Kwanini CCM Iko Matatani?

Kwanini CCM Iko Matatani?

Kwa kuwa wote (ccm) wameoza na kupungukiwa na utukufu wa Mungu
 
CCM imekumbatia siasa za kizamani. Inatumia propaganda kama silaha ya kwanza na kuu katika kushinda chaguzi. Mbinu hii ilikuwa very effective kwa miaka kadhaa iliyopita. Kwa sasa, ni vigumu sana kutumia njia hii ukapata kura.
CCM wanatakiwa kuufahamu na kuukubali ukweli huu kwamba watu wanahitaji solution ya matatizo yao ya kila siku na siyo kufahamu nani ana hati milki ya kuongoza nchi hii na nani ataleta vita. After all, watu wameshajua uhalisia wa mambo. Badala ya kuwachukulia vyama vya upinzani kama watu waliotumwa na wazungu kuirudisha nchi katika ukoloni(kama vile propaganda za CCM zilivyotaka), watu sasa wameng'amua usawa uliopo-wamefahamu kwamba vyama vyote ni vya watanzania na wote wana haki ya kuongoza nchi.
Ni vigumu kuwabadili CCM wakaacha utamaduni wao huu, na kwa hiyo ni vigumu CCM kuendelea kukubalika kwa watu.
 
Kiukweli ccm ilijisahau na ikawasahu wananchi walioiweka madarakani,Vile hawakuwa wakisoma nyakati,Waliendelea kudumisha old mordel sela na mwisho waelewa wamekuwa wengi,Challenge zimeongeza wameshindwa kwenda nazo kipindi hiki
 
CCM ni kama vile hawakuwaza kwamba kuna siku kutakuwa na upinzani aidha internally or externally. It has become a populist party ready to embrace anything or anyone ili kiendelee kutawala. They can side with corrupt pple, thieves, murderers, cons, you name it ili mradi tu kama hao waliotajwa wataihakikishia kutawala. CCM hii kamwe haiwezi kucheza "Samba" Wao wakifika golini, whateva it takes they just want to score, hawawezi kurudisha pasi nyuma kutengeneza formation na kusonga tena mbele. They have panicked, nervous,don't trust each other and worst of all they are too selfish.

The other factor kama ilivyoongelewa na baadhi yetu humu ni kwamba the party is now too big kwa hiyo CEO jk alitakiwa awe na mbinu mpya za kuiongoza. Kwa ukubwa ule style ya zamani ya Top - Down Management ni ngumu kuitekeleza. Mwalimu mfano aliwafahamu kivitendo karibu wenyeviti wote wa CCM mikoani na wilayani. I doubt kama JK anamfahamu hata Mwenyekiti wa CCM Kisarawe.

Halafu kingine ni kwamba viongozi wa CCM bado wanatawala kimazoea, hakuna tena weledi wala kanauni. Wapi chuo cha siasa Kivukoni?????? Je hao makatibu wa wilaya na wenyeviti wanasomea wapi uongozi? Have they managed anything before hizi kazi zao za sasa. Najua kuna watu watasema hata CHADEMA wamesomea wapi uongozi! I betcha kama na wao wakishika dola na mwendo ukawa kama huu wa CCM basi mambo still yatakuwa magumu. Mnakumbuka enzi zile kadi ya CCM ilikuwa mpake upigwe brash miezi mitatu? Siku hizi akina Nape just like Mrema enzi zile, sifa kuu ni kukusanya kadi za CHADEMA na kugawa za CCM as many as possible.

This party is tired, crooked, disorganized, weakened from within, unmanageable and gone... just gone! Wasitafute wachawi!!!!!!
 
CCM ni kama vile hawakuwaza kwamba kuna siku kutakuwa na upinzani aidha internally or externally. It has become a populist party ready to embrace anything or anyone ili kiendelee kutawala. They can side with corrupt pple, thieves, murderers, cons, you name it ili mardi tu kama hao waliotajwa wataihakikishia kutawala. CCM hii kamwe haiwezi kucheza "Samba" Wao wakifika golini, whateva it takes they just want to score, hawawezi kurudisha pasi nyuma kutengeneza formation na kusonga tena mbele. They have panicked, nervous,don't trust each other and worst of all they are too selfish.

