Kwa wale wazee wa suspension shuleni

Kwa wale wazee wa suspension shuleni

Nilipewa bun ya miezi sita kisa nilipigana na mwalimu staff room siku ya character assessment. Kuna mwalimu. Aliniletea shobo akaniuliza jina nikamtajia akaanza kujichekesha eti ahahahaah wewe ni kikabila ni mtani wangu lazima nikulambe mbalati(Fimbo) hata moja. Mm Nikagoma sasa yeye kuonesha umwamba kwa walimu wenzie akanikamata shingo kuniinamisha ndo utata ukaanza mara nikajamba ushuzi pyuuuuuuuuuuu. Walimu wa staff wakujua ticha mwenzao ndo kajamba wakawa wanamcheka yeye akaanza kujitetea kuwa sio yeye. Basi akaniuliza nani kajamba mimi au yeye mm nikamsonta yeye. Daaaaah ticha alimind sana akaanza kunipiga makofi
Ebwanaa nilipata hasira nikaanza kulia nilichana shati la mwalimu na walimu wote staff wakaingilia ugomvi wakati huo wanafunzi wa form 3 wapo foleni nje waingie staff daaaaaah mara nao wakavamia staff basi ikawa vita ya walimu na wanafunzi. Kama dakika 10 hivi mzee kinapigika ndani. Ikagongwa kengele ya dharula watu wakaenda assemble mimi nikajifanya nimezimia

Lakini nikashindwa coz moyo ulikuwa unadunda sana af nilivimba sana yale makondo ya uso aliyo nipiga usoni lakini na mimi nilimvunja meno ya sebuleni.
Basi tukiwa assemble huku mkuu haelewi kilicho tokea basi tukaruhusiwa mm nikaenda dispensary ya chuo nikapewa dawa nikawa najikanda na maji ya moto hadi nikapona
Basi kamati ya shule ikaunda kamati kuchunguza tukio. Mimi nikahojiwa na wale walimu wa staff wakahojiwa nikakutwa sina hatia. Ila mwalimu yule akapanic akasema kama mm sitapewa adhabu basi basi yeye atamuandikia afisa elimu wa wilaya kuacha kazi kwa jinsi nilivyo mdharilisha basi kamati ya shule kupitia mkuu wa shule wakaniambia wanisuspend kwa muda wa wiki 2. Mm nikakubali basi nikatangazwa assemble watu walimind sanaaaaa. Basi nikachukua begi langu wakati naenda kuchukua barua kwa secretary wa chuo, mkuu akanibakiza ofisini akaniuliza wewe kwenu wapi??? Nikajibu morogoro ifakara. Akaniambia sasa unaenda wapi?? Nikamwambia naenda kwa babu kyela-Mby bas akatoka akaniambia nimsubiri akaenda nyumbani kwake akarudi akanipa sh. Laki 2. Akanipa na namba ya simu nikipata shida nimpigie. Basi mm nikapanda costa hadi kyela nikawa nakula wali tu na maziwa kwa bibi huko kyela

Baada ya wiki mbili nikarejea shuleni kama shujaaa.
Wanafunzi walifurahi sana ikafika kipindi cha uchaguzi wa HP. Si unajua kwenye shule Olevel wanakua wengi kuliko Alevel basi mm nikachaguliwa kuwa HP na vise wangu alikuwa Form 5 akati mm form 3.
Basi katika zile ela laki mbili nikaenda kushona suruali mbili nzuri za shule na nikanunua na shati la mikono mirefu japo Olevel tulikua tunavaa mikono mifupi. Pamoja na viatu nilinunua basi nikawa smart sana na begi langu. Nikawa nna maisha mazuri sanaaaa hadi nikamaliza form 4

Mambo yote hayo yametokea Iyunga Technical secondary school Mbeya mjini pale

Hatariiiiiiiiiiii
Duuu,, km movie vilee……!!
 
Nilipewa bun ya miezi sita kisa nilipigana na mwalimu staff room siku ya character assessment. Kuna mwalimu. Aliniletea shobo akaniuliza jina nikamtajia akaanza kujichekesha eti ahahahaah wewe ni kikabila ni mtani wangu lazima nikulambe mbalati(Fimbo) hata moja. Mm Nikagoma sasa yeye kuonesha umwamba kwa walimu wenzie akanikamata shingo kuniinamisha ndo utata ukaanza mara nikajamba ushuzi pyuuuuuuuuuuu. Walimu wa staff wakujua ticha mwenzao ndo kajamba wakawa wanamcheka yeye akaanza kujitetea kuwa sio yeye. Basi akaniuliza nani kajamba mimi au yeye mm nikamsonta yeye. Daaaaah ticha alimind sana akaanza kunipiga makofi
Ebwanaa nilipata hasira nikaanza kulia nilichana shati la mwalimu na walimu wote staff wakaingilia ugomvi wakati huo wanafunzi wa form 3 wapo foleni nje waingie staff daaaaaah mara nao wakavamia staff basi ikawa vita ya walimu na wanafunzi. Kama dakika 10 hivi mzee kinapigika ndani. Ikagongwa kengele ya dharula watu wakaenda assemble mimi nikajifanya nimezimia

