Kwa wapenzi wa gospel karibuni

Kwa wapenzi wa gospel karibuni

msikilize na abiud misholi......baadhi ya nyimbo zake nakutajia jaribu kuzisikiliza..... (1) Ninasema (2) isaya (3) Biblia yasema (4) Baba (5) Usirudi nyuma (6) Simama mwenyewe (7) Nimebaki peke yangu (8) Moyo wangu wazi (9) Siku moja (10) Uje unitoe.

Hizo ni baadhi tu.....

sister we ndo umenena bhana....manyimbo ya kizungu aaah
 
Last edited by a moderator:
Mkuu we acha tu, huo wimbo mara ya kwanza kuusikia ilikuwa ni kupitia Redio Wapo Fm, mama mzazi alikuja kututembelea tupo sebuleni muda wa saa nane hivi ukaanza kupigwa.

Ulianza vizuri tu lakini alipofika kile kipande cha Kumamamammamamamamaaaaaa..eye yakhwe kumaaaa.....kuna kipande alisema....Kumamanayoo..nikatumia remoti kubadili nikatune PPR FM halafu nikamwambia mama naona wamekata matangazo ghafla. Hizi lugha zina mambo najua kwa lugha ya kwao hilo halina shida, shida huja pale unapoimbwa mbele ya waswahili.

Hahahahahaaaaa lol ukajua matusi jamani
 
hope mods wataitendea haki ha kupeleka jukwaa la dini.
 
Karibu tena mamitoo.....mi najiimbia kila siku nikiomba tuwapige Spurs siku ya fainali j2 lol.....!

Hahahahaha!!!! Unaniulia mbavu zangu, na Mimi naanza kuimba kila Siku ili tuchukue EPL lol
 
Kuna fanuel sedekia tangu nimekupanda mzabibu mwema na mpaka manukato na nishike mkono nisizame nazo nazifananisha na za abiud mishol wanaimba vizuri sana.
 
Hahahahahaaaaa lol ukajua matusi jamani

Halafu jamaa ana sauti imetulia na anauimba huo wimbo taratibu basi maneno yanasikika mi huwa nawahi naondoa nadhani hata redioni wanakosea kuupiga coz unatafsiri ngum sana kwa watanzania.
 
Kuna fanuel sedekia tangu nimekupanda mzabibu mwema na mpaka manukato na nishike mkono nisizame nazo nazifananisha na za abiud mishol wanaimba vizuri sana.
Fanuel Sedekia toka Enzi za Nilikupanda Mzabibu mwema, Tokeni katikati yao...nk mwishoni mwa miaka ya 90 mpaka Manukato achana nayo hiyo namba nyingine mkuu, Abihudi Misholi atasubiri kwanza.
 
Fanuel Sedekia toka Enzi za Nilikupanda Mzabibu mwema, Tokeni katikati yao...nk mwishoni mwa miaka ya 90 mpaka Manukato achana nayo hiyo namba nyingine mkuu, Abihudi Misholi atasubiri kwanza.

Namkubali sana Sedekia hasa katika ile Album ya Nyimbo za kuabudu tu, pia naupenda sana wimbo wa Manukato najiskia nimeingia patakatifu pa pakatifu ila Abiudi Misholi zaidi naingia patakatifu pa patakatifu pa patakatifu mwa Bwana, nasahau kabisa yale yanayonikabili nakuwa nimetiwa nguvu za ajabu siwezi elezea iwe ni Nyumbani, kazini ,kwenye gari,simu n.k huwezi kukosa kutoka kwangu wimbo wa Abiudi,sijawahi acha kununua Album yake hata moja katika zote alizonazo, hakika Mungu ambariki sana huyu Mtumishi wake.
 
Fanuel Sedekia toka Enzi za Nilikupanda Mzabibu mwema, Tokeni katikati yao...nk mwishoni mwa miaka ya 90 mpaka Manukato achana nayo hiyo namba nyingine mkuu, Abihudi Misholi atasubiri kwanza.

Kwakwel hata mimi sedekia ananibariki sana hasa cd yake ya katika ibada huwa nikickiliza nafarijika sana
 
Ni suala la kuelewa lugha na kumtukuza Mungu nyimbo za kizungu ni nzuri sana nimeanza kuzipenda kabla sijajua lugha vizuri mpaka sasa wanajua sana kufanya diction kwenye nyimbo zao.

kwa mtazamo wako unadhani ni kwa sababu sijui lugha. Pengine uko sahihi
 
hope mods wataitendea haki ha kupeleka jukwaa la dini.


Hatujadili mambo ya dini hapa bali tunafahamishana nyimbo mbali mbali za injili ambazo ni nzuri na zenye ujumbe mzuri hivo basi hakuna sababu kwa Mods kuuhamisha huu uzi na kuupeleka jukwaa la dini/imani.
 
Namkubali sana Sedekia hasa katika ile Album ya Nyimbo za kuabudu tu, pia naupenda sana wimbo wa Manukato najiskia nimeingia patakatifu pa pakatifu ila Abiudi Misholi zaidi naingia patakatifu pa patakatifu pa patakatifu mwa Bwana, nasahau kabisa yale yanayonikabili nakuwa nimetiwa nguvu za ajabu siwezi elezea iwe ni Nyumbani, kazini ,kwenye gari,simu n.k huwezi kukosa kutoka kwangu wimbo wa Abiudi,sijawahi acha kununua Album yake hata moja katika zote alizonazo, hakika Mungu ambariki sana huyu Mtumishi wake.


Nyimbo za injili ni nyimbo zinazoishi milele zote na zinabadilisha maisha ya wengi sn duniani na kufariji wengi nyakati za huzuni. Kweli Mungu anatawala kwa Busara na Upendo.
 
Nyimbo za injili ni nyimbo zinazoishi milele zote na zinabadilisha maisha ya wengi sn duniani na kufariji wengi nyakati za huzuni. Kweli Mungu anatawala kwa Busara na Upendo.

Ni kweli kabisa,nyimbo za injili ni ibada, maombi na sadaka kwa Mungu,ni njia mojawapo ya kupeleka ujumbe kwa haraka sana mbele za Mungu.
 
Ni kweli kabisa,nyimbo za injili ni ibada, maombi na sadaka kwa Mungu,ni njia mojawapo ya kupeleka ujumbe kwa haraka sana mbele za Mungu.


Yaah ni kweli kabisa........Ubarikiwe sn everlenk.
 
Last edited by a moderator:
Mimi joyous celebration ndo nawapenda sana,.wananibarik na nyimbo zao

Mkuuu hata mimi kwa joyous celebration nawapenda saana! Ingawa sometym siwaelewi bt nawapenda saana!
 
Wandugu kuna waimbaji wanaitwa Mungu Kwanza hwao jamaa ni hatari sana kwa shetani. Kama hujawahi kuwasikia/kuwaona tafuta Albam yao utanielewa ninachokisema, utadhani vijana wa Makoma wamerudi tena.
 
Back
Top Bottom