The other factor kama ilivyoongelewa na baadhi yetu humu ni kwamba the party is now too big kwa hiyo CEO jk alitakiwa awe na mbinu mpya za kuiongoza. Kwa ukubwa ule style ya zamani ya Top - Down Management ni ngumu kuitekeleza. Mwalimu mfano aliwafahamu kivitendo karibu wenyeviti wote wa CCM mikoani na wilayani. I doubt kama JK anamfahamu hata Mwenyekiti wa CCM Kisarawe.

Halafu kingine ni kwamba viongozi wa CCM bado wanatawala kimazoea, hakuna tena weledi wala kanauni. Wapi chuo cha siasa Kivukoni?????? Je hao makatibu wa wilaya na wenyeviti wanasomea wapi uongozi? Have they managed anything before hizi kazi zao za sasa. Najua kuna watu watasema hata CHADEMA wamesomea wapi uongozi! I betcha kama na wao wakishika dola na mwendo ukawa kama huu wa CCM basi mambo still yatakuwa magumu. Mnakumbuka enzi zile kadi ya CCM ilikuwa mpake upigwe brash miezi mitatu? Siku hizi akina Nape just like Mrema enzi zile, sifa kuu ni kukusanya kadi za CHADEMA na kugawa za CCM as many as possible.

This party is tired, crooked, disorganized, weakened from within, unmanageable and gone... just gone! Wasitafute wachawi!!!!!!
Ha ha ha Naunga mkono hoja mia kwa mia
 
..kwanza I doubt it kama CCM bado iko.

..viongozi walioko sasa hivi wamekiuka msingi na zile imani ambazo CCM ilijitambulisha nazo.

..kinachofanyika sasa hivi ni maigizo[faking] tu kwamba CCM inasimamia imani zake za awali.

..it is just a matter of time ambapo wananchi watagundua uongo na ulaghai unaoendelea na kuachana na chama hicho.
 
Sisi Wananchi wa Jimbo la Muhambwe, tuliikataa CCM baada ya kuletewa mgombea wa Elimu ya Darasa la sita, ambaye ana sifa za Ujambazi na CCM wamempitisha kwa sababu tu ya Pesa zake.

Kosa la Muhambwe liliathiri hata majimbo mengine ya Uchaguzi mkoa wa Kigoma.

Hapo hata watu wa vijijini nao wanaona na wanachoka na wanatoa uamuzi wa kukataaa chama kilichowatupa.

CCM imeacha kuwa sauti ya wanyonge, si tena ya Wakulima na Wafanyakazi.
 
Sasa kuna majibu ya haraka na ya pupa. Na yapo majibu yanayohitaji kutafakari kidogo. Kwa haraka mtu anaweza kusema kuwa CCM iko matatani kwa sababu CDM wanapandikiza mbegu ya chuki kwa wananchi. Mwingine (katika haraka yake) anaweza kuja na kusema CCM iko matatani kwa sababu wameshindwa kujivua "gamba". Mwingine naye katika kujaribu kuelezea kwanini CCM iko matatani anaweza kuja na kusema kwa sababu ndani yake kuna "migongano".

Naomba kupendekeza kwamba kuna jawabu la kina zaidi. Naamini vyote hivi tunavyoviona ni dalili tu ya tatizo (symptoms). Sasa kwa wale ambao mnaifahamu CCM labda tangu ikiwa TAA hadi leo hii mnaweza kutusaidia na kuwasaidia vijana wetu kuelewa kwanini CCM iko matatani leo hii? Kwanini inajitahidi kutumia nguvu sana kushinda uchaguzi wakati zamani ilikuwa rahisi sana. Kwanini kwa mfano mwaka 2005 ilifanya vizrui sana kuliko wakati mwingine wa vyama vingi na miaka mitano baadaye ikafanya vibaya kuliko wakati wowote wa historia yake?

Katika majibu yetu tujaribu kuleta yote bila kujali ukweli wake. Ieleweke siulizii majibu ya kisayansi; najaribu kufanya brain storming ambayo inaweza ikatuelewa kwanini hiki chama ambacho kiliwahi kuwa mashuhuri zaidi, kupendwa zaidi na hata kuhofiwa leo hii kinaonekana kigeni machoni pa watu?

