APA CHICAGO
JF-Expert Member
- Oct 20, 2019
- 259
- 293
Ul
Uliyoyaandika hapa mkuu ni karibu hospitali zote nchini dispensary na vituo vya afyaMheshimiwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, hizi ni Hospitali pacha zenye uzoefu wa uzembe zina matatizo haya matatu;
Madaktari wako hospitali za Umma kama Kituo cha kutafuta Wateja na kuwaelekeza kwenye vituo vyao vya mitaani ikiwa ni pamoja na Hospitali za binafsi. Kuna sababu gani ya kuendelea kuruhusu Daktari kuhudumu Hospitali za mitaani? Je, Askari Polisi au Askari Jeshi anaweza pia kuhudumu Kampuni Binafsi za Ulinzi?
- Madaktari Wazoefu kuhangaikia Hospitali za Mitaani kuliko mwajili wao
- Kuwatumia Wanafunzi kujifunza bila Daktari mzoefu mbele ya mgonjwa
- Madawa ’feki’ kwa wingi ndani ya Hospitali
Nasikia NHIF wanawalipa kutokana na malipo ya Mgonjwa hii ni hatari! Inawafanya kujiingiza kwenye tiba kubwa hata wasizoziweza ili tu wapate pesa
Wanafunzi wamefikia hatua ya kufanya mitihani mbele ya Mgonjwa ambaye hajapewa huduma lakini anatumiwa kama Kituo cha mtihani. Bila hata kuomba samahani, ukiwa hospitali Daktari anajiona kama anakumiliki, ni specimen yake.
Kuna madawa ’feki’ mengi yako kwenye maduka ya hospitali hizi. Yaonekana ni kwa sababu kuna Wagonjwa wengi na waletaji wana dili zao na wahusika.
Mara nyingi utapewa dawa inayoaminika kufanya vizuri katika ugonjwa lakini ukitaka usalama bora ununue ya maduka ya mitaani
Utawala wa hospitali ujiangalie upya! Hili siyo kutafuta sifa.