada. Pole sana ndugu kichwani mwako ziko negative
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru.

Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge, Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi.

Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.
Mwenge wa Uhuru, Uhuru upi ?
Kunako huu Mwenge, Mimba nje nje,
Kunako huu Mwenge, UKIMWI nje nje,
Kunako huu Mwenge, Wake za Watu wanamegwa mno,
Kunako huu Mwenge, Watoto hawaendi Shule,

Mwenge unasadikiwa kuleta Matumaini ambayo in reality hayapo.

To hell na Mwenge wenu.
 
Kuna watanzania wajinga sana....yaani unatetea mwnge ...eti unazindua miradi...so bila mwenge miradi hakuna....
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru.

Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge, Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi.
Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.[/:ban:
 
Mwenge hauna humuhimu wowote katika taifa letu zaidi ya kuendelea kumkandamiza mwananchi wa chini afadhali hizo garama za kukimbiza huo mwenge wa mafisadi zingepelekwa kule vijijini kwaajili ya kuboresha miundombinu kuliko kuendelea kujaza matumbo ya mafisadi,kwa mtanzania yoyote yule mwenye akili zake timamu hawezi kufuraishwa na swala kama hili hata kidogo lakini kama ni fisadi lazima haunge mkono hoja
 
Kwa mda mrefu sasa wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakiendesha harakati za kupinga mwenge wa uhuru.

Najiuliza chadema wanachukia mwenge wa uhuru au wanachukia shughuri zinazofanywa na mbio za mwenge, Pengine wanadhani mwenge usipopita wao watazidi kuungwa mkono kwenye maeneo mengi.

Lakini imani yangu ni kuwa chadema wanapingana na maendeleo yanayozinduliwa na kufunguliwa wakati wa mbio za mwenge kwani wao ni wapinga maendeleo ili serikali ionekane haijafanya kitu,hizi siyo siasa bali ni kupotoka kwani siyo busara kupinga kila kitu.

Kuwasha moto na kuukimbiza bila sababu yoyote ya msingi ni matumizi mabaya ya kodi za walala hoi. Huo moto unaokimbizwa nchi nzima unatumia mafuta lita ngapi na ni sawa na sh. ngapi ukiachilia mbalia gharama za wanaoukimbiza. Gharama hizo zote zinaweza kununua vitabu kila mwanafunzi akapata kitabu chake na kujenga madarasa ya kutosha kisha yakazinduliwa hata na mwalimu mkuu au monitor/montress wa darasa.
 
Back
Top Bottom