Jaribu kumwaga mtama uwanja uwanjani na kuku wakishaanza kudonoa na kuona ladha haijakole wataongeza vitunguu, nyanya, pilipili nk. Wengi wetu hatujazoea kuletea magogo tupasue kupata mbao za kujengea, ila tunauliza wapi mbao zipo. Si kosa letu na hakuna wa kumlaumu maana kazi ndo inaanza kuandaa kwa ajili ya ujio wa emanuel.
 
Kwasababu wengi wa wale wanaojiita wanachama wamekiuka misingi ya chama yaani haki, maelewano, upendo, umoja, mshikamano. Na mbaya zaidi wametoka katika hitikadi ya uhuru na umoja na ujamaa na kujitegemea vikiwakilishwa na jembe na nyundo na kuhamia kwenye ulafi na ufisadi vikiwakilishwa na uma na kisu.

Ni mwendelezo wa kufa kwa chama!
 
Mzee Mwanakijiji.
Majibu yaliyotolewa ni sawia kuongenezea jibu la swali lako ni KUWAPO KWA VIONGOZI WASIO NA UTU wanachojali ni maslahi binafsi kwa ufupi viongozi wa CCM hawawatumikii wananchi tofauti na wakati wa utawala wa Mwl. Nyerere (RIP). Katika kipindi chote cha utawala wa Mwalimu watanzania maisha yetu yalifanana mfumo wetu wa uchumi haukuwa umetoa mwanya mkubwa wa kuwapo kwa matabaka ya masikini na matajiri. Baada ya utawala wa Mwalimu viongozi wa CCM walipitisha maazimio mengi mojawapo ni AZIMIO LA ZANZIBAR ambalo lilidhiinisha rushwa ndani ya chama walichobadili ni jina waliita TAKRIMA. Mara tuu baada ya azimio la Zanzibar kupitishwa watanzania tulianza kushuhudia utitiri wa matajiri amabao vyanzo vyake vilikuwa ni ubadhirifu wa mali za umma. Watanzania wakati wa tunaingia kwenye mfumo wa vyama CCM kwa kuogopa itaingia matatani ilianza kampeni chafu za kuwalaghai wananchi eti vyama vingi vitavuruga AMANI. Watanzania walianza kupanuka kimawazo na kielimu, mambo mengi machafu yalianza kutolewa hadharani mara baada ya mfumo wa vyama vingi, hivi sasa CCM ipo matatani na itajizika yenyewe kutokana na matendo yake machafu. Upeo wa watanzania umepanuka sana vyombo vya habari vimesaidia sana kumuelemisha mtanzania, zile kauli za KIDUMU CHAMA CHETU MAPINDUZI wakati viongozi wachache na familia zao wananufaika kimaisha huku mamilioni ya watanzania wakiishi maisha duni haziisaidii CCM.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Je, tunaweza kuona mlingano wa aina gani kati ya tawala zilizotiikiswa za nchi za kiarabu na Tanzania? Nchi ambazo yawezekana zimejitahidi kufanya "vitu" vingi sana kwa wananchi wao lakini wananchi wao wameinuka dhidi yao kwa mshangao wa watawala hao?
 
The moment walipochagua wafanyabiashara kuwa nguzo ya chama, badala ya wakulima na wafanyakazi
 
Kweli imechoka ccm,imezeeka na haina mvuto ndio maana haina mvuto tena na ndio kitu inachokiweka matatani.
 
Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.ccm waliokuwa wanaccm wameshazeeka na wengine wamekufa.kwa maana hiyo waliokufa wamekufa nayo na waliozeeka wamezeeka nao.ndo maana hata wale ambao wapo wanatumia siasa za mwaka 47.mia
Mi nadhani tatizo sio uzee, ila nikwamba ccm wameacha msingi na lengo kuu la kuanzishwa kwake, Yaani Chama cha kutetelea Wananchi wa Tanzania, be they peasants or employees, Badala yake kimekuwa chama cha watu wachache tu, tena wenye uhusiano na viongozi wa juu wa chama. Hicho ndio kimesababisha watu kubadili mtizamo wao na kuanza kuona upinzani ni bora kuliko ccm.
 
