Umakini kwenye teuzi za viongozi

Ze Heby

JF-Expert Member
Jun 22, 2011
5,252
5,319
Tarehe 21 Novemba 2023, tulipata habari kuhusu kusimamishwa kazi kwa Wakurugenzi Watendaji (District Executive Directors) wawili.

Wakurugenzi hao ni, Butamo Nuru Ndalahwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro, Lena Martin Nkya. Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kutolewa kwa taarifa ya awali ya timu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za wakurugenzi hao kushindwa kusimamia miradi ya maendeleo katika halmashauri zao kwa nyakati tofauti.

Tarehe 14 Disemba 2023, Mheshimiwa Rais alifanya mabadiliko ambapo pamoja na mambo mengi aliwahamisha Wakurugenzi hao, Butamo Nuru Ndalahwa (akiwa amesimamishwa kazi) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwenda Halmahsauri ya Wilaya ya Momba na Lena Martin Nkya (akiwa amesimamishwa pia) Halmashauri ya Mji wa Ifakara kwenda Hlmashauri ya Mji wa Tunduma.

Jana tarehe 18 Disemba, 2023, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imetoa taarifa ya uteuzi, utenguzi na uhamisho wa viongozi ambapo pamoja na mambo mengine, Butamo Nuru Ndalahwa (DED mpya Momba) na Lena Martin Nkya (DED mpya Tunduma) wametenguliwa.

Ndani ya muda mfupi, gaps zimeonekana kwenye issue nzima ya uteuzi wa viongozi ambao bado wana discplinary proceedings. Nashauri washauri wa mamlaka za uteuzi wafanye kazi yao vizuri na wamshauri Rais vizuri ili makosa kama haya yasijitokeze. Tumeshashuhudia pia huko nyuma uteuzi wa watu ambao hawana sifa, wanaoteuliwa leo na kutenguliwa kesho etc.

Nadhani kuna taratibu mahususi za namna ya kufanya hivi vitu na hata kumjulusha mhusika kuhusu uteuzi huo ili ikitokea ameukataa, basi anaondolewa kabla mkeka haujaenda public.

Naomba kuwasilisha​
 
Tarehe 21 Novemba 2023, tulipata habari kuhusu kusimamishwa kazi kwa Wakurugenzi Watendaji (District Executive Directors) wawili.

Wakurugenzi hao ni, Butamo Nuru Ndalahwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro, Lena Martin Nkya. Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kutolewa kwa taarifa ya awali ya timu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za wakurugenzi hao kushindwa kusimamia miradi ya maendeleo katika halmashauri zao kwa nyakati tofauti.

Tarehe 14 Disemba 2023, Mheshimiwa Rais alifanya mabadiliko ambapo pamoja na mambo mengi aliwahamisha Wakurugenzi hao, Butamo Nuru Ndalahwa (akiwa amesimamishwa kazi) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwenda Halmahsauri ya Wilaya ya Momba na Lena Martin Nkya (akiwa amesimamishwa pia) Halmashauri ya Mji wa Ifakara kwenda Hlmashauri ya Mji wa Tunduma.

Jana tarehe 18 Disemba, 2023, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imetoa taarifa ya uteuzi, utenguzi na uhamisho wa viongozi ambapo pamoja na mambo mengine, Butamo Nuru Ndalahwa (DED mpya Momba) na Lena Martin Nkya (DED mpya Tunduma) wametenguliwa.

Ndani ya muda mfupi, gaps zimeonekana kwenye issue nzima ya uteuzi wa viongozi ambao bado wana discplinary proceedings. Nashauri washauri wa mamlaka za uteuzi wafanye kazi yao vizuri na wamshauri Rais vizuri ili makosa kama haya yasijitokeze. Tumeshashuhudia pia huko nyuma uteuzi wa watu ambao hawana sifa, wanaoteuliwa leo na kutenguliwa kesho etc.

Nadhani kuna taratibu mahususi za namna ya kufanya hivi vitu na hata kumjulusha mhusika kuhusu uteuzi huo ili ikitokea ameukataa, basi anaondolewa kabla mkeka haujaenda public.

Naomba kuwasilisha​
Hapo ukute wahusika washafika na vituo vya kazi... Rais wa nchi hii kapewa majukumu ambayo si rahisi kwake.
 
Ni kama wanatumwa kuiba ili kuboresha chama, maana wote ni makada. Ndio maana pamoja na ushahidi kuwepo hawachukuliwi hatua kama inavyotakiwa.
 
Tarehe 21 Novemba 2023, tulipata habari kuhusu kusimamishwa kazi kwa Wakurugenzi Watendaji (District Executive Directors) wawili.

Wakurugenzi hao ni, Butamo Nuru Ndalahwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro, Lena Martin Nkya. Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kutolewa kwa taarifa ya awali ya timu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za wakurugenzi hao kushindwa kusimamia miradi ya maendeleo katika halmashauri zao kwa nyakati tofauti.

Tarehe 14 Disemba 2023, Mheshimiwa Rais alifanya mabadiliko ambapo pamoja na mambo mengi aliwahamisha Wakurugenzi hao, Butamo Nuru Ndalahwa (akiwa amesimamishwa kazi) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwenda Halmahsauri ya Wilaya ya Momba na Lena Martin Nkya (akiwa amesimamishwa pia) Halmashauri ya Mji wa Ifakara kwenda Hlmashauri ya Mji wa Tunduma.

Jana tarehe 18 Disemba, 2023, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imetoa taarifa ya uteuzi, utenguzi na uhamisho wa viongozi ambapo pamoja na mambo mengine, Butamo Nuru Ndalahwa (DED mpya Momba) na Lena Martin Nkya (DED mpya Tunduma) wametenguliwa.

Ndani ya muda mfupi, gaps zimeonekana kwenye issue nzima ya uteuzi wa viongozi ambao bado wana discplinary proceedings. Nashauri washauri wa mamlaka za uteuzi wafanye kazi yao vizuri na wamshauri Rais vizuri ili makosa kama haya yasijitokeze. Tumeshashuhudia pia huko nyuma uteuzi wa watu ambao hawana sifa, wanaoteuliwa leo na kutenguliwa kesho etc.

Nadhani kuna taratibu mahususi za namna ya kufanya hivi vitu na hata kumjulusha mhusika kuhusu uteuzi huo ili ikitokea ameukataa, basi anaondolewa kabla mkeka haujaenda public.

Naomba kuwasilisha​
Huu ni uthibitisho tosha kwamba "Wajenzi wa Mnara wa Babeli kwa sasa hawaongei tena lugha moja."
 
Back
Top Bottom