Kwa Ukali Dr Kitila Amjibu Ansbert Ngurumo

Kwa Ukali Dr Kitila Amjibu Ansbert Ngurumo

Status
Not open for further replies.
hivi wanajamvi, naomba tu kuuliza.

Mbona karibia watu woote wenye nafasi/vyeo na wasomi kutoka maeneo ya singida wana midomo sana? Mfano tu kwa uchache nape, mwigulu, chiligati, dr.mkumbo etc

hata niliosoma nao wako hivyo hivyo!!!

Tatizo liko wapi?????

tindu lisu
 
Dr Kitila Mkumbo kaa kimya. Kwa sasa kila unachoandika una haribu. Kitendo cha wewe kuendelea kutetea waraka wako wa siri ni kujidhalilisha mbele ya jamii ya wasomi. Waraka wako wa siri ulikuwa mzuri ulipokuwa siri. Baada ya kuwekwa hadharani sio mzuri tena. Kaa kimya utafute namna nyingine ya kutoka lakini sio kwa staili hii unayofanya.

Hayo ni mawazo yako, wengine tunataka Dr aendelee kutililika ili mwisho wa siku pumba na mchele vijulikane. Daktari endelea kumwaga data.
 
Nimeishi kwenye familia 2 tofauti.Familia ya kwanza humaliza matatizo yao kwa vikao.watu huitwa hata kama wako mbali.Yanayozungumzwa hata jirani hawajui.Familia ya pili,tatizo likitokea usiku asubuhi liko mtaani.Hivyo kwa Kitila staili ya pili ndio sawa?
 
viongozi wa chadema wanahubiri wasichokiamini. Slaa anaposimama jukwaani na kusema matumizi ya serikali makubwa. Lakini wao chadema wanatumia fedha zote za ruzuku kwa ajili ya matumizi ya ufipa tu, ni uzandiki na unafiki wa hali ya juu.

naona unajitekenya kisha ucheke mwenyewe, unadhani chadema ni chama cha press conference ?? Ingekuwa chadema haifiki huko field mngekuwa mnalipya buku saba ili kukesha kujitekenya humu?? Hutaeleweka ni chadema tu wakurugenzi wake wanapanda daladala magari yote tena mapya yamepelekwa field kwa wananchi ,waliko watu hawa hawatakuelewa coz haya mambo ynafanywa kwa vitendo na sio maneno. By the way udc haupo kwenye rasimu kuweni makini
 
Majibu ya Dr.Kitila ni majibu ya kisomi na ya ujenzi yanaitaji nguvu ya hoja kuyajibu.

Dr.Kitila, umetimiza wajibu wako watanzania wanakusoma.

Najua kabisa majibu ya pro-Chadema yatakuwa kebehi na kejeli dhidi yako kama ulivyosema.

acha unafiki,mnasapoti hoja kinafiki,alipokuwa cdm mlikuwa mkimtukana na kumbeza sasa kafukuzwa mmegeuka mashabiki wake!!!!!?????? Hana jipya huyo kitilya,kama hayo aliyaona kwa cdm,ilikuwaje aendelee kuwemo hadi alipofukuzwa???
kama zitto rafiki yake alikuwa anasakamwa na wenzake,kwa nini hakujitoa cdm, kama sio mchumia tumbo aliyeogopa kupoteza ubunge wake????
kama ulikuwa na nia njema,kwa nini hamkujitokeza hadharani kukosoa mkaandaa liwaraka lenu gizani????
Na vp kuhusu zile laki 2 ulizokuwa --------- na MM pamoja na wenzako malengo yake yalikuwa yapi????
 
