Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,499
86,037
Kwa muda mrefu nilitaka kuandika hili la Sababu za "kitoto" za kuzuia magari yasisafiri usiku, hatimae Mbunge Tulia ameliona Hilo, tusubiri mamlaka zitekeleze. Mimi ni mdau wa safari za usiku sana, kwahio Wacha niwape experience....
1. Zile Coaster za Arusha zinazuiliwa pale Mkata wa saa Tano, matokeo yake, mkifika pale mnachangishana gari inaongeza wese mnazungukia Handeni, hii ni hatari.
2. Pale pale Mkata Kuna uchochoro, kwahio Dereva anazima Taa mnapita kwenye huo uchochoro kwenye makazi ya Watu, risk inazidi kuongezeka. Unajiuliza, hivi barabara ya Dar to Arusha Ina hatari Gani Hadi hizi gari zizuiliwe kama sio kutengeneza mazingira ya Rushwa tu?
3. Coaster za Dar to Mbeyaz wakifika Moro waliweka Picha ya Marehemu kuwa wanasafirisha msiba...tunajua kilichotokea, laiti ingekua ni route Hali.
4. Hivi kuna umuhimu Gani wa mabasi yote kuanza kufukuzana Pale stand kuu saa 12 asubuhi? Mfano, basi linalokwenda Kigoma, Kasulu, Musoma, n.k kwanini wasiondoke saa tatu asubuhi? Au saa Nne? Ili wasilale? Maana madereva ni wawili wawili, sasa watakimbizana kutwa nzima then watalala Kaliua saa nne usiku Hadi saa 12 asubuhi
5. Hivi kwanini Mabasi ya Bukoba, Ngara, Burundi, nk walazimishwe kulala Kahama na sio Nyakanazi? Siku hizi eneo lote liko salama.
6. Kwanini Mamlaka husika wasiruhu mabasi ambayo madereva wake na mabasi Yao yanatambulika kuliko hii ya kukata Kibali Cha Coaster Kila baada ya muda? Hatuna uhakika wa zile Coaster Wala madereva wake....

Inaendelea..

Inaendelea....

Muda huu ninapoandika hili ni 21:45 ukienda pale Mbezi Kituo Cha Daladala au pale Ubungo Kimara Kuna abiria wengi sana, hawa wanakwenda Mbeya, Dodoma, Mwanza na kwingine, huu ni mfano tu lakini situation kama hio utaikuta Dodoma CBE, Singida pale Nje, Makambako, Mbeya, Moro, Mombo-Tanga, na kwingine.....

Hawa wote wana-risk maisha Yao, kwanini tusiukubali ukweli kuwa route za usiku haziepukiki? Tuhalalishe hizi safari tupunguze ajali za magari ya IT na zile za magazeti, mfano, ndani ya miezi 36 MAGARI ya magazeti yameondoka na maisha ya watu wasiopungua Kumi, coaster za Usiku zimeondoka na maisha mengi the same to IT na Malori. Tukihalalisha tutapunguza tatizo

=====

“SERIKALI IRUHUSU MAGARI YA ABIRIA KUSAFIRI WAKATI WOTE HADI USIKU”- DKT. TULIA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ameitaka Serikali kuangalia upya utaratibu uliowekwa katika baadhi ya maeneo nchini wa kuyazuia magari ya abiria kufanya shughuli za usafirishaji nyakati za usiku kitu ambacho kinarudisha nyuma maendeleo ya kiuchumi.

Dkt. Tulia ameyasema hayo leo Novemba 10, 2022 wakati aliposhiriki Semina kwa Wabunge kuhusu usalama Barabarani iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyofanyika katika ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.

Amesema kuwa ni lazima ifike wakati sasa Wananchi waweze kufanya shughuli zao muda wote na kuondoa dhana iliyozoeleka ya magari ya abiria kuwekewa vikwazo vya kufanya kazi kwa sababu zizisokuwa rasmi wakati magari mengine yakiwemo ya mizigo yanaruhusiwa.

“Kunashida gani ya kuzuia gari ya abiria kusafiri usiku? Tunatamani nchi yetu kuchangamka Zaidi kiuchumi sasa kwanini magari haya yawe na zuio wakati magari mengine yanaruhusiwa kusafiri hadi usiku. Kama ni changamoto ya miundombinu basi ishughulikiwe na shughuli zifanyike” amesisitiza Dkt. Tulia
 
Kiukweli nami nakubaliana kabisa na ushauri wa Mhe Spika, ngoja tuone watatekeleza au watapuuzia?
 
Kwa muda mrefu nilitaka kuandika hili la Sababu za "kitoto" za kuzuia magari yasisafiri usiku, hatimae Mbunge Tulia ameliona Hilo, tusubiri mamlaka zitekeleze. Mimi ni mdau wa safari za usiku sana, kwahio Wacha niwape experience....
1. Zile Coaster za Arusha zinazuiliwa pale Mkata wa saa Tano, matokeo yake, mkifika pale mnachangishana gari inaongeza wese mnazungukia Handeni, hii ni hatari.
2. Pale pale Mkata Kuna uchochoro, kwahio Dereva anazima Taa mnapita kwenye huo uchochoro kwenye makazi ya Watu, risk inazidi kuongezeka. Unajiuliza, hivi barabara ya Dar to Arusha Ina hatari Gani Hadi hizi gari zizuiliwe kama sio kutengeneza mazingira ya Rushwa tu?
3. Coaster za Dar to Mbeyaz wakifika Moro waliweka Picha ya Marehemu kuwa wanasafirisha msiba...tunajua kilichotokea, laiti ingekua ni route Hali.
4. Hivi kuna umuhimu Gani wa mabasi yote kuanza kufukuzana Pale stand kuu saa 12 asubuhi? Mfano, basi linalokwenda Kigoma, Kasulu, Musoma, n.k kwanini wasiondoke saa tatu asubuhi? Au saa Nne? Ili wasilale? Maana madereva ni wawili wawili, sasa watakimbizana kutwa nzima then watalala Kaliua saa nne usiku Hadi saa 12 asubuhi
5. Hivi kwanini Mabasi ya Bukoba, Ngara, Burundi, nk walazimishwe kulala Kahama na sio Nyakanazi? Siku hizi eneo lote liko salama.
6. Kwanini Mamlaka husika wasiruhu mabasi ambayo madereva wake na mabasi Yao yanatambulika kuliko hii ya kukata Kibali Cha Coaster Kila baada ya muda? Hatuna uhakika wa zile Coaster Wala madereva wake....

