Kwa Ukali Dr Kitila Amjibu Ansbert Ngurumo

Kwa Ukali Dr Kitila Amjibu Ansbert Ngurumo

Status
Not open for further replies.
Dr Kitila. Dalili za mkosaji ni pamoja na kutumia muda mwingi kujitetea ingawa sio wote wanaofanya hivyo ni wakosaji. Ni kama vile ukiona mtu anahitaji sabuni nyingi na maji mengi wakati wa kuoga basi ujue yawezekana kachafuka sana na kweli akawa kachafuka kwa sababu hakuwa anafanya kazi au anacheza katika mazingira yaliyo safi. Na mfamaji haachi kutapa tapa. Natumaini utanielewa

acha kumtisha dr kitila we ni sisimizi tu ndani ya chadema - tunataka kuujua ukweli pumba na mchele ni upi?!
mbona wakati ule viongozi wa chama wanazunguka kuwananga dr na wenzie hukusema wanajitetea kwa lawama za kubaka demokrasia?!
mkuki kwa binadamu kwa nguruwe mchungu eeh!
dr eleza yote, unatusaidia tusiokuwa wafuasi kujua tabia halisi za 'wakombozi' wetu................
 
Kusema 'kwa ukali' ni kujaribu kufanya unnecessary amplification ya jambo ambalo hata halipo, labda kutaka kuharibu mjadala tu.

Ni vigumu kuelewa kwa nini wanatumia hata uongo kuhalalisha hoja zao au matendo yao dhidi ya CHADEMA. Ni kitu kinachoshangaza sana.

But it tells a lot.

Mimi nina Maswali yangu kwa Dr Kitila Mkumbo.

1. Je waraka alianza kuuandika lini?
2. Kwa nini anaona ni sahihi yeye kuhukumu watu wengine kwa makosa ambayo hataki kuyaweka wazi, anaona si democrasia kwa namna gani?
 
Kusema 'kwa ukali' ni kujaribu kufanya unnecessary amplification ya jambo ambalo hata halipo, labda kutaka kuharibu mjadala tu.

Ni vigumu kuelewa kwa nini wanatumia hata uongo kuhalalisha hoja zao au matendo yao dhidi ya CHADEMA. Ni kitu kinachoshangaza sana.

But it tells a lot.

Mkuu Tumaini Makene hapa umejibu hoja? Hebu twambie na uthibitishe uongo wa kitila.mkumbo.


Hapa tunataka uje na hoja si maneno matupu na hikiwezekana na umpe mualiko AnsBERT.

NI WAZI HII HOJA YA LEO HIMEKUWA NZITO SANA KWAKO.NA HII IMEDHIHIRIKA KWENYE HILI BANDIKO LAKO.

HIVI NI LINI ULISHATUMIA MUDA WAKO KUIKOSOA CHADEMA NA NI WAPI NA KWENYE JAMBO LIPI?

HAKUNA ASIYEJUA KUWA CHADEMA INAENDESHWA KWA MKONO WA CHUMA NDIO MAANA INA WARADHIMU WANACHAMA KUAMINI CHADEMA KUWA HAINA MAPUNGUFU NA WALA VIONGOZI WAKE HAWANA MAPUNGUFU.


HIVI KWELI KAMA MTU ANAWEZA KUPIGWA MBELE YA MWENYEKITI NA AKAPATA UJASIRI WA KUKISOA CHAMA?

HAKUNA ASIYE JUA KUWA MAKADA WENGI WA CHADEMA WANA SHINDWA KUKIKOSOA CHAMA KWA HOFU YA KUFUKUZWA AU KUITWA WASALITI NDIO MAANA WENGINE WANA TAFUTA NJIA YA KUSEMA.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hapa anajicontradict mwenyewe ingekuwa kweli CHADEMA haikui asingeisema kwenye makala yake niajabu katika vyama vinavyo karibia ishirini mtu anakazana kutaja CHADEMA lakini namshukuru mwishoni kaliweka vizuri kwamba yale yalikuwa maoni yake .

