Kwa Thomas - Kimara bucha

Kwa Thomas - Kimara bucha

Hahahahahaaaaa!!..........Ewaaaaa.

Sasa pale, wale wahudumu wote wanawake wameshakufa isipokuwa moja tu - anaitwa mama Sadiki kama sikosei, hakuwahi kujua kusoma wala kuandika mpaka leo hii. Dogo amecukua ile bar, ameamua kumstaafisha bibi, amemfungulia genge. na amemwambia awe anakuja kunywa bia mbili kila jumapili. Huyo maza hawezi hata kurudisha chenchi lakini amekuwa mhudumu wa Ruaha Galaxy kwa maisha yake yote...tangu usichana wake mpaka amekuwa bibi.

Namkumbuka sana......akiniona ananiita .......mwanangu siku hizi umeacha kunywa Kilimanjaro..duh....hahahahahaaa!!

Uko deep!
 
....Hivi na ule mjengo uliopo pale kimara sijui ndio wanaita korogwe uande wa kushoto kuelkea Moro unaodaiwa kuwa ndio ilikuwa garage yenyewe bado analimiliki au FBI walipiga stop kutumika tena?

Ule upo ila Tanroads wameupita X uanatakiwa kubomolewa. Siku hizi pamepooza sana. Ndani miscraper kibao!
 
The chances are, mzee akiondoka basi he will go with a big chunk of his projects.

Lijamaa linasema likifa, ile garage itajaa watoto wake wa nje........lakini halijawahi kutambulisha watoto wa nje ndani ya familia yake. Linasema limemalizana nao juu kwa juu, kwa maana ya kwamba watoto na amam zao wanajitegemea huko walipo.


Huyo ndo Thomas...ana Mercedes Benz 5 amepark nyumbani na garage zimeshajifia +other cars like 20, zote ame-park na zimeshakufa kwasababu hataki mtu aguse wala hataki kuuza.

Thomas hana mtoto mmoja. Waliokuwa wakilelewa pamoja na wa mke wake mdogo ninaowajua mimi walikuwa kumi. Kati ya watoto wake wapo walioendelea na wana nafasi zao nzuri. Hakumdekeza mtoto.
 
hahahahahaaaaa!!..........ewaaaaa.
D
sasa pale, wale wahudumu wote wanawake wameshakufa isipokuwa moja tu - anaitwa mama sadiki kama sikosei, hakuwahi kujua kusoma wala kuandika mpaka leo hii. Dogo amecukua ile bar, ameamua kumstaafisha bibi, amemfungulia genge. Na amemwambia awe anakuja kunywa bia mbili kila jumapili. Huyo maza hawezi hata kurudisha chenchi lakini amekuwa mhudumu wa ruaha galaxy kwa maisha yake yote...tangu usichana wake mpaka amekuwa bibi.

Namkumbuka sana......akiniona ananiita .......mwanangu siku hizi umeacha kunywa kilimanjaro..duh....hahahahahaaa!!

john akuchagua alimdoka na ma barmed wake wote akafa nao maskin
 
Thomas hana mtoto mmoja. Waliokuwa wakilelewa pamoja na wa mke wake mdogo ninaowajua mimi walikuwa kumi. Kati ya watoto wake wapo walioendelea na wana nafasi zao nzuri. Hakumdekeza mtoto.
Ana watoto wengi sana.......wakija wote wanaweza kujaa kwenye ile gerage au pale kwenye yard ya trailers alipowakodishi wachina.

Thom mhuni yule....anatafuna hadi mke wa mwanae.....pambafu sana!!
 
Sijui kwa kweli maana nakumbuka sehemu nyingi sana zenye majina ya kibaguzi ilihali waliobatiza maeneo hayo wakiwa tofauti sana na ukoloni, Mfano Uhindini,na Uzunguni Mbeya, afadhali hata mzee Mwakangale alipata shavu kukumbukwa kwenye uwanja wa nane nane pale RRM Uyole

na Mwanjelwa je...nasikia lilikuwa jina la mtu
 
na Mwanjelwa je...nasikia lilikuwa jina la mtu

Mwanjelwa ni jina la mtu so far wanyakyusa na mwa mwa hawajambo...kuna mwakibete, mwakangale,mwakasege,mwaifupe,mwansasu,mwasomola,mwaikokesya,mwamaso,mwakitwange,mwakaleli,mwatisi,mwandege n,n
 
huyu mzee thomas alikuwa mfanyabiashara mkubwa, alikuwa na hardware gerezani, pamoja na workshop ya kukunja bati za kutengeneza body za malory, hivyo alikuwa akifanya biashara pia ya vyuma. sasa katika hiyo karakana yake iliyoko gerezani, ndipo magaidi waliolipua ubalozi wa marekani walipopeleka kutengeneza vifaa vyao ambapo kulikuwa na mitungi ya ges ile mirefu ilichomelewa hapo.

mafundi waliofanya hiyo kazi hawakujua ni kwa ajili ya nini, wao walijua.ni kazi tu kama wanavyofanya nyingine. baada ya tukio la kulipuliwa ubaloz wa marekani kutokea, cia & fbi walipoanza kutrace vifaa vilitengenezewa wapi, ndipo ikajulikana vilipotengenezewa hapo kwa mzee thomas, hivyo akawa included, ji moja ya kesi ambazo zimechangia kuzorota kwa biashara zake amekuja kuonekana hanabhatia baada ya muda sana
 
Bado yupo maeneo ya kimara ameanzisha chuo cha Ualimu nafikiri kinaitwa Ebonite, yeye darasa la saba ingawa amejiendeleza hadi form IV. Enzi zake mabinti kama wewe ( kama kweli avatar inaendana nawe kwa angalau 75%) walikuwa hawakatizi, jamaa ana strategy kali sana. wengi wa waliokuwa wanamfundisha walikuwa wale watoto wakali toka Chuo na maeneo mengine ya mji. (kumbuka form I hadi form IV alijifunzia ofisini kwake na walimu wote mabinti wakali). Unakuwa umezubaa mara anazuka mpambe wake kuwa kuna mtu anataka twisheni malipo 5,000/= kwa saa hiyo 1990's na kweli unalipwa wewe utaacha kweli kwenda 'kufundisha'.

Pia atakumbukwa kwa kuchangia ujenzi wa nyumba mbali mbali za ibada ( Pande zote), kama kuna harambee enzi hizo kama akipelekewa mwaliko akasema ana udhuru basi harambee yahairishwa!

yupo mama mmoja anaitwa Renata Lyakurwa alikuwa mwalimu kisutu akifundisha English. huyu alinfundisha huyu mzee english mpaka akajua, alipojua akaanza route za kwenda nje kama uk, baadaye alimshawishi huyu mwalimu wa kisutu aache kazi, kweli akaacha ampa kazi ya kusimamia na kuuza duka lake liloloko gerezani likiuza angles,flat bars, round pipes, plates na takataka zote, alimshawishi kwa kumlipa mshahara mkubwa kuliko aliokuwa analipwa na serikali.

Huyu mama kama kawaida ya wachaga baadaye akaanzisha kaduka kadogo kakuuza chuma rejects na used hapo hapo gerezani. baadaye kikachanganya,akaacha kazi kwa thomas, akakomaa na duka lake hadi hivi sasa kamzidi hata huyo thomas mwenyewe, ana bonge ya store gerezani akiuza all metal product nondo, bati, flat bars ,angles etc za nje ndani na nje, pia ana maduka mengine ya jumla na rejareja Buguruni; godown ilala, buguruni na tabata matumbi. hardware zake zinaitwa MWALIMU HARDWARE. pia anauza bidhaa nyingine kama nguo toka china & other products
 
the chances are, mzee akiondoka basi he will go with a big chunk of his projects.

