Nitatumia utenguzi na uteuzi wa huyu DC kama mfano ktk uzi wangu.
Huyu alikuwa DC wa Temeke, akatenguliwa 02 June 2023. Na leo 23 Septemba 2023 ameteuliwa tena kuwa DC wa Mtwara.
Ndiyo kusema mwanamama huyu alipoteza sifa ya kuwa DC mpk kufikia hatua ya kutenguliwa 02/06/2023 lkn siku 90 (miezi 3) tu baadaye amepata sifa za kuweza kuteuliwa tena kuwa DC??
Kwa vyovyote vile huwezi kupata majibu ya swali hili. Badala yake ishie tuhitimishe tu kwa kusema uteuzi hufanywa kwa misingi ya uchawa na utenguzi hufanywa kwa majungu.
Sifa za uongozi hazizingatiwi ndiyo maana hatuoni mabadiliko ktk maendeleo zaidi ya kuona mabadiliko ya sura za viongozi.