- Thread starter
- #121
Masikini Manji.Sababu si hiyo mkuu ,magufuli aliuokota urais bila kutarajia,kilichotokea ni baada ya Lowassa kukatwa jina makusudi na kikwete,kikwete alikuwa anamtaka membe,sasa alipokatwa jina Lowassa ,usalama wa taifa waliokuwa kambi ya Lowassa wakatoa siri juu ya mil 750 zilizokuwa zimejaa kwenye mabegi zilizokuwa zimeletwa Dodoma na mhasibu wa manji maalumu kwa ajili ya kuwahonga wajumbe wa NEC ambao 85% walikuwa upande wa Lowassa ili wampitishe membe.
Baada ya siri kuvuja,mpango wa kikwete ukawa umeharibika,yakabaki majina matatu tu,1.Magufuli2.Amina 3.Migiro ndo kina mzee mwinyi na mkapa wakaona ni bora wampe magufuli tu,ila nyuma ya pazia ilikuwa ni furaha kubwa sana kwa mkapa ambaye alikuwa akimtaka magufuli ila hakuwa na uwezo wa kuchezesha karata zaidi ya kupendekeza jina lake ktk mchujo wa awali.
Kwa kikwete ilikuwa ni siku mbaya sana kuwahi kumtokea maishani mwake,kikwete anamjua magufuli vizuri mno,hampendi kabisa,na hata kumpatia uwaziri ilikuwa ni shinikizo la mkapa tu,na utakumbuka jinsi alivyokuwa akimtupa wizara tofauti tofauti.
Dhambi inayomtesa kikwete ni kumkata Lowassa makusudi,kwanza kashfa ya Richmond ilikuwa ni ya kutengeneza tu,ili kumchafua Lowassa mapema akose hadhi na mvuto wa Kugombea urais,kikwete ni mtu mbaya sana,usimwone na tabasamu lake hilo,nina mengi ya kuongea,nikisema niweke uzi maalumu wa hili jambo,mods watafuta tu.