Lakini nikashindwa coz moyo ulikuwa unadunda sana af nilivimba sana yale makondo ya uso aliyo nipiga usoni lakini na mimi nilimvunja meno ya sebuleni.
Basi tukiwa assemble huku mkuu haelewi kilicho tokea basi tukaruhusiwa mm nikaenda dispensary ya chuo nikapewa dawa nikawa najikanda na maji ya moto hadi nikapona
Basi kamati ya shule ikaunda kamati kuchunguza tukio. Mimi nikahojiwa na wale walimu wa staff wakahojiwa nikakutwa sina hatia. Ila mwalimu yule akapanic akasema kama mm sitapewa adhabu basi basi yeye atamuandikia afisa elimu wa wilaya kuacha kazi kwa jinsi nilivyo mdharilisha basi kamati ya shule kupitia mkuu wa shule wakaniambia wanisuspend kwa muda wa wiki 2. Mm nikakubali basi nikatangazwa assemble watu walimind sanaaaaa. Basi nikachukua begi langu wakati naenda kuchukua barua kwa secretary wa chuo, mkuu akanibakiza ofisini akaniuliza wewe kwenu wapi??? Nikajibu morogoro ifakara. Akaniambia sasa unaenda wapi?? Nikamwambia naenda kwa babu kyela-Mby bas akatoka akaniambia nimsubiri akaenda nyumbani kwake akarudi akanipa sh. Laki 2. Akanipa na namba ya simu nikipata shida nimpigie. Basi mm nikapanda costa hadi kyela nikawa nakula wali tu na maziwa kwa bibi huko kyela

Baada ya wiki mbili nikarejea shuleni kama shujaaa.
Wanafunzi walifurahi sana ikafika kipindi cha uchaguzi wa HP. Si unajua kwenye shule Olevel wanakua wengi kuliko Alevel basi mm nikachaguliwa kuwa HP na vise wangu alikuwa Form 5 akati mm form 3.
Basi katika zile ela laki mbili nikaenda kushona suruali mbili nzuri za shule na nikanunua na shati la mikono mirefu japo Olevel tulikua tunavaa mikono mifupi. Pamoja na viatu nilinunua basi nikawa smart sana na begi langu. Nikawa nna maisha mazuri sanaaaa hadi nikamaliza form 4

Mambo yote hayo yametokea Iyunga Technical secondary school Mbeya mjini pale

Hatariiiiiiiiiiii
Wee jamaa unaonekana, maneno mengi sana mzaramo kasingiziwa
 
nakumbuka nilipigwa bani kisa mtoto mmoja wa kike alinizimikia kinoma halafu kuna ticha alikuwa anamtaka, basi yule ticha alikuwa anachafua CV yangu kila siku darasani sababu ya uyo mtoto wa kike tu!
wisho wa siku alifanikiwa kupanga mchongo wake, siku tumekaa assemble from no wapi natajwa jina niende mbele ya kandamnasi kosa... begi langu lina bangi na sijui lilifika vipi kwa ticha
nikala bani ya mwezi na wiki 2 narudi shule ili baki wiki 1 tufanye paper na nyumban sikusoma kwasababu ya maneno kibao kwa wazee, eti nimekuwa muhuni kama sitaki shule niseme tu! sio kupoteza hela kimaajabu kama hivo!
nili data kishenzi siku ya pepa lakini nililichana vizur tu! two yangu ya 19 swaaafi!
 
Nilimtiaga Mimba Mtoto wa Mwalimu Mkuu, Nikapigwa Suspension ya Miezi Sita (Shukrani kwa Wazee Wangu walikaa na Mwalimu Mkuu kiutu Uzima) kipindi hicho niko form two...Nikaamishwa shule na kuletwa Day, Nilipofika Form Four nilimtia Mimba beki tatu wa mwalimu wa Nidhamu, Nikapigwa Suspension mpaka mtihani wa Mwisho (NECTA)...Kutokana na hiyo misukosuko Watoto wangu huwa nawaitaga Suspension Squad (SS)
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Nashukuru O level na A level nimemaliza bila kula BAN.....
 
Siku moja bhana umeme ulikatika bwenini kuna dogo akawa anarushia watu viatu kwenye vyumba vyao..

Bahati mbaya kiatu kikanipata nikamtamfuta nikampata nikampa Onyo,kwasababu nilikuwa muhuni sana pale shuleni kila mtu alishangaa nilipomsamehe yule dogo..

Nikarudi chumbani kwangu huku kuna giza kali ile napanda tu kitandani kiatu hicho shavuni..

Nikamfuata Dogo Nikapiga kichwa kwasababu ya giza sijua napiga sehemu gani kile kichwa kikampata kwenye mfupa wa pua..

Dogo si akaanguka hapohapo huku damu zinamtoka puani alaf kama anashindwa kuhema nikajua nimeua ile nabeba bengi langu nitoroke Mlinzi wa bweni akanizuia kanishikilia mpaka asbuh dogo akakimbizwa hospitali..

Asubuh naingia school nilifurahi kumuona dogo mzima kasimama na head master..

Kuna mwalimu alikuwa anaitwa NDITI alikuwa na mwalimu wa nidhamu alafu hanipendi kishenzi hapo amesha attempt mara kibao kumshawishi head master nifukuzwe shule ila Head master alikuwa anakaza kwasababu nilikuwa naongoza darasani hvyo akawa anasema huyu ataitangaza shule Form4..Basi hiyo ndio ikawa chance ya Tr.Nditi bhana akashawishi kishenzi nifukuzwe..

Head master akaingia ofisini ikapigwa kengele ya dharura m nikajua hapa ndio mwisho wangu kusoma AGAPE,nikashanga head master ananipa sunspaaa ya wiki mbili tu..

Tr.Nditi alikasirika sana kwasababu wiki kazaa nyuma alinikuta Bar nimetoroka shule usiku akamwambia Head Master nikapewa tu adhabu ya kulima shamba la shule huko kwenye shamba la shule kuna ukuta wa bweni la wasichana nikatoboa katundu kadogo nikawa nachungulia mabinti wanavyooga, Tr.Nditi anakuja kukagua nilivyolima anakuta mtu nachungulia mademu akaenda kusema tena Kwa Head Master ,akashangaa Head master kaniambia tu andika barua..

AISEE MIMI NA HEAD MASTER TULIKUWA ZAIDI YA MAGUFULI NA BASHITE..
Hehe[emoji3]
 
O-level nipo form four nilipata ban ya mwezi, kwa kukutwa kwenye kijiwe cha wavuta bangi
Kulikuwa na operation ya kuwasaka wanafunzi wavuta bangi sikuwa nafahamu ( nilikutwa kijiweni hapo Niko na ciger mkonon) kwanza nilipigwa kichurachura hadi shuleni then nikapewa suspension
Baada ya mwezi nikarudi na mzazi, tulikuwa wawili tukala fimbo assembly na afisa elimu ( alikuja kama mzazi wa huyo mwengine)
Ban nyengine ilikuwa advance tuliongoza mgomo wa kudai haki zetu na kufanya maandamano ya kufa mtu
Walikuja FFU school tukafyata, tulikula kichapo tukapelekwa central tukalala siku moja then tukapewa susp ya mwezi mzima
Lakin fujo zote hizo nilikuwa vzr upstare o-level nikapiga one
Form six nikapiga one pia ( PCB)
Mmm?[emoji53]
Sii kwa ubaya mkuu
Hebu weka hicho cheti cha Advance tuthibitishe hiyo one ya PCB.
 
Mkuu smart911 ww hujawai kula ban shulen,, au nd ulkua kondoo kila kitu sawa tuu…!!
Shule nilizosoma mimi hayo mambo ya Ban na suspension ni nadra au kama hakuna kabisa... Ukiwa mtukutu sana unapelewa for counseling... Sana sana tu uandikwe kwenye black book... Hata viboko vyenyewe kuliko hakuna...


Cc: mahondaw
 
Shule nilizosoma mimi hayo mambo ya Ban na suspension ni nadra au kama hakuna kabisa... Ukiwa mtukutu sana unapelewa for counseling... Sana sana tu uandikwe kwenye black book... Hata viboko vyenyewe kuliko hakuna...


Cc: mahondaw
Hongera sana mkuu,, mim ningesom hiyo shule nahisi wangenishaur nihame tuu…!!!
 
nakumbuka long time, tumesumbuaga sana school zetu hizi za hoe hae. ilikuwa unalishwa mzigo wa kutosha hakuna adhabu ya kufukuzwa wala nini, labda kosa liwe kubwa sana.

maana hata kuna day majamaa tuliwahi mpandia ticha kwenye kagorofa ka juu alikuwa kalewa hovyo, watu wakabeba tv lake la chogo, deki na vhs yake ya prono, wakaenda nayo bweni, kuangalia.
 
Back
Top Bottom