Kwa nini Watanzania wengi tuko hivi?

Kwa nini Watanzania wengi tuko hivi?

Ndio tulivyo wabongo yaani unafki muhimu katika kusogeza life. Tulilelewa na kukuzwa hivyo na afadhali hawa watoto waliopo under 10 kwa sasa maana wapo open minded na ndio maana tunaona hawana adabu
 
Yaani na mimi nahangaika na kitu hiki hiki unachokisema hasa hapa kazini kwangu. Yaani watu ni wazembe kiasi mnajikuta mnawafanyia kazi zao over and over again ila usijaribu kusema ukweli! Wee utashukiwa kama jeshi la shetani kuwa wewe ni snitch. Ila mie kila siku nawaeleza sijaja kazini kupendwa bali kufanya kazi!
 
Kuna pahala nilikuwa nafanya kazi, sasa utaratibu mpya ukaanzishwa kuwa tuwe tunasaini asubuhi, ambaye hatasaini hatahesabiwa haki mwisho wa mwezi.
Kutokana na mazingira ya kazi, tukapanga kwenye group wasapu kuwa tusisaini wote coz ni utaratibu mbovu ambao hatuuwezi.
Nakwambia siku ya pili nimeenda asubuhi saa nne nikaona watu wamesaini toka saa 0730 asubuhi!
Nikajiuliza kwamba hawa kwa nn wasingekuwa wazi tu kwamba wataendelea kusaini ili tusipotezeane muda kwenye magroup kumbe wenzetu wana msimamo wao tayari!
 
[emoji23] mada hii safi sana, sio uongo watanzania tunaunafiki uliokubuu asee...

Binafsi ukoo wangu asilimia 90% ni wanafiki hatari, inafika mahala mpaka nashindwa kusema mambo yangu kwa ndugu maana nikisema anaweza kuonyesha kusapoti akirudi pembeni ni kukunafikia tu....

Inafika mahala mpaka mama anamnafikia mtoto wake pembeni baada ya kumface na kumwambia....
 
Nimekuwa nikipenda sana kutumia maneno kwamba waTanzania wengi tunapenda sana kuomba, kupenda kupendwa ama kujipendekeza, sisi ni wavivu na tunapenda sana kulalamika.
Maneno haya nimekuwa nikiyasema sana na haya wakati mwingune niliyatumia humu ndani (Jf), lakini cha ajabu nilishukiwa kwa maneno kama mleta mada alivyo shukiwa.
Wanaomshukia mtoa mada nina uhakika hajaelewa mantiki husika ya mada yake,, ni miongoni mwa wanafiki wenyewe
 
We si unatabia ya kizungu watu hawapendi roho ya jpm wanapenda roho ya jk
@Billie hivi kweli kuwajibika ni uzungu...!!
Yaani unamaanisha kwamba wajibu wa mtu binafsi ni utashi...??
Ama pengine mimi sijakuelewa vizuri chief...!!??
 
Huyo jamaa kutokuja kazini kwake kulikua kunakupunguzia nini exactly?

Ungemfata umuulize tatizo nini kwanza, changamoto ziko kibao.
Bila kumuuliza mtu tatizo personally afu ukaenda kumchoma huo ni UMBEA
Kwa majibu yanayo fanana na haya, kuna jamaa nikiwahi kushuhudia akiambiwa hivi.... don't make your problems other peoples problems
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kupitia hii thread nimeamini maisha bila unafiki hayaendi. Acha tu tuendelee kuwa wanafiki.

[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Halafu nazungumzia tabia zinazotuathiri wote
ukiwa mlevi but unarudi zako kimyakimya kwako sioni kama inanihusu
lakini ukiwa jambazi na unaleta majambazi wenzio mtaani hapo
kunyamaza hadi watu waibiwe ni unafiki na hatari binafsi mapenzi naona ni kitu
cha watu wawili..unaweza ripotia mtu anachepuka kumbe mhusika anajua siku nyingi na hataki wengine wajue
Nadhani watu wengi wanapenda zaidi tunapo jadili mtu na personal zaidi ya pale tukijadili vitu na mambo yanayo igusa zaidi jamii moja kwa moja
 
Wanaomshukia mtoa mada nina uhakika hajaelewa mantiki husika ya mada yake,, ni miongoni mwa wanafiki wenyewe
Na hao ndio wengi wa wale ambao wakisha haribu humu, wanazikimbia na kuzitupa hata ID zao kwasababu wamekuwa wanafiq zaidi ya tunavyo waona humu ndani
 
Yes unakuta huko pm mijadala inaendelea ya kusema tabia mbovu ya baadhi ya ID humu lakini wakija huku jukwaani ni kusifiana tu,,,, unafiki ni donda ndugu nchi hii
Na hao ndio wengi wa wale ambao wakisha haribu humu, wanazikimbia na kuzitupa hata ID zao kwasababu wamekuwa wanafiq zaidi ya tunavyo waona humu ndani
 
Back
Top Bottom