Kwanini CCM iliwaacha wagombea bora ikatuletea Magufuli?

Kwanza naomba nikiri kuwa binafsi sikumchagua rais John Pombe Magufuli ingawa nilijua atashinda, sababu ni moja tu hakuwa mgombea bora.

Baada ya jina la Magufuli kupitishwa na mkutano mkuu wa CCM kuwa mgombea, wazo la kwanza lililonijia kichwani ni kuwa wajumbe wa CCM walijali maslahi ya chama zaidi kuliko nchi, kuwa walichoangalia wao ni chama kwanza kibaki salama lkn si kuteua mgombea bora ili aje kuwa kiongozi wa watanzania wote na sio kiongozi wa CCM.

Nikajiuliza, Usalama wa Taifa ulikuwa wapi kuzuia hili lisitokee, najua wasingeweza kupinga hadharani kutokana na maadili ya kazi lkn walikuwa na uwezo wa kuzuia kwa vile walijua fika udhaifu wa Magufuli.

Nilitaraji CCM watuletee watu kama Balozi Mahiga, Asha Migiro au Membe wazoefu wa diplomasia za kimataifa. Nilitegemea watuletee watu waadilifu wasio na doa kama kina Agustino Ramadhan, Mizengo Pinda, mama Samia au Shein, angalau basi wangetuletea jasusi la kimataifa kama Kitine kupambana na hujuma za majirani zetu kwenye soko huria la uchumi.

Hivi kweli CCM walishindwa vipi kuteua angalau mmoja bora kati ya hawa wagombea 38 waliojitokeza?

1. Bernard Membe
2. Balozi Mstaafu Agustine Mahiga,
3. Mizengo Pinda,
4. January Makamba,
5. Balozi Amina Said Alli,
6. Profesa Mark Mwandosya
7. Mama Samia Suluhu
8. Jaji Mstaafu Agustino Ramadhan,
9. Asha Rose Migiro.
10.Dk. Ali Mohamed Shein,
11.Dk. Hassy Kitine.

TUJISAHIHISHE, muda bado upo tusirudie makosa tena hapo 2020 tutajuta.

Mawazo huru kutoka kwa mwanaJF mzoefu Quinine.
Watasahihisha makosa baada ya kupata ushauri wa zito, aliutoa akiainisha kifungu cha tatiba 37(2) kitumike kuweka mambo sawa kabla nchi haijasambaratika
 
Yule ni balozi na mwana diplomasia kama alivyokuwa Kikwete.....hivyo hastahili kuwa rais kwani angechezewa akili na kudharauliwa na watendaji wake kama Kikwete. Rais ni mtu anayetakiwa kuwa na msimamo na a vision as Magufuli is, nitajei rais mwenye sifa kama Balozi Maiga aliyeheshimika ama kufanikiwa.
Uhuru Kenyatta.
 
Baada ya kusema hayo, hatukumsikia tena mpaka kifo chake kilipo fika - kilicho sababishwa na kushambuliwa na mbwa wake mwenyewe. Wakati mwingine kuweni na akiba ya maneno. Usije ukalipwa hapa hapa duniani kwa kuchongewa na mdomo wako.
Kwa hiyo kifo chake kina utata??
 
Kwanza naomba nikiri kuwa binafsi sikumchagua rais John Pombe Magufuli ingawa nilijua atashinda, sababu ni moja tu hakuwa mgombea bora.

Baada ya jina la Magufuli kupitishwa na mkutano mkuu wa CCM kuwa mgombea, wazo la kwanza lililonijia kichwani ni kuwa wajumbe wa CCM walijali maslahi ya chama zaidi kuliko nchi, kuwa walichoangalia wao ni chama kwanza kibaki salama lkn si kuteua mgombea bora ili aje kuwa kiongozi wa watanzania wote na sio kiongozi wa CCM.

Nikajiuliza, Usalama wa Taifa ulikuwa wapi kuzuia hili lisitokee, najua wasingeweza kupinga hadharani kutokana na maadili ya kazi lkn walikuwa na uwezo wa kuzuia kwa vile walijua fika udhaifu wa Magufuli.

