Kwa nini Watanzania wengi tuko hivi?

Kwa nini Watanzania wengi tuko hivi?

Watanzania tuna unafiki mwingi ndani yetu... hatupendi kuambiana ukweli ili kujirekebisha utakuta mtu anachukia kuambiwa ukweli.....we need God kwakweli ili tubadilike ndani yetu ...maana ni heri mtu yule anayekwambia ukweli au anaesimamia ukweli kuliko watu wanaokaa vilinge kusemana semana(mateto) .....
 
Watanzania tuna unafiki mwingi ndani yetu... hatupendi kuambiana ukweli ili kujirekebisha utakuta mtu anachukia kuambiwa ukweli.....we need God kwakweli ili tubadilike ndani yetu ...maana ni heri mtu yule anayekwambia ukweli au anaesimamia ukweli kuliko watu wanaokaa vilinge kusemana semana(mateto) .....

ukiwa mkweli unaweza kosa marafiki
naona wengine wanashiriki tu unafiki kwa kuhofia hili
 
Watanzania wengi ni waoga na wametawaliwa na double standards.

Wanaweza wakaliona jambo fulani ni tatizo na hawataki kabisa liwepo, lakini siku jambo hilo likitatuliwa na likaleta athari kidogo, utashangaa watu hao hao waliokuwa wanakereka na jambo hilo wanaanza kukuluamu wewe mtatuzi.

Ni watu wanaojifanya wanachukia maovu lakini hao hao ndio walea maovu.

Angalia hata humu MMU watu wanavyojifanyaga wanakemea usaliti kwenye ndoa, juzi mtu kaleta uzi hapa akielezea ni jinsi gani asivyofurahishwa na tabia mbaya ya usaliti inayofanywa na mke wa kaka yake na anafikiria kumwambia kaka yake kuhusu maovu yote yanayofanywa na shemeji yake.

Cha ajabu watu hawa hawa ambo wanajifanyaga wanakemea uchepukaji kwenye ndoa walianza kumshambulia mleta mada wakimwambia kwamba aache kihere here.

Na hawa ndio wabongo two faced people
 
Watu wengi walioshi nchi za nje ya Tanzania
hata nchi za Africa tu kama sisi wanasema hiki kitu
tunacho zaidi watanzania..ni kama utamaduni hivi''

Ntakupa mifano hai ambayo binafsi nimeshuhudia..
kuna office nilikuwa nafanya kazi..kulikuwa na jamaa
mmoja office nzima 'anajulikana' kwa uvivu
kutokuja kazini...anaweza kuja kazini siku mbili tu kwa wiki
na akija anakuja kuomba ruhusa anaumwa...

sasa cha ajabu watu wote waliokuwa wanamlalamikia hawataki
kumripoti kabisa kwa HR...HR alikuwa ofisi ingine hapo ni kama branch hivi....Nilipoamua mimi kumripoti jamaa kilichotokea
wale waliokuwa wanalalamika wote wakanishangaa mimi
kwa 'roho ngumu' na ukatili wa kutofikiria jamaa akifukuzwa kazi
familia yake itateseka.....nikabaki mdomo wazi....hii culture ya unafiki mbona tunayo sana?

Nyingine mtaani...kuna mtaa tuli organize Ulinzi hapo mtaani
tukaajiri watu wa kulinda tunawalipa..kwa kuchanga kila nyumba....kilichonishangaza kuna baadhi ya watu walipokuwa
hawalipi...na watu wengi wanalalamika chinichini...
siku moja nikawataja tu wasiolipa waziwazi huku wapo wanasikia
wale walikuwa wanalalamika wakageuka kuwa nilichokifanya
sio kizuri...tungewavumilia tu hadi wangeona aibu wenyewe..
dah kwakweli hapo nikabaki tena mdomo wazi na huu utamaduni wetu wa unafiki..kitu kinakukera hutaki kuonekana
unakereka..saa zote unataka kuonekana mwema kwa kila mtu..

nimejiuliza sana why sisi watanzania huu utamaduni tunao sana?
Hamna tabia ambayo naichukia maishani mwangu kama unafiki
 
Umenikumbusha kuna siku miaka mingi kidogo, nilikuwa naongelea uzembe serikalini.

Nikachambua wizara fulani, nikasema hapa kwa kufuata uwajibikaji Waziri alitakiwa kujiuzulu.

Uncke wangu mmoja alinitazama akaniambia ujue na hawa mawaziri wana familia zao zinawategemea.

Yani hilo ndilo lilikuwa la muhimu kabisa kwake.

Nikashangaa sana, kama wana famikia zinawategemea mbona wanafanya kazi kwa uzembe.

Nafikiri kuna generation fulani inaona kazi ni sehemu ya haki ya mtu kupata mshahara (well, to some extent ni sawa, kika mtu ana haki ya kufanya kazi ambayo ana uwezo nayo kwa kipaji chake, this is a basic human right). Lakini haki huwa zinakuja na wajibu, haki ya kupata kazi inakuja na wajibu wa kufanya kazi.
 
Umenikumbusha k7na siku miaka mingi kidogo, nilikuwa naongelea uzembe serikalini.

Nikachambua wizara fulani, nikasema hapa kwa kufuata uwajibikaji Waziri alitakiwa kujiuzulu.

Uncke wangu mmoja alinitazama akaniambia ujue na hawa mawaziri wana familia zao zinawategemea.

Yani hilo ndilo lilikuwa la muhimu kabisa kwake.

Nikashangaa sana, kama wana famikia zinawategemea mbona wanafanya kazi kwa uzembe.

Nafikiri kuna generation fulani inaona kazi ni sehemu ya haki ya mtu kupata mshahara (well, to some extent ni sawa, kika mtu ana haki ya kufanya kazi ambayo ana uwezo nayo kwa kipaji chake, this is a basic human right). Lakini haki huwa zinakuja na wajibu, haki ya kupata kazi inakuja na wajibu wa kufanya kazi.

Mimi kinachonishangaza ni ile tatizo tunalijua kuwa ni mtu fulani hafai
uki suggest huyo mtu aondolewe tu unashangaa watu wanakuona katili
 
Nimeipends sana hio Cole, ni concrete evidence ya comment yangu iliyopita.

Masuala ya mapenzi unaweza sema ni kitu binafsi zaidi
mimi sipendi wanawake waliojichubua lakini siwezi kukulaumu wewe ukichukua
mwanamke aliejichubua
sio sawa na jambo linalo tuathiri wote
mfano uwe unachafua mtaa kwa kutupa takataka na zinatuathiri wote
hapo ni kinyamaza huku sipendi ndo unafiki wenyewe
au nipinge watu kuja kukuambia live kwenye kikao huo ndo unafiki ninao ongelea
mapenzi ni kitu binafsi....

sipendi makahaba lakini wewe ukioa khaba ambae hajatulia hainihusu
 
Wewe waTz tuache ka tulivyo, utaumia tu ubongo wako, Unakuta abiria anahadithia:
''nilijua tu kuwa gari itapata ajali maana wakati napanda niliona tairi ni kipara kweli halafu sasa dreva akawana anaendesha speed kali, nikawaza hii speed na zile tairi Mmh? Ila nashukuru Mungu sijaumia sana''.
 
Mnaomshambulia mtoa mada kwa comments zake kwenye mada nyinginezo naona kama mnamuonea,

Mfano wa huyo mwanamke mchepukaji je aliyekuww akimsema huyo mwanamke yupo humu? Nilidhani labda mwanamke husika aliyekuwa akisemwa angetajwa jina lake ama ID yake humu kuwa wewe fulani unachepuka na huyu mtoa mada akapost vile ndo ingekuwa halali kuwa nae ni mnafiki tu kama wengine anaowazungumzia

Mtaamini vipi yule mtoa mada kama alikuwa anazungumzia hadithi tu na sio uhalisia

Nilivyomwelewa mtoa mada anashangazwa na watu wanaolalamikia tabia mbovu za watu katika jamii husika pasipo kuwakabili wenye tabia hizo ili wabadillike wanabaki wananung'unika pembeni na kuwachekea tu,,, huu ndo unafiki wenyewe

Mtu kachepuka huko mtaani mchane huko huko aliko unapoleta humu bila kumkanya huko huo nao ni unafiki
 
Mnaomshambulia mtoa mada kwa comments zake kwenye mada nyinginezo naona kama mnamuonea,

Mfano wa huyo mwanamke mchepukaji je aliyekuww akimsema huyo mwanamke yupo humu? Nilidhani labda mwanamke husika aliyekuwa akisemwa angetajwa jina lake ama ID yake humu kuwa wewe fulani unachepuka na huyu mtoa mada akapost vile ndo ingekuwa halali kuwa nae ni mnafiki tu kama wengine anaowazungumzia

Mtaamini vipi yule mtoa mada kama alikuwa anazungumzia hadithi tu na sio uhalisia

Nilivyomwelewa mtoa mada anashangazwa na watu wanaolalamikia tabia mbovu za watu katika jamii husika pasipo kuwakabili wenye tabia hizo ili wabadillike wanabaki wananung'unika pembeni na kuwachekea tu,,, huu ndo unafiki wenyewe

Mtu kachepuka huko mtaani mchane huko huko aliko unapoleta humu bila kumkanya huko huo nao ni unafiki

Halafu nazungumzia tabia zinazotuathiri wote
ukiwa mlevi but unarudi zako kimyakimya kwako sioni kama inanihusu
lakini ukiwa jambazi na unaleta majambazi wenzio mtaani hapo
kunyamaza hadi watu waibiwe ni unafiki na hatari binafsi mapenzi naona ni kitu
cha watu wawili..unaweza ripotia mtu anachepuka kumbe mhusika anajua siku nyingi na hataki wengine wajue
 
Halafu nazungumzia tabia zinazotuathiri wote
ukiwa mlevi but unarudi zako kimyakimya kwako sioni kama inanihusu
lakini ukiwa jambazi na unaleta majambazi wenzio mtaani hapo
kunyamaza hadi watu waibiwe ni unafiki na hatari binafsi mapenzi naona ni kitu
cha watu wawili..unaweza ripotia mtu anachepuka kumbe mhusika anajua siku nyingi na hataki wengine wajue
Yes na mie ndo nilivyokuelewa, watu kulalamika ama kukerwa kuhusu ubovu wa tabia za watu fulani pembeni pasipo kuchukua hatua za kuwabadilisha lakini akitokea mkweli mmoja akamsema muhusika hao hao wakerwaji wanaanza kumlalamikia huyu mkweli na kumuacha muovu ilhali wanakerwa na maovu yake(Unafiki)
 
Nimekuwa nikipenda sana kutumia maneno kwamba waTanzania wengi tunapenda sana kuomba, kupenda kupendwa ama kujipendekeza, sisi ni wavivu na tunapenda sana kulalamika.
Maneno haya nimekuwa nikiyasema sana na haya wakati mwingune niliyatumia humu ndani (Jf), lakini cha ajabu nilishukiwa kwa maneno kama mleta mada alivyo shukiwa.
 
Wewe waTz tuache ka tulivyo, utaumia tu ubongo wako, Unakuta abiria anahadithia:
''nilijua tu kuwa gari itapata ajali maana wakati napanda niliona tairi ni kipara kweli halafu sasa dreva akawana anaendesha speed kali, nikawaza hii speed na zile tairi Mmh? Ila nashukuru Mungu sijaumia sana''.

Hii imenichekesha sana ingawa ndo kweli tuko hivi
 
Back
Top Bottom