Mimi maoni na mtazamo wangu CHADEMA inakua tena kwa kiwango kizuri kabisa ndo maana karibu sehemu nyingi hata ambazo wengi walitarajia na kuzoea CCM ikishinda kwa mbwembwe kulikuwa na kukabana koo na mtu anatoka na ushindi mwembamba tena sehemu za vijijini kabisa .

Katika ukuaji wa CHAMA is a gradual Process ,Siasa siyo Mechi ya Ndondo hapana ni hatua na kila hatua inachangamoto zake tunachotaka kuangalia ni chama kipi kinauwezo wa kuyamsimamia kile kinacho ya sema jibu moja ni CHADEMA.kILA MWENYE AKILI HILI ANALITAMBUA Mf.tunaongelea Katiba Mpya ..katika eneo hili CHADEMA haijatetereka,Kuchukua maamuzi magumu na ya msingi katika kulinda na kujenga nidhamu ya CHAMA...hapa CHADEMA na CUF ni wakupigiwa mfano na siyo CCM ambao wanalalamikia kwenye vungu za vitanda na wengine wakiwa wamevaa vinyago usoni(Kulalamika kupitia Mamluki).

Itakuwa ni kosa kubwa sana kwa CHADEMA kusikiliza ushauri mbovu eti kwa kisingizio cha kulinda mtu...hapana mtu hana nidhamu fukuza ...Hiki ni chama siyo kikundi cha wavuta bangi.Lazima kuwe na nidhamu ya Chama.Ni hatari mtu kujikweza na kuleta uhuni kama waliofanya hao "WAFUKUZWA" kwa kukosa nidhamu na kujiona yeye kuwa bora kuliko wengine. Viongozi wako sahihi ,na CHAMA kiko katika uelekeo mzuri zaidi ni aibu kwa msomi yeyote kuzungumzia matokeo haya na kujidai kipofu kwa kuto kuzungumzia na kuona athari zinazotokana na Tume ya uchaguzi kusuasua katika uboreshaji wa daftari la wapiga kura.

Hata cc mateja na wavuta bangi tunaheshimu taratibu, kanuni na sheria tunazojiwekea gheto na maskani na akijitokeza mnafiki/msaliti adhabu atakayopata ni kali na ikiwezekana kifo kabisa
 
Dr. Kitila Tumbo hapo tu ana elimu lkn hajitambui sijui angekuwaje kama angekuwa hajasoma.

Watu wenye safari moja hamuwezi kufichana jambo la kuwafikisha salama mnapotarajia kufika.
 
mimi nina maswali yangu kwa dr kitila mkumbo.

1. Je waraka alianza kuuandika lini?
2. Kwa nini anaona ni sahihi yeye kuhukumu watu wengine kwa makosa ambayo hataki kuyaweka wazi, anaona si democrasia kwa namna gani?

hunatoka nje ya mada.
Kama unataka mada kuhusu waraka anzisha thread maalum kwaajili ya hili swala.
 
acha kumtisha dr kitila we ni sisimizi tu ndani ya chadema - tunataka kuujua ukweli pumba na mchele ni upi?!
Mbona wakati ule viongozi wa chama wanazunguka kuwananga dr na wenzie hukusema wanajitetea kwa lawama za kubaka demokrasia?!
Mkuki kwa binadamu kwa nguruwe mchungu eeh!
Dr eleza yote, unatusaidia tusiokuwa wafuasi kujua tabia halisi za 'wakombozi' wetu................

mkuu goodluck5 hii mada ni mwiba kwa chadema na hakuna anaye weza kujibu.
 
Last edited by a moderator:
sina tatizo na hoja za Kitila mkumbo ila tatizo langu ni kuwa yeye si mwanachama tena sasa anauchungu wa nini kwa cdm?angeanzisha mradi mwingine afanye.
 
kitila kabla ya kuinanga chadema kuhusu uchache wa vit vya udiwani ilivyopata ktk uchaguzi mdogo kulinganisha na umaarufu wa cdm muulize ndugu yako zito kwanini alipata madiwani 2 wakat ni maarufu kuliko hata chama ukifananisha na watu wasio maarufu ktk chama kwa mujibu wa zito kama wenje,vicent nk kama sio usaliti ni nini
 
Kitila Mkukumbo amechanganyikiwa na hoja zake, Kama ni mzalendo angeonyesha uzalendo ndani ya chama kuliko kuanza usaliti wa kukihujumu chama, hapo inadhihirisha jinsi ambavyo anatumikia waliomtuma

Unachangia bila kusoma alichoandika Mkumbo, ktk Maelezo yake ameeleza kila kitu unachojiuliza
 
Msomi mwenzangu hajui hata 2015 ni nini kitajili, hajui hata kuproject, kule kwake ilamba kulikuwa na uchaguzi, eti akashindwa kupeleka nguvu yake, badala yake Ali bananga ndiye akapeleka nguvu, watu wengi hupenda nadharia kuliko uhasilia, sasa hivi ukimuuliza Dr. Kitila amejenga ofisi ngapi za chama, atakuwa hana jibu, simbezi na simdharau, maneno yamekuwa mengi kuliko vitendo, tazama ni yeye na makala, akidhani ataiuwa nguvu ya chadema, msomi mzuri baada ya kufukuzwa angetafakari, kawadhalilisha wanyilamba wenzake, leo ukimuuliza tangu amefukuzwa amewahi kurudi ilamba? Hapa kuna mgogoro wa nafsi, najiuliza Dr. Angekuwa yeye ndiye Rowasa si yangemtoka mengi? Wamejiapiza kwamba ni lazima wataiua chadema yetu macho

Mkuu.

Umenikumbusha kitu cha msingi sana! mwaka 2012 kule Iramba kuifanyika uchaguzi wa kata ya Ulugu, msimamizi wa operation wa karibu kwenye kampeni zile alikuwa huyuhuyu Dr M1, lakini kwa kuwa nadharia za uandishi nyuma ya kipakatwa haziendani na uhalisia kwenye Field, CCM walishinda uchaguzi ule na Dr M1 huyuhuyu akishuhudia kata ikiende CCM, Anakumbuka sana lakini kwa kuwa ameandika akiwa na frustrations katika kipindi hiki kigumu kwake ni bahati mbaya kwamba anayo andika hayawezi kuwa na mashiko kwa kuwa ni amekiri ana hasira.
 
Kitila mkumbo,
Binafsi nakusalimia,na pia nakujulisha kwamba mimi si msomi,lakini naweza kupambanua uzuri na ubaya,au uchungu na utamu wa jambo!

binafsi ninachokiona ni uchungu kwako kwa deal yenu ilitibuliwa mapema(usaliti).

Na pia wewe una ile hulka ya wasomi wa kitanzania walio wengi ambao hudhani ukishasoma na kuwa na kiwango cha shahada ya chuo kikuu.basi wewe uko sahihi muda woote.
CHADEMA MNA HULKA YA KUOGOPA WASOMI HILO HALINA UBISHI.

NIAMBIE NI WAPI Kitila Mkumbo KASEMA UONGO?
Lakini kwa hakika si kweli na mimi nikionacho kwako ni mambo mawili.

*ulikwisha kuwa na ndoto za kuukwaa ubunge kupitia cdm na hivyo kutimuliwa kwako ni pigo pengine kubwa kuliko hata kupoteza kazi hapo udsm kwa sababu ulikwisha anza kula kiheshimiwa na kuota kiheshimiwa

*Pili ni kwamba huenda walio nyuma ya haya mambo bado wana kusumbua kwani mkakati umeharibika kabla ya malengo na hivyo uko kwenye plan b" ya kuiwa cdm kwa kutumia taaluma yako kwa mgongo wa makala.

Haiingi akilini kwa mtu yeyote makini asikushangae ghafla umeibuka na kuwa mshambulizi wa cdm ghafla wakati ukijinasibu kama msomi na si mwanasiasa

Umeshindwa kutofaitisha ukweli na mashambulizi na hili ni tatizo kubwa la bavicha na chadema.