Nilitaraji CCM watuletee watu kama Balozi Mahiga, Asha Migiro au Membe wazoefu wa diplomasia za kimataifa. Nilitegemea watuletee watu waadilifu wasio na doa kama kina Agustino Ramadhan, Mizengo Pinda, mama Samia au Shein, angalau basi wangetuletea jasusi la kimataifa kama Kitine kupambana na hujuma za majirani zetu kwenye soko huria la uchumi.

Hivi kweli CCM walishindwa vipi kuteua angalau mmoja bora kati ya hawa wagombea 38 waliojitokeza?

1. Bernard Membe
2. Balozi Mstaafu Agustine Mahiga,
3. Mizengo Pinda,
4. January Makamba,
5. Balozi Amina Said Alli,
6. Profesa Mark Mwandosya
7. Mama Samia Suluhu
8. Jaji Mstaafu Agustino Ramadhan,
9. Asha Rose Migiro.
10.Dk. Ali Mohamed Shein,
11.Dk. Hassy Kitine.

TUJISAHIHISHE, muda bado upo tusirudie makosa tena hapo 2020 tutajuta.

Mawazo huru kutoka kwa mwanaJF mzoefu Quinine.
mbona lowasa
simuoni.............. ngoja waje.. utaoga mitusi
 
Walijali kuokoa chama kwanza,hata nchi ikiaangamia,chama kwanza nchi baadae, si unaona yametimia,chama kinavolindwa kwa mtutu wa bunduki.Heri wangempa nywele nyeupe apambane na Slaa.
 
Which diplomasia unayozungumzia wewe aliyonayo Uhuru Kenyatta? Umesahau mauwaji baada ya chaguzi ya Kenya ile ya term ya kwanza ya Uhuru? Umeshawahi jiuliza kwanini Wakenya wanachukia Uhuruto?
Diplomasia ya Magufuli ni ipi, jana Uhuru amehutubia Baraza la Umoja wa Mataifa amejadiliana na wenzake kuhusu maendeleo ya nchi yake kimataifa sisi tumejifungia ndani na matrafiki tukinywa chai.
 
2020 ata sihitaji kusikia kampeni za mtu! tayari maamuzi ninayo kichwani mwangu kama 2015 alivyotangazwa tu JPM pale Dodoma tayari nilishauona muelekeo wa kura yangu.
 
Diplomasia ya Magufuli ni ipi, jana Uhuru amehutubia Baraza la Umoja wa Mataifa amejadiliana na wenzake kuhusu maendeleo ya nchi yake kimataifa sisi tumejifungia ndani na marafiki tukinywa chai.
Balozi Mahiga yupo huko kumuwakilisha Rais wakituletea jeuri miradi ya maendeleo tutakeleza wenyewe kwa fedha zetu za ndani kama kipande cha Dar to Moro cha SGR! magufuli alichaguliwa na watanzania wala sio west country huko.
 
Diplomasia ya Magufuli ni ipi, jana Uhuru amehutubia Baraza la Umoja wa Mataifa amejadiliana na wenzake kuhusu maendeleo ya nchi yake kimataifa sisi tumejifungia ndani na matrafiki tukinywa chai.


Kwani aliyehutubia UN ni Kenyatta peke yake tu, mbona kuna marais lukuki wamefanya hivyo pia pale jana.
 
Ulitaka niwataje wote, nimemtaja Uhuru kwa vile ndiye tuliyekuwa tunalinganisha diplomasia yake na ya Magufuli.


Sawa, sasa kwa akili yako.....unafikiri Uhuru ame gain nini baada ya kuzungumza ile siku? Viongozi wa kiafrika hata waongee huku wakilia nobody at UN takes them seriously.
 
Sawa, sasa kwa akili yako.....unafikiri Uhuru ame gain nini baada ya kuzungumza ile siku? Viongozi wa kiafrika hata waongee huku wakilia nobody at UN takes them seriously.
Au least onyesha machozi yako mbele ya jamii kuliko kulilia chumbani haisaidii.
 
Tuombe uzima tu mkuu 2025 tunawaletea chaguo la mioyo yenu hapo juu,kwny hiyo idadi ongeza na Makame Mbarawa na mama Samia
Makame Mbarawa atakuwa ni rais wa Zanzibar, Majaliwa rais wa JMT, Samia prime ninister, waziri kiongozi ama spika baraza la wawakilishi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom