BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
Kutoka maktaba ya JamiiForums. Hivi CCM hii ya kuchota pesa toka hazina bila idhini ya Bunge, ya kukaa kimya pale miili ya Watanzania inapookotwa ufukweni, ya kukosa sera za kuwavutia wanachama wapya badala yake kutumia rushwa ya pesa na vyeo, ya kudharau katiba, mahakama m, Bunge na sheria za nchi, yenye kuleta hofu na taharuki kila kona nchini ndiyo CCM ambayo Watanzania wanaitaka? Kama ndiyo CCM hii ambayo Watanzania wanaitaka kwanini ihofie katiba mpya ya rasimu ya Warioba na Tume huru ya uchaguzi? Kwanini ihofie uchaguzi huru na wa haki?