Je, tunaweza kuona mlingano wa aina gani kati ya tawala zilizotiikiswa za nchi za kiarabu na Tanzania? Nchi ambazo yawezekana zimejitahidi kufanya "vitu" vingi sana kwa wananchi wao lakini wananchi wao wameinuka dhidi yao kwa mshangao wa watawala hao?

Of all those Arab countries hakuna kama Bahrain, they have got and been given almost everything except freedom. Nchi ndogo, watu wachache shule bure, afya bure, hela nje nje, ajira kibao lakini bado jamaa wanafanya uprising!!!!!
 
CCM Imekusa Dira, wamekosa Utaifa, Wanakula mali za nchi pekee yao wao na familia zao. Kubwa ni kuwa wamesahau kuwa nchi sio yao na familia zao tu. Wao wakila , wakisomesha watoto wao na kuwa na uhakika wa leo na kesho wanaona basi. wanakuja na pambio za Tumethubutu, tumeweza na tunasongambele kwa ufisadi.

Juzi nimemsikia waziri mkuu anadai bei ya umeme itapanda kwa sababu Serikali inabeba mzigo kubwa kuiendesha TANESCO. Pinda hajui fedha za kuiendesha serikali ni ZETU wananchi , anafikiri serikali ni yeye na wanae. Hajui kwamba kodi yetu kupitia manunuzi ya bidhaa mabalimbali, PAYE ,ndiyo zinamfanya leo awe Musoma leo. Eti serikali inabeba mzigo mkubwa!!! Si iutue basi wachukue watu wenye vision waone mambo yatakavo badilika. CCM kazi yao kuimba kwaya na ukimba vizuri unapewa cheo kama KOPA, KOMBA, na wengine wengi. Nchi haiongozwi kwa usanii na danadana za kila siku. Nawaombea wafauate mwelekeo wa KANU na UNIP

Rais wao kila siku yuko njee ya nchi kuomba na kubembea chama chake kimenyamza. Wanamwogopa eti mpaka wamnyan'ganye kofia ya Uenyekiti ndio wanaweza subutu kumfunga gavana. UOngo mtupu, CCM wengi wanapenda kujikomba kwa viongozi na kushindwa kuwambia wanapokosea mpaka wanapotoka madarakani. Wamejiwekea utaratibu wa mtu kumaliza vipindi viwili vya uongozi bila kujali anaongoza vipi.
 
ccm kama vile jinamizi, sirahisi kuliua ila inawezekana kulifungia ndani ya chupa kisha kutupa hiyo chupa kwenye kilindi cha bahari na kuiacha huko.
 
Je, tunaweza kuona mlingano wa aina gani kati ya tawala zilizotiikiswa za nchi za kiarabu na Tanzania? Nchi ambazo yawezekana zimejitahidi kufanya "vitu" vingi sana kwa wananchi wao lakini wananchi wao wameinuka dhidi yao kwa mshangao wa watawala hao?

Mlinganyisho ni kwamba tawala za nchi za kiarabu zinawanufaisha viongozi wao na watu wao wa karibu, pamoja na yote hayo wamejitahidi kuboresha maisha ya watu wao kwa kutumia rasimali yao (mafuta). Kwa upande wetu CCM inawanufaisha viongozi na familia zao pamoja na makundi ya wafanyibiashara ambao wamekuwa wakishiriakiana nao kufuja rasimali za Taifa. Tofauti kubwa kati ya mifumo hii miwili tawala za kiarabu angalau zimejaribu kuhakikisha huduma muhimu zinawafikia wananchi. Kwa upande wetu wananchi wanapata huduma kwa maneno tu wakati wa kampeni ahadi nyingi zinatolewa na hakuna kinachofanyika.Mfano hospital za Mwananyamala, Temeke na Ilala wagonjwa wanalala chini je hospital zilizopo mikoani zipo kwenye hali gani?
Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Ukitaka kujua kwamba CCM imeisha na ikaishiwa mfano katikati ya hili sekeseke la Igunga ikatokea say Rostam kampiga risasi mkewe, I can assure u anaweza aachwe kwanza mpaka uchaguzi upite............ Hahaha ahahah hiyo ndiyo CCM ya sasa.
 
Back
Top Bottom