Lijamaa linasema likifa, ile garage itajaa watoto wake wa nje........lakini halijawahi kutambulisha watoto wa nje ndani ya familia yake. Linasema limemalizana nao juu kwa juu, kwa maana ya kwamba watoto na amam zao wanajitegemea huko walipo.

Huyo ndo thomas...ana mercedes benz 5 amepark nyumbani na garage zimeshajifia +other cars like 20, zote ame-park na zimeshakufa kwasababu hataki mtu aguse wala hataki kuuza.

haahaaa bez kauza nahisi ameuzia wanaouza skrepaaa haahaaa. Usicheke. Yuko. Na. Raum. Txxz acy
 
Mamaya,


Huyo cha mtoto.

Kuna jamaa anaitwa Saidi ama side kwakiingereza alikuwa akija wazungu wa misaada anaongea. Nao yeye alafu. Anamweleza Tom kwa kiswahili.

Dah. Jamaa. Asiwambiee. Anataka kuanzisha yake garage wakampa miezi. Mitatu atupe kila kitu anachoitaji na kitu gan wamsaidie. Aisee jamaa yuko pale opp. Na lions hotel sinza anatengeneza bodi kama hana akili nzuri.

Hope bado yuko maana alikuwa moto. Walikuwa wana-share na tall yule nduguye tom ambae alikuwa anasimamia garage yake akaondoka na salama.. Yake...
 
ana watoto wengi sana.......wakija wote wanaweza kujaa kwenye ile gerage au pale kwenye yard ya trailers alipowakodishi wachina.

Thom mhuni yule....anatafuna hadi mke wa mwanae.....pambafu sana!!

katafuna dadake nnmkewamwanae??akaza naemtoto bwabwa anaitwa denis mpangomzima ukibip anakuja fasta .. Sosad nayuledadake akaparalaizi upandemmoja mpakakesho ukimwona. Tom ayukosawa nwdays
 
Kwenye RED, Bucha inayotamkwa pale siyo Noah wala mbuzi katoliki bali ni kuwa pale kulikuwa na ajali nyingi sana watu wakichinjwa ni kama vile pale Chang'ombe panavyoitwa machinjioni. Hivyo si busara kuita jina hilo la kimzaha (lakini mzaha wa hatari) ndo maana waka - opt for Thomas kwani jamaa ana gereji kubwa pale, ambayo naona kama kawakodisha wachina kwa sasa.

Kuna hadithi kuwa ajali hizo zilikuwa zinasababishwa na matambiko ya huyo jamaa, ingawa ukweli ni kuwa tatizo lilikuwa ule mteremko mkali lkn binadamu wakazusha kama kawaida yao.

Acha uongo
 
Mkuu bucha inayotajwa ni ya noah aka kitimoto. Ilikua opposite kabisa na lile jengo la garage la thomas lyimo.mwenye bucha aliweka bango lake karibu na barabara likiwa limechorwa ngurue mweupe na maandishi 'pork butcher'. Bucha na bango vilibomolewa wakati zinajengwa barabara mbili. Miaka ya nyuma kituo kilikua baruti na korogwe tu. Pale palikua kushuka kwa kuomba msaada tu.watu walikua wakisema msaada bucha.fika pale uliza wenyeji pale maeneo ya wafalme bar watakuambia.mi mdau maeneo hayo toka 1984

Uko sahihi sana kaka, mi nmezaliwa bucha na nmekulia bucha huyo jamaa anatoa historia za vijiweni
 
katafuna dadake nnmkewamwanae??akaza naemtoto bwabwa anaitwa denis mpangomzima ukibip anakuja fasta .. Sosad nayuledadake akaparalaizi upandemmoja mpakakesho ukimwona. Tom ayukosawa nwdays

Dennis anaishi huku kwetu sa hivi
 
Back
Top Bottom