Kwaheri 2025, Ulikuwa Mwaka wa Majanga!. Yaliyopita si Ndwele, Tugange Yajayo!. Karibu 2026, Uwe Mwaka wa Kheri!. Ni Mwaka wa Katiba Mpya!, Inakuja..!

Kwaheri 2025, Ulikuwa Mwaka wa Majanga!. Yaliyopita si Ndwele, Tugange Yajayo!. Karibu 2026, Uwe Mwaka wa Kheri!. Ni Mwaka wa Katiba Mpya!, Inakuja..!

Unàsema yaliyopita si ndwele...kwa vile hakuna wa kwako aliyepigwa risasi, hukazika, hujauguza.... Hopeless!
Tukisema sisi akina mburumatata rukhsa kutubishia, haya sasa msikilize huyu
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emmanuel Nchimbi, ametoa wito kwa viongozi wa kisiasa, wanaharakati, na jamii kwa ujumla kuacha kurejea matukio yaliyotokea wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, ili kuruhusu Tume ya Rais kukamilisha uchunguzi wake bila upendeleo.

Huyu nae utambishia kuwa hajafiwa?.

P
 
Katiba itakayoundwa na huyu itakuwa kiini macho tu kama alivyofanya kwenye tume huru ya uchaguzi.
Be optimistic than pessimistic!
Suluhu ni Suluhu kung'atuka, halafu serikali ya mpito ije kushughulika katiba na reforms nyingine.
Hizi ndizo hoja hewa za utopian, haya yafanyike kwa mujibu wa kifungu gani cha katiba yetu, sheria, taratibu na kanuni zipi?
Mbona watu mnapenda kuzungumza hewa?.
P
 
Be optimistic than pessimistic!

Hizi ndizo hoja hewa za utopian, haya yafanyike kwa mujibu wa kifungu gani cha katiba yetu, sheria, taratibu na kanuni zipi?
Mbona watu mnapenda kuzungumza hewa?.
P
Hivi huna hata aibu?

Kwa mtindo huu tunaanzaje kusahau?


View: https://x.com/i/status/2016791551888744879

Yule mwanao Pascal Mayalla Jr angekuwa amepigwa risasi na kutupwa kama hawa ungekua umesahau saa hizi na kusema yamepita si ndwele?

Hii haitasahaulika wala haitasameheka mpaka ile siku mtu wa mwisho aliyesababisha haya naye achukuliwe hatua au kisasi kimfike.

Kinyume na hapo mnajifariji tu wala hatujasahau na ndio kwanza mwanzo kabisa.

20260203_103812.jpg
 
Hizi ndizo hoja hewa za utopian, haya yafanyike kwa mujibu wa kifungu gani cha katiba yetu, sheria, taratibu na kanuni zipi?
Mbona watu mnapenda kuzungumza hewa?.
P
Hayawezekani ni kweli, lkn siyo kwasabb ya ukosefu wa vifungu ktk katiba na sheria zetu, bali ni hulka na tabia ya Samia ya kutoheshimu matakwa ya wengi (demokrasia) na kutofuata sheria. Kifupi Samia ni dikteta.

Kwani alipokuwa anaiba uchaguzi mkuu wa 2025 alitumia vifungu vya katiba ipi na sheria zipi za nchi yetu?
 
Back
Top Bottom