Inaendelea..
Mwaka jana mwezi wa tatu, tarehe pendwa, 17.07.2021 nilipata bahati ya kusafiri kwenda Mafinga na basi la Majinja lililoanza safari ya kuelekea Mbeya saa 11 jioni pale Mbezi Magufuli. Hata ile breaking news niliipatia ndani ya basi.

Kipindi kile mabasi ya New Force na Majinja yalisafiri usiku kwa wiki moja kisha yakapigwa marufuku.

Tunataka safari za usiku zirudishwe kama miaka ya zamani
 
Root ya usiku imekaa Poa…Japo kuna changamoto kwenye barabara zetu haziruhusu root hyo ifanyike kwa fasaha.

Changamoto nyengine ni mabasi na madereva.
Hasa madereva wa Fuso pumbafu sana kuna siku walitaka kuniua saa sita usiku wanafukuzana watatu mpaka wanne akiovateki wa mbele wote wanaunganisha bila tahadhari

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Usalama wa barabarani iwepo mda wote, 24 hours. Kuna madereva wengine kutumia hii kama nafasi ya kumaliza dashboard ya basi. (120km/h). Matokeo:
Overspeeding.
Ajali
Drinking & Driving.
Trafgic wawepo mda wote na huduma zingenevyo ziwepo huko njiani. Mfano, sehemu za chakula, usalama wa abiria na mali zake. Ofisi za makamouni ya mabasi kuwa wazi, stendi iwe operational mda wote kutokana na mabasi kufika mda tofauti.
Pia, madereva wapate mda wakutosha kupumzika.

All in all, tusonge mbele!!
 
Barabara zote ni nzuri na zinaruhusu kusafiri usiku?
Mbona mna maswali ya kipimbi sanaa? Hivi mnajua miaka ya 90 mabasi yalikuwa yakisafiri usiku? Ngorika, Lang'ata kutoka Arusha kuja Dar, tena barabara ilikuwa mbaya maeneo mengine. Pale Mbwewe tulikuwa kunapiga sana vyuku... Iringa, Mbeya kulikuwa na Zainabu bus, Scandinavia etc... Songea kulikuwa na Kiswere nk.. Yote yalikuwa yakipiga ruti za usiku. Sasa tunaenda mbele au tunarudi nyuma?? Hatuwezi kuingia uchumi wa juu ikiwa watu hawawezi kufanya kazi usiku, eti hakuna kusafiri usiku na asubuhi Bus zinapangiwa wote waanze saa 12 wakimbizane njia nzima, haya mambo ya kiwaki sana aisee daaah.
 
Kwa muda mrefu nilitaka kuandika hili la Sababu za "kitoto" za kuzuia magari yasisafiri usiku, hatimae Mbunge Tulia ameliona Hilo, tusubiri mamlaka zitekeleze. Mimi ni mdau wa safari za usiku sana, kwahio Wacha niwape experience....
1. Zile Coaster za Arusha zinazuiliwa pale Mkata wa saa Tano, matokeo yake, mkifika pale mnachangishana gari inaongeza wese mnazungukia Handeni, hii ni hatari.
2. Pale pale Mkata Kuna uchochoro, kwahio Dereva anazima Taa mnapita kwenye huo uchochoro kwenye makazi ya Watu, risk inazidi kuongezeka. Unajiuliza, hivi barabara ya Dar to Arusha Ina hatari Gani Hadi hizi gari zizuiliwe kama sio kutengeneza mazingira ya Rushwa tu?
3. Coaster za Dar to Mbeyaz wakifika Moro waliweka Picha ya Marehemu kuwa wanasafirisha msiba...tunajua kilichotokea, laiti ingekua ni route Hali.
4. Hivi kuna umuhimu Gani wa mabasi yote kuanza kufukuzana Pale stand kuu saa 12 asubuhi? Mfano, basi linalokwenda Kigoma, Kasulu, Musoma, n.k kwanini wasiondoke saa tatu asubuhi? Au saa Nne? Ili wasilale? Maana madereva ni wawili wawili, sasa watakimbizana kutwa nzima then watalala Kaliua saa nne usiku Hadi saa 12 asubuhi
5. Hivi kwanini Mabasi ya Bukoba, Ngara, Burundi, nk walazimishwe kulala Kahama na sio Nyakanazi? Siku hizi eneo lote liko salama.
6. Kwanini Mamlaka husika wasiruhu mabasi ambayo madereva wake na mabasi Yao yanatambulika kuliko hii ya kukata Kibali Cha Coaster Kila baada ya muda? Hatuna uhakika wa zile Coaster Wala madereva wake....

Inaendelea..


Ni wachawi tu ndio mambo yao ni usiku, nguvu zao ni za giza.

Safari za usiku ni safari za kutoana kafara kwa nchi yetu, bado tupo nyuma sana kwa safari za usiku.
 
Back
Top Bottom