Msomi mwenzangu hajui hata 2015 ni nini kitajili, hajui hata kuproject, kule kwake ilamba kulikuwa na uchaguzi, eti akashindwa kupeleka nguvu yake, badala yake Ali bananga ndiye akapeleka nguvu, watu wengi hupenda nadharia kuliko uhasilia, sasa hivi ukimuuliza Dr. Kitila amejenga ofisi ngapi za chama, atakuwa hana jibu, simbezi na simdharau, maneno yamekuwa mengi kuliko vitendo, tazama ni yeye na makala, akidhani ataiuwa nguvu ya chadema, msomi mzuri baada ya kufukuzwa angetafakari, kawadhalilisha wanyilamba wenzake, leo ukimuuliza tangu amefukuzwa amewahi kurudi ilamba? Hapa kuna mgogoro wa nafsi, najiuliza Dr. Angekuwa yeye ndiye Rowasa si yangemtoka mengi? Wamejiapiza kwamba ni lazima wataiua chadema yetu macho
 
kitila is right na ana uelewa mkubwa zaidi ya wengi

tatizo nchi yetu tunaongozwa na hisia zaidi

we should learn from wasomi type ya kitila

uko sahihi hatofautiani na wasomi wengine kama dr,bana, prof, kapuya, dr,kikwete nk
 
hoja ya posho una kumbuka Anna Makinda alivyo mwambia ZZK kuwa hata kama utachukua sisi tutakuwekea kwenye akaunti yako tu,
suala la wenye elimu kuwadharau watu wasio na elimu ni baya sana,maana BRAZIL imefika hapa ilipofika kwa sababu rais wake alikuwa Darasa la Saba na alisha fanya kazi ya SHOE SHINE.
sasa huku kwetu afrika mtu akisoma kidogo anakukwa na dharau na kuwaone wengine si kitu.
mfalme sulemani alisha sema kuwa JAMBO LOLOTE hata likiwa sahihi ila ukilisema bila utaratibu na sehemu isiyohusika lazima litaleta malumbano
tafakuri nzuri
 
ivi uyu kitilo ni nani kwa sasa? yuko wapi na anafanya nn? y is he acting as if he is someone so important??
 
Dr Kitila Mkumbo kaa kimya. Kwa sasa kila unachoandika una haribu. Kitendo cha wewe kuendelea kutetea waraka wako wa siri ni kujidhalilisha mbele ya jamii ya wasomi. Waraka wako wa siri ulikuwa mzuri ulipokuwa siri. Baada ya kuwekwa hadharani sio mzuri tena. Kaa kimya utafute namna nyingine ya kutoka lakini sio kwa staili hii unayofanya.

Ni uungwana na jambo la kistaarabu inapotolewa hoja inayokulenga uijibu kwa uzito wa hoja iliyotolewa. Kwa hiyo ulitaka hoja ya Ngurumo ipite bila kujibiwa ili ionekana anachosema ndicho? Uungwana ni kuacha hoja zote zitolewe ili watu wapime uzito wa hoja zote mbili. Hii tabia inayoibuka ya kupenda kusikiliza yale tu tunayotaka kuyasikia tena kutoka upande mmoja tu haitatusaidia kujenga jamii inayoheshimu uhuru wa kutoa maoni kama msingi wa demokrasia. NINAUKATAA USHAURI WAKO CATEGORICALLY!
 
chukua LIKE isaya mwita,angekuwa yeye ndio LOWASA ingekuwaje?nchi hii nadhani isinge kalika
 
Hivi huyu Kitila Mkumbo ni Dr wa binaadamu, mifugo au falsafa? Hoja kuu ya ngurumo ni kwamba Hakuna records zinazoonyesha aliwahi kuwakosoa viongozi wa chama wala chama katika vikao stahiki ndani ya chama, yeye anakuja na hoja ya kuandika kwenye magazeti.

Ngurumo anasema kwa nini Kitila hakutumia fursa ya kutakiwa kujieleza kwenye kamati kuu kuelezea udhaifu na Ufisadi waliouandika kwenye waraka wao wa kishenzi kama kweli alikuwa na nia njema na chama chake, Alishindwa, ikiwa na maana kwamba ni muoga , muongo, mzandiki,pandikizi,mnafiki na msaliti.


swala la kuandika kwenye magazeti hata sisi tunaandika hapa JF.

DR Gani huyu Jamani, Hawezi kuelewa hata analalamikiwa kivipi, nadhani Ngurumo alikosea kutambua usomi wake.

