Kwa wale wazee wa suspension shuleni

proskaeur

JF-Expert Member
Mar 8, 2017
1,562
4,899
Habari za asubuhi wapendwa,

Lengo la kuanzisha uzi huu sio kujisifia kwa kupewa suspension shuleni, najaribu kukumbuka tu yale yaliyofanya nikapewa suspension shuleni.

Nakumbuka katika maisha yangu ya shule nimebahatika kupigwa suspension mara mbili, ya kwanza nikiwa o-level na ya pili nikiwa advance.

O-level nilipgwa ban shuleni kisa tu nilimbishia mwalimu darasani kwa alichokua anafundisha alkua anakosea sas kumwanbia ukwel ikawa nongwa nikapigwa ban ya wiki mbili.

Advance nikala ban kwa kumtukana mwalimu mkuu mbele ya walimu wenzake,
kulkua na kikao cha wanafunzi na waalimu, sasa katika ku-present hoja nikajikuta mizuka imenipanda nikamropokea mkuu wa shule, hapo ndio nilisoma namba maana nilikula ban ya mwezi na wiki mbili plus kupewa barua ya kupitisha kwa Afisa elimu wa wilaya yangu nakotokea.

Sasa kimbembe kikaja kwenye kupeleka barua isainiwe na Afisa Elimu wa wilaya, nilimkuta Afisa Elimu complicator balaa, cha kwanza akanambia nitafute fimbo anipigie ofisini kwake halafu ofisi yake iko mjini ghorofa kama ya pili hivi, nikashuka kutoka juu nikazunguka kwa nyuma ya jengo nikamkuta mlinzi mmoja nikamuelezea situation nzima akanikatia fimbo, sasa naanzaje kupanda nayo juu ukawa mtihani mwingine.

Lakini nashukuru nilipompelekea fimbo akasema alikua ananijarbu kama naweza kuleta au nitafanya kiburi, akadondosha sahihi nikarudi zangu school, kila nikikumbuka huwa nabaki kujicheka mwenyewe.

Karibuni wadau kwa aliyewahi kula ban enzi za shule tupeane experience ilkuaje na ni nini kilisababisha upigwe suspension?
 
Nilimtandika tofali la kichwa mwalimu wetu mlezi alikuwa mnoko sana.
nikiwa kidato cha nne miaka hiyo u-boys-ni mwezi kama wa tatu naelekea kufanya mtihani wa geresho (mock) ticha mlezi akaingia bwenini usiku mida ya kama saa 4 hivi akatukuta tunasikiliza miziki dah ticha alimaindi kwanini tunasikiliza mziki na tuna redio bwenini, akachukua redio yetu.
nilipatwa na hasira kinoma nikaona kama uonevu wa hali ya juu na mimi sikuwahi kuwa na tukio lolote baya shuleni.
akiwa anaelekea kwenye bweni lingine nikamuokotea tofali lililo pembeni ya bweni tunayoezekeaga maua nikamwambia anisaidie kubeba kwa lazima nadhani force iliyotumika kubeba tofali lile ilikuwa ni newton 90
kesho nikapewa suspensio ya miezi 8 hadi kuja kufanya pepa la necta
hatari nashukuru Mungu nilifumua pepa kama kawaida na advance nikawa boya kweli hata nionewe vipi nikawa natulia tu.
 
Nilimtiaga Mimba Mtoto wa Mwalimu Mkuu, Nikapigwa Suspension ya Miezi Sita (Shukrani kwa Wazee Wangu walikaa na Mwalimu Mkuu kiutu Uzima) kipindi hicho niko form two...Nikaamishwa shule na kuletwa Day, Nilipofika Form Four nilimtia Mimba beki tatu wa mwalimu wa Nidhamu, Nikapigwa Suspension mpaka mtihani wa Mwisho (NECTA)...Kutokana na hiyo misukosuko Watoto wangu huwa nawaitaga Suspension Squad (SS)
 
Nilimtandika tofali la kichwa mwalimu wetu mlezi alikuwa mnoko sana.
nikiwa kidato cha nne miaka hiyo u-boys-ni mwezi kama wa tatu naelekea kufanya mtihani wa geresho (mock) ticha mlezi akaingia bwenini usiku mida ya kama saa 4 hivi akatukuta tunasikiliza miziki dah ticha alimaindi kwanini tunasikiliza mziki na tuna redio bwenini, akachukua redio yetu.
nilipatwa na hasira kinoma nikaona kama uonevu wa hali ya juu na mimi sikuwahi kuwa na tukio lolote baya shuleni.
akiwa anaelekea kwenye bweni lingine nikamuokotea tofali lililo pembeni ya bweni tunayoezekeaga maua nikamwambia anisaidie kubeba kwa lazima nadhani force iliyotumika kubeba tofali lile ilikuwa ni newton 90
kesho nikapewa suspensio ya miezi 8 hadi kuja kufanya pepa la necta
hatari nashukuru Mungu nilifumua pepa kama kawaida na advance nikawa boya kweli hata nionewe vipi nikawa natulia tu.
vip mkuu ww hukupewa barua ya kupitisha cjui kwa afisa elimu mara mwenyekiti wa mtaa…??
 
Nilimtiaga Mimba Mtoto wa Mwalimu Mkuu, Nikapigwa Suspension ya Miezi Sita (Shukrani kwa Wazee Wangu walikaa na Mwalimu Mkuu kiutu Uzima) kipindi hicho niko form two...Nikaamishwa shule na kuletwa Day, Nilipofika Form Four nilimtia Mimba beki tatu wa mwalimu wa Nidhamu, Nikapigwa Suspension mpaka mtihani wa Mwisho (NECTA)...Kutokana na hiyo misukosuko Watoto wangu huwa nawaitaga Suspension Squad (SS)
Hahahaaa,, ww ulkua kichwa ngumu sana mkuu…!!
 
Nilimtiaga Mimba Mtoto wa Mwalimu Mkuu, Nikapigwa Suspension ya Miezi Sita (Shukrani kwa Wazee Wangu walikaa na Mwalimu Mkuu kiutu Uzima) kipindi hicho niko form two...Nikaamishwa shule na kuletwa Day, Nilipofika Form Four nilimtia Mimba beki tatu wa mwalimu wa Nidhamu, Nikapigwa Suspension mpaka mtihani wa Mwisho (NECTA)...Kutokana na hiyo misukosuko Watoto wangu huwa nawaitaga Suspension Squad (SS)
Hahahahaha
 
Mi nlikula ban ya kutokupiga U.E kwa week mbili ikifuatiwa na ya kupigwa bench mwaka mzima kisha replay. Ila mungu ni mwema ntamaliza ka bachelor kangu.
Kisa ilikuwa kukichana chuo na kumwandikia magu aje kuwatumbua!
 
Siku moja bhana umeme ulikatika bwenini kuna dogo akawa anarushia watu viatu kwenye vyumba vyao..

Bahati mbaya kiatu kikanipata nikamtamfuta nikampata nikampa Onyo,kwasababu nilikuwa muhuni sana pale shuleni kila mtu alishangaa nilipomsamehe yule dogo..

Nikarudi chumbani kwangu huku kuna giza kali ile napanda tu kitandani kiatu hicho shavuni..

Nikamfuata Dogo Nikapiga kichwa kwasababu ya giza sijua napiga sehemu gani kile kichwa kikampata kwenye mfupa wa pua..

Dogo si akaanguka hapohapo huku damu zinamtoka puani alaf kama anashindwa kuhema nikajua nimeua ile nabeba bengi langu nitoroke Mlinzi wa bweni akanizuia kanishikilia mpaka asbuh dogo akakimbizwa hospitali..

Asubuh naingia school nilifurahi kumuona dogo mzima kasimama na head master..

Kuna mwalimu alikuwa anaitwa NDITI alikuwa na mwalimu wa nidhamu alafu hanipendi kishenzi hapo amesha attempt mara kibao kumshawishi head master nifukuzwe shule ila Head master alikuwa anakaza kwasababu nilikuwa naongoza darasani hvyo akawa anasema huyu ataitangaza shule Form4..Basi hiyo ndio ikawa chance ya Tr.Nditi bhana akashawishi kishenzi nifukuzwe..

Head master akaingia ofisini ikapigwa kengele ya dharura m nikajua hapa ndio mwisho wangu kusoma AGAPE,nikashanga head master ananipa sunspaaa ya wiki mbili tu..

Tr.Nditi alikasirika sana kwasababu wiki kazaa nyuma alinikuta Bar nimetoroka shule usiku akamwambia Head Master nikapewa tu adhabu ya kulima shamba la shule huko kwenye shamba la shule kuna ukuta wa bweni la wasichana nikatoboa katundu kadogo nikawa nachungulia mabinti wanavyooga, Tr.Nditi anakuja kukagua nilivyolima anakuta mtu nachungulia mademu akaenda kusema tena Kwa Head Master ,akashangaa Head master kaniambia tu andika barua..

AISEE MIMI NA HEAD MASTER TULIKUWA ZAIDI YA MAGUFULI NA BASHITE..
 
Ban ya Twoo Weeks 4m3 kisa ,nilikua kiongozi haraf nilijua kuna dalili za mgomo Halaf sikutoa taarifa kwa uongoz wa shule, na mgomo kweli ulitokea.
 
Siku moja bhana umeme ulikatika bwenini kuna dogo akawa anarushia watu viatu kwenye vyumba vyao..

Bahati mbaya kiatu kikanipata nikamtamfuta nikampata nikampa Onyo,kwasababu nilikuwa muhuni sana pale shuleni kila mtu alishangaa nilipomsamehe yule dogo..

Nikarudi chumbani kwangu huku kuna giza kali ile napanda tu kitandani kiatu hicho shavuni..

Nikamfuata Dogo Nikapiga kichwa kwasababu ya giza sijua napiga sehemu gani kile kichwa kikampata kwenye mfupa wa pua..

Dogo si akaanguka hapohapo huku damu zinamtoka puani alaf kama anashindwa kuhema nikajua nimeua ile nabeba bengi langu nitoroke Mlinzi wa bweni akanizuia kanishikilia mpaka asbuh dogo akakimbizwa hospitali..

Asubuh naingia school nilifurahi kumuona dogo mzima kasimama na head master..

Kuna mwalimu alikuwa anaitwa NDITI alikuwa na mwalimu wa nidhamu alafu hanipendi kishenzi hapo amesha attempt mara kibao kumshawishi head master nifukuzwe shule ila Head master alikuwa anakaza kwasababu nilikuwa naongoza darasani hvyo akawa anasema huyu ataitangaza shule Form4..Basi hiyo ndio ikawa chance ya Tr.Nditi bhana akashawishi kishenzi nifukuzwe..

Head master akaingia ofisini ikapigwa kengele ya dharura m nikajua hapa ndio mwisho wangu kusoma AGAPE,nikashanga head master ananipa sunspaaa ya wiki mbili tu..

Tr.Nditi alikasirika sana kwasababu wiki kazaa nyuma alinikuta Bar nimetoroka shule usiku akamwambia Head Master nikapewa tu adhabu ya kulima shamba la shule huko kwenye shamba la shule kuna ukuta wa bweni la wasichana nikatoboa katundu kadogo nikawa nachungulia mabinti wanavyooga, Tr.Nditi anakuja kukagua nilivyolima anakuta mtu nachungulia mademu akaenda kusema tena Kwa Head Master ,akashangaa Head master kaniambia tu andika barua..

AISEE MIMI NA HEAD MASTER TULIKUWA ZAIDI YA MAGUFULI NA BASHITE..
Hahahaaaa,, duuuh hatar kwelkwel,, na ukatok fresh kweny Necta…!!
 
O-level nipo form four nilipata ban ya mwezi, kwa kukutwa kwenye kijiwe cha wavuta bangi
Kulikuwa na operation ya kuwasaka wanafunzi wavuta bangi sikuwa nafahamu ( nilikutwa kijiweni hapo Niko na ciger mkonon) kwanza nilipigwa kichurachura hadi shuleni then nikapewa suspension
Baada ya mwezi nikarudi na mzazi, tulikuwa wawili tukala fimbo assembly na afisa elimu ( alikuja kama mzazi wa huyo mwengine)
Ban nyengine ilikuwa advance tuliongoza mgomo wa kudai haki zetu na kufanya maandamano ya kufa mtu
Walikuja FFU school tukafyata, tulikula kichapo tukapelekwa central tukalala siku moja then tukapewa susp ya mwezi mzima
Lakin fujo zote hizo nilikuwa vzr upstare o-level nikapiga one
Form six nikapiga one pia ( PCB)
 
Nilimtiaga Mimba Mtoto wa Mwalimu Mkuu, Nikapigwa Suspension ya Miezi Sita (Shukrani kwa Wazee Wangu walikaa na Mwalimu Mkuu kiutu Uzima) kipindi hicho niko form two...Nikaamishwa shule na kuletwa Day, Nilipofika Form Four nilimtia Mimba beki tatu wa mwalimu wa Nidhamu, Nikapigwa Suspension mpaka mtihani wa Mwisho (NECTA)...Kutokana na hiyo misukosuko Watoto wangu huwa nawaitaga Suspension Squad (SS)
Duh wewe ni nyoko kweli.
 
Nilipewa bun ya miezi sita kisa nilipigana na mwalimu staff room siku ya character assessment. Kuna mwalimu. Aliniletea shobo akaniuliza jina nikamtajia akaanza kujichekesha eti ahahahaah wewe ni kikabila ni mtani wangu lazima nikulambe mbalati(Fimbo) hata moja. Mm Nikagoma sasa yeye kuonesha umwamba kwa walimu wenzie akanikamata shingo kuniinamisha ndo utata ukaanza mara nikajamba ushuzi pyuuuuuuuuuuu. Walimu wa staff wakujua ticha mwenzao ndo kajamba wakawa wanamcheka yeye akaanza kujitetea kuwa sio yeye. Basi akaniuliza nani kajamba mimi au yeye mm nikamsonta yeye. Daaaaah ticha alimind sana akaanza kunipiga makofi
Ebwanaa nilipata hasira nikaanza kulia nilichana shati la mwalimu na walimu wote staff wakaingilia ugomvi wakati huo wanafunzi wa form 3 wapo foleni nje waingie staff daaaaaah mara nao wakavamia staff basi ikawa vita ya walimu na wanafunzi. Kama dakika 10 hivi mzee kinapigika ndani. Ikagongwa kengele ya dharula watu wakaenda assemble mimi nikajifanya nimezimia

Lakini nikashindwa coz moyo ulikuwa unadunda sana af nilivimba sana yale makondo ya uso aliyo nipiga usoni lakini na mimi nilimvunja meno ya sebuleni.
Basi tukiwa assemble huku mkuu haelewi kilicho tokea basi tukaruhusiwa mm nikaenda dispensary ya chuo nikapewa dawa nikawa najikanda na maji ya moto hadi nikapona
Basi kamati ya shule ikaunda kamati kuchunguza tukio. Mimi nikahojiwa na wale walimu wa staff wakahojiwa nikakutwa sina hatia. Ila mwalimu yule akapanic akasema kama mm sitapewa adhabu basi basi yeye atamuandikia afisa elimu wa wilaya kuacha kazi kwa jinsi nilivyo mdharilisha basi kamati ya shule kupitia mkuu wa shule wakaniambia wanisuspend kwa muda wa wiki 2. Mm nikakubali basi nikatangazwa assemble watu walimind sanaaaaa. Basi nikachukua begi langu wakati naenda kuchukua barua kwa secretary wa chuo, mkuu akanibakiza ofisini akaniuliza wewe kwenu wapi??? Nikajibu morogoro ifakara. Akaniambia sasa unaenda wapi?? Nikamwambia naenda kwa babu kyela-Mby bas akatoka akaniambia nimsubiri akaenda nyumbani kwake akarudi akanipa sh. Laki 2. Akanipa na namba ya simu nikipata shida nimpigie. Basi mm nikapanda costa hadi kyela nikawa nakula wali tu na maziwa kwa bibi huko kyela

Baada ya wiki mbili nikarejea shuleni kama shujaaa.
Wanafunzi walifurahi sana ikafika kipindi cha uchaguzi wa HP. Si unajua kwenye shule Olevel wanakua wengi kuliko Alevel basi mm nikachaguliwa kuwa HP na vise wangu alikuwa Form 5 akati mm form 3.
Basi katika zile ela laki mbili nikaenda kushona suruali mbili nzuri za shule na nikanunua na shati la mikono mirefu japo Olevel tulikua tunavaa mikono mifupi. Pamoja na viatu nilinunua basi nikawa smart sana na begi langu. Nikawa nna maisha mazuri sanaaaa hadi nikamaliza form 4

Mambo yote hayo yametokea Iyunga Technical secondary school Mbeya mjini pale

Hatariiiiiiiiiiii
 
Back
Top Bottom