Olumolongez
JF-Expert Member
- Dec 19, 2015
- 818
- 295
Marufuku hiyo ilishaondolewa.Anayetaka kufanya mkutano wa hadhara atoe taarifa kulingana na sheria.
Usiseme wakavunjwe miguu boss, kuvunjwa miguu unaona swala la kawaida sana. # Ogopa sana kauli yako hiyo* Yawezekana moja ya watakao vunjwa miguu ni Demu wako hujui wewe.CCM ndio chama kilichopewa ridhaa na wananchi kuongoza nchi. Ni chama dola. Na ndio maana mambo yanayoandaliwa na CCM na Serikali yake yanaenda vizuri. Maonesho ya sabasaba yanaendelea. Yanga wamecheza na TP Mazembe hawajazuiliwa. Kagame kawasili nchini. Ukiwa mtawala maana yake unatawala kila kitu. Nyie Bavicha Nendeni Dodoma mkavunjwe miguu
KAMA UNASEMA CCM NA CHADEMA NI SAWA BASI WAAMBIE HAO BAVICHWA WATIE PUA DODOMA WAONE KAMA WATAFANIKIWA KUZIMA MKUTANO WA CCM ZAIDI YA KURUDI WAKIWA NA VILEMA!!Nimesema CHADEMA na CCM vina tofauti nyingi ikiwemo ya CCM ni chama kinachounda serikali; kikatiba hakuna chama dola. Hata kama CCM ni chama tawala bado kinalazimika kufuata sheria za nchi. Hutaki kuelewa kwa sababu umezoea ndiyoooooo?
Hujielewi aiseee!mikutano yote ya ccm ni halali, mikutanp ya chadema hainaga tija!!
Sasa wanao andamana ni nani?logic kuandamana?
CHADEMA kama chama cha siasa kipo kila wilaya ya nchi hii lakini wamezuiwa kufanya mikutano ya siasa ikiwemo ya ndani. CCM pia ni chama cha siasa; haiwezekani wao wakiuke zuio la polisi.
Tumia akili kufikiri kabla ya kuandika mkuu,usichukulie mambo kishabiki,kwanza kabla ya kubandika maswali yako ungejiuliza maswali yafuatayo;Baada ya jana Baraza la vijana la CHADEMA (BAVICHA) kutoa kauli kuwa watakwenda Dodoma kusaidia CCM kutii sheria bila shuruti, kumetokea mijadala mbalimbali juu ya suala hilo. Wengine wakiunga mkono na wengine wakipinga kitendo hicho kwa madai kuwa kinachochea uvunjifu wa amani.
Jana kwenye group moja la Whatsapp Mbunge mmoja wa CCM (simtaji kwa sasa ila akisoma hapa atajifahamu) aliandika "Chadema njooni mtufanyie fujo Dodoma mvunjwe miguu"
Nikamuuliza nani kasema BAVICHA wanaenda Dodoma kufanya fujo?
Jana nimesikiliza agizo la Makamu Mwenyekiti BAVICHA Patrick Ole Sosopi hakuna popote aliposema wanakwenda Dodoma kuwafanyia fujo CCM. Alisema wanakwenda Dodoma kuwasaidia CCM kutii sheria bila shuruti kwa kuzuia mkutano wao.
Ili kuweka kumbukumbu sawa ikumbukwe kwamba June 7 mwaka huu Jeshi la Polisi lilipiga marufuku mikutano ya hadhara na maandamano kwa vyama VYOTE vya siasa, kwa kile kilichoelezwa kuwepo kwa taarifa za kiitelijensia kuwa kutatokea uvunjifu wa amani.
Tarehe 20 mwezi June, mkoani Dodoma jeshi la Polisi likatoa taarifa mpya kuwa zuio linahusu pia Makongamano na mikutano ya ndani ya vyama vya siasa. Kwa kutumia hoja hiyo wakazuia mahafali ya CHASO Dodoma, Kilimajaro, na kongamano la ujasiriamali lililokuwa lifanyike ukumbi wa KKKT Bariadi mjini (japo vyote hivyo vilikua vifanyike kama mikutano ya ndani).
Hata hivyo "Mheshimiwa Rais wetu mwema" JPM, akaongezea kuwa kwa sasa shughuli za siasa zisimame kwa muda ili watu wafanye maendeleo. Shughuli za siasa ni pamoja na mikutano ya ndani ya vyama vya siasa.
Hivyo basi shughuli za vyama vya siasa zilizozuiwa hadi sasa ni Maandamano, Mikutano ya hadhara, makongamano ya kisiasa na mikutano ya ndani.
#MaswaliMuhimu
1. Je CCM wanachokwenda kukifanya kipo ktk orodha ya vilivyozuiwa?
2. Je agizo la Polisi limefutwa?
3. Je agizo la Rais kuzuia shughuli za kisiasa limefutwa?
4. Je walichopanga kufanya BAVICHA ni sahihi?
#MAJIBU
1. CCM wanakwenda kufanya mkutano mkuu wa chama chao. Na kwa kuwa mikutano yote ya kisiasa imepigwa marufuku, CCM wamepoteza "legitimacy" ya mkutano huo. Kwa hiyo hadi sasa mkutano huo ni batili (until further notice).
2. Kuhusu agizo la Polisi bado halijafutwa.
3. Kuhusu agizo la Rais bado halijafutwa.
4. Kuhusu kauli ya BAVICHA, hawajakosea. Hii ni kwa sababu kwa maelezo yao hawaendi kufanya fujo. Wanaenda kuhakikisha CCM wanatii sheria bila shuruti.
Nimeona watu wakiuliza eti Polisi wameomba msaada kwa BAVICHA? Swali la hovyo sana hili, na wengi wanaouliza ni wenye uelewa finyu. Lakini majibu yake ni kwamba huhitaji kuombwa na Polisi ili kumkumbusha mwenzio kutii sheria. Kwa mujibu wa Katiba kila raia ana haki na wajibu wa kutii sheria na kumkumbusha mwenzie umuhimu wa kutii sheria za nchi.
Kwa hiyo suala la kumkumbusha mwezio kutii sheria ni wajibu wa kikatiba wa kila raia. Haihitaji kuombwa na jeshi la polisi wala jeshi la zimamoto. Kwahiyo BAVICHA wanakwenda Dodoma kutimiza wajibu wao huo kikatiba.
Kuna watu wanafikiri BAVICHA wanaenda Dodoma kufanya kazi za Polisi. La hasha. Hizi ni fikra nyingine mgando. BAVICHA hawaendi kufanya kazi za polisi.
Wanakwenda Dodoma kama raia kwenda kuwakumbusha raia wenzao (wanachama wa CCM) umuhimu wa kutii sheria bila shuruti. Kwa kuwa Rais amezuia shughuli za kisiasa, CCM wanapaswa kuonesha mfano kwa kutii agizo hilo la Rais. Wasipotii basi BAVICHA watasaidia kutii kwa kuzuia mkutano huo, ili kuondoa "double standards" ktk nchi. Hicho ndicho kinachowapeleka BAVICHA Dodoma.
#Nini_Kifanyike_ili_kuisaidia_Nchi?
1. BAVICHA wapongezwe kwa ujasiri wao.
2. Jeshi la Polisi litumie BAVICHA kama kielelezo cha kuwakumbusha raia umuhimu wa kutii sheria bila shuruti.
3. Mkutano mkuu wa CCM uahirishwe.
4. CCM wapewe onyo kwa kujaribu kuandaa mkutano wa kisiasa kinyume na agizo la Rais hali inayoonesha wanaweza kusababisha uvunjifu wa amani.
5. Yakishindikana hayo manne hapo juu, basi mikutano yote ya kisiasa iruhusiwe kuanzia leo.
#Nini_Kifanyike_ili_kuisaidia_CCM?
1. Rais afute agizo lake la kuzuia shughuli za kisiasa kwa muda (anaweza kuruhusu agizo hilo liendelee baada ya July 23, CCM watakapomaliza mkutano wao).
2. Polisi wafute agizo lao la kupiga marufuku mikutano, maandamano na makongamano ya kisiasa (wanaweza kuendelea na marufuku hiyo baada ya July 23, CCM watakapomaliza mkutano wao).
3. CCM waamue kufanyia mkutano wao nje ya nchi.
NB: Kukumbushana umuhimu wa kutii sheria bila shuruti ni wajibu wa kila raia. Tuwapongeze BAVICHA kwa kuliona hili.!
Malisa G.J
Unashauri nini sasa wewe?Waache wakachezee rungu.
Chai wataita kyai
Muhogo wataita muhoho
Wala asiachwe aende akathibitishe.Mkuu kauli uliyosema amemtuma yule kijana jiandae kudhibitisha
Kabisa boss! Hawa ndio wanaohitajika, akathibishe bila shaka.Hakuna mtu atakayekuja kukuchukua samasi itakufuata.
Ulichofanya ni kosa kubwa sana kwanza,
umeidharau mahakama iliyokwisha toa hukumu,
kosa la pili ni kusema uongo na kuiaminisha jamii kuwa kuna watu wanatuma watu kumtukana rais.
Ili Malisa kujiweka kwenye safe side lazima kauli (post) yako ukaikane mahakamani ili mtu mwingine yeyote asitokee kumtukana rais akasingizia katumwa na Malisa.
Atakuja na samansi!Songea unafanya nini si ulishasogezwa ama?
Kuwepo kila wilaya ni tofauti na kushinda kila jimbo/ wilaya kutokana na matokeo ya uchaguzi. Imarisha Chadema /Ukawa maeneo "tuliyoshinda" kwa kuwaletea wananchi maendeleo ya kiuchumi na kijamii kiasi cha kuwawezesha waondokane na fikra tegemezi! Hii "itatusaidia " kuwakabili wapinzani wetu 2020.
KAMA UNASEMA CCM NA CHADEMA NI SAWA BASI WAAMBIE HAO BAVICHWA WATIE PUA DODOMA WAONE KAMA WATAFANIKIWA KUZIMA MKUTANO WA CCM ZAIDI YA KURUDI WAKIWA NA VILEMA!!
Kweli nimeamini Mungu kakunyima akili na Maarifa pamoja na wenzako yaani ndiyo umejibu HOJA nzito kwa HOJA GOIGOI hivyo???CCM ndio chama kilichopewa ridhaa na wananchi kuongoza nchi. Ni chama dola. Na ndio maana mambo yanayoandaliwa na CCM na Serikali yake yanaenda vizuri. Maonesho ya sabasaba yanaendelea. Yanga wamecheza na TP Mazembe hawajazuiliwa. Kagame kawasili nchini. Ukiwa mtawala maana yake unatawala kila kitu. Nyie Bavicha Nendeni Dodoma mkavunjwe miguu
***maelezo ya kina upewe ww?? we ushaambiwa hakuna kufanya mikutano ya kisiasa, kama unabisha Fanya!! zingine ulizoandika ni porojo tu