Kwa Taifa lenye mipango na maono mazuri huliwezi kutegemea Machinga na mama lishe kwa uchumi endelevu

Gift mzalendo

JF-Expert Member
Dec 13, 2019
1,033
1,227
Habarini wakuu,

Kwanza nipongeze juhudi mbalimbali za taifa letu katika kujikomboa kiuchumi. Niwapongeze pia vijana wenzangu tuliomua kujiajiri kwa njia mbalimbali Machinga mama lishe boda boda nk.

Nirudi kwenye mada yangu , katika kutafakari kwangu nimejaribu kuangalia Mambo muhimu yanayofanya uchumi wa nchi kuwa imara. Yapo mengi isipokuwa

Moja ya Jambo muhimu ni uimara wa sekta binafsi haswa katika suala la uzalishaji na kuajiri. Kiuhalisia hakuna serikali duniani inayoweza kuajiri watu wake wote, isipokuwa kazi kubwa ya serikali makini Ni kutengeneza mazingira mazuri kwa sekta binafsi kuajiri na kuzalisha zaidi.

Tunapokuwa na sekta binafsi imara kiuchumi pia tunakuwa na taifa imara na serikali imara kiuchumi. Tukumbuke serikali inajiendesha kutoka kwenye Kodi inazozikusanya kutoka kwenye sekta binafsi rasmi na zilizofanikiwa. Lakini ili kupata sekta binafsi zilizofanikiwa na imara lazima zitengenezewe mazingira mazuri na mifumo mizuri. So Kama tutaendelea kutengeneza mazingira ya kuwa na sekta binafsi zisizorasmi , tusitegemee ukuaji mzuri na imara wa kiuchumi.

Wakati huo huo tutakuwa tunaongeza mzigo mkubwa kwa watumiaji wa mwisho (consumer). Bidhaa moja inafa yiwa biashara na watu wengi zaidi na Kila mmoja anataka apate faida mwisho mtumiaji wa mwisho ndo atalipia faida ya mzalishaji, Kodi ya bandari, muagizaji, muuzaji wa jumla na reja reja, Machinga wa kwanza wa pili nk. Kwa hiyo mlolongo wote huo mlaji au mtumiaji inabidi azibebe.

Kwa ishu ya Machinga na mama lishe inatakiwa iwe ni mpango was muda mfupi huku tukiandaa mpango wa kuwaaandaa ili waweze kuingia kwenye mfumo was sekta binafsi rasmi , ambazo zinaweza kuwasaidia na kusaidia uchumi wetu. Niseme tu hili suala limetazamwa kisiasa zaidi kuliko kiuchumi. Siamini Kama Kuna mtu anatamani azungushe bidhaa juani , wakati huo hana uhakika was soko.

Tunahitaji kuandaa vijana waweze kuanzisha biashara ambazo ziko kwenye mifumo. Tumekuwa na biashara ambazo zinaanzishw a na zinakufa pindi mmliki akifa kutokana kutokua kwenye mifumo inayoeleweka. Mifumo imara za biashara katika sekta binafsi Ni moja nguzo imara katika uchumi endelevu.

Moja ya uimara wa uchumi wa nchi Kama marekani ni kuanzishwa kwa makampuni mengi katika sekta binafsi. Tunatamani tuone vijana wetu machinga wanaunganishwa na wanaandaliwa kuanzisha makampuni ya kutengeneza kusambaza bidhaa mbalimbali
Mama ntilie nao wanaandaliwa wanaunganishwa kuanzisha migahawa mizuri. Biashara huria inasaidia uchumi lakini biashara holela itazidi kuua uchumi.

Suala la kuruhusu Machinga na mama lishe kujaa kwenye majiji na miji yetu pasipo mpangilio maalum na bila future inayoeleweka , lisi we Ni la mpango wakudumu Bali liwe la mpito. Tukiwandaa kuingia kwenye mifumo rasmi ya biashara. Na siku moja biashara zote zikae kwenye mifumo.

Na majiji yetu yabaki kuwa majiji yenye mpangilio mzuri yaliyosayarabika.

Hayo ni maoni yangu.

Karibuni
 
Hakuja serikali tajiri Bali Kuna taifa tajiri, serikali maskini Ni matokeo ya taifa maskini
 
Ukimwambia kijana machinga ajiendeleze kielimu atakuelewa? Bila elimu bora wanaweza kumiliki viwanda?
Mkuu kwenye hoja yangu nimesema tunahitaji mpango wa kuwaanda, kwa upande wao ni ngumu kujiendeleza maana tayari wengine wameona ndo njia sahihi.

So lazima tukubali tumekosea kuandaa vijana wetu kuanzia primary

Pili tumekosea kuandaa mfumo na mazingira mazuri ya sekta binafsi

So we need new plan to change this
 
Tusipepese macho kwa namna yoyote ile Tanzania hatuwezi kuwakwepa machinga wapo na wataendelea kuwepo pengine kwa miaka 1000 ijayo.
Mkuu
Kila kitu kinaweza kubadilika
Kwanza tutakapogundua tumekosea na njia
Pili kuweka mipango na mikakati mizuri ya kubadili Hali halisi

tusigemee kuwa na uchumi imara na endelevu ,Kama nguvu kubwa tutaweka kwenye uchuuzi,
Nguvu kazi (vijana ) kubwa lazima tuwekeze kwenye uzalishaji
 
Bado naamini hutuwezi kuwa na uchumi imara na endelevu kwa kutegemea machinga, wawekewe mpango wa muda mfupi wakiandaliwa kuingia kwenye mifumo rasmi ya biashara
 
Bado naamini hutuwezi kuwa na uchumi imara na endelevu kwa kutegemea machinga, wawekewe mpango wa muda mfupi wakiandaliwa kuingia kwenye mifumo rasmi ya biashara
Haswa, zaidi maeneo yenye viwango vya kawaida ila yakiwa na usalama na yenye hadhi ya kutumia watu wenye akili timamu maana sehemu zenye viwango vibovu vinafanya wakae matapeli na watu kama wehu au wezi tu wanaoshinda hizo sehemu kwa kisingizio cha kujifanya chinga huku wakiibia watu, kutapeli na zaidi kujifanya ni watu wajuaji na wateja wao niwajinga na hela za wateja ni zakuibiwa bila kupewa walichokwenda kununua kwa vile hawalipii sehemu za biashara na kutoa receipt ya kumlinda mnunuzi yaani wao nikuuza tu au kuibia wateja bila kushiriki popote kuinua uchumi wa Nchi yao.
 
Sekta mbili kati ya nyingi za kutengeneza ajira ni kilimo na viwanda. Ni viwanda vya kuchakata mazao ya kiimo na mifugo.

Tuna chuo kikuu cha kilimo Sokoine. Tuna ardhi ya kutosha. Tuna mito na maziwa na hata bahari. Tuna nguvu kazi vijijini, vijana ambao hukimbilia mijini na kugeuka kuwa machinga.

Hiyo ni mifano michache lakini tuna vingi. Labda kinacho kosekana ni kukosa wasimamia dira na mikakati kuhusu kilimo na viwanda.

Tanzania ingeweza kuwa mzalishaji mkubwa wa mpunga, mahindi na mifugo. Ingezalisha ziada na kuuza sana.

Serikali ingeunda mfuko kusaidia watafiti, wabunifu na wasomi bobezi mbalimbali katika sekta ya kilimo na mifuko.

Serikali ingeandaa mazingira ya kuwezesha wajasiriamali kama Bakhresa kuibuka, kusindika mazao na kuuza nchi nyingine ndani ya Afrika na kwingineko.

Haya ni machache sana katika mengi ambayo yanaweza kuchambuliwa na kupangwa vizuri na wajuzi na wabobevu tulio nao Tanzania.

Hata hivyo, jambo muhimu ni kuwepo kwa dhamira thabiti ya wenye madaraka. Watakao chochea badala ya kukwamisha.

Vinginevyo kudhibiti machinga kwa kukimbizana na mgambo ni mapambano ya kudumu.
 
Afrika hatuna strategic planning ya maisha na kiuchumi, sisi kukicha ndipo mipango inaanzia hapo hapo baada ya kuweka miguu chini kutoka kitandani.

Vijana kuwa machinga inatokana na mipango isiyokuwepo kwa ajiri ya future, ndiyo maana kila kiongozi akija anakuja na njia yake ya kukusanya mapato ili ajichotee yeye mwenyewe si kulifanya taifa likue.

JKT ingekuwa ni sehemu mojawapo nzuri ya kulifanya taifa linyanyuke na kutengeneza ajira binafsi kwa vijana kujutegenea katika uzalishaji (as china) na kuepukana na lundo la machinga but now jkt imekuwa sehemu ya deal na kupoteza muda.
 
Sekta mbili kati ya nyingi za kutengeneza ajira ni kilimo na viwanda. Ni viwanda vya kuchakata mazao ya kiimo na mifugo.

Tuna chuo kikuu cha kilimo Sokoine. Tuna ardhi ya kutosha. Tuna mito na maziwa na hata bahari. Tuna nguvu kazi vijijini, vijana ambao hukimbilia mijini na kugeuka kuwa machinga.

Hiyo ni mifano michache lakini tuna vingi. Labda kinacho kosekana ni kukosa wasimamia dira na mikakati kuhusu kilimo na viwanda.

Tanzania ingeweza kuwa mzalishaji mkubwa wa mpunga, mahindi na mifugo. Ingezalisha ziada na kuuza sana.

Serikali ingeunda mfuko kusaidia watafiti, wabunifu na wasomi bobezi mbalimbali katika sekta ya kilimo na mifuko.

Serikali ingeandaa mazingira ya kuwezesha wajasiriamali kama Bakhresa kuibuka, kusindika mazao na kuuza nchi nyingine ndani ya Afrika na kwingineko.

Haya ni machache sana katika mengi ambayo yanaweza kuchambuliwa na kupangwa vizuri na wajuzi na wabobevu tulio nao Tanzania.

Hata hivyo, jambo muhimu ni kuwepo kwa dhamira thabiti ya wenye madaraka. Watakao chochea badala ya kukwamisha.

Vinginevyo kudhibiti machinga kwa kukimbizana na mgambo ni mapambano ya kudumu.
Upo sawa na vizuri ila hapo kwenye mazao ya kusindika siyo hayo mahindi na mchele pekee vitu vinavyopatikana Nchi nyingi kwa urahisi ila yapo mazao unique bado hayajapewa nguvu na yanapesa sana mfano jibini ni chakula chenye thamani sana na kinaweza kutumika kwenye Kila mlo kikipatikana kwa wingi lakini hakisindikwi kabisa Bali tunaletewa blueband isiyo na thamani yoyote kwenye miili yetu, bado matunda ya kukausha na kusagwa ungwa kama tunavyosaga mahindi vikiwepo vingetumika muda wote hata msimu wake ukiisha yaani kwenye mifugo na kilimo Kuna vitu vimefichwa makusudi mfano mtu aliyevumbua sukari ya miwa ona jinsi sukari inavyotumika kwa wingi kuliko miwa yenyewe.
 
Haswa, zaidi maeneo yenye viwango vya kawaida ila yakiwa na usalama na yenye hadhi ya kutumia watu wenye akili timamu maana sehemu zenye viwango vibovu vinafanya wakae matapeli na watu kama wehu au wezi tu wanaoshinda hizo sehemu kwa kisingizio cha kujifanya chinga huku wakiibia watu, kutapeli na zaidi kujifanya ni watu wajuaji na wateja wao niwajinga na hela za wateja ni zakuibiwa bila kupewa walichokwenda kununua kwa vile hawalipii sehemu za biashara na kutoa receipt ya kumlinda mnunuzi yaani wao nikuuza tu au kuibia wateja bila kushiriki popote kuinua uchumi wa Nchi yao.
Nashukuru mkuu
Kwa point zako
1.Vijana kutengewa eneo lenye hadhi
Itawasaidia soko , usalama na kutambulika wadau mbalimbali wenye nia ya kuwasapot
2.Kufanya mauzo rasmi kwa kutoa recit ,
hapa itawaongezea uaminifu kwa wateja na soko la uhakika
 
Tunahitaji wawekezaji ili wakwapue Rasilimali zetu.
Hapana mkuu, hapa lengo ni kuwaandaa na kuwasaidia hawa hawa vijana wawe wawekezaji wa ndani
Kwa kuwawekea mipango mizuri ili wawe wazalishaji zaidi kuliko ilivyo sasa kuwa ni nchi ya wachuuzi wengi kuliko wazalishaji
Tunahitaji wawekezaji wa nje waje tushirikiane nao kwenye mipango yetu na sio kuwa vibarua na manamba tu kwenye miradi yao
 
Sekta mbili kati ya nyingi za kutengeneza ajira ni kilimo na viwanda. Ni viwanda vya kuchakata mazao ya kiimo na mifugo.

Tuna chuo kikuu cha kilimo Sokoine. Tuna ardhi ya kutosha. Tuna mito na maziwa na hata bahari. Tuna nguvu kazi vijijini, vijana ambao hukimbilia mijini na kugeuka kuwa machinga.

Hiyo ni mifano michache lakini tuna vingi. Labda kinacho kosekana ni kukosa wasimamia dira na mikakati kuhusu kilimo na viwanda.

Tanzania ingeweza kuwa mzalishaji mkubwa wa mpunga, mahindi na mifugo. Ingezalisha ziada na kuuza sana.

Serikali ingeunda mfuko kusaidia watafiti, wabunifu na wasomi bobezi mbalimbali katika sekta ya kilimo na mifuko.

Serikali ingeandaa mazingira ya kuwezesha wajasiriamali kama Bakhresa kuibuka, kusindika mazao na kuuza nchi nyingine ndani ya Afrika na kwingineko.

Haya ni machache sana katika mengi ambayo yanaweza kuchambuliwa na kupangwa vizuri na wajuzi na wabobevu tulio nao Tanzania.

Hata hivyo, jambo muhimu ni kuwepo kwa dhamira thabiti ya wenye madaraka. Watakao chochea badala ya kukwamisha.

Vinginevyo kudhibiti machinga kwa kukimbizana na mgambo ni mapambano ya kudumu.
Nashukuru mkuu
Kilimo na viwanda ni sekta zingeweza kuajiri 60 _-70 percent ya watu wetu kama
1.Kutumia vizuri vyuo vya kilimo kutoa Maarifa
2.Kuwaandaa vizuri rasilimali watu haswa vijana vijijini na mijini kwenye hizo sekta
3.Kuwa na wasimamia Dira mipango na mikakati wazuri kwenye hizo sekta
4.Kuwa na mfuko maalum wa tafiti na wabunifu kwenyehizo sekta
5.Kushirikiana wawekezaji wakubwa wa ndani ambao wana mifumo mizuri kwenye hizi sekta
6.Dhamira nia na utayari wa kuinua sekta hizi
Hutatamani mkuu tukimbizane na machinga kila siku ni aibu kama taifa linaloendelea
 
Back
Top Bottom