Mkuu wangu Mwanakijiji majibu ulopewa nadhani viongozi wa CCM wanatakiwa kuyatazama kwa makini na kutafakari kwa sababu Ukweli upo kati yake..CCM wamekuwa wakipuuzia sana maswala muhimu ya Kichama badala yake wakafikiria kutumia fedha la ulaghai wakati wakitumikia Azimio la Zanzibar. Nakumbuka wakati wa Mwalimu wananchi wengi hawakujali umaskini wao, waliendelea kuulinda pamoja na machungu yote lakini leo wanapoona baadhi yao wakitajirika kwa jasho la wananchi na maisha na hakuna mwelekeo kabisa tumepoteza dira hapo ndipo wingu linapotanda juu ya CCM.
Tazama jinsi JK alivyoweza kuzoia kura mwaka 2005 kwa kuudangany Umma tu ya kwamba atakuwa tofauti na waliomtangulia na kuweka ule upinzani wake dhidi ya uongozi mzima wa CCM kwa kutoa ahadi zinazokabiri matatizo yao kisiasa ndipo alipowabiga bao kina Mbowe na Lipumba na wengine hata kusema ule utabiri wa Mwalimu kuwa ushindani utatoka CCM umetimia..
Leo hii wananchi hawadanganyiki tena na pengine niseme Ahsante Kikwete kwa kutuonyesha kwamba CCM haiwezi kuaminika tena lakini tukumbuke tu ya kwamba CCM bado ni maarufu sana. Tatizo la CCM ni kichwa, ni kukosa kiongozi ambaye ni MTU wa watu WATU mwenye kutukuza UTU..
Na amini maneno yangu akitokea mtu mwenye utashi na maarufu sana akaunda chama ama kujiunga na chama chochote cha Upinzani basi nina hakika kabisa CCM wataondolewa madarakani. Leo hii bado nina mashaka makubwa na viongozi waliojipanga kugombea Urais kmwaka 2015 na nachelea kusema kwamba CCM wanaweza kuitumia nafasi hiyo kumweka mtu ambaye atakuja na ahadi kama za JK na kwa sababu Wadanganyika ni wepesi wa kusahau, hawajifunzi kutokana na makosa na kuna uwezekano mkubwa sana wakarudia yale ya mwaka 2005.
Tazama jinsi JK alivyoweza kuzoia kura mwaka 2005 kwa kuudangany Umma tu ya kwamba atakuwa tofauti na waliomtangulia na kuweka ule upinzani wake dhidi ya uongozi mzima wa CCM kwa kutoa ahadi zinazokabiri matatizo yao kisiasa ndipo alipowabiga bao kina Mbowe na Lipumba na wengine hata kusema ule utabiri wa Mwalimu kuwa ushindani utatoka CCM umetimia..
Leo hii wananchi hawadanganyiki tena na pengine niseme Ahsante Kikwete kwa kutuonyesha kwamba CCM haiwezi kuaminika tena lakini tukumbuke tu ya kwamba CCM bado ni maarufu sana. Tatizo la CCM ni kichwa, ni kukosa kiongozi ambaye ni MTU wa watu WATU mwenye kutukuza UTU..
Na amini maneno yangu akitokea mtu mwenye utashi na maarufu sana akaunda chama ama kujiunga na chama chochote cha Upinzani basi nina hakika kabisa CCM wataondolewa madarakani. Leo hii bado nina mashaka makubwa na viongozi waliojipanga kugombea Urais kmwaka 2015 na nachelea kusema kwamba CCM wanaweza kuitumia nafasi hiyo kumweka mtu ambaye atakuja na ahadi kama za JK na kwa sababu Wadanganyika ni wepesi wa kusahau, hawajifunzi kutokana na makosa na kuna uwezekano mkubwa sana wakarudia yale ya mwaka 2005.