Kwa nini watanzania wengi wanasota, huku fursa za mauzo nje zikiwa nyingi?

Kwa nini watanzania wengi wanasota, huku fursa za mauzo nje zikiwa nyingi?

MBOKA NA NGAI

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2025
Posts
496
Reaction score
768
Nimekuwa nikiona vitu vingi vinavyouzika nchi za Ulaya na uarabuni. Hasa parachichi, viazi mbatata, matunda mengine yakiwemo machungwa, tikiti maji nk. Bila kusahau maua.

Ukiangalia uhitaji wa hivi vitu, utagundua asilimia kubwa ya vyakula vya asili, vinavyouzika, kwa gharama kubwa, vinatoka Africa. Kampuni za ndege zinahangaika kupata ndege za mizigo, nchi nyingine huku zikihakikisha zinapata cold rooms( vyumba vya kutunza ubaridi), kwa ajili ya mavuno ya mboga mboga na matunda.

Hivi vitu, nchi zikiwemo Kenya na Rwanda, wanapiga sana hela. Watu hawa, hawana ardhi nzuri yenye rutuba kuliko Tanzania.

Je, wale wasomi, wale wanaoenda semina za kila kukicha, wale wanaoiwakilisha nchi kutafuta fursa kwa ajili ya raia, ni kwamba haya masoko hawayaoni?

Juzi limeongelewa swala la Veta, watu hawakulipokea vizuri. Kwa sababu mara nyingi, vitu watu wanavyolishwa darasani, havina uhalisia wa maisha ya nje.

Hizi Cold rooms, ni kwamba nchi haina uwezo wa kuwadhamini wakulima?
Je, Certificates zinazohitajika kupeleka vitu hivi nje,ndo hazipatikani?

Hakuna wale wasomi wa mambo ya kilimo waliopelekwa Israel kwa pesa ya serikali? Ujuzi waliopata huko umelisaidia nini taifa?

Mashirika ya misaada, yanayonunua vyakula, kwa nini Tanzania ibaki, wakati ina kila kitu!
Miaka ya nyuma nchi moja jirani, nilishuhudia watu wakija kukagua na kuelekeza wakulima namna ya kutunza mahindi yao hadi wakati wa mavuno. Watu hawa, walinunua mahindi,kwa kilo, bila kuyapukutua. Hakika ni faida kwa mkulima.

Kwa nini wakulima wasielimishwe, wafanye kilimo cha kibiashara, na hawa wasomi wasio na ajira, wajiajili kwenye kilimo!
Kampuni za bima zihusishwe pia.
 
Sekta nzima ya kilimo haijawahi kupewa thamani hapa Tanzania, ni sekta inatotumiwa kisiasa zaidi kuliko uhalisia. " kilimo ni uti wa mgongo wa mtanzania". Kama ni hivyo kwann isiwe sekta mama na kutengewa budget kubwa?
Kuna mpango gani maalum wakuelimisha vijana kuwekeza kwenye kilimo na kupewa insurance?
 
Hapa wa kulaumiwa ni serikali yetu

Serikali ndo inaweza kuweka namna bora za mkulima kuweza kuzalisha zao lenye kiwango na kuweza kulifikisha huko nje
 
MTOA UZI, HAYA MAMBO UNAYOLETA HUKU KWETU HAYANA TIJA, SISI TUNAWAZA KUTAWALA MILELE BILA KUJALI MAISHA YA TUNAOWAONGOZA
inauma sana fursa hz zpo nchi jirani, huku tunahangaika na madeni ya mama na chawa wa mama..
 
MTOA UZI, HAYA MAMBO UNAYOLETA HUKU KWETU HAYANA TIJA, SISI TUNAWAZA KUTAWALA MILELE BILA KUJALI MAISHA YA TUNAOWAONGOZA
inauma sana fursa hz zpo nchi jirani, huku tunahangaika na madeni ya mama na chawa wa mama..
Ndo maana najiuliza, ambao hawana chochote, wana fursa. Na wanaotafutia vijana hizo fursa, ni watu ambao nchi inao, tena pengine wenye ushawishi mkubwa. Hivi, mfano ukiachana na haya machafuko ya mashariki mwa DRC, hata ukitaka mtu wa Congo aje anunue nyama Tanzania, wapo tayari?
Sasa, ndo hiki wanachotuzidi wazungu. Wao wanahangaikia maisha ya vitukuu, wenzetu tunahangaika na familia zetu.
 
Ndo maana najiuliza, ambao hawana chochote, wana fursa. Na wanaotafutia vijana hizo fursa, ni watu ambao nchi inao, tena pengine wenye ushawishi mkubwa. Hivi, mfano ukiachana na haya machafuko ya mashariki mwa DRC, hata ukitaka mtu wa Congo aje anunue nyama Tanzania, wapo tayari?
Sasa, ndo hiki wanachotuzidi wazungu. Wao wanahangaikia maisha ya vitukuu, wenzetu tunahangaika na familia zetu.
Nitakufuata pm, kuna kuna unacho mkuu
 
Mfano huku nilipo parachichi ni 9k Hadi 16k na ni kutoka India mbaya kinoma. Za kutoka Africa hasa Namibia ni kama zetu tu bei 25k pesa madafu
Siku moja mwaka 2016 niliingia supermarket ya TESLA nikakuta parachichi imeandikwa made in Tanzania!
 
Hivi vitu, nchi zikiwemo Kenya na Rwanda, wanapiga sana hela.
Mzee wa kueneza propaganda za Kagame, kakutuma kuulizia ardhi ya Tanzania???












 
Soko la nje likiwa wazi Kila mtu awe na elimu jinsi ya kulifikia watanzania wengi watainuka kiuchumi maana asilimia kubwa ya watz ni wakulima
 
Mzee wa kueneza propaganda za Kagame, kakutuma kuulizia ardhi ya Tanzania???












Na nyingine weka. Wengine wanatafuta hela, wewe majumgu tu. Propaganda za Kagame zimekujaje!?
 
Back
Top Bottom