Hebu twambie ni wapi Kitila Mkumbo amewashambulia zaidi ya kusema ukweli?
na tukizingatia kwamba una ajira serikalini na cha ajabu wao serikali wamekaa kimya bila kukuchukulia hatua zozote pamoja na wewe kukiri kufanya siasa(tena upinzani)wakati ni muajiriwa wao pale udsm kitu ambacho Proff baregu hakufanikiwa na alinyimwa mkataba wakati akiwa bado anahitajika.

HILI NDIO TATIZO LA BAVICHA KUWA NA CHUKI BINAFSI KISA MMETOFAUTIANA MITAZAMO NA WATU NA KUKOSOLEWA.

HIVI ULITAKA Kitila Mkumbo AFUKUZWE KAZI?
Kama una nguvu za kuweza kuona mbadala anahitajika kwa nini usikae na wenzako mnaoona mnaendanana kisera na kuamua kanzisha hiyo taasisi yenu,badala ya kudumaza upinzani kwa kutumia kalamu na usomi kutuchanganya tusiosoma kwa manufaa yako binafsi?
Ingawa hutaona matokeo yake kwa sasa lakini utakuja kuyaona ikiwa umeishaimaliza akiba yote ya heshima uliyokuwa umebakiza kwa wapenda mageuzi wote nchini. Kitila Mkumbo kama mwanachi wa kawaida ana haki ya kuwakosoa.
Ansbert ngurumo yuko sahihi

Hivi umeona ushahidi wa Kitila Mkumbo? Kuwa hajaanza leo kuikosoa chadema? Mwambie Ansbert hapinge yaliyo semwa na Kitila Mkumbo.
 
Last edited by a moderator:
mkuu, naamini sote ni wanamageuzi ila napingana na ww kwamba dr kitila akae kimya - tusio wafuasi tunafurahi kuujua ukweli na kwa kuwa viongozi wa chadema wamo humu waje wapinge kwa ushahidi kwamba hakuwahi kuupinga / kuukosoa uongozi ndani ya vikao halali vya chama - tuache jazba, hii ndo hoja ya msingi tungependa kuona upande wa pili unasemaje kuhusu hili?!
baadhi yetu sio wafuasi, tunahoji na hakika so far dr ana hoja za msingi!!!!

HIVI WENYE MALENGO MEMA NA CHAMA CHAO WANGESUBIRI WALIPWE NA MAMLUKI ili KULETA MABADILIKO ? HIVI UNAMJUA ALIYEGHARAMIA MCHAKATO WAO ? KWA MUJIBU WA MWIGAMBA LENGO LAO LILIKUWA KUUPINDUA UONGOZI WA CDM , NA KWAMBA ALIJUA WAKISTUKIWA NI LAZIMA WATIMULIWE ! HUNA HAJA YA KUMHURUMIA KITILA MKUMBO , ALILENGA KUUA CDM , KWA MANUFAA YA WALIOMTUMA , CHANGAMSHA UBONGO WAKO , UNAMJUA ALIYEWALIPIA UKUMBI WA SERENA ? NA UNAFAHAMU KWAMBA MKUTANO HUO ULISIMAMIWA NA UVCCM ?
 
mkuu goodluck5 hii mada ni mwiba kwa chadema na hakuna anaye weza kujibu.

mkuu kwa kweli napenda mabadiliko ya kisiasa ila naogopa yasiwe ya hovyo kuliko hata haya yaliyopo!
kwa mtu makini atagundua unafki wa viongozi wa chadema kwa kumlaumu dr kitila kwamba amekuwa hatumii vikao halali ndani ya chama ktk kukosoa ilihali amekuwa akifanya hivyo.
kwa ujasiri huo tu (bila kujali mawazo yake yalikuwa mabaya au mazuri), dr kitila hakuwa msaliti wala mnafki coz historia yake ndani ya chama inaonesha amekuwa anasimamia anachokiamini no matter what!!
tatizo ni wafuasi sasa waliokwisha karirishwa kama wataweza kudadavua haya................
 
kitila kabla ya kuinanga chadema kuhusu uchache wa vit vya udiwani ilivyopata ktk uchaguzi mdogo kulinganisha na umaarufu wa cdm muulize ndugu yako zito kwanini alipata madiwani 2 wakat ni maarufu kuliko hata chama ukifananisha na watu wasio maarufu ktk chama kwa mujibu wa zito kama wenje,vicent nk kama sio usaliti ni nini

hapa Kitila Mkumbo ana jaribu kuonesha kuwa viongozi wa chadema hawashauriki na amethibitisha amekuwa akishauri lakini hawasikii? Hebu angalia hoja ya Kitila Mkumbo aliyo mjibu ansbert.

Nakushauri ukasome waraka wa kwanza wa kitila.
 
Last edited by a moderator:
HIVI WENYE MALENGO MEMA NA CHAMA CHAO WANGESUBIRI WALIPWE NA MAMLUKI ili KULETA MABADILIKO ? HIVI UNAMJUA ALIYEGHARAMIA MCHAKATO WAO ? KWA MUJIBU WA MWIGAMBA LENGO LAO LILIKUWA KUUPINDUA UONGOZI WA CDM , NA KWAMBA ALIJUA WAKISTUKIWA NI LAZIMA WATIMULIWE ! HUNA HAJA YA KUMHURUMIA KITILA MKUMBO , ALILENGA KUUA CDM , KWA MANUFAA YA WALIOMTUMA , CHANGAMSHA UBONGO WAKO , UNAMJUA ALIYEWALIPIA UKUMBI WA SERENA ? NA UNAFAHAMU KWAMBA MKUTANO HUO ULISIMAMIWA NA UVCCM ?

kwa faida ya wanajamvi - mtaje aliyegaramia mchakato wao sambamba na vielelezo...............
sio vibaya pia uituelezea namna mapinduzi ndani ya chama yangeweza kufanyika na pengine katiba ya chama (na nchi?!) vingeweza kuyabariki............
 
sina tatizo na hoja za Kitila mkumbo ila tatizo langu ni kuwa yeye si mwanachama tena sasa anauchungu wa nini kwa cdm?angeanzisha mradi mwingine afanye.
hili ni tatizo langu pia, nimeanza kushindwa kumtofautisha yeye na wale vijana wengine ambao baada tu ya kufukuzwa CDM mtaji wao ukawa ni matusi mfululuzo wa viongozi wa CDM - sasa waulize hayo matusi yamewafikisha wapi katika safari yao ya kisiasa?

DR. na wewe usiingie katika mkumbo huu, wewe ni msomi na watu wengi wanakuamini - hakuna binadamu aliye umbwa mkamilifu, cha msingi kubali mapungufu yako na kuanza upya si kosa kisheria - maisha yatasonga tu haya mambo ya CDM yaache sababu wewe si mwanachadema leo.

Hata ukiongea hadi asubuhi haitakufanya wewe usafishike, chance yako ya kujisafisha ilikuwa pale mbele ya kamati kuu ya chama chako na ndiyo pekee inaweza kukusafisha - laa kama unaona ulionewa basi kata rufaa kama mwezako badala ya kuendelea kuandika andika vitu ambavyo mwisho wa siku watu wanaaanza kuhoji usomi wako.

Kujikwaa siyo kuanguka, na kuanza moja si dhambi - achana na CDM anza kuangalia mambo yako upya watu watakuheshimu.
 
Dr. Kitila unaonaje ukitulia kidogo naamini haya yatapita na heshima yako kwa jamii itarudi kama zamani. ukiendelea kupayuka unazidi kujionyesha udhaifu wako. CDM wamekufukuza huo sio mwisho na huna sababu ya kulipa kisasi kwa kuwasema vibaya unazidi kujiharibia kwa watu wengi hata wale ambao hawakupata nafasi ya kujua kilichotokea hadi ukafukuzwa chadema.

Ni ushauri tu unaweza kuukubali au ukaacha...kazi ni kwako.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom