Kwa picha: Ufahamu kuhusu Ulimwengu

Kwa picha: Ufahamu kuhusu Ulimwengu

Actually kuna watu huwa hawaamini na tutazidi kuburuzwa,wakati sisi tunafunga migodi wamarekani wanaandaa mipango ya kufanya exploration ya miadini katika anga
Kuna gari lile lilikuja kama mwezi hivi ,likivuka bahari tukaishia ee ona wazungu oooh gari.Lakini atakuja mwa frika hapa kashiba kande atakwambia haiwezekani kabisa.Oh ni assumptions tu.Basi na sisi tufanye assumptions tufike huko.
Elimu uliyo toa inavutia sana tena sana,unajua unasoma mpaka unasema huyu aliyeumba huu ulimwengu daah.
Haya mambo yapo,na watu kama NASA wana invest billions of dollars kwa ajiri ya projects kibao za anga.Sisi tuendelee na yetu yenye mgando finyu..Mkuu zidi kutoa elimu tamu kama hizo.
 
Ngoja nitaleta mpk aina ya madini yalioyopo kule mars aliyogundua mmrekani,hapa ndipo ujue huyu mmrekani si mtu wa mchezomchezo,yeye baada ya hapa dunian chuma imeikwisha akawa na akili ya plain b,ndipo akaaza reseach mars na kugundua hayo madin.

Kumbuka kuwa hapa dunia madin ya chuma yameisha mpk kupekekea magar na vyombo vingine kuongezewa finnishing ya plasitc, fibre km magar na vyombo vingine.
Hapa ndipo huyu mmrekan atazidi kuwa super power kwani dunia yetu inaitajia sanasan chuma na yeye tu ndie mwenye uwezo wa kwenda kuyachimba huko,chuma hiyo ya kule mars ina thaman kubwa sana.

Inakadiriwa nchi ya pil itayoenda kuchimba chuma huko inaweza kumchukua miaka km mia kumfuata mmarekani huko.

Kuna mtu atakuja hapo atakwambia kusadikika,hawa jamaa weupe wanahangaika usiku na mchana kufanya kila aina ya tafiti.Licha ya mapungufu yao ila hao jamaa watazidi kubarikiwa kwa kuwa wanatumia elimu zao na ujuzi alitupa Muumba haswa.Mkamateni sana Elimu,sidhani kama kuna sehemu Muumba alizuia watu ku explore ulimwengu maana ni vyake nasi ni wake.

Kuna project hii ya reli toka Uingereza mpaka Marekani unaweza juu tu hawa jamaa wapoje.Vipo vingi tu jamaa wanafanya.Wakati sisi tunaendelea kushanga na kuhubiri SGR,Daraja la Kigamboni na Stegler,huko watu walishapita kitambo sana.Na ndio maana tunapata watu wanabisha bisha na kuona haiwezekani.Africa tutafika ila taratibu sana
 
Naombeni mnipe elim kidogo kuhusu black hole
Ni eneo katika space/time ambalo lina mvuto mkali wa gravity,mvuto huo ambao umezigandamiza matter nyingi katika sehemu ndogo,hata mwanga wenyewe hauwezi kutoka katika mgandamizo huo,sababu ya shimo hili jeusi ni wakati nyota kubwa zaidi ya jua letu inapofikia kifo chake.
 
Black holes hutokea pale nyota inapofikia mwisho wa maisha yake na kufa, hiyo nyota hugandamizwa na kupungua size kwa kuwa na umbo dogo hivyo kuwa na nguvu ya uvutano (gravity) kubwa zaidi.
Baada ya black hole kutengenezwa huanza kuvuta na kumeza vitu vilivyo karibu yake mfano huweza kuungana na black holes nyingine, humeza nyota nyingine hivyo kuzidi kukua na kuongezeka ukubwa.
Kutokana na ukubwa wa uwezo wake wa nguvu ya kuvuta vitu, hakuna kitu chochote kinachoweza kupenya ukiwemo mwanga. Mwanga unapoingia kwenye black hole hauwezi kupenya au kuwa reflected kutokana na nguvu ya uvutano iliyopo ndani hivyo basi kila kiingiacho hakiwezi kutoka.
 
Ni eneo katika space/time ambalo lina mvuto mkali wa gravity,mvuto huo ambao umezigandamiza matter nyingi katika sehemu ndogo,hata mwanga wenyewe hauwezi kutoka katika mgandamizo huo,sababu ya shimo hili jeusi ni wakati nyota kubwa zaidi ya jua letu inapofikia kifo chake.
Kweli Mkuu
 
KUZALIWA KWA NYOTA.

Kabla ya nyota kuzaliwa inaanza kama sayari ya kawaida wakati vumbi na hewa (sana sana hydrogen) ikijikusanya. Kadri hii hewa na vumbi vinavyoongezeka basi gravity nayo pia inaongezeka. Tukichukulia ukubwa/uzito wa jua letu kama kiwango (solar-mass) basi mkusanyiko wowote ule wa vumbi na hewa chini ya 0.013 solar-mass (1.3% ukubwa wa jua letu) hiyo itakuwa ni sayari (planet) tu. Kuanzia ukubwa wa 0.08 solar-mass na kuendelea gravity inakuwa kubwa sana (kilo moja hapa duniani ukiipeleka huko itakuwa na uzito wa kilo bilioni 100 na zaidi). Huu mgandamizo mkubwa wa gravity unafanya joto kupanda zaidi ya nyuzi milioni 15 celcius. Hili joto na mgandamizo wa gravity ndio kibiriti kinachofanya hydrogen ichanganyike ketengeneza helium na kutoa nguvu hizi za nyuklia (fusion). Hivi ndio jua linavyozaliwa.

Nyota zinakufaje?
Maisha ya nyota yanategemea sana na ukubwa wake. Nyota ndogo zinaishi muda mrefu sana (zinachoma hydrogen yake taratibu taratibu) kuliko nyota kubwa. Kwa mfano, nyota ndogo kama jua letu inategemewa kuwaka kwa miaka bilioni 10 wakati nyota kubwa sana kamaBetelgeuse zinategemewa kuwaka kwa miaka million 10 tu.

Wakati nyota inawaka kunakuwa na uwiano (equilibrium)wa nguvu ya gravity na nyuklia. Gravity inakandamiza chini wakati milipuko ya nyuklia inasukuma vitu nje. Uwiano huu unaendelea hata baada ya hydrogen ikiisha. Baada ya hydrogen kuisha helium nayo italipuka kinyuklia kutengeneza Carbon na Oxygen. Baadae carbon nayo italipuka kunyuklia kutengeneza iron (chuma). Mara tu nyota inapoanza kutengeneza chuma (iron), mchezo umekwisha. Chuma ni kama maji yanayouzima huu mlipuko wa nyuklia mara moja. Milipuko ya nyuklia ikiacha, ule uwiano (equilibrium) wa gravity na nyukilia unakuwa haupo tena na gravity inashinda. Kila kitu huanguka chini na mlipuko mkubwa sana wa mwisho hutokea na mwanga mkubwa sana (super nova) huonekana.

Vitu viwili vinatokea wakati wa hii super nova. Kwanza, madini nzito zaidi ya chuma (iron) yanatengenezwa kama vile dhahabu, urani, nk. Hii ndio maana dunia yetu pamoja na sisi tunaitwa vumbi la nyota (star dust) kwa saababu kama hizi super nova zisingetokea basi dunia yetu na sisi tusingekuwepo. La pili linaliotokea baada ya kishindo (collapse) ni kuwacha tumba (core) ndogo sana lakini yenye uzito (density) mkubwa wa ajabu. Hii tumba ndio ijulikanayo kama BLACK HOLE.

(For correctness sake, not all stars die and turn into black holes. For instance, our sun is too small to turn into a black hole. When it dies it will collapse into a dense core with properties nowhere close to those of black holes)

Black holes na makaburi ya nyota.
Black holes zinazotokea baada ya nyota kubwa sana (super massive stars) ku-collapse ni vitu vya ajabu sana. Chupa moja ya bia (ujazo wa 0.5 lita) ya hii black-hole ina uzito wa zaidi ya tani 3,000,000,000,000. Gravity inayotokana na hizi black holes ni kubwa kiasi ya kumeza kitu chochote kile (majua, sayari, nk) kinachoikaribia. Hii gravity ni kubwa kiasi cha kumeza hata mwanga (even light cannot escape it) na ndio maana zinaitwa BLACKHOLE kwa sababu hazionekani (mwanga pia unamezwa). Kuwepo wa black hole kunajulikana tu kwa vitu inavyovimeza au vinavyo izunguuka. Usiku ukitoka nje angalia juu. Ukiona ukanda wa nyota nyingi basi huo ndio mkusanyiko wetu wa nyota (Galaxy yetu) unaoitwa MILKYWAY. Katikati ya hii galaxy yetu lipo hili black hole moja ambalo jua letu na nyota nyingine zote zilizopo kwenye hii galaxy yetu zinalizunguuka. Ukitaka kujua hii blackhole yetu iko wapi angalia juu na kama unaijua constellation ya Virgo basi usawa huo ndipo lilipo.

Natumaini hii itasaidia pa kuanzia katika kuzijua nyota.






Sasa tuanze na Big Bang Theory.
Hii ni dhana inayosema kuwa mwanzo kabisa hakukuwa na kitu chochote isipokuwa nishatiiliyokuwa sehemu moja ndogo sana (singularity). Ile nishati ililipuka (big bang -hakuna anaejua kwa nini ililipuka) na kwa kupitia nyenzo ziitwazo Higg's Boson hii nishati ilibadilika na kuwa element nyepesi sana ambayo ni hewa ya hydrogen. Hii hydrogen ilijikusanya kwa wingi na gravity ilipokuwa kubwa hydrogen ili-fuse kutengeneza helium katika mlipuko wa nyuklia (fusion) kama nilivyoainisha hapo awali.

Tatizo ni kuwa hii nyuklia fusion inaweza kutengeneza helium, carbon, oxygen na elements nyingine ambazo ni nyepesi kuliko iron (chuma). Chuma kikianza kutengenezwa tu basi hiyo nyuklia reaction inasimama. Kwa hiyo madini kama zinc, tin, gold, nk. ambazo ni muhimu mwilini mwetu na pia kwa matumizi mengine hizi hutengengenezeka tu wakati wa mlipuko wa supernova.
Baada ya supanova kutokea, tumba (core) inakuwa blackhole na vumbi vumbi lililosambaa linajikusanya makundi makundi na kutengeneza sayari kama dunia yetu.
 
Siku viumbe wenye akili sana kutuzidi watakapo tia timu kwenye anga yetu,mtafaruku utakuwa ni mkubwa sana kuna wanadamu watakao waabudu viumbe hao wakidhani ni miungu,kunawengine watajiandaa na vita na wengine wataamua kukimbilia misituni,viumbe hao kama watakuwa na GSH na wakiwa wamekuja kirafiki na kiroho safi kutakuwa hakuna haja ya mtafafuku.
 
Ila tujifunze angalau kujua makundi ya nyota na hata kuyatambua,ila km itakuwa ni kuandika tu lakin usiyatambue itakuwa ni kaz san kuyajua.
Kwa wale wanoenda na wageni/watalii porin angalu watakuwa wameanza kuujua anga kwa baadhi ya watalii wanakuja kwa ajili ya kutalii utalii wa angani.

Pia kuna hata baadhi ya hotel au camp zimejengwa kwa kaungalia njia za nyota angani kwa kuwavutia wana-astronomy kutoka ng'ambo ulaya au america na pande zingine za dunia hii.

Ngoja nije na ni jinsi gani unaweza ona black hole pale vigro
 
Constellation ya Virgo (au Mashuke) ni mkusanyiko wa nyota unaofananishwa na mwanamwali (Virgin).

Kwa hiyo kama unataka kujua blackhole yetu iko muelekeo gani, jua linapozama tu angalia mashariki ndipo ilipo au angalia straight up kwenye saa sita na nusu usiku. Wakati ukiiangalia hii constellation ya Virgo basi milkway galaxy yetu iko magharibi ya Virgo.Milkway galaxy huwezi kukosa kuiona (hasa usiku wa manane). Utaona nyota nyingi kama mtu amemwaga maziwa (hence milkway) huko angani. Vigro kwa sasa ipo karibu sana na maeneo ya karibu na mwezi kwa leo hii,pemben kuna spica,mars, jirani kidogo lipo jupiter na venus,mzunguko huu ubadilika kutokana na mzunguko wa mwezi,na hizo sayari zingine kwan huwa zinatengana na kuachana kina kitu kwa njia zake

Vitu vinavyomezwa na blackhole vinakuwa sehemu ya hiyo blackhole na inazidi kukua.
 
LAKINI LEO TUJUE KITU FULAN.
TUSIJE KUKACHANGANYA VITU HIVI,KUNA TOFAUTI YA ASTRONOMY NA ASTRONOLOGY.

MIE NIPO UPANDE WA MWANA ASTRONOMY.
 
Inasadikika huenda wanafanana hivi. viumbe hawa wana akili sana,swali linakuja mbona wote hawajavaa nguo,au sisi wanaadamu bado ni washamba?au labda kuficha maungo yetu ni dalili ya kuwa na ubongo ambao bado unakuwa au ni utamaduni wetu tu.
images (8).jpg
unnamed.jpg
aliensjpgjpeg.jpeg
gray-alien1-feature-image.jpg
images (9).jpg
 
Black holes hutokea pale nyota inapofikia mwisho wa maisha yake na kufa, hiyo nyota hugandamizwa na kupungua size kwa kuwa na umbo dogo hivyo kuwa na nguvu ya uvutano (gravity) kubwa zaidi.
Baada ya black hole kutengenezwa huanza kuvuta na kumeza vitu vilivyo karibu yake mfano huweza kuungana na black holes nyingine, humeza nyota nyingine hivyo kuzidi kukua na kuongezeka ukubwa.
Kutokana na ukubwa wa uwezo wake wa nguvu ya kuvuta vitu, hakuna kitu chochote kinachoweza kupenya ukiwemo mwanga. Mwanga unapoingia kwenye black hole hauwezi kupenya au kuwa reflected kutokana na nguvu ya uvutano iliyopo ndani hivyo basi kila kiingiacho hakiwezi kutoka.
Mkuu.upo vizuri
 
Kuna kile chombo maarufu kama Juno kilifika baada ya miaka kadhaa mwaka Jana jupiter.je kimeleta mrejesho gan mpaka sasa iv?
Na je kwenye gas plantes kama Uranus,Jupiter etc..tunaeza tukakanyaga ardh kama hapa.duniani?
 
Kifo cha nyota katika galaxy ya mbali,mlipuko huu (type 2b supernova)unavugumiza nishati kuliko nyota nyingine katika galaxy husika.
images (10).jpg
 
Fungi na Bacteria wa huko Mars wameanza kukishambulia chombo cha utafiti (mars curiosity) magurudumu yameshambuliwa na kuliwa,matundu makubwa yanaonekana kwenye magurudumu ya chombo hicho.
 

Attachments

  • images (11).jpg
    images (11).jpg
    10.2 KB · Views: 72
  • images (12).jpg
    images (12).jpg
    20.1 KB · Views: 77
  • Photo-Credit-NASA-JPL-Caltech-MSSS.jpg
    Photo-Credit-NASA-JPL-Caltech-MSSS.jpg
    53.7 KB · Views: 71
Back
Top Bottom