Nadhani wewe ndio uelewa wako unatakiwa kutiliwa shaka badala ya kumtupaia Dr Mkumbo maneno ya kejeli. Haya ndio matatizo ya shule za kata hata kujenga hoja huwezi. Kwa uelewa wako hujaona kwenye andiko Dr. Mkumbo alivyoeleza jinsi alivyotoa ushauri ndani ya vikao vya chama?

Hakuna records huyo Ngurumo ameleta ushahidi gani kuonesha kuwa hakuna records. Kabla ya kumkejeli Dr Mkumbo umejikumbusha kuwa Ngurumo ni mhariri wa gazeti la Mtanzania? Ulitegemea aandike mazuri kuhusu Dr. Kitila Mkumbo? Tumia akili ndugu, jenga hoja zenye mashiko na isyo ushabiki uliojaa hisia na chuki bila kuwa na facts
 
vp kuhusu video ya uzalendo,imefikia wapi??? teh teh teh teh teh teh teh...
 
Dr umepoteza ladha kabisa.... Kwangu huu ni uthibitisho tu wa namna ulivyo mzandiki, ulivyokuwa na mipango haramu wewe na huyo Zitto wako... Umebaki kuwa muimbaji taarabu zaidi na kutunga tuhuma za kubuni na kipumb..vu dhidi ya CHADEMA.. Lakini nakuhakikishia unafinya punda. CHADEMA ni annointed party kukomboa taifa toka katika mgando wa mawazo kama ulionao wewe... How sh.ame 2 U.
 
Ngurumo naona anajadili hoja kwa kutumia hisia na mapenzi yake kwa CHADEMA badala ya kutumia facts. Bahati mbaya wafuasi wengi wa CDM ndivyo walivyo. Wanataka useme kile ambacho wao wanapenda kukisikia. Ukitofautiana nao kimawazo wanakuita msaliti, gamba na matusi kibao. Bahati mbaya wanadhani watanzania wote ni mbumbumbu!

Dr. Mkumbo tupo wengi tunakukubali yaliyokukuta ni ajali kazini, kama yalivyokuwa na mwanzo yataisha pia. Waache waendelee na chama chao lakini trela la kutokushaurika wameshaliona kwenye uchaguzi wa madiwani uliopita. Picha ni 2015, CDM itapoteza wabunge wengi labda watabakiwa na Arusha na Kilimanjaro. Baada ya uchaguzi wa 2015 nadhani watakubali hata kuungana na wenzao kuunda kami rasmi ya upinzani bungeni maana jeuri ya wabunge hawatakuwa nayo tena.
 
UDSM kutakuwa na tatizo kubwa sana, mtu wa namna hii anapewa ukuu wa idara?

Kejeli ni kitu cha mwisho kabisa ambacho binadamu mwenye njaa ya elimu anaweza kumtendea mtu aisyekubaliana naye. Usichanganye kabisa usomi wa Dk Kitila na hizi takataka zenu za siasa. Never try this.

Dk. Kitila namfahamu vizuri kama mwalimu wangu at Graduate level. Ni mtu very competent mno. Tena kwenye Shule Kuu ya Elimu (SOED) ninathubutu kusema hakuna mtu unayeweza kupambana naye kwa competency na commitment ya kazi. Huyu jamaa anaipenda sana kazi yake na wanafunzi tunamkubali.

Hakupata Udaktari muda mrefu, hana umri mkubwa kivile lakini kwa bidii yake ya kazi (tafiti na maandiko yake mengi ya kitaaluma ndani ya muda mfupi) sasa hivi ni mtu anayetegemewa SOED. Tena nikwambie hata kama walijaribu kumsimamisha baada ya haya makandokando ya siasa, HAWATAWEZA KUTHUBUTU kumwacha. Time will tell. Kwa hiyo usijaribu kuhusianisha siasa na usomi wake. Hilo haliwezakani.

Hata hivyo, naamini naye ni binadamu. Katika mambo ya siasa kuna mahali aliteleza kama binadamu. Mimi ningemshauri atulie. Aachane na bidii ya kutetea EGO (of course naelewa kwa nini inabidi afanye hivi kama binadamu mwenye heshima miongoni mwa wanataaluma wenzake) lakini angetulia kwanza. Ajikite kwenye shughuli zake za kitaaluma anazoziweza ipasavyo. Baadae, achague wapi pa kwenda. Tena inaweza kuwa hata CHADEMA akionyesha kutulia. Asichukue hatua zinazofanana na zile za wale vijana Mtela Mwampamba na Shonza ambao mtu unaweza kuelewa kwa nini midomo yao haina breki. Shule na njaa ni tatizo kwao but not to a prominent academician kama wewe unayepatikana kote iwe google.scholar na kwenye machapisho ya kitaaluma yenye hadhi ya kimataifa.

Dk Kitila, haya ni mapito. Utapita. Hasira na uchungu vitapita. Ni mapito.
 
Hivi huyu Kitila Mkumbo ni Dr wa binaadamu, mifugo au falsafa? Hoja kuu ya ngurumo ni kwamba Hakuna records zinazoonyesha aliwahi kuwakosoa viongozi wa chama wala chama katika vikao stahiki ndani ya chama, yeye anakuja na hoja ya kuandika kwenye magazeti.

Ngurumo anasema kwa nini Kitila hakutumia fursa ya kutakiwa kujieleza kwenye kamati kuu kuelezea udhaifu na Ufisadi waliouandika kwenye waraka wao wa kishenzi kama kweli alikuwa na nia njema na chama chake, Alishindwa, ikiwa na maana kwamba ni muoga , muongo, mzandiki,pandikizi,mnafiki na msaliti.


swala la kuandika kwenye magazeti hata sisi tunaandika hapa JF.

DR Gani huyu Jamani, Hawezi kuelewa hata analalamikiwa kivipi, nadhani Ngurumo alikosea kutambua usomi wake.

Haya ni baadhi ya maneno yaliyoko kwenye mada ya Kitila mkumbo:

"Sijaanza kuikosoa CHADEMA leo. Nilliikosoa CHADEMA nilipokuwa mwanachama ndani na nje ya vikao. Tofauti pekee. Nitakukumbusha matukio machache".

vikao gani zaidi ulitaka aikosoe CHADEMA?
 
Nadhani wewe ndio uelewa wako unatakiwa kutiliwa shaka badala ya kumtupaia Dr Mkumbo maneno ya kejeli. Haya ndio matatizo ya shule za kata hata kujenga hoja huwezi. Kwa uelewa wako hujaona kwenye andiko Dr. Mkumbo alivyoeleza jinsi alivyotoa ushauri ndani ya vikao vya chama?

Hakuna records huyo Ngurumo ameleta ushahidi gani kuonesha kuwa hakuna records. Kabla ya kumkejeli Dr Mkumbo umejikumbusha kuwa Ngurumo ni mhariri wa gazeti la Mtanzania? Ulitegemea aandike mazuri kuhusu Dr. Kitila Mkumbo? Tumia akili ndugu, jenga hoja zenye mashiko na isyo ushabiki uliojaa hisia na chuki bila kuwa na facts

Wewe kama unazo hizo records tuwekee hapa, ni katika kikao kipi Kitila aliwahi kuelezea ushenzi walioandika kwenye waraka wao au ndugu yake Zitto pamoja na Mwigamba.

Mwigamba siku anatakwa makofi alikuwa anasifia uongozi mahili wa Mbunge Lema ndani ya kikao cha chama arusha huku anapost ushenzi JF wakati huo huo.

Kitila Mkumbo kabla waraka haujawekwa wazi siku hiyo hiyo alisifia report ya hesabu za chama.

Hawa ni wasaliti zaidi ya Yuda kama alivyosema Ngurumo, sababu Yuda alipokuwa na wenzake alikuwa kimyaaaaa, hata Yesu alipokuwa akiwauliza maswali yeye alikaa kimya, afadhali yeye alikuwa na aibu.

Hawa wahuni wanaingia kwenye vikao kusifia uongozi wakitoka wanaurushia kinyesi, hawa ni wahuni wakubwa hawa,

Kuhusu shule za kata
Kuhusu shule, usomi nilionao mimi wewe na ukoo wako itawachukua miaka kumi kutambua kwamba na nyie mnauhitaji, swala la kujielekeza kuupata nalo ni majaaliwa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom