Kwanini anga lina rangi ya blue?

Kwanini anga lina rangi ya blue?

Haya ni maoni yangu tu binafs,usiku anga ni jeusi na nyota tunaziona ,mchana kwa kuwa nguvu ya jua ni kubwa sana na anga nalo ni kubwa kupita kiasi ule weusi unapungua na kuonekana kama bluu hivi.View attachment 1245657
 
Hivi kuna teknolojia yoyote duniani ya kukamata particle za light na kuzihifadhi? Maana theorists wanataka kutuaminisha kuwa mwanga ni particles, je wameisha wahi kuziona, au hizo particle au photons ni nini hasa..
Kuna kitu inaitwa 'scattering' kama inavojulikana kwamba mwanga wajua una range tofauti za rangi na zenye wavelength tofauti kutoka x-ray hadi hizo blue..

Turudi kwenye swali.. why anga ni la blue.. sababu ni mwale unapotoka kwenye jua unabeba waves tofauti za rangi tofauti. Ktk hizo range rangi y blue ina wavelength kubwa yaani kipenyo chake kutoka crest moja kwenda nyingine, pia kitu chenye wavelength kubwa kina frequency ndogo ya kupenya vitu.. mfn xray ina frequency kubwa na wavelength ndogo ivyo unaweza pata pich ya mifupa.

Angani kuna particles tofauti, za gas na dust.. rangi ya blue inapogonga izo particles inatawanyika 'scattering' hivyo basi tunaona rangi ya blue.

Nimejaribu kudadavua ...
View attachment 1245596
 
Sunlight reaches Earth's atmosphere and is scattered in all directions by all the gases and particles in the air. Blue light is scattered more than the other colors because it travels as shorter, smaller waves. This is why we see a blue sky most of the time.
Hili ndilo jibu sahihi
 
Hivi kuna teknolojia yoyote duniani ya kukamata particle za light na kuzihifadhi? Maana theorists wanataka kutuaminisha kuwa mwanga ni particles, je wameisha wahi kuziona, au hizo particle au photons ni nini hasa..
Zinabaki kuwa ni theory tu mkuu.. wazungu ndio kazi zao hizo.

Sema zinatumika katika application mbalimbali kama mambo ya xray hayo au visible light inatumika kwenye production ya umeme (solar energy). Sijajua kama kuna teknoloji ya kuzikamata.. labda swali why wazikamate?
 
Swali zuri sana. Kwa mujibu wa neno la Mungu kinachoonekana cha blue ni Maji yaliyofungiwa kwenye kitu kama kioo.

Kwa utangulizi neno linasema

Mwanzo 1:1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

Mwanzo 1:2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Sasa unachokiona ni blue ni maji ya juu.
Mwanzo 1:6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.

Mwanzo 1:7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
Mi huyu jamaa sijamsoma hata kidogo aliye mwelewa anisaidie
 
Nakupa mfano mwepesi sana usipotafakari basi ukalale: Maji ya Ziwa , Maji ya Bahari ukiwa mbali huonekana Blue but ukisogea ukayachota yanakuwa Hayana rangi (colorless ) Hii inakuonyesha sehemu yoyote yenye kina kirefu ikipata mwanga kwasababu inakuwa aina mwisho kwa upeo wa macho yako basi huliflect rangi ya Retina ndani ya jicho la mwanadamu kuashiria hakuna Reflaction ya kutengeneza object ndani mfumo wa jicho.
Hapa ni sehemu ambapo bahari mbili zinakutana (Atlantic na Pacific), je kitaalamu hili lina uhusiano upi wa mwanga, rangi na hoja ulizozitaja hapo juu?
Ls3bRkZ-1000x500.jpeg
 
Mi huyu jamaa sijamsoma hata kidogo aliye mwelewa anisaidie
Ninacho maanisha ni kwamba kwa mujibu wa neno la Mungu juu kuna maji. Hayo maji ndio yanaonekana kama blue kwa chini.

Kama maji ya Bahari yanavyoonekana ya Blue na maji ya Juu ya Mbingu yanaonekana ya Blue.

Swali kwa nini anga lina rangi ya blue ni kwamba juu ya anga kuna maji .

Sasa kwa nini maji yakiwa mengi kama bahari yanaonekana ya blue hiyo wana science au wenye uelewa waje waseme.
 
jibu lake ninalo sema me sipendi show off kama king kiba
 
Hapa ni sehemu ambapo bahari mbili zinakutana (Atlantic na Pacific), je kitaalamu hili lina uhusiano upi wa mwanga, rangi na hoja ulizozitaja hapo juu?View attachment 1245895
Asante Sana kwa mfano huu sikutaka kwenda ndani zaidi ila nataka kukujuza kuwa macho yetu yanatoa rangi ya blue kwa sehemu ambazo mwisho wake huko mbali . Sasa mfano ulio toa huo unausisha layer za chini kabisa za bahari mbili izo .... Kiufupi bila kwenda kisayansi rangi ya maji inayoonekana ni blue ina kina kirefu Sana ambacho upeo wa macho yako huwezi fikia .. but upande wenye rangi tofauti utazamacho kwa macho Kama rangi tofauti ni rangi ya kitako Cha bahari, Yaani kitaalaam macho yameona mwisho wa bahari hiyo .... Mfano swimming pool uliflect rangi ya kuta kuwa ya maji ... Nadhani umenisoma
 
Inaonekena blue kwasababu ya mwanga wa jua Kuakisi Maji ya Bahari.

Kama unavojua, Asilimia kubwa ya sehemu ya dunia ni BAHARI.
Sahihisha hapo.maji ya bahari yanaonekana yana rangi ya blue kwa kuakisi rangi ya blue inayo onekana angani.
 
Inaonekena blue kwasababu ya mwanga wa jua Kuakisi Maji ya Bahari.

Kama unavojua, Asilimia kubwa ya sehemu ya dunia ni BAHARI.
Wakati huo huo inasemekana bahari na ziwa inaonekana blue sababu ya kuakisi anga
 
mbona usiku sio blue? kwasababu hakuna kitu kingine kinachoonekana basi utaona iyo rangi na jicho lilichagua iyo rangi ya blue
 
Anga lina onekana la blue kwa sababu the blue colour scatter more than any colour

The same scattering property of light linajibu kwa nn anga huonekana jekundu kipind jua linazama
 
Salute..

Naomba mnisaidie kufahamu hii kitu. Kwanini anga ni la blue? Nimejaribu kutumia ka elimu kangu ka Rangi na Reflection of Lights kutoka sekondari ila nimeshindwa kutambua.

Mimi nachofahamu rangi ya anga linaonekana hivyo lilivo kutokana na ukomo wetu wa kutazama, yaani hiyo rangi ya blue inaonekana kwakua hapo ndiyo macho yalipoishia kutazama.

Lakini pia kwanini tusione rangi zingine tunaona blue tu? Watalamu wa macho nisaidieni.

Karibuni mliopta shule....

Mkimaliza kujibu rangi mniambie mbinguni ni wapi, maana sijui watu wa Babeli walijenga vipi mnara ukafika mbinguni.
MICHANGO YA WADAU
Wick anasema...


Avatar mok


reyzzap
Big up umeleta kitu hatana mm huwa najiuliza lakini siku wahi pata majibu lakini shukurani kwa wana hao wametupa mwangaza
 
unaona blue kutokana na muda Mkuu,ukiwa na njaa hakuna rangi utaacha ona zote zitakuwepo
 
Asilimia kubwa ya Dunia ni maji, bahari imeipita ardhi kwa asilimia za mraba..

Anga inapata rangi ya BLUE kutokana reflection ya jua kupiga kwenye maji, yaani UBULUU wa Anga ni kioo cha maji..

Wakati wa Usiku Anga huwa nyeusi, kwasababu hakuna Jua linalomurika maji likapeleka mwanga wa Blue Angani.. 😊😊😊😊
 
Back
Top Bottom